Vioja vya watoto wadogo (0-5years), tuambie vioja vya mwanao

Vioja vya watoto wadogo (0-5years), tuambie vioja vya mwanao

Acha tu jamani hakuna jambo jema kama watoto,hii ni faraja na mapambo ya familia,watoto wamefanya weekend's zangu niwe namalizia home,once nilikua nakwaruzana na wife sana kijana wangu wa 4 years kuna siku aliniuliza why nagombana na mama yake huku akilia na nilijihisi vibaya sana from that day nimebadilika sana hata wife aliniudhi huwa sireact mbele ya watoto.
 
Mwanangu (5): Baba mbona unapunguza mwendo??
Mimi: Kuna askari mbele
Mwanangu: Sasa usipopunguza mwendo atakufanyaje?
Mimi: Atanikamata
Mwanangu: Akikukamata atakufanyaje?
Mimi: Atanifunga kamba anipeleke gerezani kunifunga.
Mwanangu: Police kazi yake kufunga kamba watu?
Mimi: Ndiyo, ila wale wakorofi tu.
Mwanangu: Hata watoto wadogo anawakamata na kuwafunga?
Mimi: Ndiyo, lakini wale watoto wakorofi wasiopenda kufanya H/W
Mwanangu: Mimi si mkorofi na nafanya HW, si ndiyo baba
Mimi: eeeee mwanangu.
(Tunawakaribia Police wa usalama barabarani tunawapita)
Mwanangu: Police nimewaona watatu pia kuna Mwanamke, baba hata Police Mwanamke yupo
Mimi: Ndiyo
Mwanangu: Na yeye anaweza kukamata watu na kuwafunga?
Mimi: Ndiyo:
(Ukimya dakika 2)

Mwanangu: Baba weka speed One hundred tumeshawapita ma police. (huku akiangalia mshale wa speed-meter)

-------------
 
1.8 anaijua simu ya mama yake na simu zangu na hataki niguse si ya mama ake ama mama yake kugusa simu yangu lah sivyo hua anakua mtata sana mpaka umuamuru akupe kwa rudhaa yake' , anajua ela kuanzia 200 kua ni ndogo na elfu kumi ni kubwa pia anaijua wallet yangu vilivyo na hua nikifika anaichukua na kuihifadhi na ikitokea safari ya dukani ama mama yake anaenda dukani hua anaitoa na kutoa elfu 10 na yeye akijichukulia 500 ama 200 ya coin na akirudi lazima adai change: akiwa macho hataki mtu yeyote kumgusa mama ake hata mm, anajua chombo kichafu na mkimaloza kula yeye ndio hutoa vyombo ikatokea umevigusa hapo ni kazi mpya ya kum'bembeleza" hapendi katuni ni muvee haswa za magari na pikipiki anajua vitu vingi kiasi kwamba namshangaa sana sana tofauti na watoto wengine ninao wa fahamu
 
mie wangu ndiyo ameanza shule, basi nina kibarua cha kuimba nyimbo za shuleni kila akirudi. kupewa story za madam wake sijui anko.

na mbaya zaidi kupigiwa ngoma ili niimbe nyimbo ya Taifa. hapa uwa nachoka sana aiseee.

kingine kila mahali panachorwa sasa hivi, ukuta imebidi tuulinde kuliko kitu kingine.
 
Nadhani hajajua kwamba mama yake ni mke wangu
emoji23.png
emoji23.png
emoji23.png
hahahahahaha
 
Asiyepata bahati ya kuishi na mtoto wake akiwa na umri wa miaka kuanzia 2 hadi 4 atakuwa amekosa uhondo wa kupindukia. Ndiyo kipindi kizuri cha kufurahia ubunifu wa mtoto aliyeanza kuongea kabla hajaanza utundu wa shuleni. Ni kipindi cha faraja ya ajabu kushuhudia ubunifu wa kiasili wa binadamu unaoonyeshwa na mtoto mkamilifu.
 
Wangu ni 1.8 yrz anavituko balaa,asubuhi nikianza kuondoka kazini anakwambia Baba Bye aenda azini au chani.(kazini au kanisani),Kwenye simu sasa ndiyo balaa akiona unaongea na simu naye atatamani lazima aongee.
 
Mtoto wa cuisine yangu miaka miwil 2 anapenda kucheza game anaijua simu yani balaa anaplay vedio anaview image anapenda kuongea na simu mukikaa chumban akitoka anajificha mlangoni anakwambia mama nakuja eenh nakuja nnh nishubir nakuja yani watoto ni raha one day I'm going to have a baby 🙂 🙂 🙂 🙂 🙂 🙂
 
Back
Top Bottom