BigTall
JF-Expert Member
- Mar 9, 2022
- 525
- 1,257
Huku Zanzibar kumeibuka tabia ya Watu ‘kupigwa’ sana pesa kwa kisingizio cha kutafutiwa safari za kwenda nje ya Nchi.
Wengi ninaowafahamu waliokutwa na changamoto hiyo wameingizwa mjini kwa kuambiwa wanatafutiwa safari ya kwenda Nchini Canada, wanashawishiwa kuwa watakuwa na maisha mazuri, wanatoa fedha ya kutengenezewa 'mchongo', baadaye mambo jiiiiii kimya
Kuna mtu anaitwa Edi Cool sijui jina lake kamili lakini wenyewe wanamuita Balozi wa Vijana anahusishwa sana na huo wizi.
Kibaya zaidi wanaofanyiwa utapeli huo na kuumizwa hawasemi baada ya kuaibika, wanaona haya. Vijana wenzangu tuache tamaa, maisha mazuri unaweza kuyapata hata ukiwa hapa nyumbani, lakini ni vizuri kufuata njia halali kama unataka kwenda nje ya Nchi, hizi mambo ya njia za panya matokeo yake huwa sio mazuri sana.
Pia soma ~ Kuajiriwa Nje ya Nchi: Njia ya Mafanikio au Mwisho wa Ndoto za Ndani?
Wengi ninaowafahamu waliokutwa na changamoto hiyo wameingizwa mjini kwa kuambiwa wanatafutiwa safari ya kwenda Nchini Canada, wanashawishiwa kuwa watakuwa na maisha mazuri, wanatoa fedha ya kutengenezewa 'mchongo', baadaye mambo jiiiiii kimya
Kuna mtu anaitwa Edi Cool sijui jina lake kamili lakini wenyewe wanamuita Balozi wa Vijana anahusishwa sana na huo wizi.
Kibaya zaidi wanaofanyiwa utapeli huo na kuumizwa hawasemi baada ya kuaibika, wanaona haya. Vijana wenzangu tuache tamaa, maisha mazuri unaweza kuyapata hata ukiwa hapa nyumbani, lakini ni vizuri kufuata njia halali kama unataka kwenda nje ya Nchi, hizi mambo ya njia za panya matokeo yake huwa sio mazuri sana.
Pia soma ~ Kuajiriwa Nje ya Nchi: Njia ya Mafanikio au Mwisho wa Ndoto za Ndani?