Viongozi wa nchi watumwa, wananchi wenye nchi watumwa, nani wa kuukomesha utumwa?

Viongozi wa nchi watumwa, wananchi wenye nchi watumwa, nani wa kuukomesha utumwa?

Sitaki kukubaliana wala kupingana na wewe, Watanzania inatupasa tujitathmini sana kwanza tusiamini sana kama Chama cha siasa ndiyo mkombozi wa matatizo yetu, bado tupo kwenye utumwa wa kuamini Samaki mmoja akioza basi wote wameoza. vyama vyote vya Siasa havina tofauti maana viongozi wake ni wanaadam wenye miili na fikra zinazolingana. sitaki kuamini kwamba CCM ni mbaya moja kwa moja ila kuna watu ndani ya CCM ambao wanaitia doa ionekane ni mbaya, hivyohivyo kwa Chadema, ATC Nk. Wanasiasa hawa usione wanalumbana na kutoleana maneno mabaya mengine hata tukadhani ni kutishiana maisha, hawa wanatuzubaisha tu, wakiwa chemba wote wanaongea lugha moja matokeo yake Wananchi ndiyo tunayumbishwa tunakosa msimamo wakati wao maisha yanaendelea kuwanyookea (Tukumbuke kwamba Vyama na wanasiasa, sisi Wananchi ndiyo Mtaji wao na ndiyo tumewaweka hapo walipo).
Kwahiyo katika hivi vyama tariban vyote vinakuwa na sera na mitizamo mizuri sana lakini ndani ya hivyo vyama ndiyo kuna vivuruge! Unaweza kuta ndani ya CCM watu wanaoifanya ionekane ni ya ovyo hawazidi 20 lakini humo humo kuna wazalendo waliopitiliza! hivyo ushauri wangu ni Wananchi kujitafakari. kutafuta njia ya kudeal na hawa wachumia tumbo kuliko kutoa hizo lawama na kuonesha moja kwa moja kukata tamaa kwa kulalamikia chama moja kwa moja wakati hivi vyama ni sisi Wananchi ndiyo tumeviweka.
Point
 
Uhafifu wa IQ zetu ni ulemavu kama ulemavu mwingine.
 
Mifumo yote ya elimu, uchumi inamilikiwa na wakuu wa dunia huna kipya utakachokwnda nao kinyume
 
Mifumo yote ya elimu, uchumi inamilikiwa na wakuu wa dunia huna kipya utakachokwnda nao kinyume
Kimtizamo ni hivyo, tatizo kwa sisi Waafrika ndivyo hali tuliyo kubaliana nayo japo hatuna hata ndoto ya uthubutu.Kwakweli tuna safari ndefu sana japo ya kufikiria tu, Wachina wamewezaje? na Wakorea wamewezaje. Tatizo sisi waafrika tunaogopa mpaka vivuli vyetu wenyewe!
 
Viongozi wetu niviranja walimu wako nje sisi niwanafunzi tu
Dhana ya utumwa imekuwa ikibadilika kulingana na vipindi tofauti vya muda. Enzi za mababu zetu utumwa ulikuwa ni wakufungwa minyonyoro na kufanyishwa kazi ngumu bila ujira. Taifa likaja kupata uhuru ikawalazimu wakoloni kuacha makoloni yao ambapo kiukweli hawakupenda ndio maana wakaendeleza dhana ya utumwa yaani tukawa huru kuendesha mambo yetu wenyewe ila kwa kupangiwa jinsi ya kuyaendesha na mataifa ya nje au na baadhi ya watu ndani ya nchi wanaohisi wana nguvu kuliko serikali hiki ndicho kile kinachoitwa utumwa huru.

Tupo katika utumwa wa fikra, Embu fikiria Hivi ni kweli hatuwezi kuunda sera zetu za elimu bili kuiga mataifa ya nje? Ni kweli hatuwezi kuendesha mambo yetu ya Kiuchumi bila mataifa ya nje (Rejea ishu ya sasa ya bandari na DP World) Hivi ni kweli hatuwezi kuwa na mifumo yetu ya ulinzi na usalama? Ujinga huu ndio uliozaa mambo ya bunge kukosa nguvu dhidi ya serikali, Mahakama kukosa nguvu dhidi ya serikali na serikali kukosa nguvu dhidi ya mabeberu.

Hapa tunaweza sema viongozi ni watumwa, lakini kwa upande mwengine wananchi wamekuwa wakiingilia kati baadhi ya mambo muhimu na kuishauri serikali ila serikali Imekuwa ikipiga teke na kunyamazia maoni ya wananchi, tafsiri yake ni kuwa wananchi nao ni watumwa.

Nani sasa wakukomesha utumwa huu?
Raisi pekeee lakini nayeye kawekwa na wao
 
Kimtizamo ni hivyo, tatizo kwa sisi Waafrika ndivyo hali tuliyo kubaliana nayo japo hatuna hata ndoto ya uthubutu.Kwakweli tuna safari ndefu sana japo ya kufikiria tu, Wachina wamewezaje? na Wakorea wamewezaje. Tatizo sisi waafrika tunaogopa mpaka vivuli vyetu wenyewe!
Hao wameweza kwa kushirikiana na wazungu hakuna maendeleo bila kuwashirikisha hao ndio wameshika ufunguo wa maendeleo Duniani
 
Mifumo yote ya elimu, uchumi inamilikiwa na wakuu wa dunia huna kipya utakachokwnda nao kinyume
Sijasema twende nao kinyume nimesema tuwe na mifumo yetu
Kwani hatuwezi kuwa na mifumo yetu bila kwenda nao kinyume??
Mfano moja katika character ya democracy ni mfumo wa vyama vingi , Tunaweza kuwa na vyama viwili tu au vitatu basi kupunguza wingi wa vyama ambao hauna tija hapo tunakuwa tupo ndani ya demokrasia lakini kwa namna yetu.
Mfano mwingine kwani ni lazima primary iwe miaka saba? Mbona kenya ni sita. Kwahiyo ninaposema tuwe na mifumo yetu namaanisha tuchuje mifumo yao iliyo bora na yenye manufaa tuchukue isiyo na manufaa tuache na iliyo na udhaifu turekebishe.
Mbona watu wamesimama hadharani kupinga ushoga hao wakubwa wa dunia wamewafanyia nini??
 
Sitaki kukubaliana wala kupingana na wewe, Watanzania inatupasa tujitathmini sana kwanza tusiamini sana kama Chama cha siasa ndiyo mkombozi wa matatizo yetu, bado tupo kwenye utumwa wa kuamini Samaki mmoja akioza basi wote wameoza. vyama vyote vya Siasa havina tofauti maana viongozi wake ni wanaadam wenye miili na fikra zinazolingana. sitaki kuamini kwamba CCM ni mbaya moja kwa moja ila kuna watu ndani ya CCM ambao wanaitia doa ionekane ni mbaya, hivyohivyo kwa Chadema, ATC Nk. Wanasiasa hawa usione wanalumbana na kutoleana maneno mabaya mengine hata tukadhani ni kutishiana maisha, hawa wanatuzubaisha tu, wakiwa chemba wote wanaongea lugha moja matokeo yake Wananchi ndiyo tunayumbishwa tunakosa msimamo wakati wao maisha yanaendelea kuwanyookea (Tukumbuke kwamba Vyama na wanasiasa, sisi Wananchi ndiyo Mtaji wao na ndiyo tumewaweka hapo walipo).
Kwahiyo katika hivi vyama tariban vyote vinakuwa na sera na mitizamo mizuri sana lakini ndani ya hivyo vyama ndiyo kuna vivuruge! Unaweza kuta ndani ya CCM watu wanaoifanya ionekane ni ya ovyo hawazidi 20 lakini humo humo kuna wazalendo waliopitiliza! hivyo ushauri wangu ni Wananchi kujitafakari. kutafuta njia ya kudeal na hawa wachumia tumbo kuliko kutoa hizo lawama na kuonesha moja kwa moja kukata tamaa kwa kulalamikia chama moja kwa moja wakati hivi vyama ni sisi Wananchi ndiyo tumeviweka.
Kama viongozi wakubwa wanaiba mabilioni na adhabu yao kubwa ni kuondolewa madarakani badala ya kushitakiwa unategemea nini? Mkapa alikiri kuiba 100B ajili ya uchaguzi hatukusikia hata TAKUKURU inamhitaji hata kwenye mahojiano tu.
 
Hao wameweza kwa kushirikiana na wazungu hakuna maendeleo bila kuwashirikisha hao ndio wameshika ufunguo wa maendeleo Duniani
Brother!, unyonge wetu na kutojiamini kwetu ndiyo mtaji mkubwa sana kwa hao wazungu. Amini usiamini mbwembwe zote za wazungu na kujiamini kwao ni sababu ya Unyonge wa Mwafrika na huo ndiyo mtaji wanaoulinda na wanahakikisha kuulinda mpaka kiama(kama kweli kipo!) Afrika tuna kila kitu kilichopo huko kwa wazungu tatizo letu moja tu, ni kukubali kuwa tegemezi na kujirahisisha kupita kiasi kwa hao wazungu na kuwapa utukufu na hatma ya maisha yetu.
 
Brother!, unyonge wetu na kutojiamini kwetu ndiyo mtaji mkubwa sana kwa hao wazungu. Amini usiamini mbwembwe zote za wazungu na kujiamini kwao ni sababu ya Unyonge wa Mwafrika na huo ndiyo mtaji wanaoulinda na wanahakikisha kuulinda mpaka kiama(kama kweli kipo!) Afrika tuna kila kitu kilichopo huko kwa wazungu tatizo letu moja tu, ni kukubali kuwa tegemezi na kujirahisisha kupita kiasi kwa hao wazungu na kuwapa utukufu na hatma ya maisha yetu.
Ubinafsi ndio msingi wa upumbavu wote,mtu anawaza kukopa tu akijua anayo percentage yake,mzigo masikini watalipa
 
Kama viongozi wakubwa wanaiba mabilioni na adhabu yao kubwa ni kuondolewa madarakani badala ya kushitakiwa unategemea nini? Mkapa alikiri kuiba 100B ajili ya uchaguzi hatukusikia hata TAKUKURU inamhitaji hata kwenye mahojiano tu.
Hicho ndicho nilichokieleza kwamba Wananchi tunatakiwa tujitafakari, vinginevyo tutakuwa kilasiku ni mashuhuda wa kufanyiwa hizo sarakasi kila siku, na kubaki kutafuta kauli ja kujiliwaza kama hizo "CCM haifai tuitoe madarakani!" kwangu hizo ni kauli za kutafuta faraja ya kuidanganya mioyo yetu kwamba CCM ni mbaya tukiitoa madarakani tutakuwa na hali nzuri badala ya kujiuliza sababu ya CCM kufanya vibaya ni nini? maana wanasiasa ni wale wale kesho ukiwapa Dora Chadema utakuta walewale ulio wakimbia CCM wapo chadema au ACT tatizo mimi nasema sio chama ni watu, na hao watu ninauhakika wanaweza wasifike hata 20 ndiyo wameshika akili za Watanzania wote 61 millioni.
 
Hicho ndicho nilichokieleza kwamba Wananchi tunatakiwa tujitafakari, vinginevyo tutakuwa kilasiku ni mashuhuda wa kufanyiwa hizo sarakasi kila siku, na kubaki kutafuta kauli ja kujiliwaza kama hizo "CCM haifai tuitoe madarakani!" kwangu hizo ni kauli za kutafuta faraja ya kuidanganya mioyo yetu kwamba CCM ni mbaya tukiitoa madarakani tutakuwa na hali nzuri badala ya kujiuliza sababu ya CCM kufanya vibaya ni nini? maana wanasiasa ni wale wale kesho ukiwapa Dora Chadema utakuta walewale ulio wakimbia CCM wapo chadema au ACT tatizo mimi nasema sio chama ni watu, na hao watu ninauhakika wanaweza wasifike hata 20 ndiyo wameshika akili za Watanzania wote 61 millioni.
Katiba mbovu tudai katiba mpya
 
Back
Top Bottom