Vijana sahauni kuhusu ajira, wenzenu wanafanikiwa kwenye biashara mbalimbali

Vijana sahauni kuhusu ajira, wenzenu wanafanikiwa kwenye biashara mbalimbali

Championship

JF-Expert Member
Joined
Aug 7, 2019
Posts
5,500
Reaction score
10,616
Nimefurahi sana nilipokutana na jamaa zangu tulimaliza chuo mwaka mmoja na wamefanikiwa kimaisha japo hawakuwahi kuajiriwa

Mmoja aliamua kuwa bodaboda pamoja na digrii yake. Kwasasa amejenga nyumba mbeya mjini. Anazo bajaji kadhaa kaajiri vijana na analo duka kubwa la jumla.

Mwingine yeye alizama sokoni kule mafinga na sasa hivi ana duka kubwa sana la vitenge na anao mjengo wa maana sana pale. Watoto wake anasomesha shule kali za Moshi na Dar es salaam.

Mwingine alianza na duka dogo la mangi ambalo lilifilisika. Akapata mkopo kwa ndugu akawa anauza mayai kwenye kibanda. Alipolipa deni akaanza kiduka cha hardware. Leo hii ni supplier mkubwa wa vifaa vya ujenzi.

Ukisikiliza hustling walizopitia sio kitoto. Wamepambana kiume haswa na sasa hivi wameona nuru. Hawa wote wamefight kwa takribani miaka 15 sasa.
 
Nilichojifunza wote wamerudi kwao wakatumia fursa....Vijana wengi wamebanana hapa Dar hata wawe mawinga hawa progress ya maana ,pesa zinaishia kweny kodi ,usafiri na kula bata.

Kuna jamaa alienda Mpanda kwao maika 3 yupo mbali sana , hapa Dar anakuja chukua mzigo wa spears tu.
 
Nilichojifunza wote wamerudi kwao wakatumia fursa....Vijana wengi wamebanana hapa Dar hata wawe mawinga hawa progress ya maana ,pesa zinaishia kweny kodi ,usafiri na kula bata.

Kuna jamaa alienda Mpanda kwao maika 3 yupo mbali sana , hapa Dar anakuja chukua mzigo wa spears tu.
Uko sahihi sana mkuu. Kijana kujitafuta akiwa dar anahitaji nidhamu ya hali ya juu sana. Inakuwa vigumu kwasababu gharama za maisha zipo juu.
 
Hiyo text imejaa uchungu na jealously.

Hakuna mtu asiyejifunza kutoka kwa waliomtangulia kwa mafanikio.

Matajiri wote duniani, kuna sehemu wamejifunza.
Kila tajiri ana historia yake ya kutajirika ambayo haifanani na mtu yoyote.na kila tajiri ana siri yake ya utajiri ambayo haifanani na mtu yoyote.kwanini sitaki kumuangalia mtu.ni kwa sababu nitajiona NIMECHELEWA.nitajiona nimepoteza,nitajiona sina maana,nitajiona nimefeli n.k.
Yaani nikikuona wewe unaendesha gari wakati mimi natembea kwa miguu lazma nitajihisi kufeli nitakapotaka kujilinganisha na wewe.
 
Kila tajiri ana historia yake ya kutajirika ambayo haifanani na mtu yoyote.na kila tajiri ana siri yake ya utajiri ambayo haifanani na mtu yoyote.kwanini sitaki kumuangalia mtu.ni kwa sababu nitajiona NIMECHELEWA.nitajiona nimepoteza,nitajiona sina maana,nitajiona nimefeli n.k.
Yaani nikikuona wewe unaendesha gari wakati mimi natembea kwa miguu lazma nitajihisi kufeli nitakapotaka kujilinganisha na wewe.
Kumbe hata hujaelewa mtoa mada.

kumbe unataka kujilinganisha?

Usifanye hivyo mkuu, kujifunza si kujilinganisha.
 
Nimemuelewa sana.ila na mimi nimeweka kanuni yangu ya maisha.
Labda nikuulize swali ukienda kwa bakhresa utajifunza nini kutoka kwake?
Mosi, sio rahisi kukutana nae, lakini ninaweza kukutana nae.

Lakini naweza kukutana na bakhresa hata kama ana vitabu alivyoandika kama marehemu mengi mfano.

Pili, nitajufunza atakachosema kwa maneno yake au vitendo.

Kwani hujasoma Rich dad poor dad?

Kwan Robert hakujifunza?
 
Mosi, sio rahisi kukutana nae, lakini ninaweza kukutana nae.

Lakini naweza kukutana na bakhresa hata kama ana vitabu alivyoandika kama marehemu mengi mfano.

Pili, nitajufunza atakachosema kwa maneno yake au vitendo.

Kwani hujasoma Rich dad poor dad?

Kwan Robert hakujifunza?
Yaani hapo unamaanisha utapigq nae stori tu.mbona haujamuomba msingi wa biashara unadhani maneno matupu yatakusaidia kufanikiwa?
 
Back
Top Bottom