Vijana Msijidanganye: Ukiamua kujiajiri ni lazima uwe na nidhamu ya kazi (Self-Discipline) mara kumi (10) zaidi ya ulivyoajiriwa ndio utafanikiwa

Vijana Msijidanganye: Ukiamua kujiajiri ni lazima uwe na nidhamu ya kazi (Self-Discipline) mara kumi (10) zaidi ya ulivyoajiriwa ndio utafanikiwa

Naona waajiriwa mnatiana moyo huku mkijua maisha yenu ni magumu na mshahara hautoshi, discipline ni kila mahali na siyo kwenye kujiajiri tu. Nyie endeleeni kutoa Muda wenu kwa boss na kumtajirisha huku yeye akiwapangia hela za kuwapa ili mkidhi mahitaji yenu ya kula na kuvaa. 😂😂😂
Stress ziko kila kona na siyo kwenye biashara tu, hivyo iyo "displini" siyo kwenye kujiajiri tu. Biashara mjini ndo zina mapato, mishahara imejaa makato.

Hamjiulizi kwanini 75% ya waliojariwa wana maisha magumu zaidi kuliko waliojiariji?

Biashara yeyote mwanzo lazima iwe ngumu na nguvu nyingi huitajika ili kuipush..ila ikisimama utaona matunda yake, ila ajira kwanzia unaajiriwa hadi unakuja kuacha mwanzo mwisho ni mateso tu hasa ya kifikra na kiuchumi. Siku zote mshahara huwa hautoshi na huo ndo ukweli.

Ajira haitakupa utajiri wowote ule na ndio maana tunaona wazee wengi wakistaafu wanakufa na presha maana hakuna chochote wanachomiliki kwa kuwa waliuza Muda wao mwingi kwa boss huku wakilipwa percent ndogo ya Muda wanaotoa.
Hapa suala ni desiplini na ina apply kote kote kwenye ajira na kujiajiri. Lakini desiplini ya kuajiriwa haitokupa chochote zaidi ya sifa tu kama vile mfanyakazi bora, boss atakupamba na kamshahara kazuri ili aendelee kutumia Muda wako.
Kuna mbinu moja sisi maintaprinyua huwa tunatumia inaitwa "teka moyo wake mwachie akili yake" hahaha hapo mtajiongeza wenyewe, kujiajiri kuna ongeza akili zaidi kuliko izo ajira huwa zinadumaza akili kabisa.

Twende mbele turudi nyuma .."hakuna mtumwa m'baya kama kujiona uko huru"
 
Ukifika stage ya kuajiri watu unaweza relax kwanini mkuu? Huu ndio mwanzo wa kupigwa changa la macho alafu baadaye mtu anaanza kulalamika humu JF.
Mkuu inaonekana kabisa hujawahi kufanya biashara yeyote ile na tangu umemaliza chuo wewe ni mtu wa kuajiriwa tu. Kuna kitu kinaitwa system na ndio maana pesa inaweza kufanya kazi kwa ajili yako wewe ukiwa umerelax tu. Tatizo wafanyakazi wengi kama wewe mnafanya kazi kwa ajili ya pesa. Waliojiari kama sisi tunajenga 'mfumo' ambapo pesa inakufanyia kazi, unaweza wewe usiwepo na pesa inaingia kama kawaida.

Shtuka bro, 11 years umemaliza chuo na bado umeajiriwa. Bado una nafasi ya kufikiri upya
 
Mkuu inaonekana kabisa hujawahi kufanya biashara yeyote ile na tangu umemaliza chuo wewe ni mtu wa kuajiriwa tu. Kuna kitu kinaitwa system na ndio maana pesa inaweza kufanya kazi kwa ajili yako wewe ukiwa umerelax tu. Tatizo wafanyakazi wengi kama wewe mnafanya kazi kwa ajili ya pesa. Waliojiari kama sisi tunajenga 'mfumo' ambapo pesa inakufanyia kazi, unaweza wewe usiwepo na pesa inaingia kama kawaida.

Shtuka bro, 11 years umemaliza chuo na bado umeajiriwa. Bado una nafasi ya kufikiri upya
Dogo comments zako kadhaa hapo juu nimezikubali. Uko vizuri tatizo lako ni kushabikia lile timu bovu tu!
 
Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa jamiiforums.

Ndugu zangu vijana msijidanganye;

Ukiamua kujiajiri ni lazima uwe na nidhamu ya kazi (Self-Discipline) mara kumi (10) zaidi ya ulivyoajiriwa ndio utafanikiwa.

Nimeamua kutoa ushauri huu kwa maana kwamba, juzi nilikuwa nimepanda daladala ya kutoka Mnazi Mmoja huku Dar nikawa ninaelekea Kigogo kwenda kumsalimia rafiki yangu mmoja hivi, classmate wa Secondary School, aliyefiwa na baba yake weeks chache zilizopita.

Sasa mimi nilikuwa nimekaa siti ile ya nyuma kabisa maeneo ya dirishani kwa maana ndio pande zangu hizo ninazopendaga mimi, then kiti kinachofuata mbele yangu walikuwa wamekaa wasichana/wadada wawili ambao wanaonekana ni University graduates wa miaka ya hivi karibuni (mimi ni University Graduate wa miaka 11 iliyopita) alafu walikuwa wametoka kazini ila kuna changamoto moja ilikuwa imewakera wakawa wanapiga story kwa sauti kidogo bila kujua kama mimi ninawasikia.

Wale akina dada wakawa wanaambizana kuwa ni bora wajiajiri tu kwa maana kuajiriwa ni utumwa. Ukijiajiri unakuwa na nafasi kubwa sana ya kujitawala na unakuwa free sana kujipangia mambo yako uingie kazini saa ngapi na utoke muda gani tofauti na kuajiriwa katika ofisi za watu wengine ambao wanakupangia kila kitu cha kufanya.

Mimi ninaomba kuchukua wasaa huu kutuma salamu zangu za pole sana kwa vijana wenye akili kama za hawa akina dada wanaofikiri kwamba kujiajiri sio utumwa.

Ndugu zangu kujiajiri ni utumwa na kama unataka kuacha kazi ya kuajiriwa na kutaka kujiajiri kwa kudhani kwamba ukifungua biashara yako hautakiwi kuwa na nidhamu ya kazi, basi ni bora hiyo pesa uende uka-bet kwa mhindi labda zali linaweza kuwa lako ukafanikiwa lakini usifungue biashara yako.

Nidhamu ya kazi kwa aliyeajiriwa ni ile ile kwa hata wewe unayetaka kujiajiri. Usifikiri eti kwa kuwa wewe ndio boss basi ukitaka kuingia kazini hata saa 5 asubuhi basi sawa tu kwa kuwa biashara yako. Hapana ndugu yangu. Unapojiajiri wewe ndiye unayepaswa kuonesha nidhamu ya hali ya juu sana kazini ili uwe mfano wa kuigwa kwa wafanya kazi wako.

Wewe kama top boss ndiye unayepaswa kuwa panctual, yaaani kama reporting time ni saa 2 asubuhi, basi wewe ikifika tu saa 1:30, upo kazini. Kama hairuhusiwi kutupa takataka hata karatasi sakafuni boss ndiye anayepaswa kuwa wa kwanza kuonesha hilo na sio vinginevyo

Kijana kama unataka kuacha kuajiriwa na kuanza biashara yako kwa kufikiri eti ukiwa na chako ndio unapaswa kukosa nidhamu ya kazi, you are wrong na tafuta mambo mengine ya kufanya. Nakushauri nenda hata uka-bet. Yangu mimi ni hayo tu.

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Magufuli hawezi kuuza Nchi ni Mzalendo haswa Usimfananishe na wale waliotumwa na Wazungu.
 
Dogo comments zako kadhaa hapo juu nimezikubali. Uko vizuri tatizo lako ni kushabikia lile timu bovu tu!
Hahaha hapo kwenye timu tutatofautiana sana. Kumbuka Chelsea ni timu ya baba, timu ya mama, timu ya babu na bibi pia ..kwanini mimi niwe tofauti nao? Hahaha unataka nipate laana mkuu..

Anyway shukrani mkuu.
 
Dogo comments zako kadhaa hapo juu nimezikubali. Uko vizuri tatizo lako ni kushabikia lile timu bovu tu!
Hahaha hapo kwenye timu tutatofautiana sana. Kumbuka Chelsea ni timu ya baba, timu ya mama, timu ya babu na bibi pia ..kwanini mimi niwe tofauti nao? Hahaha unataka nipate laana mkuu..

Anyway shukrani mkuu.
 
Naona huu mjadala watu wanaufanya kishabiki, imekuwa ligi Kati ya walioajiriwa vs waliojiajiri
Mtoa mada alikuwa na lengo zuri tu Wala sio kuwakatisha tamaa watu kujiajiri, Ni kuwa kujiajiri hasa pale mwanzo sio kitu rahisi Kama unataka kukua kimaisha kweli

Faida kubwa ya kujiajiri kunakupa nafasi ya kujikuza we mwenyewe kadri uwezavyo badala ya kumtegemea bosi afurahishwe na wewe akupandishe cheo na kujipangia ratiba zako mwenyewe

Lakini hili linakuja na price yake pia, hasa pale mwanzo unatakiwa uwe na nidhamu kubwa ili kukuza huo mradi wako na kujijengea reputation nzuri kwa wateja wako (brand)

Kuajiriwa pia sio vibaya unaweza kupata kazi nzuri inayolipa vizuri na ukawa unakua kikazi na kipato pia, lakini hata hili linahitaji nidhamu pia
Lakini kwa sababu kuajiriwa kunakuwa na misingi tayari iliyowekwa na mwenye hiyo taasisi, aliyeajiriwa hana kazi kubwa sana, yeye ni kuendeleza tu pale palipofikiwa na hiyo taasisi iliyomuajiri
Tofauti na anayeanza from scratch kujiajiri mwenyewe
 
Back
Top Bottom