Wakuu kuhusu yule jamaa wa Airtel aliyetumwa na kiongozi wake.
Jamaa akanicheki mapema leo kaniambia baadaye saa 10 anaibuka. Nikasema poa.
Baada ya muda kidogo kupita akanipigia simu kuwa vifaa vinechukuliwa sana kwa hiyo imebaki device moja (maana nili request Router mbili)
Nikamwambia njoo na hiyo moja hiyo nyingine naweza kuifata mwenyewe ofisini kwenu directly.
Lakini kwasababu umeme umekatika nikawaza vipi akihitaji maswala ya tin, leseni itakuwaje?
Ikabidi nimuulize mahitaji yanayotakiwa yanaweza kuwekwa kwa mfumo wa soft copy. Akakinijibu kuwa hayo yote hayahitajiki cha msingi namba ya NIDA tu.
Nikastuka! Ikabidi nimuulize "lakini baada ya wewe kuleta hicho kifaa si hapo hapo uta activate na mimi kuanza kutumia unlimited internet kuanzia muda huo?"
Akasema huduma hii sio unlimited unapewa GB100 tu.
Ambapo zikiisha kabla ya mwezi utakuwa unapewa GB 3 kila siku mpaka mwezi uishe.
Ambapo hiyo Router utauziwa kwa 75,000
Nikamuambia basi hatukuelewana jana maana mimi nilitaka unlimited na nilisisitiza.
Kwa hiyo mchongo ukaishia hapo.