Viroja: Siku ya kwanza kupanda ndege (ushamba mzigo)

Viroja: Siku ya kwanza kupanda ndege (ushamba mzigo)

Mbona kimo humu? Ni mengi yalitokea siku hiyo ila kubwa kuliko yote usiku sikulala, lakini pia niliwahi kuliko kiumbe yeyote yule ,si wanasemaja 2hr? Basi mimi 5hrs before nilikuwa pale.

Utamu wa ndege haujawahi mwacha mtu, na ukubwa huu ndege nimepanda mara kibao ila naona vioja haviishi.

Mwaka jana kuna sehem nilikuwa naenda basi niko airport kuelekea dar basi kuna msanii mmoja wa kile nae kalikuwa kanaelekea dar amefika pale alikuwa kananukia perfume kali balaa kalipopita kila mmoja airport alitamani ajuwe ni perfume gani kapaka.

Nikasema hapana hii chimbo ya hii perfume naijuwa nikampigia mwarabu huyu kaka anauzaga perfume za kupima akikuchanganyia perfume lazima ukubali.

Basi si ndo akaniambia huyu msamii wakati anaelekea airport alipitia dukani kwake akasetiwa ndo akaelekea airport.

Nikajisemea nextime airport nzima watanikoma[emoji23][emoji23][emoji23]

Juzi tu kakatokea ka safari ka chap dar,nikampigia mwarabu siku mbili kabla nikamuekeza kesho kutwa nipitie kwakwe anichanganyizie ya kupandia ndege[emoji2][emoji2][emoji2] akanambia siku hiyo nikivaaa nisipake chochote,ile muda naenda nipitie kwake.

Nikafata maelekezo ,nikamwambia staki iwe kali lakini nataka airport nzima waulize niwaachie no. Mweeeeee alinichanganyizie perfume 4 chap nikaelekea airport. Siku hizi siwahi sana na mimi najichelewesha kidogo[emoji1787]
Kwanza nilianza kumkomesha alonipeleka, pili tumefika tu wale wakaka wanakuja kutupokea mizigo nilisikia " dada unanukua"

Kwenye line ya ukaguzi nilikuwa naona watu wanaangaika kuniuliza. Ndani kuna sehem kama 3 za ukaguzi wale wadada kila mtu aliniuliza napaka perfume gani, mmoja nilimwachia no ya mwarabu.

Yeyote alonisalimmia siku hiyo kwa kunikumbatia basi mwaka mzima hiyo nguo alokuwa anaivaa hatopakaga perfume.

Mimi ile nguo nilokuwa nimevalia siku ile hata niifue vip itachukuwa miaka mitano perfumu ile kuisha.

Tangu nijuwe kwa mwaramu. Ni mwenye wa kwenda kupimiwa vichupa, leo nanukia hivi ,kesho vile.
Niseme tu pilikapilika za kupanda ndege naona kwangu hazitoisha maana kila ninapopanda naona kama vile ni mara ya kwanza.

Kuna wakati nilikuwa nawaza nivae kisuti matata maana wale wadada wa air tanzania wengine hata hawapendezagi, ila kuna wengine zile uniform zinawakaa balaa.ila baadae nikawaza huu uzi wanaopanda ndege wanavaa simple sio unavaa suti kama vile unaenda mahakamani [emoji2][emoji3][emoji3]

Ndege oyeeeeeee!!!
Unanikumbusha...kuna mchungaji alikuja airport na suti ya wachungaji wa vijinini alikaguliwa hadi biblia watu walicheka sana alivyokuwa na wenge
 
Unanikumbusha...kuna mchungaji alikuja airport na suti ya wachungaji wa vijinini alikaguliwa hadi biblia watu walicheka sana alivyokuwa na wenge
Ahaaaa Muwege mnatuchukulia hata tu video. Airport vioja haviishagi wewe waweza kuwa unapanda kwa mara ya 1000 ila wanaopanda kwa mara ya kwanza hawakosagi.

Udumu huu uzi
 
Kuna mtu alipiga magoti Amsterdam wakati wanaunga ndege waende switz. Haya ni maneno waliokuwa karibu walimsikia akisema.

"Eh baba! ushukuriwe kwa kunifikisha huku juu mbinguni baba! duniani dhiki na shida nyingi baba! Mweh ndaga mwalafyale mweh"
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 

Nakumbuka ilikuwa Mwaka 2008 mwezi Juni nilikuwa naenda kikazi Lusaka, Zambia basi sijui hili wala lile kwenye tiketi iliandikwa saa ya ndege kuondoka saa 12 asubuhi (ndege ndo inapaa) mimi nikajipa kama dakika 20 kutoka home Tabata mpaka Airport, nikidhani ni kama Mabasi ya Mkoani pale Ubungo stendi duuh ile kufika nikaambiwa muda umeisha daah! Nilichokaje. But taratibu nikajifunza muda wa kufika airport, vitu visivyoruhusiwa kubeba kwenye ndege.

**NEW DEVELOPMENT
Mwezi Juni 2015 nilipata safari ya kwenda CAMEROON (kwa hisani ya Watu wamarekani USAID) sasa tukiwa huko tukalipwa posho kwa hela ya huko Central African Franc sasa nikazibana nije kubadilishia Bongo nafika bongo Bureau De Change zote hawabadilishi hizi pesa yaani nmepagawa sijui nikazitupe Coco maana....

****MPYA ya 2016

Mwezi Januari nilienda NEW DELHI duuh pale airport hakuna sijui kutangaza wala nini ni KIMYA KIMYA tu ukisubiri matangazo utastukia ndege ishakuacha.

View attachment 336440
HAKIKA USHAMBA MZIGO!

Huu Uzi ungetungiwa kitabu kabisa, kiwe moja ya Vitabu vya Fasihi kwa wanafunzi wa Sekondari.

Ni kati ya nyuzi murua kwa kuelimisha na kuburudisha.
 
Natamani ningekutana na huu Uzi kabla ya June 2021. Ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kupanda ndege. Nilipokuja kuusoma kwa mara ya kwanza, nafikiri mwanzoni mwa mwaka Jana(2022) kama siyo mwishoni mwa mwaka 2021, nilicheka sana. "Washamba" wanafanana. Kama ningeusoma kabla, ningepata maarifa ambayo yangesaidia kupunguza "ushamba"

Ilikuwa Alhamisi Usiku, 30/06/2021. Nilikuwa natoka Zanzibar kwenda Dar es Salaam kwa ndege ya ATCL.

Alfajiri ya siku hiyo, nilipigiwa simu na mmoja wa watu wangu wa karibu lakini sikuipokea. Nilihisi kuwa pengine huenda kashafahamu kuwa siku hiyo napanda ndege. Sikutaka aniambie chochote kuhusiana na ndege, asije akanivunja moyo kusafiri kwa ndege. Nilikuja kumpigia baada ya kufika Dar es Salaam.

Nilifika mapema sana Airport. Ilibidi nikae kwa massa kadhaa kwenye mgahawa ulio pale Uwanjani, nafikiri unaitwa JAMBO CAFE, kusubiria muda wa kuripoti kuwadia.
Nikiwa hapo, nilianza kuingiwa na hofu, kiasi cha kuishiwa na hamu niliyokuwa nayo ya kupanda ndege. Nilitamani kuahirisha. Hata hivyo, nilijipa moyo, nikajisemea moyoni liwalo na liwe lakini ndege lazima nipande.

Nilitamani nikae kiti cha dirishani ili niwe ninachungulia mandhari ya ardhini nikiwa angani, na kwa bahati nzuri, ikawa hivyo. Nilikaa kiti cha dirishani, lakini siku "enjoy" kama nilivyokuwa nikitarajia. Nilitishwa na umbali tuliokuwepo angani.

Dakika chache baada ya ndege kuruka, nilipochungulia chini kupitia dirishani, taa za majengo zilionekana kwa mbaali. Sikuwa na hamu ya kuendelea kufanya hivyo. Niliamua kukafunga kabisa kale "kapazia" ka dirishani ili nisiendelee kupaona chini. Ule umbali ulikuwa unanitisha. Ila abiria wenzangu walikuwa na amani sana. Kuna waliokuwa wakichezea simu zao na wengine kompyuta pakato zao, na wengine walikuwa wakipiga stori kwa furaha kabisa. Mimi nilikaa kimya, kama vile sitaki kuongea, kumbe nilikuwa nimegubikwa na hofu.

Mkao na ukimya wangu, ulikuwa kama wa mtu anayetafakari jambo kwa kina . Lakini sikuwa natafakari, nilikuwa nimezama katika maombi, japo yalikuwa ni maombi ya kimya kimya. Niliomba safari nzima, kuanzia ndege iliporuka uwanja wa ndege wa Abeid Amani Karume Hadi ilipotua Dar.

Wakati ndege inatua, nilifikiri huo ni uwanja mwingine huko Zanzibar, kwa hiyo baada ya kushusha au kupandisha abiria wengine, tungeendelea na safari hadi Dar. Lakini kumbe sivyo, tulikuwa tumewawasili jijini.


Tulipotangziwa kuwa hapo tulipo ni Uwanja wa Ndege wa Dar Es Salaam, kwangu ilikuwa ni furaha isiyo na kifani.
Sikutarajia ingetuchukua muda mfupi kiasi hicho. Tulitumia kama dakika kumi na mbili hivi angani. Mimi nilitarajia tungekaa angani kwa dakika kama 30 hivi.

Njiani baada ya kutoka Airport, nilikuwa nikitabasamu na wakati mwingine kucheka mwenyewe, kila nilipokumbuka heka heka za kuanzia maandalizi hadi nilipokuwa kwenye ndege.

Bora tu ilikuwa ni one way, pengine kesho yake ningetakiwa kupanda tena ndege, sijui ingekuwaje. Huenda ningekataa. Hata wiki mbili baadaye, bado sikuwa tayari. Hofu bado ilikuwepo.

Ilinichukua zaidi ya mwezi mmoja hiyo hali ya hofu kunitoka. Ilipoisha, shauku nayo ilirejea.

Kwa kweli, usafiri wa ndege ni mzuri sana!

Hongera zake mkuu Clasi! Uzi wake umekuwa burudani na "darasa" kwa wengi, Mimi nikiwa mmoja wao!!!
 
Nilisoma vizur ndio maana nikajibu labda ewew ndio usome upya.,...kwa kukusaidia nilimqoute aliesema kuhusu mkusanyiko wa mabati na injini ubungo akimaniisha mabasi,,,nikamuulize kwani ndege Ni mkusanyiko wa chuma Hadi awe na uhakika wa usalama kiasi hicho!!!!nachoamini hakuna usafir salama duniani Kama siku ya ajali imefika..kikubwa kumuomba mungu na kuwa waangalifu tu.
Usafiri wa ndege ndio usafiri salama kuliko wowote
 
Mje mpokee mabegi yenu 😁
C3AE5CC2-C34C-476E-A27C-F44CDDFE28BF.jpeg
 
Mimi natamani nikipanda ndege niende hata huko bafuni/ chooni nikaone kulivyo ila cha ajabu sijawahi kwenda. Maana nikikaa tu muda kidogo nasikia matangazo ya kushuka ati tumefika.

Ati nimeisha kaa niamke wanione naenda huko naonaga kama sio ustaarabu najikuta siendi.
Hivi kukoje huko toilet kwenye ndege?
 
Mimi natamani nikipanda ndege niende hata huko bafuni/ chooni nikaone kulivyo ila cha ajabu sijawahi kwenda. Maana nikikaa tu muda kidogo nasikia matangazo ya kushuka ati tumefika.

Ati nimeisha kaa niamke wanione naenda huko naonaga kama sio ustaarabu najikuta siendi.
Hivi kukoje huko toilet kwenye ndege?
Zichange uende New Zealand hamu itakuisha kmmk
 
Mimi natamani nikipanda ndege niende hata huko bafuni/ chooni nikaone kulivyo ila cha ajabu sijawahi kwenda. Maana nikikaa tu muda kidogo nasikia matangazo ya kushuka ati tumefika.

Ati nimeisha kaa niamke wanione naenda huko naonaga kama sio ustaarabu najikuta siendi.
Hivi kukoje huko toilet kwenye ndege?
Choo ni kidogo...

Niliingia ndege ilitua Zanzibar kutokea KIA to Dar....Na mimi ni kama wewe..nikasema leo wacha nikavione....kwanza na Mlango ukataka kunizingua[emoji1787]

Mimi kwenda Chooni ndege inatembea hapana aisee...Naona itadondoka
 
Back
Top Bottom