Vijana sahauni kuhusu ajira, wenzenu wanafanikiwa kwenye biashara mbalimbali

Vijana sahauni kuhusu ajira, wenzenu wanafanikiwa kwenye biashara mbalimbali

Nimefurahi sana nilipokutana na jamaa zangu tulimaliza chuo mwaka mmoja na wamefanikiwa kimaisha japo hawakuwahi kuajiriwa

Mmoja aliamua kuwa bodaboda pamoja na digrii yake. Kwasasa amejenga nyumba mbeya mjini. Anazo bajaji kadhaa kaajiri vijana na analo duka kubwa la jumla.

Mwingine yeye alizama sokoni kule mafinga na sasa hivi ana duka kubwa sana la vitenge na anao mjengo wa maana sana pale. Watoto wake anasomesha shule kali za Moshi na Dar es salaam.

Mwingine alianza na duka dogo la mangi ambalo lilifilisika. Akapata mkopo kwa ndugu akawa anauza mayai kwenye kibanda. Alipolipa deni akaanza kiduka cha hardware. Leo hii ni supplier mkubwa wa vifaa vya ujenzi.

Ukisikiliza hustling walizopitia sio kitoto. Wamepambana kiume haswa na sasa hivi wameona nuru. Hawa wote wamefight kwa takribani miaka 15 sasa.
Na Wewe???
 
Kwahiyo hao wanne ndo wamefanya umekuja na generalization ya kiboya hivyo
 
Nimefurahi sana nilipokutana na jamaa zangu tulimaliza chuo mwaka mmoja na wamefanikiwa kimaisha japo hawakuwahi kuajiriwa

Mmoja aliamua kuwa bodaboda pamoja na digrii yake. Kwasasa amejenga nyumba mbeya mjini. Anazo bajaji kadhaa kaajiri vijana na analo duka kubwa la jumla.

Mwingine yeye alizama sokoni kule mafinga na sasa hivi ana duka kubwa sana la vitenge na anao mjengo wa maana sana pale. Watoto wake anasomesha shule kali za Moshi na Dar es salaam.

Mwingine alianza na duka dogo la mangi ambalo lilifilisika. Akapata mkopo kwa ndugu akawa anauza mayai kwenye kibanda. Alipolipa deni akaanza kiduka cha hardware. Leo hii ni supplier mkubwa wa vifaa vya ujenzi.

Ukisikiliza hustling walizopitia sio kitoto. Wamepambana kiume haswa na sasa hivi wameona nuru. Hawa wote wamefight kwa takribani miaka 15 sasa.
Upo sahihi lakini nikuhakikishie kuwa haya mambo yanahitaji kutafakari kwa kutumia upeo mkubwa wa akili na siyo kama tunavyofanya. Ni hivi: serikali yetu imeshafeli na nchi sasa hivi ipo inajiendea kama gari lisilo na breki. Nikuulize: hivi vijana wote wasio na ajira wakinunua bodaboda na au wakifungua maduka ni nani atamhudumia mwingine? NI nani atakuwa mteja na nani atakuwa mtua huduma?
 
Nilichojifunza wote wamerudi kwao wakatumia fursa....Vijana wengi wamebanana hapa Dar hata wawe mawinga hawa progress ya maana ,pesa zinaishia kweny kodi ,usafiri na kula bata.

Kuna jamaa alienda Mpanda kwao maika 3 yupo mbali sana , hapa Dar anakuja chukua mzigo wa spears tu.
Hivi hili neno winga ndio dalali.?.Maana kuja nako mjini uzeeni ni kazi😂😂
 
Muwe mnatoa na mifano ya waliofeli pia maana hao ndio wengi, wote tunajua hali ya kujiajiri kwa hapa bongo haina tofauti sana na hali ya kuajiriwa, hii mifano mnayoitoa ya wachache waliofanikiwa haisaidii wala haielezei hali halisi

Hayo ya kusema ukifanya biashara ndio una uhakika wa kuwa millionaire kuliko ukiajiriwa ni huko mbele siyo bongo, huku kuna wafanyabiashara kibao hawatajiriki hadi wanazeeka na kufa, ilihali kuna waajiriwa wanakuwa mamillionaire kupitia ajira zao na usitake kujua wametajirikaje

Hata kwenye ajira nako watakupa mifano ya waliofanikiwa kupitia kuajiriwa kwao
 
Braeburn, IST, Feza, DIA, FK nk
Nilikuwa nakusubiri hapo tu. Mkuu vijana uliowataja kwenye uzi wako hawana uwezo wa kusomesha hizo shule kidooogo labda feza. Nje ya hapo labda green acres,mbezi beach,st.marry's ambapo kwa sasa hizo shule ni bora za serikali au shule yangu pendwa tegeta zamani kwa sasa ni mzumbe university
 
Back
Top Bottom