Viongozi imarisheni vyama, maandamano Bado muda wake

Viongozi imarisheni vyama, maandamano Bado muda wake

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Muda wa maandamano ya vyama vya siasa Bado kabisa, ukifika hakutakuwa na chombo kitakachoweza kuyazuia kufanyika. Hakuna nguvu itakayoweza kuzuia nguvu ya umma muda ukitimia. Sasa hivi mnachofanya ni vurugu TU (nuisance), wananchi hawawaelewi mnachomaanisha, ndiyo maana maandamano yenu yanadhibitiwa kirahisi TU.

Jengeni vyama kwanza hadi kwenye ngazi ya mioyo ya watu kule mashinani. Waelezeni watu njia mbadala za kuboresha maisha yao wanakoishi ili waelewe. Ishini nao, kuleni, vaeni, laleni na somesheni watoto wenu kama wao.

Haiwezekani mwenyekiti wa chama amekamatwa lakini nchi yote imetulia tulii kama vile hakuna kilichotokea, mko peke yenu TU na wapendwa wenu TU.
 
Ni pale viongozi wakuu wa chama wanakamatwa lakini watu wako bize na kazi zao. Wanawawakilisha akina nani? Nani anataka maandamano, wanachama? viongozi? wananchi? wafadhili?

Tujenge vyama kwanza la sivyo ni mahangaiko TU.
 
Muda wa maandamano ya vyama vya siasa Bado kabisa, ukifika hakutakuwa na chombo kitakachoweza kuyazuia kufanyika. Hakuna nguvu itakayoweza kuzuia nguvu ya umma muda ukitimia. Sasa hivi mnachofanya ni vurugu TU (nuisance), wananchi hawawaelewi mnachomaanisha, ndiyo maana maandamano yenu yanadhibitiwa kirahisi TU.

Jengeni vyama kwanza hadi kwenye ngazi ya mioyo ya watu kule mashinani. Waelezeni watu njia mbadala za kuboresha maisha yao wanakoishi ili waelewe. Ishini nao, kuleni, vaeni, laleni na somesheni watoto wenu kama wao.

Haiwezekani mwenyekiti wa chama amekamatwa lakini nchi yote imetulia tulii kama vile hakuna kilichotokea, mko peke yenu TU na wapendwa wenu TU.
Sahau Kwa Tanzania haiji kutokea.ubinafsi Ni utamaduni Wetu na uoga.Hata Vita siye hatuwezi Ni mbwembwe tunaweza
 
Maandamano Bado kabisa Tanzania, ardhi Bado ipo, sehemu za kuegesha bodaboda Bado zipo, sehemu za kupanga bidhaa chini Bado zipo, viwanja Bado vinapatikana, ajira Bado zipozipo na 70% Bado wanajilimia chakula chao. Iko siku ikifika wananchi ndio watakaoitisha maandamano bila kujali ni chama gani na dini gani na kabila gani
Well said, Watanzania Wataandamana kwa hiyari yao, pale serekali itakapojisahau, hasa kushughulikia suala la mlundikano wa wahitimu wasio na kazi, it may burst automatically, Nchi itapasuka yenyewe, kwa hali ngumu itakayokuwepo, kwa wakati huo!, kwa tanzania yetu bado sana, maana muhitimu anakuwa na options, ya kuhusika kwenye kilimo, n. k.
Serekali yetu ni lazima ijiwekeze kwenye agro industry haraka katika kupunguza tension za ajira,ikiwepo kuleta wawekezaji wakubwa wa kilimo cha kibiashara.

Sahau Kwa Tanzania haiji kutokea.ubinafsi Ni utamaduni Wetu na uoga.Hata Vita siye hatuwezi Ni mbwembwe tunaweza
Africa hakuna nchi iliyojikomboa kwa maamdamano, ni mahangaiko tu
 
Kweli kabisa, maji ya kupikia ugali hayajachemka, wanataka kuweka unga
Ni kujidanganya TU, huwezi kujigamba kuwa wewe ni chama chenye wafuasi wengi lakini ukikamatwa na kuwekwa iela wao wanaendelea na mambo yao unabaki mwenyewe jela, kama Alparslan akikamatwa na adui utana patakavyochimbika, lakini chadema utakuta viongozi wao wooooote wameswekwa lakini wafuasi wao wako kwewny mishemishe zao
 
Chama ni wanachama, na wananchama ni wananchi. Vitisho vyoote hivyo, wanatisha wananchi wasiunge mkono CHADEMA tu, nasio vyama vingine, sasa wana imarisha chama gani?
 
Ni kujidanganya TU, huwezi kujigamba kuwa wewe ni chama chenye wafuasi wengi lakini ukikamatwa na kuwekwa iela wao wanaendelea na mambo yao unabaki mwenyewe jela, kama Alparslan akikamatwa na adui utana patakavyochimbika, lakini chadema utakuta viongozi wao wooooote wameswekwa lakini wafuasi wao wako kwewny mishemishe zao
Halafu hawajifunzi, wakati Mbowe ana kesi ya ugaidi au Lissu kashambuliwa, kila mtu alikuwa anaendelea na shughuli zake. Chadema ilipata umaarufu kutokana na uwezo wa hoja hasa wakati Slaa akiwa ndio Katibu M kuu, tangu waanze siasa za vurugu umaarufu wao unashuka. Warudi kwenye siasa za hoja majukwaani.

Lissu ambaye anaonekana kuwa na nguvu katika chama hicho ni muumini wa siasa za vurugu, kajaribu maandamano kabla ya mikutano ya hadhara miezi kadhaa iliyopita, lakini alifeli, ila anarudia tena
 
Muda wa maandamano ya vyama vya siasa Bado kabisa, ukifika hakutakuwa na chombo kitakachoweza kuyazuia kufanyika. Hakuna nguvu itakayoweza kuzuia nguvu ya umma muda ukitimia. Sasa hivi mnachofanya ni vurugu TU (nuisance), wananchi hawawaelewi mnachomaanisha, ndiyo maana maandamano yenu yanadhibitiwa kirahisi TU.

Jengeni vyama kwanza hadi kwenye ngazi ya mioyo ya watu kule mashinani. Waelezeni watu njia mbadala za kuboresha maisha yao wanakoishi ili waelewe. Ishini nao, kuleni, vaeni, laleni na somesheni watoto wenu kama wao.

Haiwezekani mwenyekiti wa chama amekamatwa lakini nchi yote imetulia tulii kama vile hakuna kilichotokea, mko peke yenu TU na wapendwa wenu TU.
Wewe umesaidia lipi katika kutaka wananchi tupate haki ya kuishi bila wasiwasi.
 
Mambo ya kisiasa hayeawezi watoa watanzania ndani wakaandamana ila mambo ya kijamii yanaweza watoa watanzania ndani wakaungana na wakandamana nakupa mfano uko simiyu watoto kupotea na polisi kukosa majibu uliona wanainchi walivyo kiwasha jambo la pili

Yule binti kubakwa na askari uliona lilivyoubua hisia za watu so mambo kama haya yanaweza ibua hisia za watu wakaingia barabarani na wakiingia tu ndio hapo hapo wanaunga na mambo ya kisiasa so mziki wake siku ikitokea hakuna wakuuzima mpaka kitaeleweka
 
Chama ni wanachama, na wananchama ni wananchi. Vitisho vyoote hivyo, wanatisha wananchi wasiunge mkono CHADEMA tu, nasio vyama vingine, sasa wana imarisha chama gani?
Muda wa kuandamana badoo, kama ukifika hakuna mwanachama atatishwa na chombo chochote. Ndoyo maana nasema vyama vije na sera na hoja zinazowagusa wananchi Moja kwa Moja, badala ya kuwataka kuandamana kwa hoja dhaifu. Yaani waandamane kwakuwa mtu wasiemfahamu katekwa? Waandamane kwakuwa nchi imeuzwa, wanajiuliza nchi imeuzwaje? Waandamane kwakuwa wewe hukushimda ubunge? Waandamane kudai katiba mpya, hiyo mpya italeta nini jikoni kwake? Hayo ndiyo maswali wanayojiuliza wananchi kuhusu kuandamana.

Kama Angekuwa mm ningewaacha waandamane TU hao watu 15. Maandamano yanatumia pesa nyingi kuyalinda ambazo zingetumika kuwapa mikopo watoto wetu wasome.
 
Halafu hawajifunzi, wakati Mbowe ana kesi ya ugaidi au Lissu kashambuliwa, kila mtu alikuwa anaendelea na shughuli zake. Chadema ilipata umaarufu kutokana na uwezo wa hoja hasa wakati Slaa akiwa ndio Katibu M kuu, tangu waanze siasa za vurugu umaarufu wao unashuka. Warudi kwenye siasa za hoja majukwaani.

Lissu ambaye anaonekana kuwa na nguvu katika chama hicho ni muumini wa siasa za vurugu, kajaribu maandamano kabla ya mikutano ya hadhara miezi kadhaa iliyopita, lakini alifeli, ila anarudia tena
Malezi yetu sisi kwenye familia sio ya kidemokria, tulifundishwa kutii wakubwa, walimu mashuleni, viongozi na wageni bila kuhoji. Tulikatazwa kujamba mbele za watu , kutukana na kujisaidia hadharani. Jamii inamshangaa Lissu kuweza kutukana na kubeza viongozi wakuu hadharani kinyume Cha malezi yao. Ni utamaduni wa watu wengine kabisa ambao mtu anaweza kujamba, kupenga kamasi, na kutukana popote mbele ya yeyote.

Lissu ndiye anaua chadema kwa siasa zisizo na staha ambazo zinamkera mtu yeyote kwenye tamaduni zetu za kiafrika. Ni meanaharakati badala ya mwanasisa.
 
Wee choko fyata mdomo wako huo kama shimo la choo!
Eleza Hela ya ruzuku ilipo na imesaidia nn wapiga kura. Je, ubunge wangu umesaidia watoto wa wapigakura kulipa karo ya shule. Tumeshuhudia wabunge wa upinzani wakinunua V8 pia na kujenga mahoteli na majumba badala ya kuimarisha chama vijijini.
 
Muda wa maandamano ya vyama vya siasa Bado kabisa, ukifika hakutakuwa na chombo kitakachoweza kuyazuia kufanyika. Hakuna nguvu itakayoweza kuzuia nguvu ya umma muda ukitimia. Sasa hivi mnachofanya ni vurugu TU (nuisance), wananchi hawawaelewi mnachomaanisha, ndiyo maana maandamano yenu yanadhibitiwa kirahisi TU.

Jengeni vyama kwanza hadi kwenye ngazi ya mioyo ya watu kule mashinani. Waelezeni watu njia mbadala za kuboresha maisha yao wanakoishi ili waelewe. Ishini nao, kuleni, vaeni, laleni na somesheni watoto wenu kama wao.

Haiwezekani mwenyekiti wa chama amekamatwa lakini nchi yote imetulia tulii kama vile hakuna kilichotokea, mko peke yenu TU na wapendwa wenu TU.
Hata wakiimarisha vyama, hakuna chama cha kisiasa ambacho kinaweza kuiondoa CCM kwa mfumo uliopo wa uchaguzi
 
Hata wakiimarisha vyama, hakuna chama cha kisiasa ambacho kinaweza kuiondoa CCM kwa mfumo uliopo wa uchaguzi
Muda haujafika kaka, usiwe na haraka ya kukiondoa CCM. Hata Nchi za kiafrika zilizofanikiwa kuondoa vyama vyao tawala Bado wako palepale TU, wamebadilisha wapigaji TU kupata wapya. Muda ukifika hata Wana CCM wenyewe watajutia kuimba iyenaiyena kwa miaka yote hiyo. Muda huo ni pale ambapo ardhi ya bure hakuna na hakuna mashamba makubwa (plantations), super markets na Malls ziko Kila mtaa kwenye majiji na miji, maeneo ya maegesho ya magari na bodaboda hakuna, ajira hakuna na matibabu sio bure.
 
Hapo ndiyo ukomo wa akili zako, zaidi ya hapo utawehuka!
Kuandamana ni sawa na kusema abiria chunga mizigo Yako. Yaani park for your own risk. Ukikamatwa hakuna nguvu ya umma itakutoa, utasubiri huruma ya waliokukamata. Maana yake muda wa kuandamana haujafika bali mnalazimisha watu kuandamana kwa maslahi (saccos) yenu. Ni afadhali Mh. Mbowe alikwenda kwenye maadamano na mtoto wake Nicole, lakini wengine wameficha familia zao nje ya nchi. Wanapata wapi pesa za kuishi na kusomesha nje ya nchi ghali? Nani anagharamia? Kama ni mkopo watalipa nini? Kama ni fadhila watalipa nini? Tuwasaidie wapate ubunge/Ikulu and then?.

Tuimarishe vyama na sera safi mbadala zinazouzika kwa wananchi. Sera nzuri ni zile zinazogusa watanzania wote bila kubagua kabila, dini, elimu Wala Kanda.

Mimi nilikuwa miongoni mwa watu waliwahi kuandamana chini ya Mchungaji Mtikila na sera yake ya Magabachori. Aliweza kujenga hoja na watu wakamwelewa namna akina Patel, Gulamali, na kanchibai walivyoukamata uchumi wakati ule hadi watu wakaelewa somo. Hawa wa sasa wanalazimisha watu waandamane eti kijana mmoja huko Nanjilinji amekatamwa na polisi bila kusema huyo kijana alifanya nn hata akakamatwa na polisi. Kila aliyekamatwa au kutekwa lazima anajua kwa nini amekamatwa au kutekwa, na mara zote huwa wanamfahamu aliyewakamata au kuwateka.
 
Wee mburula kudai haki kuna gharama huwezi kuipata kwa kupiga ngonjera kama zako. Watu wanataka haki, ukamatwe, ushtakiwe na uhukumiwe kwa haki! Siyo uko kwenye mishemishe zako au nyumbani kwako watu wanakuteka na kukuua kwa kificho!

Watu wamesema sana lakini serikali imeweka pamba masikioni kwa hiyo kuandamana ni mwendelezo wa kuiambia serikali na dunia kwa ujumla kuwa kuna mambo hayaendi sawa! Hivyo kwa kusema au kuandamana ni kujitoa muhanga, lazima kuwe na wachache wanaojitoa muhanga ili wengi wapate haki.

Tangu zama za ukoloni watu wachache walijitolea kupigania haki na matunda yake yanaonekana. Kwa hiyo huna sababu za msingi kuwabeza wanaojitolea kwa kuwa wanafahamu kuna kuumizwa, kufungwa na hata kufa. Serikali dhalimu kama ya Samia si tofauti inategemewa kufanya hivyo hivyo lakini pia mwisho wa yote lazima itaondoka ama kwa mazungumzo mezani au kwa nguvu za umma. Nguvu ya Umma haioti kama uyoga inajengwa kwa mchakato wa muda mrefu. Kuwabeza au kuwakatisha tamaa hawa wachache wanaojitolea ni kudhoofisha mchakato na kikua kwa nguvu ya Umma!
Kama ukiwa ndani ya msitu huwezi kuuona msitu bali utaona miti, mawe, vichaka na utajiona wewe mwenyewe ukishangaa na kuogopa Kila kitu. Sisi tulioko nje mbali ya msitu ndio tunauona vizuri msitu. Tunaeaona wanasiasa kama wanasaccos. Unawapa kura Yako na kuondoka nayo kwenda CCM kuunga juhudi. Hakuna haki kuu kushinda haki ya kuishi, Tanzania haki hiyo ipo ya kutosha.
 
Ni mpumbavu pekee anayeweza kulinganisha vitu visivyofanana!
Hata Mzee Kibao (RIP) nadhani alilijua kosa lake pia, bila shaka hata watekaji wake alijua ni akina nani nankwanin walimshusha kwenye gari na bila shaka waliwahi kumuonya. Kwakuwa hawezi kujitetea Wala kujibu hoja hizi sipaswi kumsemea sana. Hoja yangu hapa tuangalie tuliposimama.

Natamani watekwe wale wote niliosukuma magari yao wakati wa kampeni, nikawapa kura yangu, kikalinda kura zao na kutangazwa wameshinda lakini wakaondoka kwenda kuunga juhudi na kusababisha taifa kuingia kwenu uchaguzi mdogo Tena. hahaja
 
Wewe umesaidia lipi katika kutaka wananchi tupate haki ya kuishi bila wasiwasi.
Sasa kama wewe unatembea na mke wa mtu utashangaa nini siku ukiona umetekwa na watu usiowajua? Inawezekana watekaji huwajui lakini kwanini wamekuteka utakuwa unajua. Haki Yako lazima ikomee pale haki ya mtu mwingine inapoanzia. Kutembea na mke wa mtu ni haki lakini mwenyewe akikuteka unang'aka.
 
Back
Top Bottom