Vijana tunapitia wakati mgumu sana kwenye utafutaji. Chukua hii, itakufikirisha zaidi

Kwa sangoma ni big NO kurudi, ni bora nikapambana na mishe zangu tu zinazoniingizia pesa nzuri tu ya kujimwambafai hapa mjini...
Usisahau umeshasajiriwa kule kwa Sangoma kwa hio wewe ni mwanachama hai wa wachawi maana data zako zote wanazo ulishaziacha kule namaanisha kule Gizani bado wanakutambua wewe ni mchawi mwenzao hata km umesitisha kuzitumia dawa zao

Ni km unavyojiunga na Mfuko wa Bima za Afya ukishatibiwa hospital data zako zote zinabaki kwenye database ya Mfuko wa Bima za Afya
 
Aisee umeamua kunipa ukweli mchungu ujue?!
 
Uko sahihi asilazimishe biashara ya mabegi tu kila siku,sio kila siku watu wanatumia mabegi na hata mtu akinunua begi hadi lipasuke itachukua miaka miwili.
Angejaribu na biashara ya chakula au vinywaji ambavyo kila binadamu ananunua na anatumia kila siku kisha alete mrejesho tena
 
Soma hadithi yote kisha ujibu upya, hakuna sehemu yoyote nilipoandika nimeng'ang'ana na hiyo biashara
 
Kama ni mkristo nunua ubani ule wa kanisani sio ule wa kuitia maruhani kwa waganga wa kienyeji ni ule ambao mapadri wa kikatoliki uchoma altareni wakati wa misa takatifu ni tabu kidogo kuupata kisha tafuta siku tulivu isiyo na vurugu hasa usiku ni vizuri zaidi uwe msafi kimwili uchome huku ukimuita Mungu, mwambie Mungu mikwamo yako na changamoto zako, Mungu ndiye muumba wa kila kitu duniani anatujua tungali tumboni mwa mama zetu anajua kila pito lako atakuwekea njia pasipo na njia kwasababu njia za Mungu hazichunguziki.

Nakupa mfano: rafiki yangu alipoteza mke na mtoto wakati wa kujifungua muhimbili baada ya maziko mke alimtokea sana mumewe kwenye ndoto za kila wakati akimuita mumewe amfuate alipo, alizunguka kwa waganga kupata dawa lakini wapi siku moja wazo likanijia nikamwambia tafuta ubani wa kanisani choma kisha lalamika kwa Mungu, mwambie tisho lako Mungu ndiye kila kitu ataleta solution, sasa ni mwaka wa kumi na mbili mke hajamtokea tena ndotoni. God knows everything.
 
Nitafanyia kazi hili suala
 
Biashara ni lazima uwe vizur kiroho ...

Jifunzen Kwa wahindi,waarabu na wakinga..Kila siku kabla hajaanza biashara kuchoma maudi na ubani...msifikiri anaigiza..wanajua wanachofanya.

Na Kwa sisi wakristo tumieni damu ya Yesu but hakikisha una uhusiano mzuri nae...

Biashara sio lelemama biashara sio ya watu laini laini.. ndio maana wengi wanakimbilia kuajiiriwa.

Biashara ni vitaa kama zilivyo vita zengine za Russia na Ukraine
 
Kabla hujaanza Biashara yako,ita viongozi wa Dini waiweke Wakfu kwa Mungu wako,Kisha toa Zaka na Sadaka,Hakuna Mchawi wala Shetani atakaye gusa hiyo Biashara mana umeikabidhi kwa Mungu.
 
Kabla hujaanza Biashara yako,ita viongozi wa Dini waiweke Wakfu kwa Mungu wako,Kisha toa Zaka na Sadaka,Hakuna Mchawi wala Shetani atakaye gusa hiyo Biashara mana umeikabidhi kwa Mungu.
Mi najuaga wakfu kwenye nyumba na unaandaa chakula vinywaji kidogo, kumbe mpaka biashara.
 
Mkuu kwanini uliachana na uyo mtaalamu kama hana masharti yanayopingana na misimamo yako.
 

Yaani kila msimu abadili biashara .
Sio lazima utoe ushauri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…