Vipindi vya dini katika shule za msingi na Sekondari za Serikali vifutwe

Vipindi vya dini katika shule za msingi na Sekondari za Serikali vifutwe

Kulazimishana au kulazimisha watu kuamini hiki au kile sio ustaarabu..., vilevile kuwanyima fursa watu kuamini / kujifunza wanachokiamini au kupata elimu ya imani hii au ile pia sio ustaarabu...

Cha maana tusilazimishane wala imani yako au yake isiwe kero kwa huyu au yule..., kila mtu kwa nafasi yake
 
Uko sahihi mkuu
Mashahidi wa YEHOVA hawashiriki vipindi vya dini shuleni,wamepata hasara gani? Lakini wao ndio wanaongoza kwa heshima kwa kila mtu.

Serikali haina dini basi swala la dini ziachiwe taasisi za dini. Kwani mashahidi watoto wao heshima na biblia wanajifunzia wapi?
 
Hii ni bullying. Inabidi bill of rights ifundishwe kuanzia darasa nne.
Hapa mie nakazia, hili la kulazimisha wanafunzi wote kwenda kwenye vipindi vya dini, sijawahi kuelewa kwa kweli.
 
Hii sio sawa kabisa
20210727_155743.jpg
 
Muda wa kuendeleza vipaji vya mtu ni wakati akiwa bado mtoto, huo muda ukishapita sio rahisi tena kuviendeleza. Taifa letu linazalisha watu wengi wasio na ujuzi/ufundi/ubunifu wowote wa ziada zaidi ya masomo waliyokariri darasani.

Badala ya kuwajazia watoto mambo ya dini shuleni ungewekwa mpango wa kuwapa ujuzi wa nje ya masomo.
Dini uleta ustaarabu kwenye Jamii
 
Ukwata imenilea nami nikaja kulea vijana kupitia Ukwata.

Binafsi nakiri kabisa vipindi vya dini shuleni vina msaada mkubwa sana.
 
Kama ishu ni muda bora kuviondoa vipindi vya michezo havina tija
Navyoona Mimi vipindi vya dini kwa wale wenye kutaka kujifunza dini wahudhurie na wale wasiohitaji wasilazimishwe kwa namna yoyote ile iwe kwa viboko au kwa adhabu ya aina yoyote ile sio sawa kumlazimisha mtu kuamini kitu asichotaka kuamini
 
Bora umuambie anadhan ushoga unahusiana na dini, khaaah.
Anachanganya mambo huyu vipi kuhusu mashekhe wanaolawiti watoto madrasa , mapadre,makadrinali wanaolawiti watoto, wachungaji wanaolawiti watoto hao wote wanadini na wanafanya Mambo ambayo yeye anaamini wasio na dini ndio hufanya

# HAUITAJI DINI ILIKUJUA KUWA KUUA MTU ASIYE NA HATIA SIO SAHIHI ILA UNAHITAJI UTU TU ILIKUJUA KUFANYA HIVYO SIO SAHIHI MWISHO.
 

Wale waliofanikiwa kupata elimu ya darasani angalau ya darasa la saba na kuendelea watakumbuka vipindi vya dini ambavyo vilitengwa rasmi kulingana na madhehebu mbalimbali na wanafunzi wote ni lazima kuhudhuria katika vipindi hivyo.

Mara nyingi vipindi hivi huwa Ijumaa kuanzia muda wa saa nne ili kuwapa fursa waislamu kwenda msikitini kwa sababu mara nyingi wao huwa hawatumii madarasa kuswali katika vipindi vya dini kama wenzao Wakristo.

Wakati mjadala wa tija elimu yetu ukiwa mkali bungeni na mtaani ipo haja ya kuliangazia pia jambo hili na kuona kama kuna tija yeyote kuwa na hivi vipindi.

Ukiangalia kwa makini utagundua vipindi hivi vya dini havina tija yoyote kwa wanafunzi zaidi ya kuwachukulia muda wao ambao ungweza kutumika katika mambo mengine muhimu kama sanaa za uchoraji, uchongaji, kuimba, kuogelea, ushonaji n.k

Ni wakati sasa mamlaka zinazohusika na elimu zitoe muongozo wa vipindi hivi kufutwa na kuongeza mambo mengine secular au kupunguza muda wa wanafunzi kukaa darasani.
Yoda, Yoda Yoda hata kama umeshuhudia matengano mbalimbali etc, kaa tu ukijua kuwa moja kati ya kitu kinachoweza kuliunganisha na kulinyanyua taifa ni dini! yes Dini ya kweli inajenga sana tu

Tena mi ningeshauri uboreshaji huu;mkwamba badala ya kila watu kujitenga na kakikundi kao ka kidini, wanafunzi wote wangekuwa wanabaki madarasani mwao na kunakuwa na zamu ya kila kikundi kuwafundisha wenzao mazuri/uzuri wa dini yao. Kunakuwa na sheria[tayari ipo] ya kutokashifiana tu. Hapa tunajenga uvumilivu/tolerance na harmonization baina ya dini mbalimbali
 
Anachanganya mambo huyu vipi kuhusu mashekhe wanaolawiti watoto madrasa , mapadre,makadrinali wanaolawiti watoto, wachungaji wanaolawiti watoto hao wote wanadini na wanafanya Mambo ambayo yeye anaamini wasio na dini ndio hufanya

# HAUITAJI DINI ILIKUJUA KUWA KUUA MTU ASIYE NA HATIA SIO SAHIHI ILA UNAHITAJI UTU TU ILIKUJUA KUFANYA HIVYO SIO SAHIHI MWISHO.
Yaan wa TZ ukitaka kuwaweza waweke kwenye Dini, hata mwenye PhD anakua mbulula tyuuh, wanakera mnooo.
 
Sio sawa .sio wote ni watu wenye kuamini katika dini Kama wewe unaamini katika dini usiwalazimishe wengine waamini katika dini .hivyo hivyo Kama wewe hauamini katika dini usiwalazimishe wengine wasiamini katika dini

# SIO WATANZANIA WOTE NI WAKRISTO AU WAISLAMU MWISHO
Yaani wewe hamjajua vile ambavyo nipo na uwanda mpana utashangaa;

Yaani katika hivyo vipindi hata atheist nao wanaweza kupewa kuusema uzuri mazuri ya watu kuishi bila dini kama watakuwa nayo. Sikupendekeza watu fulani wakatazwe. La. Pendekezo langu lilikuwa tu ni sheria iwe kali kuzuia kukashifu dini nyingine. Technically atheist watabaki na mambo machache sana maana mara nyingi wao ni hamna/utupu wanasubiri hoja za wengine ndio wazipinge so wanaweza kuamua kutofundisha ila kuwa wasikilizaji
 
Atheist mnao mchango mkubwa tu tena mda mwingine mnafanya kazi ya MUngu bila kujijua. Unajua kazi ya kuzipinpointi errors/makosa katika ufikiri na mantiki zinazotawala kidini huwa ni kazi ya manabii!!

Hiyo ni kwa sababu watu waliozama katika kitu ni vigumu kuyajua makosa yao. You, it is harder to see the frame when you are in the picture.

Tuendelee na kazi watu wote wa Mungu😂😂
 
Shule zinapaswa kuwa sehemu za watoto kujifunza hesabu, sayansi, sanaa, historia na michezo. Dini wakajifunze makanisani, misikitini, mahekaluni na nyumbani kwao.
Yaani wewe hamjajua vile ambavyo nipo na uwanda mpana utashangaa;

Yaani katika hivyo vipindi hata atheist nao wanaweza kupewa kuusema uzuri mazuri ya watu kuishi bila dini kama watakuwa nayo. Sikupendekeza watu fulani wakatazwe. La. Pendekezo langu lilikuwa tu ni sheria iwe kali kuzuia kukashifu dini nyingine. Technically atheist watabaki na mambo machache sana maana mara nyingi wao ni hamna/utupu wanasubiri hoja za wengine ndio wazipinge so wanaweza kuamua kutofundisha ila kuwa wasikilizaji
 
Shule zinapaswa kuwa sehemu za watoto kujifunza hesabu, sayansi, sanaa, historia na michezo. Dini wakajifunze makanisani, misikitini, mahekaluni na nyumbani kwao.
Kuna kitu hujakitafakari kwa upana hapo. Kukiwa na sehemu moja ya kufundishana dini hiyo ni hatua nzuri kwenye kuelewana. Tena mimi sipendekezi dini ziungane. La. Ila kuwe na uelewano na check and balance.

Tunakubaliana katika hoja za kisayansi, kihistoria na kihesabu kwa sababu tunajifunza sehemu moja.
Fikiria tu mfano hawa watu wakijifunza historia nyingine wanaanza kuja oof waafrika waliwachukua waligundua hiki, sijui nani alikuwa mweusi kunakuwa hakuna mshikamano tena

Na sisi tunataka mshikamano wa kitaifa hapa. Mi ningekuelewa kama ungesema labda badala ya dini wafundishwe falsafa fulani itakayokuwa imeunganisha mazuri ya dini zote tulizonazo - This sasa will be the game changer
 
Yoda, Yoda Yoda hata kama umeshuhudia matengano mbalimbali etc, kaa tu ukijua kuwa moja kati ya kitu kinachoweza kuliunganisha na kulinyanyua taifa ni dini! yes Dini ya kweli inajenga sana tu

Tena mi ningeshauri uboreshaji huu;mkwamba badala ya kila watu kujitenga na kakikundi kao ka kidini, wanafunzi wote wangekuwa wanabaki madarasani mwao na kunakuwa na zamu ya kila kikundi kuwafundisha wenzao mazuri/uzuri wa dini yao. Kunakuwa na sheria[tayari ipo] ya kutokashifiana tu. Hapa tunajenga uvumilivu/tolerance na harmonization baina ya dini mbalimbali
Mmh!
 
Back
Top Bottom