Viongozi wetu wa Afrika wanakaa kimya juu ya vita ya Urusi na Ukraine kwasababu wanaogopa watanyimwa misaada

Hivi unajua kwamba ukraine ilishakuwa na kinu cha nuclear na ilikuwa na silaha za nuclear??
Kuwa na kinu cha nuklia kwa ajili ya kutoa nishati na kutengeneza silaha za nuklia ni vitu viwili tofauti.
Ukraine ilikuwa na silaha za nuklia enzi za USSR, baada ya ussr kuvunjika Ukraine iliziachia hizo silaha, zikaharibiwa na zingine zikatwaliwa na Russia, na ikasaini mkataba wa kutotaka kutengeneza wala kuwa na silaha za nuklia. Unalijua hilo?
 
Wapi wamesema wanataka kutawala dunia yote? Mpaka sasa wametawala nchi ngapi na ngapi zimesalia? Ku share ideals haina maana unakuwa puppet.
Ni kweli kabisa marekani anataka kutawala dunia na ndo chanzo cha migogoro
 
Ni kweli kabisa marekani anataka kutawala dunia na ndo chanzo cha migogoro
Inaweza kuwa ni kweli. Ila ninachoomba ni wewe kunihakikishia huo ukweli, la sivyo inabaki kuwa story ya kijiweni.
 
Naomba iseme hiyo ya wazi, manake kama siri hata wewe huijui. Mbona misaada ya nchi za magharibi kwetu ni wazi tu uki google unapata data zote?

Nchi za magharibi zimekufanya uamini kuwa wanazipa nchi za Afrika misaada mingi lakini ukichunguza utagundua Kuwa wanachochukua toka nchi hizi ni mara dufu ya hiyo wanayosema misaada wanaleta!!! There is no free lunch ; hiyo sio misaada ni ndoana ya wao kuchukua vile wavitakavyo kutoka Africa yakiwemo madini etc.

Hakuna haja kwa Nchi za Afrika kujiingiza kwenye vita hivi kati ya Nchi za magharibi[ UKRAINE] na Russia kwasababu; hivi vita kutokana na uchumi wetu kuwa tegemezi ,nchi zitaathirika sana kwa bei za bidhaa muhimu kupanda sana na hivyo mfumuko wa bei kuathiri nchi nyingi hasa zile ambazo hazina Mafuta! Hence Africa has enough of its problems!

Hata hivyo Nchi za Africa hazina budi kuangalia fursa zinazoweza kujitokeza kutokana na vita hivi na hivyo kuzitumia kusaidia uchumi wa nchi zao. Kwa Nchi kama Tanzania inaweza kufaidika sana kutokana na vita hivi kama wataalam wetu wanaweza kuwa wabunifu!
 
Kwani Urusi haitaki kujitanua na kutawala dunia? Wanataka ila wamefilisika ndiyo maana wanashindwa. Enzi ya vita baridi Warusi walijitanua mpaka huku Afrika na walikuwa na vikaragosi wao madarakani wakina Lumumba, Samora, Joshua Nkomo, Dos Santos, Sam Nujoma na wengine.
 
Hiyo ni large scale, hii inaanzia kwenye ngazi ya familia zetu nyingi ukiwa mdogo kiumri au kiuchumi ushauri wako kwa waliokuzidi ambao muda mwingine huwa ni msaada kwako huonekana kama fujo au kelele na lazima uombe kabla upate ruhusa kushauri... Nchi zetu za Africa hakuna ya kujilinganisha kwa lolote na Russia kuanzia uchumi, ulinzi hadi utawala bora na hata tuungane nothing we can do... kwa hiyo hapo viongozi wetu kukaa kimya nadhani ni best option.
 
Yes
 

Inanishangaza 2022 bado mawazo yetu ya kwanza ni 'misaada'

NINACHOIOMBA SERIKALI YANGU NI HIKI - ndio tubaki neutral, sio vita vyetu wala siasa zetu. Ila hebu tucheze mchezo aliocheza mzungu kwetu miaka nenda miaka rudi - kutajarikia majanga yetu.

Tanzania tuna gesi, tuna uwezo wa kulima ngano nk ... serikali inahitaji kuvamia masoko wazi yalioachwa na hawa wanaopigana, tuingie mikataba ya miaka kadhaa. Ama gesi yetu inamtosha mchina na sisi tu?
 
China, india nk pia ni tegemezi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…