Vifurushi vya intaneti 'visivyo rasmi' kwa kampuni za simu

Hawana kwa sasa, ila trend ya sasa ni kila anaetoa 5G anakuja na unlimited service. Tigo pia kuna wadau humu walisema wanakuja na bando kama supakasi.
Naona sasa hivi kuna kaushindani kwa haya mashirika ya simu,kuna kipindi ilikua package zao zinafanana na wakipandisha bei wote wanapandisha ila kwa sasa vifurushi na ofa zao zinatofautiana kidogo
 
Naona sasa hivi kuna kaushindani kwa haya mashirika ya simu,kuna kipindi ilikua package zao zinafanana na wakipandisha bei wote wanapandisha ila kwa sasa vifurushi na ofa zao zinatofautiana kidogo
Tatizo ni serikali, kwenye oligopoly vitu kama Mafuta, Mitandao wanapanga bei.

Ila hivi vifurushi kama postpaid na vyengine vya biashara havipo mkumbo huo ndio maana unaona wanatoa GB nyingi. Wakiachiwa washindane vifurushi vya usiku, unlimited kama zile za Royal bundle zitarudi kwa kasi.
 
HUDUMA YA nn Hii mkuu
 
Wakuu kuhusu yule jamaa wa Airtel aliyetumwa na kiongozi wake.

Jamaa akanicheki mapema leo kaniambia baadaye saa 10 anaibuka. Nikasema poa.

Baada ya muda kidogo kupita akanipigia simu kuwa vifaa vinechukuliwa sana kwa hiyo imebaki device moja (maana nili request Router mbili)

Nikamwambia njoo na hiyo moja hiyo nyingine naweza kuifata mwenyewe ofisini kwenu directly.

Lakini kwasababu umeme umekatika nikawaza vipi akihitaji maswala ya tin, leseni itakuwaje?

Ikabidi nimuulize mahitaji yanayotakiwa yanaweza kuwekwa kwa mfumo wa soft copy. Akakinijibu kuwa hayo yote hayahitajiki cha msingi namba ya NIDA tu.

Nikastuka! Ikabidi nimuulize "lakini baada ya wewe kuleta hicho kifaa si hapo hapo uta activate na mimi kuanza kutumia unlimited internet kuanzia muda huo?"

Akasema huduma hii sio unlimited unapewa GB100 tu.

Ambapo zikiisha kabla ya mwezi utakuwa unapewa GB 3 kila siku mpaka mwezi uishe.

Ambapo hiyo Router utauziwa kwa 75,000

Nikamuambia basi hatukuelewana jana maana mimi nilitaka unlimited na nilisisitiza.

Kwa hiyo mchongo ukaishia hapo.
 
Huyu jamaa hapa na kuna mwingine pia wamesema huduma hii ni buree kiukweli inasaidia sana kuliko hata postpaid kama itadumu mda mrefu.

Hivi vifurushi naona watu kama wanavipotezea fulani lakini mi binafsi nmevipenda sana ni mtandao wa halotel laini unasajili ni kwa ajili ya internet tu haipigi simu wala haitumi sms, haipigiwi wala haipokei sms...


Laini hizi mpya kwa ajili ya internet tu Ukipiga unaambiwa namba hii haipo nasikia namba yake haianzi na ziro hapana ni huduma mpya.. Mimi pia nimepewa haya maelekezo na mtu aliepost humu ukihitaji huduma unapata.


Mimi kwa sasa nipo na postpaid ya tigo nina mwezi wa 4 sasa ila nampango nikifikisha miezi 6 nivunje mkataba na tigo sjui wtanikubalia hivi kuna ambae amefanikiwa kuvunja mkataba huu, alifanyaje naomba anielekeze na mi nivunje aisee wakati najiunga sijujaza mkataba wowote wa tigo maana niliungwa na mdau nilimtumia taarifa zangu kweny WhatsApp nataka nihamie kweny hii halotel aisee mambo ni fire[emoji91][emoji91][emoji91]
 
Hivi ni vifurushi vya Halotel vile ambavyo unasajili laini?

Hicho cha 5,000 nimejiunga sana tangu kilivyokuwa kikiuzwa 3,000 kwa 9GB
 
Hivi ni vifurushi vya Halotel vile ambavyo unasajili laini?

Hicho cha 5,000 nimejiunga sana tangu kilivyokuwa kikiuzwa 3,000 kwa 9GB
Bila shaka unasajili laini ila ni kwa ajili ya internet tu haipigi simu wala haitumi sms wala haipigiwi nasikia ina speed hatari.. Pia namba yake haianzi na ziro.
 
Bila shaka unasajili laini ila ni kwa ajili ya internet tu haipigi simu wala haitumi sms wala haipigiwi nasikia ina speed hatari.. Pia namba yake haianzi na ziro.
Laini ya mfumo huo niliwahi kusajiliwa mwanzo ilikuwa inatoa 31GB yani unapewa 27GB hakafu baada ya muda zinaingia 4GB kwa ajili ya 4G

Tulikuwa tunalipia 15,000

Laini inakuja na sms na dakika lakini hazifanyi kazi. Hakikukaa muda mrefu likafungwa
 
Laini ua mfumo huo niliwahi kusajiliwa mwanzo ilikuwa inatoa 31GB yani unapewa 27GB hakafu baada ya muda zinaingia 4GB kwa ajili ya 4G

Tulikuwa tunalipia 15,000

Laini inakuja na sms na dakika lakini hazifanyi kazi. Hakikukaa muda mrefu likafungwa
Inawezekana ikawa ndo hiyo Dah! Watu mna siri yaani nawe ulikaa kimya mpka leo ndo unasema?? Mbona ilikuwa kitonga sana ilikuwa mwaka gani mkuu.
 
Inawezekana ikawa ndo hiyo Dah! Watu mna siri yaani nawe ulikaa kimya mpka leo ndo unasema?? Mbona ilikuwa kitonga sana ilikuwa mwaka gani mkuu.
Hapana ile ilikuwa ni mpaka mtu mkutane physically

Kwa hiyo huku mtaani kulikuwa kuna dogo ambaye alikuwa anafanya kazi Halotel

Baadaye nilikuja kujua kuwa kila mwezi wale ma super agent wa Halotel huwa wanapewa task ya kusajili laini zaidi ya 200 kwa mwezi ili walipwe hele nyingi.

So hapo ndio wanapotuma vijana kwenda mitaani waje wasajili.

Kifurushi hicho cha 31GB nimeunga mara moja tu.

27GB hizo unapewa hapo hapo halafu baada ya muda zinakuja 4GB kama device yako inatumia 4G.

Hizo 4GB zilikuwa zinadumu kwa siku 3 tu wakati 27GB ni mwezi

 
Sa unazani unajua Kila kitu mie nimekuja kushtuka na. VPN za ttcl Baada ya siku 10 tu kikasanuka alafu nasikia watu wametumia miezi 4 nyuma
Hata mimi mwenyewe sikujua.

Nimetumia wiki moja baada ya hapo wakaikata.

Ila so far kwenye hiyo wiki moja sikuwa mzembe.

Nimekula 64GB ndani ya wiki
 
Fellas

Kwenye hii menu ya Airtel tambueni kuna kifurushi kimoja tu hapo ambacho ni 30Mbps kwa Sh. 110,000

Hakuna kifurushi cha 70,000 msihadaike hilo ni pambo na ni mbinu ya kibiashara tu.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…