Vioja vya watoto wadogo (0-5years), tuambie vioja vya mwanao

Vioja vya watoto wadogo (0-5years), tuambie vioja vya mwanao

Watoto ni karaha, furaha, Amani na faraja kubwa kwetu sie Wazazi wao! Mambo ya Watoto ni mengi mengine hayana haja hata kuandika hapa!
 
Nilipomaliza chuo nilifanya kazi kampuni moja ya binafsi, ilikuwa ya ukandarasi huyo bosi alikuwa na watoto 6, kati ya hao mmoja tu ndio alikuwa wa kiume na wa mwisho mwisho kuzaliwa, akawa anasema natamani ingekuwa na uwezo wa kumvuta mtoto akue haraka ili huyu jembe anisaidie majukumu wakati huo alikuwa class seven, sasa hivi yule kijana kamaliza chuo ana degree baada ya kumaliza form four pale ST.. Costantene Arusha akampeleka chuo Nairobi, ila jamaa amekuwa MZIGO, ZOBA yaani hana afanyalo pale zaidi ya kuendesha magari ya baba, siku moja nikaenda kusalimia maana nilishaondoka kitambo hapo, nikamuuliza vipi sasa amekua kuna msaada unaopta kama ulivotamani kumkuza fasta, aliniangalia kwa huruma sana yaani kama anajuta mtoto kukua, alijua acha tu nibebe msalaba wangu nikifa vikiisha basi sitakuwa na la kulaumiwa, nilimuhurumia.. Alipokuwa mdogo alikuwa anapenda sana kuja ofisini na hukaa na mzee wake kwa umakini kama kuna jambo ana hakikisha haliharibiki.
Malezi duni mkuu, unajua watu wanadhani kumlea mtoto ni kumlisha, kumsomesha na kumvalisha wanasahau kuwasimamia na kuwaongoza watoto kwenye njia sahihi, wanawaacha watoto watazame chochote kwenye TV na kwenda kucheza kwenye mazingira ambayo si rafiki kwa akili ya mtoto na matokeo yake ndio hayo. Kwa mfano mtoto wa huyo mzee aliridhika kwa sababu aliona babake ana maisha mazuri na kitendo cha kukaa naye ofisini kilimjengea mtoto mtazamo wa uhakika wa kula bila jasho ndio maana mzee wake amemuona hayuko kama alivyotegemea.
 
Babyboy wangu wa miezi 6 yani nikimchemki DNA zangu kabisa naziona anavyolala anavyosmile akikasirika
 
Huyu dogo an 3Yrs

#1. Siku moja aliniambia "Baba nataka kuolewa"... Nikamuuliza unataka kuolewa na nani akanijibu " na wewe"..... Nikapigwa na butwaa.


#2. Siku nyingine akaniambia "Baba nina mimba".... Nikajifanya kama sijamsikia.


#3. Siku nyingine akaja na ua anaiambia "Baba ua la bibi harusi".

#4. Siku moja nilienda naye nyumbani akamuuliza baba yangu " Babu wazazi wako wapi?.... Baba akamjibu " wamefariki"... Dogo akasema "unaishi vipi bila ya wazazi".


Hayo ni machache
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Wangu mm ana 4 years yani yeye akiamka asubuhi Tu ni kuwasha laptop na kuanza kuangalia katuni hata Kula anasahau ,simu ya mamake ndo anaimiliki muda wote yy ni kuangalia katuni tu
 
Mdogo wake anaekaribia miaka 3 ni mtundu na mbabe. Yeye anapenda magari na ufundi. Yaani umuoneshe video ya magari kwenye simu imekula kwako huna jinsi ya kujitoa atakavyotupa tantrums.
Usije ukaanza kumlazimisha asome awe daktari au mwanasheria hicho ni kipaji tayari anacho kitamtoa aongezewe tu elimu kiasi sio madegree ili mzazi ujisifie.

Hongera sana Mkuu
 
Wangu 1.5 yrs anapenda kuandika andika kuna sehem yake ukutan ndo hapo hapo kila siku.kinachonishangaza zaid hatakag na hapend tushikiane simu mm na mama yake, nikishika ya mama yake anaichukua na kuitupa ila mama yake akiishika yangu anamnyan'ganya na kuniletea
 
Mtoto wako anatazama movie kama za bongo movie ndio maana amejua kuna kitu kinaitwa mimba na kuolewa au amejifunza kutoka kwa watu. Katika umri huo ni mapema mno kufikiria mambo hayo.


Itakuwa ni hizi Movie za Kibongo.... ila nashukuru sasa kanashinda shule akirudi amechoka sana..
 
Back
Top Bottom