Uchaguzi 2020 Vijana kuweni makini kwa ahadi za uongo kutoka Vyama vya Upinzani

Uchaguzi 2020 Vijana kuweni makini kwa ahadi za uongo kutoka Vyama vya Upinzani

1.ewe ni nani hata utufokee vijana?

2. Mageuzi ndani ya chama yanatuhusu nini sisi?

3. Mambo ya Misri usituambie kabisa

4. Hakuna anayesema kutakuwa na ajira 100%, mmefanya mambo ya ovyo yaliyopelekea kupungua kwa ajira

#USITUFOKEE
Kabla ya uhuru tanganyika ilikuwa imeendelea kuliko japan mavijana hayahaya yakadanganywa yakachagua tanu miaka mitano badae tulikuwa masikini wa pili duniani nyuma ya bangladesh, leo tumefika uchumi wa Kati yameanza tena kudanganywa,

Mwaka 1954 chama Cha Nationalist ndio kilikuwa na sera nzuri hawahawa vijana wakadanganywa na mwalimu wa form two.
 
magufuli ni bonge la rais kuwahi tokea tanzania bt kinachomponza zaidi ni ile team maslahi ndani ya ccm, hawa mabwana maslahi yao yalipominywa wamekua na chuki za wazi wazi na ndo watukanaji wakubwa wa magufuli mitandaoni, hawa ndo wanachagiza kuupa nguvu upinzani ulojifia.
 
Baada ya kufuatilia hotuba nyingi za vyama vya upinzani ninapenda kuwasihi vijana kuwa na tahadhari kwa ahadi zisizoweza kutekelezeka.

Nikianzia suala la ajira ni tatizo la sehemu kubwa duniani watu wamepoteza kazi kwa hali mbaya ya kiuchumi pamoja na tatizo la ugonjwa huu wa COVID19 ulipojitokeza.

Suala la kusema kuwa wakishika madaraka wataruhusu wananchi wataruhusiwa kwenda kuishi kwenye hifadhi ni la upotoshaji mkubwa kwani tukiruhusu utekelezaji huo ina maana utalii utakufa.

Ninatoa mfano nchi ya Misri 2011 wananchi walimuondoa madarakani Rais Hussein Mubarak kupitia chama cha Muslim Brotherhood baada ya chama hicho kutoa ahadi nyingi zisizoweza kutekelezeka kufika mwaka 2013 wananchi hao hao waliiingia mitaani kupinga hicho chama matokeo Jeshi la nchi hiyo likatwaa madaraka tena.

Tumeona hapa majirani zetu Kenya baada ya kuiondoa KANU madarakani na kupata katiba mpya leo wakenya wanaikumbuka KANU kwani Ufisadi na ukabila umekuwa mkubwa sana kufikia kuhatarisha umoja wa nchi hiyo. Katika uchaguzi wa mwaka 2007 wananchi kupitia vyama hivyo vilipigana vita vya kikabila na maelfu ya wananchi walipoteza maisha.

Kwa mustakabali wa nchi yetu Tanzania bado CCM ni chama pekee kinachoweza kuipeleka nchi katika uchumi mzuri na umoja wa kitaifa.

Tusijaribu kufanya kosa kubwa la kutoipigia kura CCM na haswa Rais Magufuli ambaye ameleta mageuzi makubwa ndani ya chama hicho na serikali kwa ujumla.
Vijana wawemakini na ahadi za uongo za wagombea ,sikilizeni na chambueni,huwezi tafuta ufafanuzi was kilichozungumzwa
 
Hakika mkuu!
FB_IMG_15993755231329679.jpg
 
Mku swala la ajira kwa ujumla ninaamini viongozi waliopewa mamlaka kuongoza nchi hii sio creative ya sio wabunifu.
Hivi tuu kwa akili ya kawaida sector ya Kilimo inauwezo wa kuajiri watu wote wasiokuwa na ajira nchi nzima.
Mfano Rais fedha zilizonunulia ndege angeziingiza ktk kilimo cha umwagiliaji leo kiajira tungekuwa wapi. Kingine Watanzania wengi kujiajiri ni kawaida sasa niambie huyu ambaye aliyejiari katika kilimo cha msimu kama Serikali ingemjengea Malambo ya kuhifadhia Maji na kuzijenga Skimu za kupeleka maji mashambani leo hii tusingetumia nguvu kubwa kuomba kura au kulalamika swala ajira. Kwa ujumla chama changu hapa kimechemka kwa huko ktk nchi zingine tumeona serikali zikiondolewa madarakani kwa ajili ya ajira kwa hiyo tangu pale Lowassa alipozungumzia swala la ajira leo hii ni miaka ishirini imepita hakuna ufumbuzi wake. Na pale wasomi wasiokuwa na ajira anavyooji au kuwa na maswali mengi juu ya serikali ya chama changu anaitwa sio mzalendo na kumbuka hawa wanaoitwa sio wazalendo kwa kuuliza yaliyohaki yao wanazidi kuongezeka kila mwaka kwani idadi ya wasomi inazidi kuongezeka kila mwaka na kukosa ajira kwa hiyo tukubaliana na lolote kwani tulipewa miaka mingi ya kulishughulikia hili swala. Na baada wapinzani wetu kujua uwezo wakuongeza ajira wanao ndo maana wamelishikilia kwani strategy .
Hivi inakuwaje Uganda inapitishia mizigo yao ktk bandari yetu then ss watz tunaenda kununua bidhaa kwao badala ya Waganda kuja kununua Tz hivi kweli hii ni akili. Watanzania wa leo sio wajinga kwa wanaona na wanaelewa
Tatizo wakishajiona wao wapo kwenye mifumo rasmi basi wanasahau kilakitu juu ya wengine hilo ndio tatizo kubwa
 
Naunga mkono hoja 100%

Yani mtoa uzi anataka kwa mara nyingine tuchague:

Kuuliwa na kuokotwa baharini

Kubambikiwa kesi na kufungwa bila hatia (Masheikh)

Kufilisiwa na TRA kwa maelekezo ya maguful

Kunyimwa uhuru wa kujieleza

Kukosa ajira

Kutoongezewa mishahara kwa miaka 5 tena ( lakini wao wanasiasa wanajipendelea mishahara minono na marupurupu kibao)

Kunyang'anywa pension kwa kutumia kikokotoo kipya inaanza 2023
(Wakati huo bungeni wanapewa milioni 282 kila baada ya miaka 5

Tuchague jitu libaguzi na likabila

Tuchague mropokaji asiyejua anazungumza nini na wapi

Tuchague kujengewa chatto, wanyama kuhamishiwa chatto, uwanja wa mpira kujengwa chatto

Tumeshachagua madaraja, ndege na barabara, dharau, vitisho na mauaji Inatosha!
Sasa tunachagua maendeleo ya watu na utu.

Twende na Lissu.
Pamoja sana Mkuu! Umesema vema.
 
Acha kudanganya wewe. Uko zama gani wewe? Viwanda vya zama hizi siyo labour intensive kwasabb ya kukua kwa teknolojia.

Wewe unapuyanga, I have all, the knowledge, skills and expertise in the field.

Kama huelewewi kaulize kuanzia ground at gin stands to a finished product ......what it takes forgetting about cotton farming, sells, transporting seed cotton, loading etc.
 
Kabla ya uhuru tanganyika ilikuwa imeendelea kuliko japan mavijana hayahaya yakadanganywa yakachagua tanu miaka mitano badae tulikuwa masikini wa pili duniani nyuma ya bangladesh, leo tumefika uchumi wa Kati yameanza tena kudanganywa,

Mwaka 1954 chama Cha Nationalist ndio kilikuwa na sera nzuri hawahawa vijana wakadanganywa na mwalimu wa form two.
Wakubwa huwa hawadanganyi,sasa inakuwaje wewe ni mkubwa halafu unadanganya?
 
Tatizo wakishajiona wao wapo kwenye mifumo rasmi basi wanasahau kilakitu juu ya wengine hilo ndio tatizo kubwa
Hapo ndipo kwenye matatizo zaidi has hizi siasa za kusifiasifia zinamfanya kiongozi kutokuona kuna mahali penye shida.
Hili la ajira sio la kubeza kabisa kwani tulishughudia yaliyowapata Tunisia na ukifuatilia kwa umakini tatizo lilikuwa ni ajira.
 
UZWAZWA nao ni KIPAJI. Eti huyo anayejiita kichaa kaleta mageuzi makubwa. UPUMBAVU Nchini unazidi kushamiri kwa kasi ya kutisha. Mxiewwwwwwwwww!



Baada ya kufuatilia hotuba nyingi za Vyama vya Upinzani ninapenda kuwasihi vijana kuwa na tahadhari kwa ahadi zisizoweza kutekelezeka.

Nikianzia suala la ajira ni tatizo la sehemu kubwa duniani watu wamepoteza kazi kwa hali mbaya ya kiuchumi pamoja na tatizo la ugonjwa huu wa COVID19 ulipojitokeza.

Suala la kusema kuwa wakishika madaraka wataruhusu wananchi wataruhusiwa kwenda kuishi kwenye hifadhi ni la upotoshaji mkubwa kwani tukiruhusu utekelezaji huo ina maana utalii utakufa.

Ninatoa mfano nchi ya Misri 2011 wananchi walimuondoa madarakani Rais Hussein Mubarak kupitia chama cha Muslim Brotherhood baada ya chama hicho kutoa ahadi nyingi zisizoweza kutekelezeka kufika mwaka 2013 wananchi hao hao waliiingia mitaani kupinga hicho chama matokeo Jeshi la nchi hiyo likatwaa madaraka tena.

Tumeona hapa majirani zetu Kenya baada ya kuiondoa KANU madarakani na kupata katiba mpya leo wakenya wanaikumbuka KANU kwani Ufisadi na ukabila umekuwa mkubwa sana kufikia kuhatarisha umoja wa nchi hiyo. Katika uchaguzi wa mwaka 2007 wananchi kupitia vyama hivyo vilipigana vita vya kikabila na maelfu ya wananchi walipoteza maisha.

Kwa mustakabali wa nchi yetu Tanzania bado CCM ni chama pekee kinachoweza kuipeleka nchi katika uchumi mzuri na umoja wa kitaifa.

Tusijaribu kufanya kosa kubwa la kutoipigia kura CCM na haswa Rais Magufuli ambaye ameleta mageuzi makubwa ndani ya chama hicho na serikali kwa ujumla.
 
Baada ya kufuatilia hotuba nyingi za Vyama vya Upinzani ninapenda kuwasihi vijana kuwa na tahadhari kwa ahadi zisizoweza kutekelezeka.

Nikianzia suala la ajira ni tatizo la sehemu kubwa duniani watu wamepoteza kazi kwa hali mbaya ya kiuchumi pamoja na tatizo la ugonjwa huu wa COVID19 ulipojitokeza.

Suala la kusema kuwa wakishika madaraka wataruhusu wananchi wataruhusiwa kwenda kuishi kwenye hifadhi ni la upotoshaji mkubwa kwani tukiruhusu utekelezaji huo ina maana utalii utakufa.

Ninatoa mfano nchi ya Misri 2011 wananchi walimuondoa madarakani Rais Hussein Mubarak kupitia chama cha Muslim Brotherhood baada ya chama hicho kutoa ahadi nyingi zisizoweza kutekelezeka kufika mwaka 2013 wananchi hao hao waliiingia mitaani kupinga hicho chama matokeo Jeshi la nchi hiyo likatwaa madaraka tena.

Tumeona hapa majirani zetu Kenya baada ya kuiondoa KANU madarakani na kupata katiba mpya leo wakenya wanaikumbuka KANU kwani Ufisadi na ukabila umekuwa mkubwa sana kufikia kuhatarisha umoja wa nchi hiyo. Katika uchaguzi wa mwaka 2007 wananchi kupitia vyama hivyo vilipigana vita vya kikabila na maelfu ya wananchi walipoteza maisha.

Kwa mustakabali wa nchi yetu Tanzania bado CCM ni chama pekee kinachoweza kuipeleka nchi katika uchumi mzuri na umoja wa kitaifa.

Tusijaribu kufanya kosa kubwa la kutoipigia kura CCM na haswa Rais Magufuli ambaye ameleta mageuzi makubwa ndani ya chama hicho na serikali kwa ujumla.
Milioni 50 kwa kila Kijiji ahadi hiyo ni nani ALIYETUTAPELI, ili tusimpe nafasi hiyo tena?
 
Ukosefu wa ajira nchi hii haujasababishwa na corona, upo miaka yote hasa hii ya Magufuli. Kwanza corona Tanzania haipo, sasa hizo ajira zimepoteaje wakati corona haipo?

Ccm kwa miaka zaidi ya 60 imeshindwa kuleta maendeleo leo hii ndio ilete maendeleo?

Magufuli amefanya kitu gani? Kununua ndege na kujenga madaraja? Leo hii karne ya 21, miaka 60 ya uhuru unakuja kutuambia madaraja na ndege ndio mabadiliko ya maendeleo? Wakoloni walifanya haya miaka zaidi ya 60 iliyopita.

Ccm ambayo imekua ikitoa ahadi zisizotekelwzeka kwa miaka 60 unaizungumziaje? Mfano ahadi ya 50m kila kijiji?

CCM hata ipewe miaka 500 haina mbinu mpya tena ya kutuvusha kutoka sehemu moja kwenye nyingine. Hapo ilipofika imefika mwisho.
Naona Umeandika Upuuzi mtupu. Hivi unadhani ukidanganywa kwamba Madaraja na ununuzi wa ndege hauna manufaa kwa watanzania kwa sababu watanzania hawana uwezo wa kupanda ndege unaacha kuwaza nje ya box kwamba kazi ya ndege ni kutuingizia fedha za kigeni zitakazopelekea wewe na watoto Wako kuhudumiwa na Serikali yako hata hilo hujui?


Barabara na madaraja visipojengwa nani Atakubali kupeleka. Chombo chake kubeba mazao kwa gharama nafuu?

Je!unajua kwa kukosa miundombinu bora ndiko kunakochangia Mfumuko wa bei? Hivi hata kama ungekua na fedha mfukoni kwa kutokuwekeza kwenye miundombinu hata hiyo PESA hisingekua na thamani kwako.

Sidhani kama wewe ulikuwepo wakati nchi hii imetoka kwenye utawala wa mkoloni. Tuulize sisi tuliokuwepo ndugu ndio tutakusimulia shida na Hadha tuliokua tunaipata.

Nyie mmezaliwa juzi mmekuta CCM imefanya kazi kubwa kuboresha nchi hii Leo unatumia Smartphone kutukana serikali? Hujui CCM ilipoitoa nchi hii KIJANA.

Leo unapanda gari unaenda kila maali kwa wakati sisi tulikua tunakesha kutoka mkoa 1 kwenda mwingine nyie mmekuta Neema mmevimbiwa na kutukana.

Ni mjinga tena lofa Atakae sema Serikali ya chama cha mapinduzi haijafanya kitu kwenye nchi hii.
 
Naona Umeandika Upuuzi mtupu. Hivi unadhani ukidanganywa kwamba Madaraja na ununuzi wa ndege hauna manufaa kwa watanzania kwa sababu watanzania hawana uwezo wa kupanda ndege unaacha kuwaza nje ya box kwamba kazi ya ndege ni kutuingizia fedha za kigeni zitakazopelekea wewe na watoto Wako kuhudumiwa na Serikali yako hata hilo hujui?


Barabara na madaraja visipojengwa nani Atakubali kupeleka. Chombo chake kubeba mazao kwa gharama nafuu?

Je!unajua kwa kukosa miundombinu bora ndiko kunakochangia Mfumuko wa bei? Hivi hata kama ungekua na fedha mfukoni kwa kutokuwekeza kwenye miundombinu hata hiyo PESA hisingekua na thamani kwako.

Sidhani kama wewe ulikuwepo wakati nchi hii imetoka kwenye utawala wa mkoloni. Tuulize sisi tuliokuwepo ndugu ndio tutakusimulia shida na Hadha tuliokua tunaipata.

Nyie mmezaliwa juzi mmekuta CCM imefanya kazi kubwa kuboresha nchi hii Leo unatumia Smartphone kutukana serikali? Hujui CCM ilipoitoa nchi hii KIJANA.

Leo unapanda gari unaenda kila maali kwa wakati sisi tulikua tunakesha kutoka mkoa 1 kwenda mwingine nyie mmekuta Neema mmevimbiwa na kutukana.

Ni mjinga tena lofa Atakae sema Serikali ya chama cha mapinduzi haijafanya kitu kwenye nchi hii.
Ccm imefanya kazi kubwa ipi?

Unasema ulikuwepo enzi za wakoloni, je hao wakoloni hawakua na ndege, wahakujenga barabara, hawakujenga reli? Leo hii miaka 60 bado tunakuja kuambiwa eti reli ni maendeleo, basi wakolni walishayaleta zaidi ya miaka 60 iliyopita kama hayo ndio maendeleo.

Miaka 60 ya uhuru bado serikali inazungumzia ndege, barabara, reli huku watu hawana huduma za afya, hakuna maji, hakuna madawa, hakuna wauguzi, hakuna madawati, hakuna madarasa, eti ndege na barabara.

Ccm kwa miaka 60 ilichokifanya kwa Tanzania ni sawa na kijana wa miaka 25 kufanya matendo au mambo ya mtoto wa miaka 3, kuchezea kinyesi chake, kuchezea mkojo, kula matope. Huwezi kusema huyo kijana wa miaka 25 anaefanya mambo ya mtoto wa miaka 3 kua amekua.

Mimi kutokuwepo huko nyuma bado hakuondoi ukweli kua hakuna kitu ccm imefanya kwa nchi hii zaidi ya kuwafanya raia waendelee kua fukara wa kutupwa.

Wazee kama nyie wenye mawazo ya hovyo ndio bado mnasababisha hii nchi kuendelea kua masikini.

Wazungu huwema age comes with experience and wisdom but sometimes age comes alone, wewe age came alone.(kwa kiswahili hata wajinga huzeeka).
 
Back
Top Bottom