Yoda toka uache skul ambapo vipindi vya dini vilikuwepo umekuwa huru na muda mwingi tuu umegundua nn cha maana ambacho wasoma bible na quruan hawajakigundua??
Serikali haina dini ila watu wake wana diniSio kazi ya serikali kuhakikisha wasiokuwa na dini wanaipata dini.
Katika maisha kila jambo lina muda wake na maana yake hata likiwa dogo kiasi gani so relax
Wale waliofanikiwa kupata elimu ya darasani angalau ya darasa la saba na kuendelea watakumbuka vipindi vya dini ambavyo vilitengwa rasmi kulingana na madhehebu mbalimbali na wanafunzi wote ni lazima kuhudhuria katika vipindi hivyo.
Mara nyingi vipindi hivi huwa Ijumaa kuanzia muda wa saa nne ili kuwapa fursa waislamu kwenda msikitini kwa sababu mara nyingi wao huwa hawatumii madarasa kuswali katika vipindi vya dini kama wenzao Wakristo.
Wakati mjadala wa tija elimu yetu ukiwa mkali bungeni na mtaani ipo haja ya kuliangazia pia jambo hili na kuona kama kuna tija yeyote kuwa na hivi vipindi.
Ukiangalia kwa makini utagundua vipindi hivi vya dini havina tija yoyote kwa wanafunzi zaidi ya kuwachukulia muda wao ambao ungweza kutumika katika mambo mengine muhimu kama sanaa za uchoraji, uchongaji, kuimba, kuogelea, ushonaji n.k
Ni wakati sasa mamlaka zinazohusika na elimu zitoe muongozo wa vipindi hivi kufutwa na kuongeza mambo mengine secular au kupunguza muda wa wanafunzi kukaa darasani.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Tuanzishe cha historia ya MAGUFULI.
Hapa mie nakazia, hili la kulazimisha wanafunzi wote kwenda kwenye vipindi vya dini, sijawahi kuelewa kwa kweli.Hata wapagani ni raia kamili na wana haki zote katika hii nchi. Kuna shule zinalazimisha kwa viboko wanafunzi wote waende kwenye vipindi vya dini. Hii sio sahihi.
Wee nae una mawazo mfu na duni, kwahiyo dini ndo inazuia mtu kuwa shoga?Mwanao akiwa shoga ndio utajua umuhimu wa hofu ya Mungu.
Kumbuka kumcha Bwana/Mungu ni chanzo cha maarifa.
Maarifa yote chanzo chake ni Mungu.
Ipo sana hasa shule za bweni.Sio kweli,hakuna mwanafunzi anayelazimishwa kwenda kwenye vipindi vya dini.
Naungana na wee, uko sahihi sana.Kuna wengine wengi walikuwa na tabia mbovu sana, tena wakiwa viongozi wa dini shuleni.
Shule inaendeshwa kwa sheria na taratibu kama mwanafunzi hazifuati kuna adhabu zake zimeainishwa, sio kazi ya vipindi vya dini kudumisha amani, utulivu na utaratibu shuleni.
Hakika umenena na ndio ukweli wenyewe, ubarikiwe sana.Watu badala ya kujibu hii mada kwa hoja wanaanza kuleta nonsense na personal attacks.
Alafu hawa wanaopiga promo hapa tabia zao na dini ni tofauti trust me asilimia 90 ya wote waliocomment kuhusu vipindi vya dini vimewasaidia na blahblah wapo kwenye ule uzi wa kula tunda kimasihara.
Na wao ndio walikuwa wakitongozana na kufanya ngono hukohuko shule baada ya kutoka kwenye hivyo vipindi vya dini.
Wewe unayesoma hapa na mfuasi wa dini nafsi yako yenyewe inakwambia ukweli.
Haya ndio mazao ya dini Unafiki na Uvivu wa kufikiri hata uwe na PhD.
hivi vipindi havina faida wala impact yoyote kwa wanafunzi tabia chafu, uhuni, ngono zembe, mimba za utotoni, uvutaji bangi na ujeuri uko palepale.
Pia serikali haina dini, kwani hujui hili?
Ni kazi ya nyumba za dini, shule za dini, na kwingineko sio shule za serikali.Mojawapo wa faida za vipindi vya dini katika shule za msingi na sekondari ni kuwajengea utamaduni wa kutambua na kuvumilia itikadi za dini/imani zingine. Ndiyo maana tunaweza kuwa na staha dhidi ya imani ya mwingine.
Sio wakati huo tyuh, hadi sasa hivi ni lazima wanafunzi wote kuhudhuria vipindi vya dini, hili jambo sio sahihi kabisa.Shule zote nilizosoma ilikuwa ni lazima kuhudhuria vipindi vya dini, na viranja walikuwa wanawawinda wanafunzi waliokuwa hawaendi kwenye hivyo vipindi. Pia walimu walikuwa wanacharaza sana bakora wakikuta nje ya kipindi wakati wenzako wakiwa wanaendelea na kipindi.
Kwa wanafunzi wasiotaka kwenda kwenye hivyo vipindi waachwe wajisomee au wakacheze uwanjani.
Nakazia hapa.Mashahidi wa YEHOVA hawashiriki vipindi vya dini shuleni,wamepata hasara gani? Lakini wao ndio wanaongoza kwa heshima kwa kila mtu.
Serikali haina dini basi swala la dini ziachiwe taasisi za dini. Kwani mashahidi watoto wao heshima na biblia wanajifunzia wapi?