Vijana ni wakati wa kupiga pesa kwenye biashara ya mpunga

Vijana ni wakati wa kupiga pesa kwenye biashara ya mpunga

Molembe

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2012
Posts
9,917
Reaction score
11,801
Wakati huu maeneo mengi yanavuna mpunga, na tayari mchele mpya umeisha anza kuuzwa, kwa yule kijana mwenye uchu na mafanikio ni wakati wa kutengeneza pesa tena kwa mtaji kidogo.

Biashara ya mchele ni biashara ya nzuri na hasara zake ni ndogo kutokana na ukweli kwamba huvunwa nchini kwa muda mmoja, yaani kule Morogoro, mbeya na huku kanda ya Ziwa wote huvuna kwa wakati mmoja, sio kama Mahindi ambayo huvunwa mida tofauti na hivyo kufanya soko lisieleweke mfano huku kanda ya Ziwa wanaweza ukanunua mzigo baadae wanavuna Mbeya na kuharibu soko maana bei hushuka.

Ili ufanye biashara ya mpunga wakati inakubidi kwanza ujue aina za mpunga na ubora wake, baada ya hapo tafuta eneo ambalo lina Mavuno mengi na muingiliano mzuri yaani wafanyabiashara hufika kuchukua mzigo, tafuta mtu wa kuuzia mzigo yaani pindi utakapo koboa mpunga wako na kupata mchele uwe na mtu ambae utamuuzia huo mchele, hapa kuna wale wenye mastore.

Baada ya anza kuzunguka kwenye minada (kwa huku kanda ya ziwa) unanunua mpunga unakoboa unaenda kuuza mchele kwa wenye store.

Kama uko serious na kazi kwa ndani ya msimu utakuwa umetengeneza faida mathalani kwa kila gunia la mpunga uwe unapata faida ya shilingi 5,000/= na kwa siku uuze hata gunia 5 za mchele sawa gunia 10 mpunga maanake utakuwa unatengeneza faida ya shilingi 30,000/=~50,000/=.

Jambo la msingi ni kujitoa na kujua thamani ya muda wako, jua mbegu nzuri na jenga uaminifu kwa watu, kwa mtaji mdogo wa 1,000,000/=utakupa faida kubwa.

1621682894758.png
 
Habari yako ni nzuri sana,sema matapeli wameharibu sana masoko na biashara ya mazao,unashangaa mtu anakupigia eti anauza mahindi ukimuuliza maswali mawili matatu ya ufahamu anazima simu.

Sasa na wewe weka namba zako za mawasiliano kama upo serious uwasaidie vijana maana inaonekana una ufahamu juu ya hizi biashara.
 
Nimefanya biashara ya mpunga kwa miaka mitatu sasa, Hasara zipo usiseme hasara ni kidogo usidanganye watu kama kusingekuwa na hasara basi wafanyabiashara wote wangenunua mpunga na kuuza Mchele, umesema uuze Gunia 5 kila siku kivipi???

Mpunga unalimwa vijijini interior huko vijini mbali sana naxsehemu za mashine kubwa na wateja, kwa hiyo. 1M kwa bei ya Elf50 mfano, utanunua gunia 20 hizo gunia waweza zikusanya kwa siku 2,3 au hata 4, una gunia 20 hakuna Fuso itakayokufuata kijijini kukupeleka mjini gunia 20 itakubidi ukae huko pori usubiri wenye mitaji mikubwa wapate mzigo ili na wewe wakubebee hizo gunia zako 20 hapo utakaa tena siku zisizopungua 2, ni siku 5 au 6 tayari unafika town kwenye machine hujaanika huo mpunga wako siku 1 au ili ufae kukobolewa then upange foleni ya kukoboa, upige test utafute mteja ndo ukoboe, hivyo kwa trip 1 lazima utumie Siku 10,

Hivyo kwa mwezi mzima utaenda pori Mara 2 pekee, unakuja kupiga hesabu kila gunia moja ukitoa gharama zote unapata elf 10 au wakati mwingine ukutane na biliani unapata faida ya Elf5, hivyo kwa gunia zako 20 unapata faida ya 150,000 ukienda Mara 2 ndo utaipata Laki 3, kwa mwezi mmoja, hivyo Hii biashara siyo nyepesi na uwe mwanamme kweli siyo mla chipsi, maana unaenda pori week 2 unalala kwenye carpet lile lile mnaloanikia mpunga mchana, kulalia mifuko ya kupimia mpunga na chakula cha kijijini viazi na mihogo uwe umejiandaa kisaikolojia, maana kupata ukurutu ni kitu cha kawaida tu,, Biashara inalipa lakini Mara nyingi kwa wenye mitaji mikubwa, yule anayejaza fuso pekee ake gunia 100 ndo anapata faida maana akijaza mzigo siku hiyo hiyo anapiga simu na kutoka pori wewe wa gunia 10,20,30 unabaki huko.
 
Kabla ya kuingia huko,.nadhani vijana wanahitaji "upepumbuzi yakinifu" juu ya hiki ulichokisema.
Haswaa! Tena kwa mvua za mwaka huu bila shaka mavuno ya mpunga yatakuwa mengi kiasi kwamba ukiingia kichwa kichwa kwenye hii biashara unaweza kujikuta unauza mchele kwa bei ya hasara sana.
 
Haswaa! Tena kwa mvua za mwaka huu bila shaka mavuno ya mpunga yatakuwa mengi kiasi kwamba ukiingia kichwa kichwa kwenye hii biashara unaweza kujikuta unauza mchele kwa bei ya hasara sana.
Yes yes dear,.kuna hii kitu pia "over production" lazima tuangalie nn tunataka kukifanya kwa wakati gani na mazingira yapi..kuingia kichwa kichwa bila kufanya chunguzi za awali na ukajiridhisha ni hatarii..
 
Yes yes dear,.kuna hii kitu pia "over production" lazima tuangalie nn tunataka kukifanya kwa wakati gani na mazingira yapi..kuingia kichwa kichwa bila kufanya chunguzi za awali na ukajiridhisha ni hatarii..
Labda kwa mwenye mtaji wa kutosha kusafirisha nje ya nchi huyo atakuwa na uhakika japo hiyo nayo inahitaji kibali cha serikali
 
Jamani msikurupuke kama nguruwe pori aliyekurupushwa kwenye shamba la muhogo fanya walau abc zifuatazo.

Kwanza fanya market research Je kule unapotaka kupeleka huo mpunga/mchele kuna mahitaji makubwa? tani ngapi? je uhitaji huo unasababishwa ni nini? Je waliokua wanapeleka wameishia wapi? Je bei ikoje? aina gani inapendwa?

Pili fanya utafiti kuhusu wapi unaptikana huo mpunga? kwa bei gani? je aina hiyo ndio inapendwa sokoni? je gharama za kununua maka kufika sokkoni ni kiasi gani? what will be your competitive advantage?

Tatu: ikitokea vinginevyo (worse case scenario) unaweza kuhifadhi usubirie soko likae vizuri ama una njia zingine za kurudisha gharama zako?

Mwisho wajue vizuri washindani wako kina nani, wana nguvu kiasi gani, wanawezaje kuwa tishio kwako.

Ukishajipima huko kote nenda kafanye biashara ukiwa unafahamu mazingira yanayokuzunguka
 
Nimefanya biashara ya mpunga kwa miaka mitatu sasa, Hasara zipo usiseme hasara ni kidogo usidanganye watu kama kusingekuwa na hasara basi wafanyabiashara wote wangenunua mpunga na kuuza Mchele, umesema uuze Gunia 5 kila siku kivipi??? Mpunga unalimwa vijijini interior huko vijini mbali sana naxsehemu za mashine kubwa na wateja, kwa hiyo. 1M kwa bei ya Elf50 mfano, utanunua gunia 20 hizo gunia waweza zikusanya kwa siku 2,3 au hata 4, una gunia 20 hakuna Fuso itakayokufuata kijijini kukupeleka mjini gunia 20 itakubidi ukae huko pori usubiri wenye mitaji mikubwa wapate mzigo ili na .....
Kama umefanya miaka 3 na hujaacha basi hiyo biashara inalipa, nije kwenye mchanganuo wako kwamba upate faida ya 150, 000/=kila trip ndani ya siku kumi, hivyo basi kwa mwezi utaenda trip 3 mpaka 5 kutegemea na ushapu wako. Kwa mtaji wa million 1 kupata faida ya laki 3 kwa mwezi sio haba.
Vijana twendeni pori.
 
Kiongozi me nakaswali kamoja tu. Vipi kama ukinunua huo mpunga na ukaamua kuuweka je unaweza ukaharibika kama mahindi yanavyoharibika kwa kubunguli!
 
Kama umefanya miaka 3 na hujaacha basi hiyo biashara inalipa, nije kwenye mchanganuo wako kwamba upate faida ya 150, 000/=kila trip ndani ya siku kumi, hivyo basi kwa mwezi utaenda trip 3 mpaka 5 kutegemea na ushapu wako. Kwa mtaji wa million 1 kupata faida ya laki 3 kwa mwezi sio haba.
Vijana twendeni pori.
Rudia nilichoandika sijasema hakuna faida nimesema siyo Rahisi kama ulivyoandika wewe, yaani kama kuweka 1m kwa msimu utapata 10M, hicho kitu hakipo waeleze hatua kwa hatua faida zinapatikanaje na changamoto zake zikoje MTU asije soma bandiko lako na kwenda kuchukua mkopo aje kwenye hii biashara, pointi yangu angalau ukitaka kupata faida Uwe na 5M ndo utaiona faida, pili usiniongelee mimi nimefanya biashara miaka3 hivyo kuna faida,

Hujui kwamba bado nafanya hiyo Biashara au Hapana, pili hujui Mimi Nilikuwa na mtaji kiasi gani, pili hujui Mimi nilikuwa nanunua na kukoboa na kuuza kila trip na kurudi pori au nilikuwa nanunua gunia 200 naweka store nakuja kukoboa Mara 1 kwa msimu, hivyo Achana na kuni judge mimi, nimetoa ushauri kwa uzoefu wangu Ili MTU Aingie kwenye biashara Akitegemea na Hasara pia, msiwaaminishe tu watu raha na faida tu, changamoto pia waambieni.
 
Rudia nilichoandika sijasema hakuna faida nimesema siyo Rahisi kama ulivyoandika wewe, yaani kama kuweka 1m kwa msimu utapata 10M, hicho kitu hakipo waeleze hatua kwa hatua faida zinapatikanaje na changamoto zake zikoje MTU asije soma bandiko lako na kwenda kuchukua mkopo aje kwenye hii biashara, pointi yangu angalau ukitaka kupata faida Uwe na 5M ndo utaiona faida, pili usiniongelee mimi nimefanya biashara miaka3 hivyo kuna faida, hujui kwamba bado nafanya hiyo Biashara au Hapana, pili hujui Mimi Nilikuwa na mtaji kiasi gani, pili hujui Mimi nilikuwa nanunua na kukoboa na kuuza kila trip na kurudi pori au nilikuwa nanunua gunia 200 naweka store nakuja kukoboa Mara 1 kwa msimu, hivyo Achana na kuni judge mimi, nimetoa ushauri kwa uzoefu wangu Ili MTU Aingie kwenye biashara Akitegemea na Hasara pia, msiwaaminishe tu watu raha na faida tu, changamoto pia waambieni.
Mkuu kwa uzoefu wako wa hii biashara kati ya kununua mpunga mashambani na kuja kuuza machineni baada ya kuukoboa na kununua machine kuja kuwauzia akina mangi madukani ipi risk yake ina afadhali
 
Back
Top Bottom