Vita ya Ukraine; Waafrika tuamke, ni ubeberu wa Magharibi dhidi ya walimwengu

Vita ya Ukraine; Waafrika tuamke, ni ubeberu wa Magharibi dhidi ya walimwengu

kmbwembwe

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2012
Posts
10,892
Reaction score
7,780
Waafrika tuamke wenzetu asia amerika latino wanaelewa nini kinaendelea.

Ukiangalia vita vya ukraine ni kwamba hapo pamekua tu uwanja wa mapambano. Ni kati ya nchi za kibeberu za marekani na ulaya ya magharibi wakiongozwa na marekani wakipigania hati miliki kudhibiti uchumi wa dunia.

Utaona hata zile nchi wajomba wa nchi za magharibi kama australia na new zealand na japan japo hazipo ulaya wala amerika wapo kwenye ugomvi upande wa nato dhidi ya Urusi.

Nato lengo lao kuidhibiti urusi kijeshi ili kuigeuza shamba la bibi. Urusi siku zote hofu yao ni lengo la ulaya ya magharibi. Hawataki kuiona Urusi kama nchi yenye uwezo mkubwa kiteknolojia huru kutoka nchi za magharibi.

Hawataki kuona ustaarabu mbadala wa kijamii na kiteknoloji tofauti na ule wa magharibi. Walijitahidi kuidhibiti china ikawashinda.

Hili la urusi kutaka kulipwa kwa ruble ni mojawapo ya mambo yanazidisha chuki ya marekani kwa urusi. Wao wanataka hela yao dola iendelee kua hela ya biashara duniani hasa kwa mafuta. Pia hela yao ndio ibakie hela ya kuweka akiba kwa nchi zote tena kwenye benki zao.

Tatizo kubwa linatokea pale ukikorofishana na marekani anakupora akiba yako ya fedha kwenye bank zao. Huu ni ukoloni mpya na udhalimu.

Kinachoendelea sasa ni nchi mbalimbaki kuanzisha namna ya kufanya biashara ya kimataifa kwa kutumia fedha tofauti na kuweka akiba zao kwenye fedha tofauti na dola ya Kimarekani.
 
Urusi ni nchi inayomiliki eneo kubwa sana katika Dunia hii kuliko nchi nyingine yoyote. Himaya ya Urusi imeenea hadi kwenye eneo la ardhi iliyoko katika ncha ya kaskazini ya Dunia hii.

Maliasili iliyoko kwenye eneo lote linalomilikiwa na Urusi ni mali ya warusi na hili haliwafurahishi mabeberu wa Magharibi.

Ili kupora mali za Urusi ni kuuvunja muungano wa kisovoeti kwanza na mkakati huo ulishaanza kutekelezwa tangu mwaka 1989. Poland ndio nchi kibaraka inayotumika kuisambaratisha Urusi, Tatizo ni kuwa Poland iliishajiunga na NATO kitambo, hivyo haiwezi kuichokonoa Urusi moja kwa moja maana NATO itahusika, ndio maana nchi za Magharibi zimetafuta nchi nyingine kibaraka (Ukraine) itumike kuleta chokochoko itakakayofanikisha lengo lao.
 
Urusi ni nchi inayomiliki eneo kubwa sana katika Dunia hili kuliko nchi nyingine yoyote. Himaya ya Urusi imeenea hadi kwenye eneo la ardhi iliyoko katika ncha ya kaskazini ya Dunia hii...
you guys hizi porojo hazisaidii kitu, dunia ilishahama uko kwenye hizo dhama za kuporana kwa nguvu rasimali.
wenzenu wanapiga hatua kwa kuwekeza kwenye tafiti na kuuza technolojia nyie mmejaliwa kupiga domo tu et wanaiba rasimali!!.
 
yo

you guys hizi porojo hazisaidii kitu, dunia ilishahama uko kwenye hizo dhama za kuporana kwa nguvu rasimali.
wenzenu wanapiga hatua kwa kuwekeza kwenye tafiti na kuuza technolojia nyie mmejaliwa kupiga domo tu et wanaiba rasimali!!.
Na jinsi unavyoona wewe ni matokeo ya kufanikiwa ubeberu. Eti 'wenzenu wameshatoka huko' kama vile unawajua sana😂
 
yo

you guys hizi porojo hazisaidii kitu, dunia ilishahama uko kwenye hizo dhama za kuporana kwa nguvu rasimali.
wenzenu wanapiga hatua kwa kuwekeza kwenye tafiti na kuuza technolojia nyie mmejaliwa kupiga domo tu et wanaiba rasimali!!.
Kaka kupata analytical mind hapa utakesha, story za vijiweni na inferiority complex zinaharibu vijana wengi. Watu wanawekeza kwenye tafiti kufanya innovative culture kwenye nyanja zote za Maisha yao sisi ni porojo. Kingine pedagogies zinazotumika kufundisha mashuleni sio nzuri.
 
Na jinsi unavyoona wewe ni matokeo ya kufanikiwa ubeberu. Eti 'wenzenu wameshatoka huko' kama vile unawajua sana😂
bahati nzuri UMEHISI kuwa siwajui, nilidhani UNAJUA kuwa siwajui.

Acheni porojo,lisheni wana wenu Ngano si Ugari kila siku ili wawe na walaghu akili ya kupambanua mambo.

katika huo unaouita ubeberu Nchi za watu wenye akili zinapiga hatua. S/Korea, China, Malaysia, Ufiripino, Vietnam the list goes hawa hawapo Jupiter, wapo hapa hapa ndani ya dunia ya Beberu na wanapiga hatua kila uchao. nyie bakini hapo hapo na kudhani kuna watu wanapanga njama za kuwaondolea nguvu za kiume ilimsiazilianae kama bata.

Leo Ukraine imechakaa kwasababu ya mabomu ya Urusi vita ikiisha leo baada ya miaka 5 Ukraine itakuja kuchangia kwenye bajet ya nchi yako na kukujengea vyoo mashuleni.

mmekaa kulia Lia ubeberu ubeberuuu.

fool and ungrateful animal.
 
Magharibi ndio wamevamia Ukraine?chanzo cha yote ni nani kama sio Russia!!
Ukraine ni nchi huru ina maamuzi yake kuchagua upande wowote amechukua crimea na sasa hivi anataka kuchukua donbas huyu jamaa ana ubabe wa kizamani sana,kila nchi ikiamua kuvamia maeneo ya wengine duniani hapatakalika
 
Kwenda zako. Yaani hapo unaona porojo?
niende zangu wapi? hiyo mamlaka umeitoa wapi? hata Melo tu hawezi niambia hivyo wala nifukuza. hata nikipigwa ban nitavist as Guest.
wakunizuia nisiione Jf ni Mabeberu tu kwasababu internet ni yao na saver za Jf ni zao wakizima ndiyo itakuwa mara yangu ya mwisho kuiona Jf sio wewe choka mbaya mwenzangu.
 
Kaka kupata analytical mind hapa utakesha, story za vijiweni na inferiority complex zinaharibu vijana wengi. Watu wanawekeza kwenye tafiti kufanya innovative culture kwenye nyanja zote za Maisha yao sisi ni porojo. Kingine pedagogies zinazotumika kufundisha mashuleni sio nzuri.
kabisa
 
Urusi ni nchi inayomiliki eneo kubwa sana katika Dunia hili kuliko nchi nyingine yoyote. Himaya ya Urusi imeenea hadi kwenye eneo la ardhi iliyoko katika ncha ya kaskazini ya Dunia hii. Maliasili iliyoko kwenye eneo lote linalomilikiwa na Urusi ni mali ya warusi na hili haliwafurahishi mabeberu wa Magharibi.
Ili kupora mali za Urusi ni kuuvunja muungano wa kisovoeti kwanza na mkakati huo ulishaanza kutekelezwa tangu mwaka 1989. Poland ndio nchi kibaraka inayotumika kuisambaratisha Urusi, Tatizo ni kuwa Poland iliishajiunga na NATO kitambo, hivyo haiwezi kuichokonoa Urusi moja kwa moja maana NATO itahusika, ndio maana nchi za Magharibi zimetafuta nchi nyingine kibaraka (Ukraine) itumike kuleta chokochoko itakakayofanikisha lengo lao.
😍
 
yo

you guys hizi porojo hazisaidii kitu, dunia ilishahama uko kwenye hizo dhama za kuporana kwa nguvu rasimali.
wenzenu wanapiga hatua kwa kuwekeza kwenye tafiti na kuuza technolojia nyie mmejaliwa kupiga domo tu et wanaiba rasimali!!.
Mkuu, hili ni jukwaa la kujadili na mtoa hoja ameleta hoja ambayo iko kwenye chati sasa hivi. Kuijadili ni halali ya kila mwanachama wa jukwaa hili aliye na facts zinazochangia kuwepo kwa mgogoro ambao upo kwa miaka zaidi ya nane, Sasa wewe unapoona mawazo ya watu wengine kuwa ni porojo, huwatendei haki waliochangia. Cha msingi wewe changia kwa kuweka hoja zako kinzani ili zichambuliwe, kukataza watu wasichangie eti ni porojo za vijiweni siyo haki wala sio sawa.
 
yo

you guys hizi porojo hazisaidii kitu, dunia ilishahama uko kwenye hizo dhama za kuporana kwa nguvu rasimali.
wenzenu wanapiga hatua kwa kuwekeza kwenye tafiti na kuuza technolojia nyie mmejaliwa kupiga domo tu et wanaiba rasimali!!.
Wewe nae kibaraka wa wamagharibi tu, hivi unadhani ulaya magharibi na marekani zinafurahi urusi kutegemewa kwa kiasi kikubwa kwenye nishati ya gesi na mafuta? US anataka kuitawala dunia, ameshafanikiwa kwa kiasi kikubwa mno, ndio maana ulaya magharibi yote(umoja wa ulaya) wanakubaliana na kila marekani anachotaka, Japan, Korea ya kusini, Australia, Canada...zote hizi hazimpingi mmarekani kwa lolote.

Urusi ana resources za kutosha sana, vikwazo alivyopigwa ingekuwa nchi yoyote, na hasa ingekuwa nchi ya kiafrika hadi leo hii uchumi ungekuwa umeanguka mazima, mkate ungeuzwa hata 200,000, lakini utegemezi was ulaya kwa urusi ndicho mmarekani hakipendi.
 
Kaka kupata analytical mind hapa utakesha, story za vijiweni na inferiority complex zinaharibu vijana wengi. Watu wanawekeza kwenye tafiti kufanya innovative culture kwenye nyanja zote za Maisha yao sisi ni porojo. Kingine pedagogies zinazotumika kufundisha mashuleni sio nzuri.
Hebu jiulize kwanza kama vijiweni unaweza kupata story kama hii.

Hivi unajua au hujui kama ni dola ya kimarekani tu inakubalika kwenye biashara ya mafuta? Unafikiri ni nchi zote zenye mafuta zinaridhika na nguvu ya dola ya kimarekani kwenye biashara ya mafuta?

Kitu kama hujui acha dharau kujifanya ni habari za vijiweni. ...Badala yake tafuta kujua. Kwenye dola ya kimarekani upo unyojaji na ubeberu mkubwa. Hizi ndio unaona habari za vijiweni? Google upate kujua acha dharau.
 
Mkuu, hili ni jukwaa la kujadili na mtoa hoja ameleta hoja ambayo iko kwenye chati sasa hivi. Kuijadili ni halali ya kila mwanachama wa jukwaa hili aliye na facts zinazochangia kuwepo kwa mgogoro ambao upo kwa miaka zaidi ya nane, Sasa wewe unapoona mawazo ya watu wengine kuwa ni porojo, huwatendei haki waliochangia. Cha msingi wewe changia kwa kuweka hoja zako kinzani ili zichambuliwe, kukataza watu wasichangie eti ni porojo za vijiweni siyo haki wala sio sawa.
Unanionea, sijui ni kwa bahati mbaya ama maksudi. Lissu aliposema Ripoti Mruma ni taka taka hakuwa na maana kwamba wajumbe wengine wasiijadili hiyo Ripoti, hakuzuia isijadiliwe, na kauli yake haikuzuia Ripoti hiyo kujadiliwa.
mimi sizuii mtu kujadili, nyie jadilini ila huu uzi ni Porojo tupu.

huu uzi nimeuita Porojo unless mleta Uzi ali- refute kuwa si porojo, amwage facts.

Mimi sijafanya kosa kwa kuuita huu uzi ni porojo, kosa ni pale ningelitaka Mods wauondoe huu uzi(ufutwe kwasababu ni porojo) hapo nitakuwa nimefanya makosa.

kuna Dogo uko juu kanifukuza kwenye huu uzi as if anafukuza li-dudu, kwa wapenda haki na ukweli alipaswa akemewe huyo na si mimi nilieokoment kinyume na mleta mada.

huu ni mjadala gani mtu akikoment kinyume na mleta mada anaitwa mkosaji?.
 
Back
Top Bottom