Vijana wanawezeshwa vipi kujiajiri

Vijana wanawezeshwa vipi kujiajiri

Vitabu vingine vizuri ni E-Myth kinaongelea kuhusu kuanzisha MFUMO WA BIASHARA ambao ndio kiini cha mafanikio kwenye biashara. Kingine ni 21 Secrets of Self Made Millionaires, kuna Richest Man in Babylon, pia kipo The millionaire Next Door, Get Rich Your Own Way n.k

Ukivisoma hivyo huwezi kubaki kama ulivyokuwa mwanzo
 
Uzi mzuri coz hakuna tajiri mwajiriwa Bali kuna tajir anaeajir watu
Ujue tajiri anae ajiri watu wale watu wanamsaidia kutimiza ndoto zake za kuwa tajiri na wale waajiriwa wanakuwa wanapambana na mkate wa kila siku ila uhai wao uwepo

Kinacho takiwa tukiwa kazini tujenge mazingira ya kutengeneza akiba na tujujifunze namna ya kuwekeza katika miraadi midogo kulingana na vipato vyetu

Na tunapaswa kujua miradi tunayoa anzisha inatakaiwa ijiendeshe baada ya muda gani hapa namaanisha kuwa kama ulikuwa unachukua mshahara kuongeza kwenye mradi ili uende basi kuna wakati mradi unatakiwa ujisimamie na uweze kuleta faida kidogo amabayo itakupa mwanga namna ya kutanua mradi wako


Heshimu ndoto zako utafanikiwa
 
Heshima kwenu viongozi

Nimeona ni vyema na sisi wenye lengo la kuacha kazi tukawa na uzi wetu kama wenye agenda nyingine walivyoanzisha uwanja wao.

Lengo la nyuzi hii ni kupeana mawazo, moyo na uzoefu wa mbinu bora tunazotumia katika maandalizi yetu ya kuachana na aina Mpya ya utumwa, yaani KUAJIRIWA.

Lengo lingine la uzi huu ni kuonesha sababu ya uamuzi wa kutaka kuacha kazi ili kila mtu apime kama sababu yake ni sababu tosha ya kufanya hivyo ama la, lakini hii pia inatoa fursa kwa wachangiaji wengine kufanya assessment ya maamuzi hayo.

Kuacha kazi na kujiajiri na pengine baadae kufikia hatua ya kuajiri ni uamuzi wa kuyatoa maisha yako mikononi mwa mtu mwingine (muajiri) na kuyakabidhi mikononi mwako mwenyewe. Ni kujitoa katika kutawaliwa na kuamua kujitawala mwenyewe. Ni vyema pia tukajulishana gharama za maamuzi hayo mazito ya kutoka Misri kuelekea Kanani. NI WAZI HAITAKUWA SAFARI NYEPESI.

Tushauriane time scale, mfano mimi ninakimbizana na miaka Mitatu kabla sijatoka kwenye hii Jela. Baada ya hapo ntarudi uraiani, nyumbani kuishi maisha yangu ya uhuru.

Tunaotaka tutoke hii Jela Tushauriane humu, je tukusanye mtaji sasa bila kufanya ujasiriamali na tutakapoacha tu kazi ndio tuanze rasmi ujasiriamali? Ama tuanze sasa hivi kufanya kazi na ujasiriamali ili tu-taste ladha ya ujasiriamali kabla hatujaacha kazi? (Ila hata mambo yakiwa magumu kwenye ujasiriamali kipindi tupo kazini na tunafanya ujasiriamali, kuendelea na kazi sio option). Kubaki Jela haiwezi kuwa option kisa kuna dona na maharage ya bure, bora kuwa uraiani ule mlo mmoja wa maharage na ugali kwa mwaka mmoja ili uje kula asali na maziwa kwa miaka mingi ijayo.

Kila mtu anaweza kuwa na sababu yake ya kuacha kazi. Wengine watakwambia kazini kipato kidogo, lakini amini nakwambia hata ukiajiri na kutoweka mwili, moyo na roho yako kwenye hiyo kazi, unaweza kupata kipato kidogo kuliko hata kile cha kazini. Katika swala la kipato, tofauti ya kipato cha kuajiriwa na kujiajiri ni kipato kimoja Anapanga mtu akulipe kiasi gani, na Kingine Unapanga wewe uingize kiasi gani.

Wengine watakwambia, wanataka waache kazi sababu ya Mateso kazini,ubabe wa mwajiri, kutojali kwa mwajiri. Yote hayo yanakupa HASIRA, geuza hasira zako kuwa DRIVES, zigeuze kuwa USONGO.

Kwanini nataka niache kazi, nataka kuwa huru, nataka kusafiri huku na kule bila kujali bosi atahesabu siku tatu sipo kazini anifute kazi. Sitaki kumpigia mtu mmoja Magoti (bosi) ili kipato changu kiendelea kutiririka. Bora nipigie magoti watu wengi (wateja) ili kipato kiingie, kwani mteja mmoja akiamua kunifukuza kazi ntakuwa na option kwa mteja mwingine.

Uzi wetu TUNAOPANGA KUACHA KAZI, the clock is clicking....LET'S DO IT, LET'S GO.... Tunapenda pia kuchota busara za wale walioacha kazi na wapo wanaendelea kupambana.
Good idea lakin mziki wake mh
 
Good idea lakin mziki wake mh
Inawezekana, iwapo mtu utajipanga vyema. Hasa hasa baada ya kuhakikisha mzunguko wako wa fedha uko imara kulingana na vitega uchumi ulivyo jiwekea.

Wapo walio acha kazi na kujilaumu kwanini amechelewa kuchukua uamuzi wa kucha kazi ya kuajiriwa mapema.

Mfano hai: Kuna walimu wengi Kiteto wameacha kazi ya ualimu na kujiajiri katika kilimo.

Kikubwa ni kujipanga
 
Good idea lakin mziki wake mh
Mkuu ni kweli mziki wake ni mnene. Imagine sasa hivi ukivyoajiriwa ukichalewa kutofika kazini mwisho wa mwezi mshahara upo pale pale, lakini ukichelewa au kutofika kazini kwenye kazi yako mwenyewe ina maana tayari pato ulilotarajia kulipata limeshapungua.

Cha msingi ukiamua Kujiajiri na baadae kuajiri lazima uwe committed 100%
 
Mkuu ni kweli mziki wake ni mnene. Imagine sasa hivi ukivyoajiriwa ukichalewa kutofika kazini mwisho wa mwezi mshahara upo pale pale, lakini ukichelewa au kutofika kazini kwenye kazi yako mwenyewe ina maana tayari pato ulilotarajia kulipata limeshapungua.

Cha msingi ukiamua Kujiajiri na baadae kuajiri lazima uwe committed 100%
Kweli
 
wazo zuri, sana ...ukisimama mwenyewe private unaweza kujitanua to level ambayo... you can feel as upo angani
 
Miezi miwili ijayo natarajia kuacha kazi.nahitaji kuwa free na kuwa karibu na watoto wangu na mume wangu.huku kuajiriwa naona kama utumwa tu.hakuna muda mzuri napata wa kukaa na familia yangu na kuwatake care kwa ukaribu zaidi kama mama na mke pia.sijali kwamba mambo ya huko kujiajiri yatafail au la nimeamua kutoka na mambo yatakuwa poa tu.naamini hivyo.
 
Kwanini nataka niache kazi, nataka kuwa huru, nataka kusafiri huku na kule bila kujali bosi atahesabu siku tatu sipo kazini anifute kazi.
Unataka kusafiri ''huku na kule'' katika michakato ya kutengenzeza mpunga au kula bata tu? angalia baada ya bata na kumaliza savings zote, usirudi kumpigia goti tena Boss na kumwambia ''ulighafirika'' wakati unaacha kazi kwa mbwembwe. Kuacha kazi na kujiajiri haimaanishi utaacha kuhustle na kula bata full time
 
Unataka kusafiri ''huku na kule'' katika michakato ya kutengenzeza mpunga au kula bata tu? angalia baada ya bata na kumaliza savings zote, usirudi kumpigia goti tena Boss na kumwambia ''ulighafirika'' wakati unaacha kazi kwa mbwembwe. Kuacha kazi na kujiajiri haimaanishi utaacha kuhustle na kula bata full time
Mkuu nakuelewa vizuri. Kusafiri huku na kule bila kujali bosi atanifanya nini ni tafsiri tu ya UHURU ambao ndio ninaoutafuta

Kusafiri huku na kule ni baada ya ku retire early, ni baada ya kutengeneza mpunga wa kutosha (ambao obvious siwezi kutengeneza kwa posho inayotambulika kwa jina la mshahara). Ni baada ya kugundua na MONEY MAKING FOMULA YANGU. Kusafiri huku na kule ni baada ya Kuacha kufanya kazi kutafuta fedha, badala yake fedha kuanza kufanya kazi kwa ajili yangu

Hicho ndicho nilichomaanisha mkuu
 
Back
Top Bottom