Vita ya Gaza: Uchumi wa Israel wasinyaa kuliko ilivyotarajiwa

Ezekiel was to use the poop as fuel for his cooking fire. The symbolic purpose was to teach Israel that they too would eat unclean food, as the human excrement would defile the food
Unayapata kitabu gani maelezo hayo uliyoyaandika ?
 
hilo linatuhusu nini sisi watu wa Manzese aisee. wanajuana wenyewe hukohuko middle east.
 

HOW tall?


"It seems to be universally held that the Clementines are based upon the doctrines of the Book of Elchasai or Helxai, which was much used by the Ebionites.


The contents of it were said to have been revealed by an angel ninety-six miles high to a holy man Elchasai in the year 100 ..."


The Catholic Encyclopedia, IV.
 

Kuna vifungu vingi katika Agano Jipya vinavyokana uungu wa Yesu.

Kwa mfano, katika Mathayo 19:17, Yesu alimjibu yule aliyemtambulisha yeye kama ni “Mwalimu mwema” kwa kusema “Akawaambia, Kwani kuniuliza habari ya wema? Aliye mwema ni mmoja…”

Kama Yesu amekataa kuitwa “mwema”, na ameeleza kuwa ni mungu pekee ndiye aliye mwema wa kweli, naye kwa uwazi kabisa ameashiria kuwa yeye si Mungu.

Katika Yohana 14:28, yesu alikuwa anasema: “Mlisikia ya kwamba mimi niliwaambia, Naenda zangu, tena naja kwenu. Kama mngalinipenda, mngalifurahia kwa sababu naenda kwa Baba; kwa maana Baba ni mkuu kuliko mimi.” Kwa kusema “Baba” ni mkuu kuliko yeye, Yesu amejitenganisha na Mungu.

Pia katika Yohana 20:17, Yesu alimwambia Mariam Magdalene awaambie wafuasi zake:

"Yesu akawaambia, Usinishike, kwa maana sijapaa kwenda kwa Baba. Lakini enenda kwa ndugu zangu ukawaambie, ninapaa kwenda kwa Baba yangu naye ni Baba yenu, kwa Mungu wangu naye ni Mungu wenu.”

Yesu amemwashiria Mungu kuwa ni “Baba yangu na Baba yenu” amesisitiza zaidi, tofauti yake na Mungu.

Zaidi ya hayo, Yesu amemwashiria Mungu kuwa ni “Mungu wake”, hakutoa nafasi kwa yoyote kudai kiujanja ujanja kuwa Yeye Yesu ndiye Mungu.

Katika baadhi ya maandiko ya Paulo, yaliyochukuliwa na kanisa kuwa ni matakatifu, Yesu anaonyeshwa kuwa ni “mtu” ametofautiana na kutengana na Mungu.

Katika 1 Timotheo 2:5, Paulo anaandika

“Kwa sababu Mungu ni mmoja, na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja, Mwanadamu Kristo Yesu.
 
Alhaa sio Mungu wake Wakristo!! Mtume aliuguwa akafa!! Na ameshuudia Yesu Kurudi Duniani!!!na Ametaja mama ake Yesu zaidi ya mara 100 kwenye Quraan! SALAAM MARIA UMEJAA NEEMA NA YESU MZAO WA TUMBO LAKO AMEBARIKIWA🙏

1. Mwanzo na Mwisho

Katika kitabu cha Ufunuo 1:8, inadokezwa kuwa Yesu amesema yafuatayo kujihusu yeye mwenyewe:

“Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, asema Bwana Mungu, aliyeko na aliyekuwako na atakayekuja, Mwenyezi”.

Hizi ni sifa za Mungu.

Kwa hiyo, hapa Yesu, kwa mujibu wa Wakristo wa mwanzo, anadai uungu.

Hata hivyo, hayo maneno yaliyotajwa hapo juu ni kwa mujibu wa toleo la King James Version.

Ama katika toleo la Revised Standard Version, wasomi wa Biblia wanarekebisha makosa ya kitafsiri na wameandika:

“Mimi ni wa mwanzo na wa Mwishom” asema Bwana Mungu,..”.

Pia, marekebisho yalifanywa katika toleo la New American Bible iliyotayarishwa na Wakatoliki.

Tafsri ya aya hiyo imerekebishwa ili iwekwe katika muktadha wake ulio sahihi kama ifuatavyo: “Bwana Mungu anasema: “Mimi ni wa mwanzo na wa Mwisho…” Ikiwa na marekebisho haya, inadhihirika kuwa, mstari huu ulikuwa ni maelezo ya Mungu na sio maelezo ya Mtume Yesu.
 
Jagina !! Nyie mnasali na Majini sisi Majini ni Laana na atujiusisi nao ata ! Quraan ina Injili, Zaburi na vitabu vingii tuu vya kwenye Bibilia!!!Mtume wenu watu walimkataaa yaani na mpaka leo Nyie ndo Tatizo Duniani!

Maisha ya kabla ya Kristo

Mstari mwingine unaotumiwa sana ili kuunga mkono uungu wa Yesu ni Yohana 8:58:

“Yesu akawaambia, amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko.”

Mstari huu umechukuliwa na kuashiria kuwa Yesu alikuwepo kabla ya kudhihiri kwake duniani.

Uamuzi uliofikiwa kutokana na mstari huo ni kuwa Yesu lazima awe Mungu, kwa kuwa kuwepo kwake kumetangulia tarehe ya kuzaliwa kwake duniani.

Hata hivyo, dhana ya kuwepo kabla ya kudhihiri kwa mitume, na kwa watu wengine, ipo katila vitabu vyote viwili, Agano la Kale, vilevile katika Quran.

Yeremia anajielezea mwenyewe katika Kitabu Cha Yeremia 1:4-5 kama ifuatavyo:

“Neno la BWANA lilinijia, kusema, Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.”

Nabii Suleimani anaripotiwa katika Mithali 8:23-27, ya kuwa amesema,

“Nalitukuka tokea milele, tangu awali, kabla haijawako dunia. Wakati visipokuwako vilindi nalizaliwa, Wakati zisipokuwako chemchemi zilizojaa maji. Kabla milima haijawekwa imara, Kabla ya vilima nalizaliwa. Alipokuwa hajaiumba dunia, wala makonde, Wala chanzo cha mavumbi ya dunia; Alipozithibitisha mbingu nalikuwako…"

Kwa mujibu wa Ayubu 38:4 na 21, Mungu amemtambulisha Nabii Ayubu kama ifuatavyo:

“Ulikuwa wapi nilipoiweka misingi ya nchi? Haya! Sema, kama ukiwa unafahamu.”

Katika Quran, Sura ya Al-A’aaraf, 7:172, Mungu anaeleza kuwa mwanadamu alikuwepo kiroho kabla ya kuumbwa ulimwengu wa kimwili.

تَ 􀑧 هِمْ أَلَسْ 􀑧 ى أَنفُسِ 􀑧 هَدَهُمْ عَلَ 􀑧 تَهُمْ وَأَشْ 􀑧 "وَإِذْ أَخَذَ رَبُّكَ مِن بَنِي آدَمَ مِن ظُهُورِهِمْ ذُرِّيَّ
بِرَبِّكُمْ قَالُواْ بَلَى شَهِدْنَا أَن تَقُولُواْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ إِنَّا كُنَّا عَنْ هَذَا غَافِلِينَ."

"Na pale Mola wako Mlezi alipowaleta katika wanaadamu kutoka migongoni mwa kizazi chao, na akawashuhudisha juu ya nafsi zao, akawaambia: Je, Mimi si Mola Mlezi wenu? Wakasema: Kwani! Tumeshuhudia. Msije mkasema Siku ya Kiyama sisi tulikuwa tumeghafilika na hayo." Al-A’aaraf, 7:172

Kwa hiyo, maelezo ya Mtume Yesu, “Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko”. Hayawezi kutumiwa kuwa ni ushahidi wa uungu wake.

Katika muktadha wa Yohana 8:54, Yesu amedaiwa kuwa ametamka kuhusu ujuzi wa Mungu kwa Mitume yake, ambayo inatangulia tarehe ya kuumbwa kwao katika ulimwengu huu.
 
Mtume alikuwa anapata Maono mpaka akivaa Chupi ya Mkewe!! Hapa lete haya inayokataa hii katuni

Mwana wa Mungu

Ushahidi mwingine uliotumiwa kwa ajili ya uungu wa Yesu ni kule kutumiwa sifa ya “Mwana wa Mungu” kwa Yesu.

Hata hivyo, kuna sehemu nyingi katika Agano la Kale ilipotumiwa sifa hiyo kwa watu wengine.

Mungu alimwita Israeli (Nabii Yakubu) “Mwanawe” pale alipomuelekeza Mtume Musa aende kwa Firauni katika Kutoka 4:22-23,
“Nawe umwambie Farao, BWANA asema hivi, Israeli ni mwanangu mimi, mzaliwa wa kwanza wangu; nami nimekuambia, Mpe mwanangu ruhusa aende, ili apate kunitumikia…”

Katika 2 Samweli 7:13-14, Mungu anamwita Nabii Suleimani Mwanawe,

"Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa jina langu, nacho kiti cha enzi cha ufalme wake nitakifanya imara milele. Mimi nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwanangu…"

Mungu alimuahidi Nabii Daudi kumfanya mwanawe katika Zaburi 89:26-27:

“Yeye ataniita, Wewe baba yangu, Mungu wangu na mwamba wa wokovu wangu. Nami nitamjalia kuwa mzaliwa wangu wa kwanza, Kuwa juu sana kuliko wafalme wa dunia.”

Malaika wanachukuliwa kuwa ni “wana wa Mungu” katika kitabu cha Ayubu 1:6,

“Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za BWANA, Shetani naye akaenda kati yao”.

Katika Agano Jipya, kuna marejeo mengi ya “mwana wa Mungu” ya watu wengine wasio Yesu.

Kwa mfano, pale mtunzi wa Injili kwa mujibu wa Luka amewaorodhesha wahenga wake hadi kwa Adamu, ameandika: Luka 3:38 “Wa Enoshi, wa Sethi, wa Adamu, wa Mungu”.

Baadhi ya watu wanadai kuwa kile cha kipekee kilichopo kwa Yesu ni kuwa yeye ndiye mwana wa pekee wa kuzaliwa Mwana wa Mungu, huku hao wengine ni “wana wa Mungu tu.”

Hata hivyo, Mungu ananukuliwa akimwambia Mtume Daudi, katika Zaburi 2:7,

“Nitaihubiri amri, BWANA aliniambia, Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa.”

Pia inapaswa ijulikane kuwa hakuna hata sehemu moja katika Injili ambapo Yesu alijiita yeye mwenyewe kuwa yeye hasa ndiye “mwana wa Mungu”.

Badala yake, amenukuliwa kuwa amekariri kujiita “Mwana wa Adamu” (mfano Luka 9:22) kwa mara zisizohesabika.

Na katika Luka 4:41, kwa hakika amekataa kuitwa “Mwana wa Mungu”:

“Pepo nao waliwatoka watu wengi, wakipiga kelele na kusema, Wewe u Mwana wa Mungu. Akawakemea, asiwaache kunena, kwa sababu walimjua kuwa ndiye Kristo.”

Kwa kuwa Wayahudi wanaamini kuwa Mungu ni Mmoja, na hana mke wala mtoto kwa maana halisi yoyote ile, ni wazi kuwa ibara “mwana wa Mungu” kwa Wayahudi ina maana ya “Mtumishi wa Mungu tu” yaani mtu aliye karibu na Mungu, kwa sababu ya huduma yake ya kiimani, akiwa kama mtoto kwa baba yake.

Wakristo waliokuja kutoka katika historia za kuwa walikuwa ni Wagiriki au Warumi, baadaye waliitumia vibaya istilahi hiyo.

Kwani katika urithi wao, “mwana wa Mungu” inamaanisha mungu ana mwili au mtu aliyezaliwa kwa muungano wa kimwili kati ya mungu mwanamume na mwanamke.

Wakati Kanisa lilipoacha msingi wa Kiyahudi, lilitwaa dhana ya kipagani ya “mwana wa Mungu”, ambayo kwa ukamilifu, ilikuwa ni tofauti na matumizi ya Kiyahudi.

Kwa hiyo, matumizi ya istilahi “mwana wa Mungu” inafaa ifahamike kuwa ni alama ya ufahamu ya kisemintiki yenye maana “mtumishi wa Mungu”, na sio katika ufahamu wa kipagani wa uhalisi wa kuwa kinda la Mungu.

Katika Injili nne, Yesu anarekodiwa akisema: “Heri wapatanishi; Maana hao wataitwa wana wa Mungu.” Mathayo 5:9.
 
Mungu wa Waislam sio Mungu wa Wakristo!! Ni Mungu wawili tofauti. Mnasali na Mashetani(MAJINI) Mama ake Yesu Bikira maria Amemponda Shetani na Miguu yake

Kwa maana Mungu hawezi kujaribiwa na uovu, na yeye mwenyewe hamjaribu mtu yeyote

Mtu anaweza kuuliza ni nini kimetokea juu ya hatua hiyo, ni kitu gani kinamfanya Mungu kudai hamjaribu mtu yeyote.

Hapa kuna sehemu ya kupendeza, tusome Mwanzo 22 mstari wa 1 ambayo inasema:


Gen 22:1 Ikawa baada ya mambo hayo Mungu alimjaribu Ibrahimu, akamwambia, Ibrahimu! Naye akasema, Tazama, mimi hapa.

Sasa na tuangalie mistari yote miwili tena, Yakobo 1 13:15, na Mwanzo 22:1 na kuziweka pamoja:

Yakobo 1:13-15 : “Mtu ajaribiwapo, asiseme, Ninajaribiwa na Mungu; kwa maana Mungu hawezi kujaribiwa na maovu, wala yeye mwenyewe hamjaribu mtu ye yote. Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa. Kisha tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi; na dhambi ikiisha kukoma, huzaa mauti."

Linganisha na Mwanzo 22:1

Gen 22:1 Ikawa baada ya mambo hayo Mungu alimjaribu Ibrahimu, akamwambia, Ibrahimu! Naye akasema, Tazama, mimi hapa.


Nadhani umejionea wenyewe, tunaona wazi Mungu akimjaribu Ibrahimu kwenye Mwanzo 22:1, ndiyo Yakobo 1:13-15 inadai kwamba Mungu hamjaribu mtu!

je, Mungu hujaribu au Mungu hamjaribu?
 

Pamoja na Mungu

Wale wanaodai kuwa Yesu alikuwa Mungu, wanashikilia kuwa yeye hakuwa Mungu aliyetengeka, bali ni mmoja na ni Mungu yule yule mwenye mwili.

Wao wanaunga mkono imani hii kutokana na mstari wa 30 wa Injili kwa mujibu wa Yohana, sura 10, ambayo ndani yake Yesu anaripotiwa kuwa amesema, “Mimi na Baba ni kitu kimoja.”

Nje ya muktadha, mstari huu unaashiria uungu wa Yesu.

Hata hivyo, pale Wayahudi walipomtuhumu kwa kudai uungu, kwa kutegemea sentesi hiyo, Yohana 10:34

“Yesu akawajibu, Je, haikuandikwa katika Torati yenu ya kwamba, Mimi nimesema, Ndinyi miungu? Ikiwa aliwaita miungu wale waliojiliwa na neno la Mungu;"

Amewabainishia, kwa mfano wa maandiko unaojulikana sana kwao, kuwa yeye alikuwa anatumia lugha ya kistiari ya manabii ambayo haipaswi kufasiriwa kwa kujipachika uungu yeye mwenyewe au kwa mtu mwingine yoyote.

Ushahidi zaidi unachukuliwa kutoka katika mstari wa kumi na wa kumi na moja wa Injili kwa mujibu wa Yohana, sura ya 14, pale watu walipomtaka Yesu awaonyeshe Baba, naye inaaminiwa alisema:

"Husadiki ya kwambi mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu; Hayo maneno niwaambiayo mimi siyasemi kwa shauri langu; lakini Baba akaaye ndani yangu huzifanya kazi zake. Mnisadiki ya kwambi mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu; la! Hamsadiki hivyo, sadikini kwa sababu ya kazi zenyewe.”

Ibara hizi zingeashiria uungu wa Yesu, kama sehemu iliyobakia ya Injili hiyo hiyo inapuuzwa.

Hata hivyo, aya tisa baadaye, katika Yohana 14:20, pia Yesu anarekodiwa akiwaambia wanafunzi wake,

"Siku ile mtatambua ya kuwa mimi ni ndani ya Baba yangu, nanyi ndani yangu, nami ndani yenu.”

Kwa hiyo, kama maelezo ya Yesu "Mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu; yanamaanisha kuwa yeye ni Mungu, basi vivyo hivyo iwe kwa wanafunzi wa Yesu.

Hii sentensi ya kiishara inamaanisha umoja wa lengo na sio umoja wa asili.

Tafsiri ya kiishara inasisitizwa zaidi katika Yohana 17:20-21, pale Yesu aliposema,

"Wala si hao tu ninaowaombea; lakini na wale watakaoniamini kwa sababu ya neno lao. Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ili ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma.”
 

"Hapo mwanzo kulikuwa na Neno"

Huenda ‘ushahidi’ wa uungu wa Yesu ulionukuliwa sana ni Yohana 1:1 na 14,

“Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, na Neno alikuwa Mungu… Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli.”

Hata hivyo, maelezo haya hayakutolewa na Yesu Kristo, wala hayakuhusishwa naye na mtunzi wa Injili kwa mujibu wa Yohana.

Hivyo, mistari hii haiundi ushahidi wa uungu wa Yesu, hasa hasa kuzingatia shaka inayoshikiliwa na wasomi wa Kikristo juu ya Injili ya Nne.

Wasomi wa Biblia waliotunga Injili tano: “Picha mbili zilizochorwa na Yohana na muhtasari wa injili (yaani Injili ya Mathayo, Marko na Luka) zote mbili haziwezi kuwa ubainifu wa kihistoria.

Neno lilohusishwa na Yesu katika Injili ya Nne limeundwa na wainjilisti kwa sehemu kubwa, na linaakisi mwendelezo wa lugha ya jamii ya Wakristo wa Kiyohana.

Neno la Kigiriki lilotumiwa na mtunzi wa Injili ya Nne asiyejulikana kwa “neno” ni logos.

Kwa kufanya hivyo, huyo mtunzi anamtambulisha Yesu kwa logos la wanafalsa wapagani wa Kigiriki, neno ambalo lilikuwa na lengo takatifu na thabiti lililojitokeza ulimwenguni, huyo mtunzi akalipangilia neno hilo na kulipa mfumo na maana.

Wazo la logos katika fikra za Kigiriki huenda linarejea nyuma, kwa uchache hadi kwa mwanafalsafa wa karne ya sita BC, Heracleitus, aliyependekeza kuwa, kulikuwa na logos ulimwenguni anayetenda kwa mwanadamu kulingana na nguvu ya hoja.

Baadaye, Stoics analitambulisha logos kuwa ni tendo, mantiki, na kanuni ya kiroho inayosambaa katika ukweli wote.89F90 Mwanafalsafa wa Kiyahudi anayeongea Kigiriki, Judaeus Philo wa Alexandria (15 BC -45 CE), amefundisha kuwa logos alikuwa ni mpatanishi baina ya Mungu na ulimwengu, kwa kuwa na sifa mbili za uwakala wa Mungu na ulimwengu, na kuwa na sifa mbili za uwakala wa viumbe na wakala wa ambaye kupitia kwake akili ya mwanadamu inaweza kumfahamu Mungu.

Maandiko ya Philo yalihifadhiwa na kutunzwa na kanisa, na kueneza ufunuo kwa mafundisho ya kistaarabu ya tiolojia ya kifalsafa ya Kikristo.

Aliacha mafundisho ya fikra za Kipilato wakichukulia logos (Neno) na kuliita “mtoto wa kwanza wa kuzaliwa na Mungu.”

Utambulisho wa Yesu kwa logos, uliendelezwa katika kanisa la kwanza ikiwa ni tokeo la majaribio yaliyofanywa na wanatiolojia wa kwanza wa Kikristo pamoja na watetezi kuielezea imani ya Kikristo kwa istilahi ambayo ingekuwa wazi kwa ulimwengu wa Wayunani.

Zaidi ya hayo, ilikuwa ni kuwavutia wasikilizaji wao na mtazamo wao kuwa Ukristo ulikuwa unashinda, au mrithi wa wale wote waliokuwa wanafalsafa bora wa kipagani. Kwa hiyo, katika kazi zao za utetezi na ubishani,

Mapadri wa Kikristo wa kwanza wameeleza kuwa Yesu alikuwa ni logos aliyekuwepo hapo kabla.

Neno la Kigiriki lililotumika kwa maana ya ‘Mungu’ katika hiyo ibara ni “na Neno lilikuwa kwa Mungu,” lipo katika mtindo wa “definite form- yaani mtindo uliowazi, au unaofahamika” batheos, Linalomaanisha “Huyo Mungu, au Mungu maalum”.

Hata hivyo, katika ibara ya pili “na Neno alikuwa Mungu”, neno la Kigiriki lililotumika kwa maana ya ‘Mungu’ katika ibara lipo katika mtindo wa “indefinite form- yaani mtindo usiowazi, au usiofahamika” tontheos, Linalomaanisha ‘mungu yoyote, yaani mungu asiyejulikana, au mungu yoyote asiye maalumu’.

Kwa hiyo, Yohana 1:1, kwa uwazi zaidi ilipaswa itafsiriwe, “Hapo Mwanzo kulikuwa na Neno, na hilo Neno lilikuwa kwa Mungu, na hilo Neno lilikuwa mungu mwingine.”

Kwa hiyo, kama hilo neno lilikuwa mungu mwingine kwa ufahamu wa kifasihi, itamaanisha kuwa kulikuwa na miungu miwili na sio mmoja.

Hata hivyo, katika lugha ya Kibiblia, neno ‘mungu – asiyefahamika’ linatumika kwa maana ya istiari ili kuashiria nguvu.

Kwa mfano, Paulo alimtaja shetani kuwa ni ‘mungu – asiyefahamika’ katika 2 Wakorintho 4:4,

"ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu."

Pia, Musa alitajwa kama ni ‘mungu – asiyefahamika’ katika Kutoka 7:1, "BWANA akamwambia Musa, Angalia, nimekufanya wewe kuwa Mungu kwa Farao; na huyo ndugu yako Haruna atakuwa nabii wako.
 
mungu wako kabebwa na shetani , anakwenda kuonyeshwa miji


View attachment 2918436
Usiqote Bibilia! Lete yaliomo kwenye Kitabu chako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…