Vijana wa siku hizi ni wavivu na wanachagua kazi

Vijana wa siku hizi ni wavivu na wanachagua kazi

The Lastdream

JF-Expert Member
Joined
Jan 23, 2024
Posts
1,970
Reaction score
4,616
Jamani wakuu kama kichwa cha habari kinavyosema. Nimeona ndugu yangu Mlundilwa Jr kaandika uzi wake akisema alimwambia dogo atoe elf20 lakini akagoma akasema bora atafute mwanamke aimalizie huko. Sitaki kujua ni stori ya kweli au ni uongo, lakini uhalisia upo hivyo.

Sasa hivi kwa tunaoishi mitaani tunaelewa. Utakuta kijana shule ilimshinda, wazazi walishaongea mpaka wamechoka. Kazi ni kunyoa na kuweka engo kwenye nywele na kupaka mablaki kama waziri fulani katika nchi fulani.

Unajaribu hata kuonyesha upendo kwa madogo mtaani njoo golini nikufindishe jinsi ya kukata viazi vya chipsi anakuja siku ya kwanza ya pili wiki mara humuoni!

Unabaki unashangaa tu anarudi kushinda kwenye saluni kujipaka poda na jioni kwenye madubu baadae anamalizia Kvant huku anacheza mziki wa singeli. Huyo kijana miaka 27 anakimbilia 30 jitu kubwa halijielewi.

Bado kuna tatizo kubwa sana katika jamii yetu. Haswa kwa vijana wakiume ambao sisi ndio mababa wakesho.

Kuna dogo wazazi waliongea mpaka wamechoka peleka shule wapi. Kaishia kuvuta madawa baba kachoka kaenda kumpumzisha jela. Mama yake alipoenda kumuona tumbo la uchungu likamshika mtoto kakonda vbaya sababu amekosa vile vitu wapo mahakamani wanataka kukata rufaa wamtoe.

Vijana tusichague kazi, tuchape kazi. Haya tujiandae kwenda kwenye kuomba maombi ya semina kwa ajili ya uchaguzi mwakani elfu 50 sio ndogo.

Usiku mwema.
 
Ahsante mkuu ingawa moderator wameufuta yaani wao kilichowauma kuona napromote Rushwa ila ile kauli ya yule dogo waliona iko sawa...
hawana lolote kwani si tunasema mambo ambayo yapo mtaani na uhalisia, huyo dogo mkuu muache apigike akose hata mafuta ya kupaka atakuja kukutafuta. Vijana wengi wanaharibika sababu ya kutaka maisha ya wepesi na kupata haraka. N kujtuma hawataki
 
Ahsante mkuu ingawa moderator wameufuta yaani wao kilichowauma kuona napromote Rushwa ila ile kauli ya yule dogo waliona iko sawa...
Mkuu uliandika kibabe sana ule Uzi wako yaan bila kupepesa macho Wala kumumunyaa maneno 😅😅😅
Na wadau walivyooanza comment zao nikajua hapa Uzi wako haudumu unafutwa. Polee afisa
 
Hasa vijana wa Dar hovyo sana..
Wenye wewe wanajiita watoto wa town ila kichwani hamna kitu..

Kutwa kushinda saloon na library.
Utakuta wamevaa vi sendroz vyao na soksi hapo wanaona washayapatia maisha.

Sisi wa kuja tikifika mjini tuna wapiga gape kubwa sana.. wanaanza kuleta shobo za kingese..

Mdogo angu alianza nae kuleta habari kama hizo ubishoo mwingi...

Chapa sana now amejilekebisha
 
Kaka umeandika uzi mzuri sana, Hongera kwa hilo. Lakini ukweli ni kwamba vijana wa namna hiyo ni wachache sana huku JF. Ni kweli JF kuna wapumbavu wengi sana kama wakina Genta lakini hawafikii kiwango cha vijana hao. Natamani kungekuwa na namna ya kuwafikia na kuwapa hii elimu (kuwachana makavu) labda ingewasaidia.
 
Kaka umeandika uzi mzuri sana, Hongera kwa hilo. Lakini ukweli ni kwamba vijana wa namna hiyo ni wachache sana huku JF. Ni kweli JF kuna wapumbavu wengi sana kama wakina Genta lakini hawafikii kiwango cha vijana hao. Natamani kungekuwa na namna ya kuwafikia na kuwapa hii elimu (kuwachana makavu) labda ingewasaidia.
aiseeee GENTAMYCINE 😂😂
 
Back
Top Bottom