unaweza kujibizana umeandika pointi sana sana kamasi zimejaa kichwani.
Hao wazamani walikuwa wanachagua kazi kwa fact zipi?
Mkuu hata kusoma hujui ? Ulizia watu waliokuzidi kila mtu alikuwa akitoka Shule kuna mkeka wa Kazi..., Kazi kama Ualimu, Unesi, Upolisi, Uanajeshi watu walikuwa hawawezi kwenda (labda kwenye Jeshi wengi walikwenda Wakurya)....; Watu walikuwa wakipangiwa Ualimu sehemu fulani hawaendi...., Kazi kama kuuza Bar n.k. mtu akifanya huko anaonekana amelost...; (Sasa hivi Hospitality na Kazi kama hizo watu wanafanya)
Kusukuma mkokoteni au toroli labda uwe Mkara....; wengine wagogo walikuwa wanaona bora tu wawe ombaomba....; Wengine town walikuwa wanawaza kuwa ma-baharia kwenda kuzamia meli....
Sasa hivi tangaza kazi ya ualimu hata kama ni watu kukaa kwenye kichali cha ndege (hakuna nyumba uone wangapi wata-apply)
Now kama ulikuwa hujui hizo juu nilizoweka ndio facts... To be precise Historical Facts...
Kuwepo kwa vitu hivyo vyote nilivyoisema ni matokeo ya akili za vijana wa sasahivi . Kama utashindwa kulea mtoto wako katika njia sahihi dunia itakusaidia kumelelea. Kuwepo kwa vipombe vya bei rahisi ni namna ambavyo vijana wa sasahiv mentality zao zilivyo.
Kwahio hawa vijana walikuwa wakubwa wakatengeneza viwanda vya pombe au kuachia pombe za nje kuingia kwa bila kuzipiga kodi kubwa hence kuwa bei rahisi alafu wakawa re-incarnated wakawa vijana tena ili waje wanunue hizo pombe ?
Mkuu unaangalia vitu kwa mafungu bila kuona the whole picture..., Unajua kwanini Russia watu ni walevi sana wa Vodka (urahisi wa bei za Vodka na ugumu wa maisha) ni rahisi kwa mtu kupata Vodka kuliko menu ya siku anaona bora tu apige tungi huenda akapata usingizi na kusahau matatizo yake
Kuwepo kwa betting ni sababu ya vijana wa sasahiv hawapendi kazi na ni WAVIVU. Mbona haya mabetting Hayajasambaa kwa kiasi kikubwa nchi za kwanza ?
Unamaashisha nini nchi za Kwanza ? Kama unamaanisha nchi za nje rudia tena kufanya research..., Nenda Ulaya au USA kwenye China Town yoyote uone jinsi wachina wanavyocheza kamari (Chinese are addicted Gamblers) unadhani hizi Ladbrokes, WilliamHill, BetFair n.k. zimetokea wapi au ni za wapi (kama sio hizo so called nchi za kwanza)..., Tena bora huko UK wanapiga marufuku baadhi ya matangazo ya Betting (Huku Serikali imeachia hadi kipindi cha Taarifa ya Habari) sasa hapo makosa ni ya hawa addicted people (na sio vijana tu) au ni makosa ya Serikali ?
Huelewi kwamba betting ni kazi? Kitu kinachoingiza pesa na watu wanewekeza pesa hiyo si kazi? Upo sawa kichwani kweli au unatumia dawa mkuu?😂😂 au kazi ni nini? Ni ku drain energy peke yake bila kuingiza chochote?
Betting ni kazi kwa nani ? Bookmaker (Anayechezesha / Kampuni) au Punter / Anayecheza Bahati Nasibu na uhakika wa kupoteza ni 100% ?
Hivi wewe kama unajipinga mwenyewe mimi ndio taweza kukupinga kweli ? Sio wewe uliyesema kwamba vijana wa sasa ni wavivu na wanachagua kazi ? Sasa kama Betting ni Kazi uvivu wao upo wapi ? Si wanafanya kazi ?
Ila betting sio Kazi / Betting ni Kamari na kamari mwisho wake unless unauza tips / vitabu au wewe ndio mchezeshaji mwisho wa siku itakula pesa zako na wewe sio kula (Na hakuna kazi ambayo haina malipo, na in so far as betting is concerned mwisho wa siku utapoteza)
Uwepo wa vitu vyote nilivyotaja ni matokeo ya vijana na wala siyo kuwa indoctrinated kama unavyosema. Hawataki kufanya kazi, wanacheza madubu kwa pesa za kuiba kwao.
Eti zamani walikuwa wanachagua kazi! Walikuwa wanachagua kazi gani?
Betting ambayo umesema ni kazi na sasa unasema kwamba hawataki kufanya kazi ?!!!, Au kila ukiweka nukta unasahau ulichoandika kabla ?
Kama na wewe ni mmoja wao au una kijana wako limekaa tu nyumbani linasubiri kuletewa mwisho wa siku atapakatwa. Atoke afNye kazi.
Sasa umeanza Vioja kama mimi sitaki kufanya kazi na ni mvivu inamaanisha wengine ni wavivu ? Tumeingia kwenye kuongelea mtu na sio issue at hand ?