Katika kupambana na corona, Tanzania tumekuwa tofauti sana na wenzetu kiasi kwamba unajiuliza kama ile dhana ya dunia ni kijiji ina-apply katika nchi yetu.
Tumekuwa very selective katika kuamua ni aina gani ya mikusanyiko ipigwe marufuku na ipi iachwe wakati ukweli unabaki mikusanyiko ni mikusanyiko bila kujali nature ya mikusanyiko hiyo.
Kwa mfano,tunajidanganya sana kwa kujifanya wacha Mungu kwa kutozuia mikusanyiko katika nyumba za ibada kwa imani eti tusioogope huu ugonjwa mpaka tukashindwa kwenda kumuomba Mungu wakati unaweza kumuomba Mungu hata nyumbani kwako na akakusikiliza hasa katika kipindi hiki cha hili janga.
Sasa, wakati tumeacha kudhibiti baadhi ya mikusanyiko huku idadi ya wagonjwa ikiongezeka,ni jambo la kushangaza kuona tumeshindwa hata kuzuia mikusanyiko kwenye mabaa ambapo watu wanajazana na huku wakinywa kwa pamoja katika meza moja kanakwamba hatuna tishio la corona.
Kwa hakika tunashangaza sana, ila muda si mrefu tutavuna tunachopanda kama Taifa.