Inna
JF-Expert Member
- Jan 13, 2017
- 11,193
- 27,078
[emoji23] [emoji23]Nimpate wapi,..!?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
[emoji23] [emoji23]Nimpate wapi,..!?
[emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13]Yuko na mama yake huko anakopiga job (as no uhamisho) ana 2.6 yrs siku mbili mfululizo kagoma kila kitu anataka amwone baba...nikipiga simu analia tu na kusema njoo huku haraka, niletee mkoba na peni!!!!
Mtafute huyo mtoto ndugu yangu..
Hakuna raha kama kucheza na kuwa rafiki wa watoto wako..
Mnawakosea haki sana watoto nyinyi watelekezaji.
[emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13]Ana miezi 5 yeye hata akiwa analia jifanye unaongea na simu ananyamaza kusikiliza maongezi ukiacha tuu anashusha kilio....anapenda sana kusikiliza maongezi ya simu hata kama anasinzia ataamka
[emoji87] [emoji87] [emoji87] [emoji87] [emoji87] [emoji87]Aisee mie sitaki hata kukumbuka,mwanang alikuwa mtundu balaa at least sasa hivi nimepumua,wakati akiwa na miaka mitano akiwa shuleni (boarding) sijui alitoa wapi mfuko ule wa Salfeti akawachukua watoto wadogo watatu akawafungia kwenye mfuko halaf akawaambia atakayepiga kelele namchapa viboko,akatoka akaenda kucheka bahati nzuri mwalimu akapita pale akaona mfuko unacheza cheza akashangaa kuufungua akakuta watoto walishaanza kuchoka, huku na huku nani kafanya hivi wakamtaja,mwalimu wake ananipigia simu mwanao leo kafanya kosa hili yaani nliishiwa pozi, nkaenda shuleni kwao namuuliza akanambia ahaa niliwaweka watulie maana walikuwa wanasumbua,siku nyingine karudi likizo niko kazini , akaweka Cd tano kwenye radio inayobeba cd tatu, nilivyorudi kanipokea getini akanambia yaani Mom radio yako imegoma kabisaa kuimba leo ahaa itakuwa ulinunua radio ya kichina,nafungua pale kaweka cd kushinda uwezo na sijui alichokonoa nn radio ikafa kabisaaaa
[emoji14] [emoji14] [emoji14] [emoji14] [emoji14]Haahaahaa..... Jamani msianze chai sasa..
[emoji23] [emoji23]mpaka kufikia page hii ya tatu, inaonekana watoto wengi wa siku hizi wanapenda sana simu, naendelea kusoma.
Tuliotelekeza mimba haituhusu hii
[emoji14] [emoji14] [emoji14]Mimi mwanangu ana miaka mitatu aliniuliza mbona mama nikimwita Asha (sio jina lake halisi) ananichapa lakini wewe mbona hakuchapi?
[emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13]Wakwangu anamiaka 4 juzi kaniuliza baba nani kamzaa shetani
AhahahahhahahhaJembe langu lina miaka3,akimuona mtu flani akiongea kwenye tv,anakimbilia remote na kubadili chanel.Simply ana aleji naye.
[emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji14]Mwanangu (5): Baba mbona unapunguza mwendo??
Mimi: Kuna askari mbele
Mwanangu: Sasa usipopunguza mwendo atakufanyaje?
Mimi: Atanikamata
Mwanangu: Atakukamata atakufanyaje?
Mimi: Atanifunga kamba anipeleke gerezani kunifunga.
Mwanangu: Police kazi yake kufunga kamba watu?
Mimi: Ndiyo, ila wale wakorofi tu.
Mwanangu: Hata watoto wadogo anawakamata na kuwafunga?
Mimi: Ndiyo, lakini wale watoto wakorofi wasiopenda kufanya H/W
Mwanangu: Mimi si mkorofi na nafanya HW, si ndiyo baba
Mimi: eeeee
(Tunawakaribia Police wa usalama barabarani tunawapita)
Mwanangu: Police nimewaona watatu pia kuna Mwanamke, baba hata Police Mwanamke yupo
Mimi: Ndiyo
Mwanangu: Na yeye anaweza kukamata watu na kuwafunga?
Mimi: Ndiyo:
(Ukimya dakika 2)
Mwanangu: Baba weka speed One hundred tumeshawapita ma police. (huku akiangalia mshale wa speed-meter)
-------------
Mungu akutangulie.Ooh Mwenyezi Mungu Anisaidie Nijifungue Salama Ili Nishuhudie Vituko Vya Mwanangu Na Mie Nipate Cha Kusimulia
[emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13]mie wangu ndiyo ameanza shule, basi nina kibarua cha kuimba nyimbo za shuleni kila akirudi. kupewa story za madam wake sijui anko.
na mbaya zaidi kupigiwa ngoma ili niimbe nyimbo ya Taifa. hapa uwa nachoka sana aiseee.
kingine kila mahali panachorwa sasa hivi, ukuta imebidi tuulinde kuliko kitu kingine.
Wa kwangu ameanza kulipenda ilo tangazo akiwa na miezi mitano hata kama ungekua analia likianza anajipa break ya kulitizama likiisha anaanza upya na program yake ya kulia ila mpaka Leo ana 1.1year still analipendawatoto ni faraja sana wangu ana 1.5 analipenda lile tangazo la cocacola hata akiwa mbali vp akisikia tu anakuja.. Anavoitamka cocacola ss... Ndo kichekesho
Wazazi wakongwe wakoje?
Kuna mtu alizaliwa akiwa na watoto tayari?