Vita dhidi ya Corona: Mikusanyiko ya watu isiyo lazima isitishwe, misongamano idhibitiwe ili kuepusha madhara makubwa zaidi

Muda umefika kwa serikali kusitisha makundi ya maombezi kama ilivyositisha makundi mengine, makundi haya huambatana na watu kuanguka na kugalagala chini vinginevyo hao manabii na mitume watakusanya watu ili kuwaponya na kuwakinga na Corona.
Siloam washasema wameifuta Corona kwenye uso wa dunia
 

Hahaaaa yawezekana aisee 😄
Shame!

Kesho Serikali wakijitokeza wakasema daladala zisijaze watu mtajitokeza hapa kushangilia, Yan nyinyi akili zenu sijui zipoje
 
Mimi mkigusa bia tu hapo ndiyo nitajua mnahitaji ugomvi usio wa lazima, maana nitaichukia CCM Kuzidi covid yenyewe

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Leo Kuna jamaa ana lorry kaniambia anarudi na mzigo wote wa pombe kwa sababu pub wameukataa wanasema hakuna wateja
Hapa ni sehemu moja karibu na Heathrow [emoji23]


Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Acha akili hizo wewe, health guidelines zinazotolewa Kote Ulimwenguni wakati huu ni kwa ajili ya Watanzania tu?
Usiwe kama digidigi inaonekana bila serikali kukuambia ununue pedi utumie kwenye siku zako huwezi kununua.

Kuna mambo hayahitaji muongozo wa serikali unajiongeza tu mwenyewe na kuona usalama wako. Halafu serikali ni watu sio Rais wala Waziri mkuu nyie watu mnapaswa kuwa na tahadhari kabla ya kusikia matamko ya viongozi sio ukae kulaumu serikali kuwa haijakuruhusu kujisaidia haja kubwa.
 
Sheria iwe ni level seat kwa muda , kama kufunga shughuli zote kwa muda itashindikana.
 
Jankoliko,
Ieleweke nimesema hii ni tetesi tu.
Huyu dada alijua tangia ulaya kuwa ni muathirika. Kwa akili za kawaida alitakiwa ajisalimishe kwa matibabu kwenye hospitali za huko Ulaya ambazo zina vifaa tiba na utalaamu mkubwa kuliko hizi za kwetu bongo. Ndiyo maana tetesi zinasema alikuwa katumwa (kalipwa pesa nyingi) ili aje kuleta maangamizi nchini kwetu, yeye akiwa raia wa Tanzania tusingalimshuku sana.

Baada ya kuvuka vizingiti vya pale KIA angaliweza kabisa kuendelea kuusambaza huo ugonjwa kwa kujichanganya hususani kwenye mikusanyiko ya watu kama kwenye masoko, super markets, mikutano ya kisiasa ya hadhara, kukutana na watu maarufu wakiwemo viongozi wa vyama vya kisiasa na kadhalika. Na angaliweza kufanya hivyo kwa siku nyingi tu maana afya yake ilikuwa nzuri. Na kama afya yake ingeanza kuteteleka baadaye angaliweza kurudi Ubeligiji kwa matibabu mazuri zaidi.

Hakufanya hivyo bali alienda kujifungia hotelini (self quaranteen) na kesho yake kujisalimisha hospitalini. Kitendo hiki ndicho ninakiita uzalendo ulimurudia.

Unaona hata kwa kufanya huo uzalendo ndani ya siku moja tu maelfu ya watu inawezekana alishawaambukiza. Ikumbukwe kuwa ugonjwa huu hasa husambazwa haraka na mikono kugusa vitu mbali mbali. Virusi hivi huweza kuishi kwa siku nne kwenye maeneo (surfaces) zilizoguswa na mwenye virusi hivyo. Kwa mfano vitasa vya magari aliyoyagusa (ya huyo dreva na ya hao wakina Gumbo walioenda kumuchukua hapo hotelini), maeneo aliyogusa akiwa hotelini na hospitalini n.k.

lazima yaliendelea kuguswa na mikono ya watu mbali mbali na baadaye nao kwenda kugusa maeneo mengine nakadhalika. It spreads like fire. Kitendo cha kupeleka msafara mkubwa uliotumwa na mkuu wa mkoa kwenda kumchukua muathirika ni kitendo cha kulaaniwa. Daktari aliyemshauri mkuu wa mkoa kufanya hivyo anapaswa kuwajibishwa. Kitendo hiko kimechangia kusambaza virusi hivyo.
 
Kuna mtu kanitaarifu hapa huko aliko vyuo vimefungwa mpaka september.
 
Wewe ni mbinafsi mno...unajifikiria mwenyewe kwa vile unakiSwift chako basi Unajiona Uko salama...kama Arteta kaambukizwa who are you? Complete idiot
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…