Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Inaumiza sana nguvu kazi ya taifa inazidi kupoteasi watoto tuh pia vijana wanakimbiza sana hiyo midoli
unaweza kuta jitu liko katikati ya town unahisi anapiga mishe ya mana kumbe kajifungia kwenye banda la kukimbiza mdoli
ETI Wanaongoza kwa kulipa kodi!!!!!Kheri ya mwaka mpya wakuu?
Mimi binafsi mtaani nilipopanga na ninapoishi naitwaga mshamba na washkaji sababu nikitoka asubuhi kwenye mishe zangu kariakoo kurudi saa3 usiku au saa2 nikiwahi.
siku ya mwaka mpya hapa mtaani kuna vijana wengi walioshindwa kusoma, wasio na kujua nini wanataka kwenye maisha yao.
Hawa vijana walinunua visungura vingi sana sijui idadi kamili. Walianza kunywa mida ya saa4 usiku mpaka saa6 mwaka mpya unafika kilichokuwa kikiendelea ni kusikia tu k....ma wewe, unato...bwa na mengine mengi.
Baada ya muda kidogo tukasikia kama ugomvi tukajua kama kawaida yao, ugomvi ulipoendelea baadae tukasikia mmoja analia akasema UNANIUA!!
Kumbe yale matusi tuliyoyasikia na pombe zilizonywewa pale tayar zipo kichwani, wakawa wanabishana kuhusu mademu, mmoja mkubwa wao pale akamchoma visu vtatu tumboni.
Baada ya kuona mwenzake anagugumia maumivu dogo akakimbia na pikipiki ya jamaa mmoja pale mtaani huwa anampaga dogo deiwaka.
Kumbe pikipiki imefungwa gprs wakamkuta dogo kaanguka mtaroni na pikipiki imeharibika sababu ya ulevi kuwa mwingi kichwani.
Dogo yupo nyuma ya nondo mpaka sasa, pamoja na wenzake na mwenzao mmoja kachomwa visu na amepoteza maisha.
Naomba nitoe rai kwa vijana wenzangu, hizi kismart, visungura vinamaliza sana vijana.
sasahiv wanapewa mpaka ya kupima ili waendelee kumaliza vijana.serikali yetu tunaomba iliangalie hili hivi vidude vinamaliza vijana mitaani.
Victim wengi wakiwa ni vijana miaka kuanzia miaka15_ 25
Sikatai kweli ni starehe na nimekua nikiongea baadhi na vijana wenzangu ila nimeishiwa kuonekana mshamba.
Serikali yetu kuna vitu huwa vinapotezea lakini vijana ndio taifa la kesho, pombe ni starehe hatukatai lakini hii sasa ni harmful
Naomba vyombo husika na serikali litazame hili kwa jicho la tatu.
Nawasilisha.
Mtibeli mimi ni fan wako mkubwa sana hapa JF na hata wewe unafahamu kwa kukuweka 5 bora yangu.
Unafikiri nini kifanyike mkuu?
Inaumiza sa naMfumo ndy unataka hivyo
Vijana waconcerntrate kwenye mitungi,miziki+starehe +mipira
Wakati wenzenu na familiaaa zao wanasongaaa
Ova
Hivi visungura ndio vinini?? Nasikia wanavisema sema humu hata sielewi ni vitu gani!
Mie sijui kisungura ni nini, naomba picha ya kisungura pleaseKula sungura mkuu
Vinafaninia hivi mkuu hicho kinauzwa mpaka nusu.Mie sijui kisungura ni nini, naomba picha ya kisungura please
Hapana mkuu kuna tukio kama hili limetokea huko?Upo kigamboni?
Mkuu hii ni ipi ?Unaisahau AMBIANCE