The Watchman
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 896
- 1,427
VIONGOZI wa Makanisa Katoliki Nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (CENCO) pamoja na Kanisa la Kristo nchini humo (ECC), mapema leo Februari 12, 2025 wamekutana na kufanya mazungumzo na waasi wanamgambo wa AFC-M23 lengo likiwa ni kujadili udumishaji amani nchini humo.
Viongozi hao wamekutana na sehemu ya uongozi wa M23 katika Hoteli ya Serena mjini Goma ambako pamoja na mambo mengine wamewashukuru wanamgambo hao kwa kuendelea kudumisha amani katika mji huo walioutwaa hivi karibuni.
Wamesema kwa mara ya kwanza, Goma inafanya kazi saa 24 kwa siku, bila matukio ya wizi wa kutumia silaha au vurugu za aina yoyote tofauti na ilivyotarajiwa.
Vilevile kabla ya kikao hicho viongozi hao wanaelezwa kukutana na kufanya mazungumzo na Rais wa DRC Felix Tshisekedi.
Katika mwendelezo wa mzozo huo ambako serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo inaishutumu Rwanda kufadhili moja kwa moja mashambuli hayo mapema leo imefunga anga yake kwa ndege zote za kiraia na za serikali zilizosajiliwa au kutoka Rwanda.
Viongozi hao wamekutana na sehemu ya uongozi wa M23 katika Hoteli ya Serena mjini Goma ambako pamoja na mambo mengine wamewashukuru wanamgambo hao kwa kuendelea kudumisha amani katika mji huo walioutwaa hivi karibuni.
Wamesema kwa mara ya kwanza, Goma inafanya kazi saa 24 kwa siku, bila matukio ya wizi wa kutumia silaha au vurugu za aina yoyote tofauti na ilivyotarajiwa.
Vilevile kabla ya kikao hicho viongozi hao wanaelezwa kukutana na kufanya mazungumzo na Rais wa DRC Felix Tshisekedi.
Katika mwendelezo wa mzozo huo ambako serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo inaishutumu Rwanda kufadhili moja kwa moja mashambuli hayo mapema leo imefunga anga yake kwa ndege zote za kiraia na za serikali zilizosajiliwa au kutoka Rwanda.