Vipindi vya dini katika shule za msingi na Sekondari za Serikali vifutwe

Vipindi vya dini katika shule za msingi na Sekondari za Serikali vifutwe

Mtoa mada kama unatolea hoja shule za vijijini upo sahihi kwa asilimia elfumoja (1000%)
 
Huo ni mchango wa mtu ambae hana dini sizani kama huwa unaenda kumwabudu Muumba wako wewe bila shaka ni muumini wa vit vilefu wewe
Kwanini mnalzimisha mtu kuwa na dini? Ingependeza kama kila mtu akawa free kuamini kivyake.
Vipindi vya dini viwepo lakini isiwe kwa kulazimishwa.
 

Wale waliofanikiwa kupata elimu ya darasani angalau ya darasa la saba na kuendelea watakumbuka vipindi vya dini ambavyo vilitengwa rasmi kulingana na madhehebu mbalimbali na wanafunzi wote ni lazima kuhudhuria katika vipindi hivyo.

Mara nyingi vipindi hivi huwa Ijumaa kuanzia muda wa saa nne ili kuwapa fursa waislamu kwenda msikitini kwa sababu mara nyingi wao huwa hawatumii madarasa kuswali katika vipindi vya dini kama wenzao Wakristo.

Wakati mjadala wa tija elimu yetu ukiwa mkali bungeni na mtaani ipo haja ya kuliangazia pia jambo hili na kuona kama kuna tija yeyote kuwa na hivi vipindi.

Ukiangalia kwa makini utagundua vipindi hivi vya dini havina tija yoyote kwa wanafunzi zaidi ya kuwachukulia muda wao ambao ungweza kutumika katika mambo mengine muhimu kama sanaa za uchoraji, uchongaji, kuimba, kuogelea, ushonaji n.k

Ni wakati sasa mamlaka zinazohusika na elimu zitoe muongozo wa vipindi hivi kufutwa na kuongeza mambo mengine secular au kupunguza muda wa wanafunzi kukaa darasani.
Kasome objectives za education of secondary au primary education
 
Ikiwa mtu ni muumini wa dini fulani inamaana ataisoma na kuijua vizuri.

Hivyo unamaana gani unaposema kuichunguza dini?

Na ikiwa mtu anaweza kuikosoa dini anayoiamini si ndio maana yake inakasoro? hivyo hana haja ya kuendelea kuiamini.

Kuhoji napo ikiwa unahoji kutaka kujua sawa, ila kama unahoji kwa kuona sheria fulani ya dini yake haipo sahihi si tunarudi palepale kwenye kukosoa?
Kukichunguza kitu Ina maana kuujua undani wa hicho kitu mfano historia ya dini, dhumuni la kuanzishwa kwa dini, mapungufu yaliyo katika dini na faida zake Kama dini ili Mwisho wa siku penye kasoro parekebishwe ili kuifanya dini kuwa na usawa au ukamilifu.na sio kwamba kila kitu chenye kasoro tunapaswa kuitupa la hasha Bali tunapaswa kurekebisha hizo kasoro na kukifanya kuwa sawa
 
Ikiwa mtu ni muumini wa dini fulani inamaana ataisoma na kuijua vizuri.

Hivyo unamaana gani unaposema kuichunguza dini?

Na ikiwa mtu anaweza kuikosoa dini anayoiamini si ndio maana yake inakasoro? hivyo hana haja ya kuendelea kuiamini.

Kuhoji napo ikiwa unahoji kutaka kujua sawa, ila kama unahoji kwa kuona sheria fulani ya dini yake haipo sahihi si tunarudi palepale kwenye kukosoa?
Yah! Ni lazima pakosolewe pale palipo kosewa kwa sababu dini ni matokeo ya uanzishwaji na wanadamu wenyewe na siku zote Cha mwanadamu hakina ukamilifu
 
Yaani mtu aseme dini hii imetoka kwa Mungu ila hapa pamekosewa, naparekebisha.

Sasa hapo nani Mungu na nani kiumbe?

Nani aliyekamilika na nani mwenye mapungufu?

Nani aliyepatia na nani aliyekosea?

Nani mwenye elimu na nani mjinga?
Hakuna dini iliyotoka kwa Mungu hayo ni mahaba niuwe ya Baadhi ya watu tu dini zote ni kazi ya mikono na fikra za mwanadamu yeye mwenyewe kwa sababu kazi za fasihi zote za dini zimeandaliwa na mwanadamu mwenyewe hapa hapa duniani
 
Unadhani hilohalipo hivyo mbona kujirekebisha kupo kwingi tu kwenye misahafu na biblia? Kitu ambacho hakitabadilika ni kuwa tu Mungu ni mmoja ila haya mengine ya kimaisha na kijamii yanabadilika vizuri tu ntatoa mfano;

Tulianza tupo free tunakunywa pombe na tunalewa na sio dhambi.
Tukakatazwa kunywa pombe kwa wanaoswalisha kwanza
Ilipoonekana wanaosali wanakuja wamelewa ndiyo ikakatazwa wote kulewa wakiendakuswali
Baadae ilipoonekana vipi ikakatazwa sasa jumlajumla! Je? hayo sio mabadiliko kulingana na hali? Ukweli upo uliosimama na upo huu tunaoushi. Huu tunaoushi tunaubadilisha kulingana na jambo litakaloleta afya kwa mtu na jamii kwa ujumla. Ndio maana manabii wakija huwa wanakuja kutuweka sawa tulipokuwa tunakosea.

Mungu amekamilika lakini wanadamu tunayo mapungufu ndiyo maana check and balance lazima ziendelee
Sawa kabisa
 
Hakuna dini iliyotoka kwa Mungu hayo ni mahaba niuwe ya Baadhi ya watu tu dini zote ni kazi ya mikono na fikra za mwanadamu yeye mwenyewe kwa sababu kazi za fasihi zote za dini zimeandaliwa na mwanadamu mwenyewe hapa hapa duniani
Hapana mkuu....Quran ilishushwa
 
Huo mfano wako hayo mabadiliko ya sheria yalifanywa na Mwenyezimungu, pia tunaweza tusiseme ni mabadiliko maana jambo ni lilelile ila lilikatazwa kidogo kidogo.

Hebu nipe mfano wa jambo ambalo tunaweza kulirekebisha hivi sasa katika msahafu kulingana na hali ya sasa? au ambalo limebadilishwa?
Kupiga mawe wanawake wanaozini mpaka kufa , jino kwa jino , upanga kwa upanga saa hizi Kuna mahakama unaweza kumfungulia mshitakiwa wako kesi kuliko kujichukulia sheria mkononi
 
Wasioamini Mungu(atheists) huwa hawana mafundisho yoyote, labda ungesema waruhusu waganga wa jadi na matambiko.
Kama nchi Ni ya demokrasia basi waruhusu mafundisho ya atheists (wasioamini Mungu) pia kuwepo masculine.....ili kuwe Na usawa
 
Kwanini mnalzimisha mtu kuwa na dini? Ingependeza kama kila mtu akawa free kuamini kivyake.
Vipindi vya dini viwepo lakini isiwe kwa kulazimishwa.
Yaan hata nashindwa kuelewa.
 
Hapana mkuu....Quran ilishushwa
Hata kama tukiamua kukubali kuwa ndio hivyo bado kuna nafasi sasa ya kutumia akili zetu kuielewa ndiyo maana kuna ma Imamu. Najua ukweli huwa haujipingi so huna haja ya kuogopa uchambuzi.

Lakini pia ipo haja ya kuupata muktadha wa zama za kabla ya qurani [taurat/injil] wakati wa quran na baada ya quran ndio maana kuna vitu kama hadithi broh. So tukisema kurekebisha tuna maana kurekebisha hata uelewa kwa yale ambayo yapo sio kufuta kilichopo. Ni kama kutimiliza fulani hivi.
 
Back
Top Bottom