Vipi wake zetu wangekuwa kama mdada wa tangazo la Tigo?

Ndio mama sema mie leo nna buku 5 tu! Fanya maajabu bas.[emoji23][emoji23][emoji23]
Yule Kaka anaonekana kabisa ni mkweli na mwaminifu kwa mkewe ndio maana hata alivyomwambia mkewe mkewe alimuelewa.
Hakuna mwanamke atashindwa kumuelewa mwanaume wa aina ile.
Sasa tukija upande wenu nyie Kaka zetu vichomi na wadanganyifu..mwanamke gani atakubali kuwa vile kwa wanaume waongo waongo? Huyo mwanamke hayupo,labda zezeta
 
Kuwa mwaminifu si inategemea na huyo unaemfanyia uaminifu. Sasa mwanamke mpole mnyenyekevu na muelewa unaanzaje kumdanganya.

Mwanamke anajua kunata na biti sio wale kasuku mapenzi ukiwa uko njema tu siku ukifulia unatangazwa na makelele hata ndani hapakaliki.
 
Ningeua mtu,mwanamke yule anauza mechi halafu anadanganya eti,,tuliza honey...
 
Wao wanachokifanya akiwa na pesa anakuwa kunguru asiye fugika na siku akifulia anakuwa njiwa [emoji23][emoji23]
 
Acheni uongo..
Kila siku mpo kwenye Uzi wa kimasikhara halafu mnasema ni waaminifu.

Hata kea mwanamke ni hivyohivyo, Mwanaume mjanja mjanja hapaswi kufanyiwa vile..

Nyie hampo Kama yule mwanaume wa lile tangazo,kwahiyo kumtaka mwanamke wa vile ni ndoto zenu za kusadikika.
 
Inashangaza sana, mtu kamtoa kwao kamaleta kwake, hivi kama anafanyiwa mazuri anaanzaje kuwa hovyo? Maranyingi wake hubadilika kulingana na mdudo unavyopigwa
Ndiyo
Hakuna mwanamke anaweza kuwa mkorofi kwa mwanaume mtulivu.
Ujanja ujanja wao ndio huwa unawabadilisha wanawake.
 
Ndiyo
Hakuna mwanamke anaweza kuwa mkorofi kwa mwanaume mtulivu.
Ujanja ujanja wao ndio huwa unawabadilisha wanawake.
Ndiyo hivyo, ujanja utasikia eti wanapenda vipande vipande [emoji23][emoji23] sasa aliyewadanganya mwanamke yeye anapenda vizima vizima nani? Wao wakigeuziwa vibao haraka sana kutafuta panga haa haaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…