Mashahidi wa YEHOVA hawashiriki vipindi vya dini shuleni,wamepata hasara gani? Lakini wao ndio wanaongoza kwa heshima kwa kila mtu.
Serikali haina dini basi swala la dini ziachiwe taasisi za dini. Kwani mashahidi watoto wao heshima na biblia wanajifunzia wapi?
Hapa naungana na wewe upo sahihi, Ila vipindi vya dini kufutwa sioni usahihi wa ilo.Hata wapagani ni raia kamili na wana haki zote katika hii nchi. Kuna shule zinalazimisha kwa viboko wanafunzi wote waende kwenye vipindi vya dini. Hii sio sahihi.
Hapana haupo sahihi.Mtu asiye amini Mungu hawezi kuwa na wazo la kuboresha hata siku moja,.
Wapo wanaolazimishwa tena na viboko juuSio kweli,hakuna mwanafunzi anayelazimishwa kwenda kwenye vipindi vya dini.
Kama ishu ni muda bora kuviondoa vipindi vya michezo havina tijaHapana haupo sahihi [emoji35]
Dini uleta ustaarabu kwenye JamiiMuda wa kuendeleza vipaji vya mtu ni wakati akiwa bado mtoto, huo muda ukishapita sio rahisi tena kuviendeleza. Taifa letu linazalisha watu wengi wasio na ujuzi/ufundi/ubunifu wowote wa ziada zaidi ya masomo waliyokariri darasani.
Badala ya kuwajazia watoto mambo ya dini shuleni ungewekwa mpango wa kuwapa ujuzi wa nje ya masomo.
Bora umuambie anadhan ushoga unahusiana na dini, khaaah.Hapana kutokuwa shoga hakusababishwi na kuwa na hofu ya Mungu
Navyoona Mimi vipindi vya dini kwa wale wenye kutaka kujifunza dini wahudhurie na wale wasiohitaji wasilazimishwe kwa namna yoyote ile iwe kwa viboko au kwa adhabu ya aina yoyote ile sio sawa kumlazimisha mtu kuamini kitu asichotaka kuaminiKama ishu ni muda bora kuviondoa vipindi vya michezo havina tija
Anachanganya mambo huyu vipi kuhusu mashekhe wanaolawiti watoto madrasa , mapadre,makadrinali wanaolawiti watoto, wachungaji wanaolawiti watoto hao wote wanadini na wanafanya Mambo ambayo yeye anaamini wasio na dini ndio hufanyaBora umuambie anadhan ushoga unahusiana na dini, khaaah.
Yoda, Yoda Yoda hata kama umeshuhudia matengano mbalimbali etc, kaa tu ukijua kuwa moja kati ya kitu kinachoweza kuliunganisha na kulinyanyua taifa ni dini! yes Dini ya kweli inajenga sana tu
Wale waliofanikiwa kupata elimu ya darasani angalau ya darasa la saba na kuendelea watakumbuka vipindi vya dini ambavyo vilitengwa rasmi kulingana na madhehebu mbalimbali na wanafunzi wote ni lazima kuhudhuria katika vipindi hivyo.
Mara nyingi vipindi hivi huwa Ijumaa kuanzia muda wa saa nne ili kuwapa fursa waislamu kwenda msikitini kwa sababu mara nyingi wao huwa hawatumii madarasa kuswali katika vipindi vya dini kama wenzao Wakristo.
Wakati mjadala wa tija elimu yetu ukiwa mkali bungeni na mtaani ipo haja ya kuliangazia pia jambo hili na kuona kama kuna tija yeyote kuwa na hivi vipindi.
Ukiangalia kwa makini utagundua vipindi hivi vya dini havina tija yoyote kwa wanafunzi zaidi ya kuwachukulia muda wao ambao ungweza kutumika katika mambo mengine muhimu kama sanaa za uchoraji, uchongaji, kuimba, kuogelea, ushonaji n.k
Ni wakati sasa mamlaka zinazohusika na elimu zitoe muongozo wa vipindi hivi kufutwa na kuongeza mambo mengine secular au kupunguza muda wa wanafunzi kukaa darasani.
Yaan wa TZ ukitaka kuwaweza waweke kwenye Dini, hata mwenye PhD anakua mbulula tyuuh, wanakera mnooo.Anachanganya mambo huyu vipi kuhusu mashekhe wanaolawiti watoto madrasa , mapadre,makadrinali wanaolawiti watoto, wachungaji wanaolawiti watoto hao wote wanadini na wanafanya Mambo ambayo yeye anaamini wasio na dini ndio hufanya
# HAUITAJI DINI ILIKUJUA KUWA KUUA MTU ASIYE NA HATIA SIO SAHIHI ILA UNAHITAJI UTU TU ILIKUJUA KUFANYA HIVYO SIO SAHIHI MWISHO.
Yaani wewe hamjajua vile ambavyo nipo na uwanda mpana utashangaa;Sio sawa .sio wote ni watu wenye kuamini katika dini Kama wewe unaamini katika dini usiwalazimishe wengine waamini katika dini .hivyo hivyo Kama wewe hauamini katika dini usiwalazimishe wengine wasiamini katika dini
# SIO WATANZANIA WOTE NI WAKRISTO AU WAISLAMU MWISHO
Yaani wewe hamjajua vile ambavyo nipo na uwanda mpana utashangaa;
Yaani katika hivyo vipindi hata atheist nao wanaweza kupewa kuusema uzuri mazuri ya watu kuishi bila dini kama watakuwa nayo. Sikupendekeza watu fulani wakatazwe. La. Pendekezo langu lilikuwa tu ni sheria iwe kali kuzuia kukashifu dini nyingine. Technically atheist watabaki na mambo machache sana maana mara nyingi wao ni hamna/utupu wanasubiri hoja za wengine ndio wazipinge so wanaweza kuamua kutofundisha ila kuwa wasikilizaji
Kuna kitu hujakitafakari kwa upana hapo. Kukiwa na sehemu moja ya kufundishana dini hiyo ni hatua nzuri kwenye kuelewana. Tena mimi sipendekezi dini ziungane. La. Ila kuwe na uelewano na check and balance.Shule zinapaswa kuwa sehemu za watoto kujifunza hesabu, sayansi, sanaa, historia na michezo. Dini wakajifunze makanisani, misikitini, mahekaluni na nyumbani kwao.
Mmh!Yoda, Yoda Yoda hata kama umeshuhudia matengano mbalimbali etc, kaa tu ukijua kuwa moja kati ya kitu kinachoweza kuliunganisha na kulinyanyua taifa ni dini! yes Dini ya kweli inajenga sana tu
Tena mi ningeshauri uboreshaji huu;mkwamba badala ya kila watu kujitenga na kakikundi kao ka kidini, wanafunzi wote wangekuwa wanabaki madarasani mwao na kunakuwa na zamu ya kila kikundi kuwafundisha wenzao mazuri/uzuri wa dini yao. Kunakuwa na sheria[tayari ipo] ya kutokashifiana tu. Hapa tunajenga uvumilivu/tolerance na harmonization baina ya dini mbalimbali