Vioja vya watoto wadogo (0-5years), tuambie vioja vya mwanao

Vioja vya watoto wadogo (0-5years), tuambie vioja vya mwanao

Yani naona kila mwenye mtoto utaskia nimtundu mala anaakili sana mala mjanja mjamja mala nini naona sifatu inamaana nyie wenye watoto wote hakuna mwenye mtoto zoba anae lialia nakulamba kamasi mdawote anae pigwa nakila mtoto humu hakuna du!!! Ebu ongeeni ukweli wenu msifate mkumbo
Hata mimi nimegundua wengi wamekuwa waongo sana humu
Wengine watoto wao wazembe Ila wanashindwa kusema tu
 
Siku moja nilirudi home toka mihangaikoni nikakuta kabinti kangu kanaogeshwa chumbani kwakuwa kulikuwa na baridi kali, ile nazama tu chumbani kakanirudishia mlangoni "baba rudi chebuleni uchinchungukie" nikasema asante Mungu kameanza kujitambua bado kadogo, nikatulia sebuleni, mamake alivyokachomoa ktk beseni la maji akakapaka mafuta huku amekaandalia nguo za kuvaa, ila mamake amejipindua tu, mara hako kakaja na nguo mkononi katupu kama kalivyozaliwa kakisema "baba nivalishe nguo nimechaoga".
Sijasahau hadi leo, nitamkumbusha siku ya harusi yake Mungu akipenda nikisimamishwa na MC kutoa neno kama Mzazi.
 
Hata mimi nimegundua wengi wamekuwa waongo sana humu
Wengine watoto wao wazembe Ila wanashindwa kusema tu
[emoji23] [emoji23] [emoji23]
Hata kama wewe ulikua kilaza shuleni bado huwezi kumwambia ukweli mwanao.
Sasa kama mwanao kilaza utaanzaje kusema hapa wakati wataalamu wanajua akili za mtoto ni suala la kurithi inamaana ukisema mwanao ni kilaza simply unamaanisha wewe ndo kilaza au mkeo[emoji23] [emoji23] [emoji23]
Je uko tayari kusema wewe ni kilaza??
 
Mm mwanangu anamsumbua sna babaake, muda wa usiku akitaka kulala babaake anamvalisha pampers sasa hataki kuvaa anaangusha kilio anataka na babaake avae
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] wafanane
 
aise watoto ni raha sana.uyu wakwangu mdogo mwenye mwaka 1na miezi 8 sitaki kabisa akue kwa vituko anavyonipa.yaani ningekua na uwezo wakuzuia ujuaji wake ningefanya ivyo kwa kweli.yeye katuni anaita kukuti na anakatuni yake moja anataka iyo iyo iwekwe siku nzima.ukibadilisha tu vi ugomvi.akishasema kukuti kuwe na umeme kusiwe yeye ilo hajui ata taarifa ya habari imekua shida kuangalia.ila sasa hivi nimemuweza,nimemtafutia mtumba wa laptop kupunguza kelele.
Good lkn tuwe makini mwanga huo na macho cyo salama
 
Wangu ana 4yrs last week walikuwa kwenye exam ya midterm kwa elimu yake ya kindergarten sasa mwalimu akaandika vitu amabvyo hawajawahi kusoma aisee aligoma kuufanya huo mtihani mpaka akaenda mama yake siku iliyofuata ikabidi afanye kama special mbele ya mama yake na kumbembeleza kwa sana tu.
Huyo atakuja kuwa kiongozi wa migomo mingi huko mashuleni
 
Ukongwe wako hautuhusu na hakuna aliyekuita uje kusoma huu uzi.
Ukisema ukongwe kila mtu ni mkongwe kwa mwenzake.
Usilete stress zako za maisha mkuu kama unaona uzi hauna maana tembelea jukwaa la ufugaji, siasa n.k
Hahahaaaaa bora umempa vyake asitukate stimu buana[emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji38]
 
Haya mambo ya wazazi kutopata muda wa kukaa na watoto wao, kuna dogo aliharibu ndoa ya wazazi wake, bila baba wala mama kujua kwamba dogo miaka 4 ameshajua kusoma vizuri alichukua simu ya baba yake, sasa bahati mbaya sijui ilikuwaje wakashtuka anasoma meseji ya mchepuko kwa kwa sauti mpaka akaimaliza, ma mama alikuwa hana tabia ya kugusa simu ya mume wake.

Kilichoendelea hapo ni mtafaruku.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Siku moja nilirudi home toka mihangaikoni nikakuta kabinti kangu kanaogeshwa chumbani kwakuwa kulikuwa na baridi kali, ile nazama tu chumbani kakanirudishia mlangoni "baba rudi chebuleni uchinchungukie" nikasema asante Mungu kameanza kujitambua bado kadogo, nikatulia sebuleni, mamake alivyokachomoa ktk beseni la maji akakapaka mafuta huku amekaandalia nguo za kuvaa, ila mamake amejipindua tu, mara hako kakaja na nguo mkononi katupu kama kalivyozaliwa kakisema "baba nivalishe nguo nimechaoga".
Sijasahau hadi leo, nitamkumbusha siku ya harusi yake Mungu akipenda nikisimamishwa na MC kutoa neno kama Mzazi.
Amen
 
Mwanangu one year now...ameonyesha kupenda sana mziki akisikia wimbo wa jux hapalaliki....anaimba na kupiga kelele ....na akiwa amelala akisikia tangazo LA airtel money lzm aamke acheze kwanza ndio alale tena....yan nafurah sana kuona vituko vyake
 
Mungu wangu...!! yani watoto niliowatupa bafuni nadhan wangekua wananipa furaha sasa hivi daah...anyway tusubir labda next day inshalah nitapata furaha na watoto wangu wajao...
 
Mi wa kwangu balaa natamani akue kidogo labda nitapata zuri la kueleza, leo ni wiki ya tatu sijalala nakesha, dogo analala mchana wakati mimi nipo job, usiku halali na akilala mikononi ukimuweka kitandani tuu yani kabla hata hujakiacha kitanda kishaamka na kelele nyingi, kingine asee usikae karibu na mamaake ugomvi wake c mdogo atalia hapo hadi utashangaa, kingine tangu wiki iliyopita hajacheka sijui ndo kutabasamu hakuna. Ana miezi 4. Hataki kulazwa kama watoto wengine anapokuwa macho, yeye anataka kukaa na anakaa...huyo ni mdogo, kakayake yeye anapenda ngumi, anajua bunduki zote kwa majina, hili nimejaribu kumuonya mamayake asiwe akimuwekea movie za mapigano zaidi ya cartoon lakini sijui huyu kijana anajifunzia wapi maana hakawii kukwambia anataka awe mwanajeshi sababu hapendi majambazi, huyo Ana miaka mi 4, anajua kikorea, kajifunza wapi mi sijui...ila ana shida moja anapenda tambi tuu, vyakula vingine kula mpaka mpigizane kelele sana na husingizia anataka kukojoa akienda harudi..ana huruma sana na mamayake, mjanja mjanja sana ukikasiririka atajua jinsi ya kukufanya ucheke tuu, shida usimuache na mdogo wake peke yao, unaweza kuta mtoto analishwa ugali.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] huo ugali sasa
 
Mwanangu is so sweet kwa kweli,hadi huwa natamani muda uende haraka nitoke kazini nimuwai kabla hajalala

Akinisikia tu nje ya geti ananikimbilia huku anashangilia mama mama utasema hajaniona mwezi mzima

Atataka nimpe pochi,tukiingia ndani,anataka kunitoa viatu,ananiingizia pochi na viatu ndani

NB: huwa anachukua remote ya TV anaweka sikioni alafu anaongea eti ndio simu

Au akifanya kosa,ukamuita,akifika tu anaanza Ku count numbers/alphabets au kuimba nyimbo zake za shule,nabadilisha mawazo ya kumgombeza

Next month anatimiza 4 years
 
Back
Top Bottom