franktemu123
JF-Expert Member
- Mar 3, 2011
- 1,406
- 1,475
Mkuu hii Lazima itakua intercontinental unapasua mabara mengine ya Afrika kama si Australia huko basi itakua mbali sanaHii ni kwasababu labda unapanda za safari fupi ndani ya saa 1 na madakika, ukipanda ya masaa mengi hutaogopa kwasababu baada ya masaa kadhaa utakuwa ukiona watu wakipishana kwenda uani.
Mimi pia nilizoea hizi safari za ndani so nilikuwa naona sio ustaarabu kuamka amka na kwenda uani, nilipoanza kusafiru safari ya masaa mengi uoga uliishia pale hasa niliposafiri kwa masaa 13 mfululizo
Bara to bara mkuu sema ni ile ya kubadilisha ndege ndio ufike uendakoMkuu hii Lazima itakua intercontinental unapasua mabara mengine ya Afrika kama si Australia huko basi itakua mbali sana
Masaa13 safarini, si unakaa mpaka makalio yanawaka moto!Hii ni kwasababu labda unapanda za safari fupi ndani ya saa 1 na madakika, ukipanda ya masaa mengi hutaogopa kwasababu baada ya masaa kadhaa utakuwa ukiona watu wakipishana kwenda uani.
Mimi pia nilizoea hizi safari za ndani so nilikuwa naona sio ustaarabu kuamka amka na kwenda uani, nilipoanza kusafiru safari ya masaa mengi uoga uliishia pale hasa niliposafiri kwa masaa 13 mfululizo
[emoji23][emoji23][emoji23]😀 Hii Ilishanikutaga, Nikiwa Na Mwenzangu, Ilibidi tudanganye ni Wanasheria, Suti Kuubwaa! Kumbe Hatuna Lolote, Ushamba tu
toilet papers, kama unakunya kutu ngumu ya kuganda km ugali wa muhogo utajua hujui...😂Eee mbona haya makunwa sasa kama hakuna maji unajitawaza na nini jamani?
Ni kweli, ni raha sana, hasa kwa aliyezoea.Mkuu mbona safari ya Zanzibar..dar ni fupi sana na ndege wala haipai juu sana?.kutoka Karume ukipaa dakika 10 hivi unaiona Dar, na kushuka ni ndani ya dk 15 hadi 20 hivi.
Kwa airbus toka Zanz to Dar ni dakiko 15 tu.
Naam kukaa dirishani raha sanaView attachment 2610712
Mkuu kwanza kutoka Zanzibar to Dar ni dakika 15 tu, Pili ndege inapaa futi 5000 tu ukilingalisha na Futi 25,000 hadi futi 38,000 anga za kimataifa, sasa huko si utakufa??🤣🤣🤣Natamani ningekutana na huu Uzi kabla ya June 2021. Ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kupanda ndege. Nilipokuja kuusoma kwa mara ya kwanza, nafikiri mwanzoni mwa mwaka Jana(2022) kama siyo mwishoni mwa mwaka 2021, nilicheka sana. "Washamba" wanafanana. Kama ningeusoma kabla, ningepata maarifa ambayo yangesaidia kupunguza "ushamba"
Ilikuwa Alhamisi Usiku, 30/06/2021. Nilikuwa natoka Zanzibar kwenda Dar es Salaam kwa ndege ya ATCL.
Alfajiri ya siku hiyo, nilipigiwa simu na mmoja wa watu wangu wa karibu lakini sikuipokea. Nilihisi kuwa pengine huenda kashafahamu kuwa siku hiyo napanda ndege. Sikutaka aniambie chochote kuhusiana na ndege, asije akanivunja moyo kusafiri kwa ndege. Nilikuja kumpigia baada ya kufika Dar es Salaam.
Nilifika mapema sana Airport. Ilibidi nikae kwa massa kadhaa kwenye mgahawa ulio pale Uwanjani, nafikiri unaitwa JAMBO CAFE, kusubiria muda wa kuripoti kuwadia.
Nikiwa hapo, nilianza kuingiwa na hofu, kiasi cha kuishiwa na hamu niliyokuwa nayo ya kupanda ndege. Nilitamani kuahirisha. Hata hivyo, nilijipa moyo, nikajisemea moyoni liwalo na liwe lakini ndege lazima nipande.
Nilitamani nikae kiti cha dirishani ili niwe ninachungulia mandhari ya ardhini nikiwa angani, na kwa bahati nzuri, ikawa hivyo. Nilikaa kiti cha dirishani, lakini siku "enjoy" kama nilivyokuwa nikitarajia. Nilitishwa na umbali tuliokuwepo angani.
Dakika chache baada ya ndege kuruka, nilipochungulia chini kupitia dirishani, taa za majengo zilionekana kwa mbaali. Sikuwa na hamu ya kuendelea kufanya hivyo. Niliamua kukafunga kabisa kale "kapazia" ka dirishani ili nisiendelee kupaona chini. Ule umbali ulikuwa unanitisha. Ila abiria wenzangu walikuwa na amani sana. Kuna waliokuwa wakichezea simu zao na wengine kompyuta pakato zao, na wengine walikuwa wakipiga stori kwa furaha kabisa. Mimi nilikaa kimya, kama vile sitaki kuongea, kumbe nilikuwa nimegubikwa na hofu.
Mkao na ukimya wangu, ulikuwa kama wa mtu anayetafakari jambo kwa kina . Lakini sikuwa natafakari, nilikuwa nimezama katika maombi, japo yalikuwa ni maombi ya kimya kimya. Niliomba safari nzima, kuanzia ndege iliporuka uwanja wa ndege wa Abeid Amani Karume Hadi ilipotua Dar.
Wakati ndege inatua, nilifikiri huo ni uwanja mwingine huko Zanzibar, kwa hiyo baada ya kushusha au kupandisha abiria wengine, tungeendelea na safari hadi Dar. Lakini kumbe sivyo, tulikuwa tumewawasili jijini.
Tulipotangziwa kuwa hapo tulipo ni Uwanja wa Ndege wa Dar Es Salaam, kwangu ilikuwa ni furaha isiyo na kifani.
Sikutarajia ingetuchukua muda mfupi kiasi hicho. Tulitumia kama dakika kumi na mbili hivi angani. Mimi nilitarajia tungekaa angani kwa dakika kama 30 hivi.
Njiani baada ya kutoka Airport, nilikuwa nikitabasamu na wakati mwingine kucheka mwenyewe, kila nilipokumbuka heka heka za kuanzia maandalizi hadi nilipokuwa kwenye ndege.
Bora tu ilikuwa ni one way, pengine kesho yake ningetakiwa kupanda tena ndege, sijui ingekuwaje. Huenda ningekataa. Hata wiki mbili baadaye, bado sikuwa tayari. Hofu bado ilikuwepo.
Ilinichukua zaidi ya mwezi mmoja hiyo hali ya hofu kunitoka. Ilipoisha, shauku nayo ilirejea.
Kwa kweli, usafiri wa ndege ni mzuri sana!
Hongera zake mkuu Clasi! Uzi wake umekuwa burudani na "darasa" kwa wengi, Mimi nikiwa mmoja wao!!!
Mdege za wenzetu tamu ValeMasaa13 safarini, si unakaa mpaka makalio yanawaka moto!
Sent from my vivo 1906 using JamiiForums mobile app
Uchukue tahadhari unapoflash huwa inatoka sauti kauli usijezimia😂Nikipanda tena lazima niende sema kwenda ndege inatembea mmmh labda ikitua ndo nitakimbia chap.
Oh kumbe ni vidogo? Basi hapo hakuna kusindikizana.
Uko sahihi, unaweza kuwa mzoefu but kuna siku mkikutana na hewa mbona utatamani ushukeSema ndege wakati mwingine haizoeleki...inategemea umekutana na dhoruba gani..ndo maana ukiangalia kila mtu kama yuko kwenye mawazo...
I see [emoji4]Mdege za wenzetu tamu Vale
Bora ulikuwa na mwalimuSikuwahi kupata changamoto maana aunt yangu alinielekeza taratibu masharti yote kuanzia kg ngapi nibebe na pia hand luggage ya kuingia kwenye ndege vitu kama perfume lotion ujazo upi haruhusiwi na nikifika transit Nairobi na nikifika OR Tambo South Africa uwanja wao mkubwa nifate watu na vibao sehemu za kuchukua begi Taxi ziko wapi na nauli rand ngapi alinipa address basi akiniona mlangoni tu akashangaa sana.
Endelea kumshukuru Mungu na kumuomba Mungu. Kuna mambo, utamuona aunt yako muongo!Sikuwahi kupata changamoto maana aunt yangu alinielekeza taratibu masharti yote kuanzia kg ngapi nibebe na pia hand luggage ya kuingia kwenye ndege vitu kama perfume lotion ujazo upi haruhusiwi na nikifika transit Nairobi na nikifika OR Tambo South Africa uwanja wao mkubwa nifate watu na vibao sehemu za kuchukua begi Taxi ziko wapi na nauli rand ngapi alinipa address basi akiniona mlangoni tu akashangaa sana.
Kwa nini nife mkuu? Maadam hizi za ndani hazinipi hofu tena, naamini hata za masafa marefu hazitanisumbua. Ikimpendeza Mungu, nitakuwa na safari ya kulivuka bara la Afrika siku za usoni, na naamini nitakuwa comfortable sana. Shuhuda za wadau kwenye huu uzi zimenitoa matongo tongo kwa kiasi kikubwa. Sitakuwa na sababu ya kuogopa. "Nimechagua" kutokuogopa.Mkuu kwanza kutoka Zanzibar to Dar ni dakika 15 tu, Pili ndege inapaa futi 5000 tu ukilingalisha na Futi 25,000 hadi futi 38,000 anga za kimataifa, sasa huko si utakufa??🤣🤣🤣
Natamani na mimi nije kuimiliki ya kwangu binafsi. I believe, there's one day called YES!Ndege raha
Mbona vitisho sasa! 🤣Uchukue tahadhari unapoflash huwa inatoka sauti kauli usijezimia😂
Kwa kweli nashukuru Mungu changa moto nilokutana nayo ni uhamiaji wa Tz kunisumbua kuniona punda nahojiwa sana kwanini nasafiri sana na kipato gani niliwaambia tu sio swali la kuuliza mwanamke😁changamoto nyingine nchi za watu nikionekana Mtanzania tu naambiwa kaa pembeni napelekwa room napekunyuliwa begi mwili wangu mpaka sehemu za Siri kwa kweli ilikuwa ni usumbufu na udhalilishaji mpaka nikachukia kusafiri nikatulizana Hadi mwanangu mdogo alishapekuliwa labda nimetia drugs kwenye diaper.Bora ulikuwa na mwalimu
Aisee!!! Nahisi kukasirika lakini sijui nimkasirikie nani! Pole sana!Kwa kweli nashukuru Mungu changa moto nilokutana nayo ni uhamiaji wa Tz kunisumbua kuniona punda nahojiwa sana kwanini nasafiri sana na kipato gani niliwaambia tu sio swali la kuuliza mwanamke😁changamoto nyingine nchi za watu nikionekana Mtanzania tu naambiwa kaa pembeni napelekwa room napekunyuliwa begi mwili wangu mpaka sehemu za Siri kwa kweli ilikuwa ni usumbufu na udhalilishaji mpaka nikachukia kusafiri nikatulizana Hadi mwanangu mdogo alishapekuliwa labda nimetia drugs kwenye diaper.