Vioja vya watoto wadogo (0-5years), tuambie vioja vya mwanao

Vioja vya watoto wadogo (0-5years), tuambie vioja vya mwanao

Mwanangu (5): Baba mbona unapunguza mwendo??
Mimi: Kuna askari mbele
Mwanangu: Sasa usipopunguza mwendo atakufanyaje?
Mimi: Atanikamata
Mwanangu: Atakukamata atakufanyaje?
Mimi: Atanifunga kamba anipeleke gerezani kunifunga.
Mwanangu: Police kazi yake kufunga kamba watu?
Mimi: Ndiyo, ila wale wakorofi tu.
Mwanangu: Hata watoto wadogo anawakamata na kuwafunga?
Mimi: Ndiyo, lakini wale watoto wakorofi wasiopenda kufanya H/W
Mwanangu: Mimi si mkorofi na nafanya HW, si ndiyo baba
Mimi: eeeee
(Tunawakaribia Police wa usalama barabarani tunawapita)
Mwanangu: Police nimewaona watatu pia kuna Mwanamke, baba hata Police Mwanamke yupo
Mimi: Ndiyo
Mwanangu: Na yeye anaweza kukamata watu na kuwafunga?
Mimi: Ndiyo:
(Ukimya dakika 2)

Mwanangu: Baba weka speed One hundred tumeshawapita ma police. (huku akiangalia mshale wa speed-meter)

-------------
[emoji16][emoji16][emoji16] watoto kweli ni rahaa
 
Watoto katika umri mdogo pale wanapokua wana shauku ya kujifunza kila kitu ni wanaleta burudani kweli kweli.
Mtoto anauliza baba hii redio ya nani? Unamwambia yetu wote
Anauliza yetu hata mimi?(akimaanisha yeye).
Kesho anauliza hiki kitanda cha nani[emoji23] [emoji23]
 
Wa kwangu ana miaka 3, kuna siku nimetoka safari nimekaa sebuleni akanifata na kuniuliza "baba leo unalala na mkeo?"
Siku ingine naongea nae kwenye Simu nikamtia mkwara ili ale chakula nae akanambia " baba ntakufumua" Daaaahh nkaona sasa hapa ipo haja ya kununua bunduki mapema.
Ikitokea akaona nimemshika mkono tu mama ake anakasirika sana na kwakua anajua mi haniwezi inabidi aanze kumpiga mama ake ili atoke hapo nilipo (Huyu jamaa anajionaga kama ye ndo ana hati miliki kwa mama ake)
Watoto ni raha sana, wana mambo yao ambayo ni ya kushangaza na kufurahisha kwa pamoja.
 
8d65a875ed859e8de6b61117c2894bbd.jpg

Huyu anapenda mapicha kama msanii ukiacha sim utakuta kajipiga selfie zaidi ya 100 nacho mpendea ni mwerevu
Miaka mingap mkuu
 
Mtoto wa cuisine yangu miaka miwil 2 anapenda kucheza game anaijua simu yani balaa anaplay vedio anaview image anapenda kuongea na simu mukikaa chumban akitoka anajificha mlangoni anakwambia mama nakuja eenh nakuja nnh nishubir nakuja yani watoto ni raha one day I'm going to have a baby 🙂 🙂 🙂 🙂 🙂 🙂
cuisine=aina/namna ya upishi wa chakula
Natumaini ulikusudia cousin.
 
mie wangu ndiyo ameanza shule, basi nina kibarua cha kuimba nyimbo za shuleni kila akirudi. kupewa story za madam wake sijui anko.

na mbaya zaidi kupigiwa ngoma ili niimbe nyimbo ya Taifa. hapa uwa nachoka sana aiseee.

kingine kila mahali panachorwa sasa hivi, ukuta imebidi tuulinde kuliko kitu kingine.
Hilo la kuchorwa liache mumy halikwepeki mana kama kwangu ukija utacheka chumba kilichopona ni cha kwangu tu kwa sababu hawaingii hovyo hovyo ila nyumba nzima imechorwa chorwa na chumbani kwao ndio usiseme.
 
Da
mie wangu ndiyo ameanza shule, basi nina kibarua cha kuimba nyimbo za shuleni kila akirudi. kupewa story za madam wake sijui anko.

na mbaya zaidi kupigiwa ngoma ili niimbe nyimbo ya Taifa. hapa uwa nachoka sana aiseee.

kingine kila mahali panachorwa sasa hivi, ukuta imebidi tuulinde kuliko kitu kingine.
Dah me hilo swala la kuchora ukuta nimepiga kelele hadi nimeamua niachane nalo achore hadi atakapopata akili ndo nipake rangi upya
 
Wa kwangu ana miaka 3, kuna siku nimetoka safari nimekaa sebuleni akanifata na kuniuliza "baba leo unalala na mkeo?"
Siku ingine naongea nae kwenye Simu nikamtia mkwara ili ale chakula nae akanambia " baba ntakufumua" Daaaahh nkaona sasa hapa ipo haja ya kununua bunduki mapema.
Ikitokea akaona nimemshika mkono tu mama ake anakasirika sana na kwakua anajua mi haniwezi inabidi aanze kumpiga mama ake ili atoke hapo nilipo (Huyu jamaa anajionaga kama ye ndo ana hati miliki kwa mama ake)
Watoto ni raha sana, wana mambo yao ambayo ni ya kushangaza na kufurahisha kwa pamoja.
Huyo ana dalili za wivu kama mwanangu , hata akiwa anacheza bize kiasi gani ukimkumbatia mama yake dogo anakuja mbio mbio anataka mama yake ambebe[emoji23] [emoji23]
 
Kuna watoto wengine wanachagua watu..akiwa analia ukitokea wewe ananyamaza na anakukimbilia umbebe!!
 
Mi mwanangu kuna siku nimetoka kazini nimechoka, mama yake yupo mbali kikazi...akaniambia baba kwanini usiwe na mke mwingine, yani alikua very serious!!!nikamwambia mama yako akijua atalia sana, akanijibu mama akiwa anakuja unamwambie mwingine aondoke mpaka mama atakapoondoka......aisee ni mengi sana, ila kwa kifupi he is real my friend.
 
Miaka mingap mkuu
Mitano mkuu huwa yuko mbali namm siku tukionana huwa haach gape anahakikisha ananiganda kila sehem napo enda juzi usiku wa UEFA nika mwambia naenda kuangalia mpira akanambia dady unampenda Ronaldo namm naenda kumwona nika mkatalia niusiku akachukua funguo anajidai ananifungilia mlango kutoka nje kavaa ndala moja yake moja ya maza ake namm kumkomoa nikaenda nae hvy[emoji23] [emoji23]
 
Hahaa. Kumbe ni karibia watoto wote tabia hiyo ya kuchora chora wanayo. Daah
Yaan ni balaa me mbaya zaid huwa wanapewa rangi za kufanyia hmwrk nyumban sasa naona zote zinaishia ukutan,ukiwa na mtoto mdogo kuna baadhi ya vitu kufanya ni ishu kama sitting room ukipanga akirud unakuta kumevurugwa balaa hapawez kuwa smart kama unavyotaka
 
Jembe langu lina miaka3,akimuona mtu flani akiongea kwenye tv,anakimbilia remote na kubadili chanel.Simply ana aleji naye.
Mtu gani Mkuu.?[emoji12] [emoji12] [emoji12] [emoji12] [emoji12]
 
Back
Top Bottom