Vita ya kisiasa baina ya Tanganyika na Zanzibar ipo wazi sasa

Vita ya kisiasa baina ya Tanganyika na Zanzibar ipo wazi sasa

Unamlaumu nan sasa? Nyerere ndio alilazimisha huo muugano.

You must be joking. Watanzania wenzangu tuwe tuna tabia ya kutafuta elimu na kujisomea. Hadithi za mitaani nyingi ni za kutunga.
Zanzibar imeungana na Tanganyika sababu ya matakwa ya wakubwa na mwitikio wa vita baridi. Haya mengine ya kumsikiliza sijui nani ambaye elimu yake kwanza ni questionable na facts hana, wala hajafanya research yoyote yanatufanya kuendelea kuwa wajinga
 
You must be joking. Watanzania wenzangu tuwe tuna tabia ya kutafuta elimu na kujisomea. Hadithi za mitaani nyingi ni za kutunga.
Zanzibar imeungana na Tanganyika sababu ya matakwa ya wakubwa na mwitikio wa vita baridi. Haya mengine ya kumsikiliza sijui nani ambaye elimu yake kwanza ni questionable na facts hana, wala hajafanya research yoyote yanatufanya kuendelea kuwa wajinga
Kwamba unapinga nyerere hakulazimishwa kulazimisha muungano?
Na kama ni hivyo sasa kwanini bara ndio wanakataa kuvunja muungano wakati zenji wao wameonesha nia ya kuukataa na hata kuanzisha harakati za uamsho na walipoishia tumeona?

Ushahidi waa mazingira
 
1722434333236.png

Kamanda Mkuu wa Idara Maalum ya Vikosi vya Serekali ya Mapinduzi Zanzibar,Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr Hussein Ally Mwinyi akikagua vikosi Maalumu.
 
Kwamba unapinga nyerere hakulazimishwa kulazimisha muungano?
Na kama ni hivyo sasa kwanini bara ndio wanakataa kuvunja muungano wakati zenji wao wameonesha nia ya kuukataa na hata kuanzisha harakati za uamsho na walipoishia tumeona?

Ushahidi waa mazingira

Kuna wakati tunajizima data. Ila kitu kibaya sana kwetu waafrika ni kuchukulia mambo magumu kirahisi rahisi. That is a sin and crime.

Kama hujui jambo, tafuta elimu from all angles ili uwe na balanced opinion. Kumsikiliza mtu mmoja na kuchukua anayosema ndio ukweli wote, ni kama ile hadithi ya mtu aliyepewa talanta moja akaifukia ardhini. Akitegemea boss wake atamuelewa
 
meanza kueleweka hadi ndani ya CCM. Ugomvi mkubwa wa Kinana, Makamba na wanaCCM wengi ni Tanganyika kutawaliwa na Rais kutokea nchi ya Zanzibar ambaye amekuwa dalali mkubwa wa kuuza rasilimali za Tanganyika.
Uwasilishaji na utetezi wa mada yako ni hafifu sana, pamoja na kwamba ni mada nzito hii.

Kwa mfano: unao ushahidi wowote wa kuonyesha unayo yaelezea katika huo mstari hapo juu, na uhusika wa hao ulio wataja katika kuidai Tanganyika?
 
Zenji ni nchi kamili kila kitu wanacho isipokuwa jeshi tunashare.
Hoja za watanganyika hudumazwa na njaa, kiongozi akishiba hawezi kamwe kuona udhaifu na madhara ya Muungano kwa Tanganyika lakini akiwa na njaa ataona kero nyingi sana za Muungano na kutamani kuhuishwa kwa Tanganyika.
Waathirika wakubwa wa Muungano ni vijana wa Tanganyika lakni wao ndiyo wanaukumbatia na kuutetea kuliko Wazenji.
Miaka ya hivi karibuni vijana wengi wameteuliwa na kuchaguliwa kuwa viongozi lakini wengi wao wameishia kuwa chawa badala ya kusaidia kuleta mabadiliko!
 
Wazanzibari always wamedumu na msimamo wao kwenye suala la muungano katika mazingira yoyote, kwanini nyinyi huwa munalalamikia muungano Raisi anapokuwa Mzanzibari tu? mbona wakati wa JPM hamkuwa mkilalamika?
Nyinyi sio kama hamtaki muungano, bali hamtaki viongozi wa serikali watoke Zanzibar. Ni ubaguzi tu, munaojifichia kwenye mgongo wa matatizo ya Muungano.

..vyama vya upinzani vimekuwa vikidai serikali 3 tangu vianzishwe.

..nitastaajabu ukinitajia walau chama kimoja cha upinzani kinachounga mkono serikali 2.

..kwa historia hiyo sio sahihi kusema Watanganyika wanaupinga muungano pale tu Rais wa muungano anapotoka Zanzibar.

..pia sio sahihi kudai Wazanzibari wanapinga muungano pale wakati Rais anatokea Tanganyika, akitoka Zanzibar wanaunga mkono muungano.

..sio sahihi wale tunaotaka marekebisho ktk muungano wetu kuanza kushutumiana, au kalaumiana, kwa Utanganyika au Uzanzibari wetu.

..tusipoteze focus ktk suala hili. Wanaolinda muungano huu wa serikali 2 ni genge la watawala wa Ccm. Na genge hilo lina watu toka Tanganyika na Zanzibar.
 
..tusipoteze focus ktk suala hili. Wanaolinda muungano huu wa serikali 2 ni genge la watawala wa Ccm. Na genge hilo lina watu toka Tanganyika na Zanzibar.
Hasa hasa toka Zanzibar, ambako hao CCM wanajuwa, bila mwamvuli wa CCM toka Tanganyika, CCM huko visiwani hawana uwezo wa kubaki madarakani.

Na hali hiyo ndiyo inayo fanya hata huku Tanganyika CCM ifanye kila inachoweza kufanya, ikiwa ni pamoja na kuiba kura/kulazimisha ushindi huku Tanganyika, kwa sababu bila CCM huo muungano kama ulivyo sasa hauwezekani.

Mkuu 'Joka', kwa mara nyingine nikuhimize/kukumbushe..., achana na hiyo fikra ya serikali 3. Serikali ni moja tu Tanzania.
 
Hasa hasa toka Zanzibar, ambako hao CCM wanajuwa, bila mwamvuli wa CCM toka Tanganyika, CCM huko visiwani hawana uwezo wa kubaki madarakani.

Na hali hiyo ndiyo inayo fanya hata huku Tanganyika CCM ifanye kila inachoweza kufanya, ikiwa ni pamoja na kuiba kura/kulazimisha ushindi huku Tanganyika, kwa sababu bila CCM huo muungano kama ulivyo sasa hauwezekani.

Mkuu 'Joka', kwa mara nyingine nikuhimize/kukumbushe..., achana na hiyo fikra ya serikali 3. Serikali ni moja tu Tanzania.

hicho kitu hakipo, ni either 3 au watu wagawane mbao
 
Kama Bara hawataki Rais kutoka Zanzibar ni Bora kugawana fito tuu Kwa sababu Haina maana ni upuuzi
Kwanza bara ni mdude gani? Wananchi wa Tanganyika useme ndio hawataki rais toka nchi ya Zanzibar hapo utaeleweka. Acha kutuita bara nchi ambayo hajawahi kuwepo dunia hii. Acheni dharau.
 
Zanzibar na Tanganyika ni nchi mbili tofauti kila moja ina Rais wake, jeshi lake, bendera yake, wimbo wa Taifa lake, benki kuu yake , passport yake, je bado tu hamuelewi?
Wameelewa kuwa wanatawaliwa na mtu wa inchi nyingine.
Walitolewa kwa mkoloni mzungu wamewekewa mweusi.
 
Mkuu 'Joka', kwa mara nyingine nikuhimize/kukumbushe..., achana na hiyo fikra ya serikali 3. Serikali ni moja tu Tanzania.
Hili la serikali 1 umelirudia sana, huenda kuna hoja. Tujadili kidogo
1. Ikiwa sasa hivi Wazanzibar hawataki hata hizo 2 hiyo moja unawezaje kuwaeleza?
2. Serikali 1 ni kwa masilahi gani ya Tanganyika? Kwamba bila Zanzibar , Tanganyika ina kipi cha kupoteza!

JokaKuu
 
Mama yuko makini, kazi yake ameimudu vizuri mno, makapi yote wanafki na vizabizabina na vibwengo na takataka zingine katupa kule, hongera sana Mama , ila Mama mbona virusi na mchwa wengine wasaka urais bado hujatupa kule?ujue wanakuharibia sana your good momentum and integrity.

Namuomba sana Bimkubwa atufikishie SGR Mwanza na Kigoma tu atakuwa kaifanyia nchi yetu jambo la kutukuka, nasi tutamuimba kwenye mchakamchaka milele, hao wawekezaji wengine ni minor issue. Iko siku ya kuwafurusha wote itafika kuleeee 2032 kama itaonekana ni wanyonyaji tu.
 
1. Makamu Mwenyekiti CDM Salim Mwalimu.
2. Dr Mwinyi Rais wa Zanzibar Mkuranga.
hayo ya Mwenyekiti Salim siyajui na inawezekana kabisa huyo ni wa bara amehamia tu Zanzibar.

Dr Hussen Mwinyi kwao Mkuranga, jamani someni historia ya Mzee Ali Hassan Mwinyi ameeleza vizuri sana
 
Hili la serikali 1 umelirudia sana, huenda kuna hoja. Tujadili kidogo
1. Ikiwa sasa hivi Wazanzibar hawataki hata hizo 2 hiyo moja unawezaje kuwaeleza?
2. Serikali 1 ni kwa masilahi gani ya Tanganyika? Kwamba bila Zanzibar , Tanganyika ina kipi cha kupoteza!

JokaKuu
Huu mjadala nautaka sana, na ninajuwa wewe na mimi hatupo mbali mbali kuhusu hili swala la huu muungano wetu.
Nikukumbushe pia, siyo muda kitambo sana tumejadili haya haya; hasa kuhusu "waZanzibar kutoutaka muungano", jambo ambalo hatukuafikiana juu yake.

Msingi wangu wa kutaka serikali moja ni ule ule, uliokuwepo tangu kuasisiwa kwa muungano wenyewe. Lengo lilikuwa kufikia serikali moja baada ya hofu za "kumezwa" kufifia.
Hoja yangu ni kwamba hiyo hofu ya Zanzibar kumezwa haipo tena; kwani wengi wao tayari tunao hapa hapa Tanganyika. Hawa ni waTanzania, siyo waZanzibar tena.

Kelele za kikundi kidogo cha akina OMO na maJussa hakiwezi kamwe kuwa ndicho kiwe na uwezo wa kuamua hatma ya Tanzania.
Kwa bahati mbaya sana, CCM ndiyo imekuwa mlezi mkuu wa hiki kikundi na kusababisha hata waZanzibari walikokuwa tayari kuwa waTanzania kuanza kuwa na mashaka juu ya hatua hiyo. Kwa hiyo, kuondoka kwa CCM; kazi ambayo waTanzania sasa wapo ayari kabisa kuitekeleza kukiwepo na uongozi imara, hiyo ndiyo hatua muhimu itakayo tuelekeza kwenye serikali moja.
Serikali tatu, ni za nini tena! Miungano ya aina hiyo tuishiriki tukiwa huko kwenye EAC au huko SADC.

Ni matumaini yangu utaelewa msingi huu wa hoja yangu; na kusema kweli sidhani kuwa nitakuwa na hoja zaidi nje ya msingi huu katika majadiliano haya. Kwa hiyo naomba tusiyapanue sana bila ya sababu, kwa vile tunayo mambo mengine ambayo yanahitaji muda wetu.
 
Back
Top Bottom