Vijana ni wakati wa kupiga pesa kwenye biashara ya mpunga

Vijana ni wakati wa kupiga pesa kwenye biashara ya mpunga

Very true, mie nimeifanya kwa msimu mmoja na changamoto ndo kama alivyosema Swahiba. Yabidi mtu ujipange haswa na uwe na mtaji wa kutosha ili uweze ona faida yake
Mkuu naomba nikuulize
Mimi nataka niifanye hii biashara kati ya kununua mchele uliokobilewa na kununua mpunga alafu niukoboe mwenyewe ni kipi kina afadhali kwa sisi wenye mitaji ya m1
 
Mkuu naomba nikuulize
Mimi nataka niifanye hii biashara kati ya kununua mchele uliokobilewa na kununua mpunga alafu niukoboe mwenyewe ni kipi kina afadhali kwa sisi wenye mitaji ya m1

..Kwa uzoefu mdogo nilionao mpaka sasa na kwa capital hiyo, nadhan ununue mchele kwenye machine kwa sababu kwa mchele angalau unaweza kuona ubora wake (rangi, unyoofu-kwa maana utaona haujakatikakatika). Lakini kununua mpunga ambao utakuletea mchele bora inahitaji uzoefu na utaalam sana. Pia ubora wa mchele hutegemea pia matunzo wakati mpunga tangu ukiwa shambani, muda uliovunwa na hata storage baada ya kuvunwa
 
..Kwa uzoefu mdogo nilionao mpaka sasa na kwa capital hiyo, nadhan ununue mchele kwenye machine kwa sababu kwa mchele angalau unaweza kuona ubora wake (rangi, unyoofu-kwa maana utaona haujakatikakatika). Lakini kununua mpunga ambao utakuletea mchele bora inahitaji uzoefu na utaalam sana. Pia ubora wa mchele hutegemea pia matunzo wakati mpunga tangu ukiwa shambani, muda uliovunwa na hata storage baada ya kuvunwa


Kwa hiyo millioni1 mchanganuo wa faida unakuwaje nduu
 
E
Jamani msikurupuke kama nguruwe pori aliyekurupushwa kwenye shamba la muhogo fanya walau abc zifuatazo.

Kwanza fanya market research Je kule unapotaka kupeleka huo mpunga/mchele kuna mahitaji makubwa? tani ngapi? je uhitaji huo unasababishwa ni nini? Je waliokua wanapeleka wameishia wapi? Je bei ikoje? aina gani inapendwa?

Pili fanya utafiti kuhusu wapi unaptikana huo mpunga? kwa bei gani? je aina hiyo ndio inapendwa sokoni? je gharama za kununua maka kufika sokkoni ni kiasi gani? what will be your competitive advantage?

Tatu: ikitokea vinginevyo (worse case scenario) unaweza kuhifadhi usubirie soko likae vizuri ama una njia zingine za kurudisha gharama zako?

Mwisho wajue vizuri washindani wako kina nani, wana nguvu kiasi gani, wanawezaje kuwa tishio kwako.

Ukishajipima huko kote nenda kafanye biashara ukiwa unafahamu mazingira yanayokuzunguka
True
 
Kwanini ulale kwenye Tutubai wakati unaweza nunua sleeping bag ukaenda nalo?,

kwanini ule mihogo daily,wakati unaweza kwenda na ready to eat meal,ukawa unapasha moto kwenye microwave.......ooh wait...
Broo we acha tu, wa tz noma
 
Kwanini ulale kwenye Tutubai wakati unaweza nunua sleeping bag ukaenda nalo?,

kwanini ule mihogo daily,wakati unaweza kwenda na ready to eat meal,ukawa unapasha moto kwenye microwave.......ooh wait...
we jamaa bhana...hv microwave yaweza kufanya kaz bila umeme?? unajua mzngira wanakolima mpunga ww??
 
..Kwa uzoefu mdogo nilionao mpaka sasa na kwa capital hiyo, nadhan ununue mchele kwenye machine kwa sababu kwa mchele angalau unaweza kuona ubora wake (rangi, unyoofu-kwa maana utaona haujakatikakatika). Lakini kununua mpunga ambao utakuletea mchele bora inahitaji uzoefu na utaalam sana. Pia ubora wa mchele hutegemea pia matunzo wakati mpunga tangu ukiwa shambani, muda uliovunwa na hata storage baada ya kuvunwa
Naelewa sasa
 
Nmefanya biashara hii pia...kilichosemwa hapa ndo uhalisia wenyewe. Hongera mkuu kwa upembuzi yakinifu
Nimefanya biashara ya mpunga kwa miaka mitatu sasa, Hasara zipo usiseme hasara ni kidogo usidanganye watu kama kusingekuwa na hasara basi wafanyabiashara wote wangenunua mpunga na kuuza Mchele, umesema uuze Gunia 5 kila siku kivipi??? Mpunga unalimwa vijijini interior huko vijini mbali sana naxsehemu za mashine kubwa na wateja, kwa hiyo. 1M kwa bei ya Elf50 mfano, utanunua gunia 20 hizo gunia waweza zikusanya kwa siku 2,3 au hata 4, una gunia 20 hakuna Fuso itakayokufuata kijijini kukupeleka mjini gunia 20 itakubidi ukae huko pori usubiri wenye mitaji mikubwa wapate mzigo ili na wewe wakubebee hizo gunia zako 20 hapo utakaa tena siku zisizopungua 2, ni siku 5 au 6 tayari unafika town kwenye machine hujaanika huo mpunga wako siku 1 au ili ufae kukobolewa then upange foleni ya kukoboa, upige test utafute mteja ndo ukoboe, hivyo kwa trip 1 lazima utumie Siku 10, hivyo kwa mwezi mzima utaenda pori Mara 2 pekee, unakuja kupiga hesabu kila gunia moja ukitoa gharama zote unapata elf 10 au wakati mwingine ukutane na biliani unapata faida ya Elf5, hivyo kwa gunia zako 20 unapata faida ya 150,000 ukienda Mara 2 ndo utaipata Laki 3, kwa mwezi mmoja, hivyo Hii biashara siyo nyepesi na uwe mwanamme kweli siyo mla chipsi, maana unaenda pori week 2 unalala kwenye carpet lile lile mnaloanikia mpunga mchana, kulalia mifuko ya kupimia mpunga na chakula cha kijijini viazi na mihogo uwe umejiandaa kisaikolojia, maana kupata ukurutu ni kitu cha kawaida tu,, Biashara inalipa lakini Mara nyingi kwa wenye mitaji mikubwa, yule anayejaza fuso pekee ake gunia 100 ndo anapata faida maana akijaza mzigo siku hiyo hiyo anapiga simu na kutoka pori wewe wa gunia 10,20,30 unabaki huko.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama hautaweza kufikiria jambo kwa miaka 50 ijayo kuna uwezekano mkubwa ukafa maskini, ndo wale wazee walikua kariakoo enzi hizo kimara ni mapori na hawakununua viwanja.
Akili ya kitoto hii.

Nikuulize we una hekari ngapi dodoma mjini na ulinunua kabla ya dodoma haijawa jiji?
 
Hakuna biashara Rahis niongezee tu kitu kwa jamaa aliesema kafanya miaka mitatu alichoongea ni hakika.

Lakin changamoto nyingine ambayo hamjui ni upimaji wa mpunga we toka tu huko dar uje ujipendekeze pori huku ukadhani hakuna wajanja utapigwa unakuja kusituka muda ushaenda. Kupima mpunga kuna utaalamu wake. Kama hujui waweza kuwa hapo unapimiwa unaona unafika kumbe unaliwa. Iyo Mosi

Pili kujua mpunga mzuri na namna ya kuuandaa kama unaweka store ili kiuza msimu usio mzuri. Walau hili waweza lipa vijana wakaanika badae wakawa wanapiga miguu na wakatupia store. Wafanyakazi biashara siku wanakuja kwanza anaekecha mkononi. Anaona inakatika au inasimama. Then mnakoboa sampo

All in all ukifata procedure na wazoefu waaminifu wakakuongoza. Mungu bariki ukaweka store ukakutana na msimu....ha ha ha utafurai mwenyewe.

Kila la heri kama mnataka mali mtazipata Shambani
Wanapimaje boss tuelimishe tusije kupigwa za uso
 
Faida ya laki tatu ,kwa mtaji wa millioni, kwa mwezi si haba! Ni uwiano mzuri.na ndo inatakiwa hivyo kuanza taratibu huku unaisoma biashara vizuri.

Kiukweli hapa watu wanajitahidi kutoa elimu na maarifa ya maana sana kila wakati,mfano huyu jamaa ameelezea nje ndani angalau,hadi faida ikapatikani laki tatu,ila kuna wengi wana mentality ya kuamini kushindwa tu kila jambo,hasa ukishawagusia biashara.

Hawataki kushirikishwa biashara siku hizi,wana msemo wao wanasema ukiitwa au kupewa taarifa fahamu wewe ni fursa,..huu mtazamo ni mbaya sana,tubadilike kifikra.

Tuamini kwenye kutafuta taarifa na maarifa sahihi kwa wakati sahihi ndo yatatusaidia,sio kubaki na uoga tu siku zote,una pesa zako,huna maarifa ya biashara fulani,tafuta wazoefu wa hyo biashara msaidiane nao.,mbona kesi mahakamani watu wanatafuta wanasheria na mawakili ili wawasaidie ili kushinda kesi? Sembuse biashara ambayo ikikubali inakupa manufaa zaidi wewe mwenye mtaji.

Kama tuna update simu,computer,na apps mbalimbali,kwanini wewe usikubali kuji update ubongo na akili yako ili uendane na dunia ya technolojia na taarifa? Kubali kufanya biashara za kushirikisha wajuzi na wazoefu walio kwenye biashara husika,chota maarifa kwa gharama zozote.

Michango mingi sana mizuri inatolewa na wazoefu na wajuzi,binafisi,nimejaribu kuelewesha na kushauri juu ya biashara za nafaka,faida yake na namna zinazoweza kumpa mtu faida,kwenye maada hizi za nafaka,ila hatimaye mtu anakuja kusema ni utapeli tu,hakuna lolote...duh!

Sasa unaona hapo Jamaa kasema faida laki tatu kwa mwezi kwa mtaji wa millioni moja,hapo ni makadirio ya chini,..je ukiwa na 3mill,5mill,nakuendelea...utapata faida ya shilingi ngapi hadi msimu huu wa nafaka uishe...? Chukulie ufanye kwa miezi hata minne.!
#usichukuliepoa mawazo ya watu...hasa yanayoongelea biashara...wewe kama ni muoga wa biashara baki na uoga wako.

"Hatari kubwa kabisa kwenye maisha ni kuacha kufanya chochote" bora ufanye ukishinda itakuwa vizuri zaidi na ukishindwa utakuwa umejifunza njia mojawapo ya kuelekea kushinda...ndiyo naamanisha kushinda.

Maana nyuma ya ushindi kuna kushindwa...kushindwa...kushindwa...kushindwa...kushindwa...zote hizo ni njia za kuelekea ushindi.,bahati nzuri ukiona ushindi wa mtu unafikiri alianza kwa ushindi tu.

Ni hayo tu kwa wale (Big opened mind).

Asante, asante ,asante kwa kunisoma.
 
Hii biashara ya mpunga watu wanapiga pesa kihivi.

Mtu mwenye mtaji mkubwq ananunua mashamba kabla ya kuvuna. Au kuna wale wanakopa wakulima kabla ya kuvuna kwa makubaliano kuwa, atanunua mpunga kwa bei flani. Mara nyingi huwa chini ya bei ya soko. Mfano sasa kanda ya ziwa gunia la mpunga ni 45,000 had 55,000. Ila kuna waliolangua kwa 30,000 had 35000. Hawa wengi huwa ni wamiliki wa magodowns au mashine za kukobolea.

Kuna wanaonunua gunia mpaka zaid ya 10,000 wanatunza kwenye ma Godowns.

Then wanatafta masoko ya kimataifa mfano kenya, sudan, ethiopia na dubai. Wanapeleka mzigo kwa contract. Unakuta gunia moja anauza zaidi ya 100,000tsh. Ofcoz anapeleka mchele na sio mpunga tena 1st grade.

Wengine wanasubiri bei zinapopanda na kuuzia hapa hapa nchini.

Mtu anakopa hata 300million. Anachukua shehena ya mzigo anatunza. Siku akienda kuuza anapata 600million anarudisha almost 400m mkopo then kama 200m ni faida yake. Hii ni faida ndani ya mwaka 1 tu.

Maana yake biashara hii kwa utaratibu huu. Faida inakuwa haipungui 30%.
 
Wanapimaje boss tuelimishe tusije kupigwa za uso

Kwenye kupima mpunga siku zote mnunuzi ndo anapimaga mpunga ..usikubali kupimiwa na mwenye mpunga kamwe!
1.!unakua na ndoo yako...lita 20 zilw za rangi .coral paints .chukua mchanga uweke kwa sufuria uchemke kiasi ..ukishapata moto umwage mle kwenye ndoo then funika .! Ndoo itatanuka😊!..ukiingalia huoni tofauti ila inatanuka ..so ukiweka wewe debe lako moja ndoo inaendelea kudai mpunga...so debe 1 la ndoo y kawaida mle inaingia moja na nusu
Pili kupima mpunga sio unamimina ..usimimine utajipunja!..weka mpunga huku unaitwist ndoo unaizingusha had kitokee kitobo pale kati kadri unavyozidi kuweka endelea kuzungusha ndoo yako mpunga utakuwa unajishindikia .ukifika pale juu mara nyingi huwa no kisado kimoja kinajaza .sasa wataalam wanaweka sado 2! Ukifika pale juu anza kumimina mpunga wako .means unauweka mkononi mwako unaumimina ..pale utaingia mpunga mwingi sana mimina kwa mikono had kiweke kishungi juu..hilo debe ukijalipma kwa ndoo za kwaida ni ndoo 2 kamili...ndo maana unaona mwingine anakuambia kwa kila gunia unapata faida 10000!anakua hajuo kupima! Hizo ni tecnics tu za biashara y mpunga .sema ni wizi kama wizi mwingine!bila hivo mhh
Na
 
Back
Top Bottom