Vita yetu dhidi ya ushoga ni dhaifu sana

Ni kweli wao wanatoa uhuru kwa watu wao kufanya wanachokitaka bila kuulizwa? wacha uongo aloo.
 
Unataka kufirwa?
shida yenu hamuoni shida kufirwa ili mpate ahueni ya maisha. Kuna vijana wetu wengi wanafirwa kule marekani kutoka na ughali wa maisha. Wakishafirwa wanageuka mawakala na makuwadi wa ufiraji kwenye nchi zao walikotoka. wanapewa seed money (fedha) za kushawishia vijana na vitendea kazi kama vilainishi, bendera ya upinde wa mvua na mavulana. Vijana hawa wanapandikizwa kupitia mashirika (NGOs) zenye mafungamano na nchi za magharibi. Vijana wetu wanaoanzisha NGO zao za vijana na kuomba misaada kutoka magharibi, misaada hiyo inafungamanishwa na kueneza ushoga. Kila msaada na kila NGO (asasi za kiraia) zenye mahusiano na nchi za western lazima zipekuliwe.
 
Waafrika tujifunze kutatua matatizo yetu bila kuwasingizia wazungu.

Kuna unafiki mkubwa sana kati yetu kwenye jamii, kama wote tungekuwa tunachukizwa na ushoga kama tunavyoonyesha kuchukizwa nao huku mitandaoni na tukiwa tunajadiliana sidhani kama hali ingekuwa mbaya kama ilivyo sasa. Lazima tukubali, hali ni mbaya.

Wapo baadhi ya watu wanashabikia kuwaingilia wanawake kinyume na maumbile (huu ni kama vile umekuwa ujanja kwa sasa) sasa huyu watu kama hao si wamebakiza hatua moja kuwa mashoga?

Hawa mashòga tunaowaona ni kina nani wanafanya nao huo ushenzi? Hao wanaofanya nao pia ni mashoga.

Ndio maana nasema kuna unafiki mwingi sana kwenye jamii katika kupambana na ushoga.
 
Shida yako unashindwa kutofautisha kati ya inavyotakiwa kuwa na ilivyo sasa. Sasa hivi kuna maaskofu na masheikh feki, kuna walimu feki, kuna askari feki, watumishi wa afya feki, wazazi feki, wajomba feki, babu feki ambao haadhi yao wamo mashoga pia. Mitandao, television, video, nyimbo zote n
 
Last time waliufuta muswada baada ya kupigwa biti sidhani kama sahivi watakua na ubavu wa kutekeleza hiyo sheria. Maana Kuna misaada watakosa kisa hiyo sheria, swali ni je Uganda itaweza toboa ikiwekewa vikwazo vya Kibiashara?
Ngoma ishapitishwa sema na marekani washaibuka tena kuipiga biti Uganda,Nashangaa Marais wa Afrika mashariki wapo kimya,Tulipoteza chuma chetu kingeshatoa Tamko.
 
Kinachotokea wanatumia ile kitu inaitwa "divide and rule" kwa kutumia mikopo na misaada yao. Kwanjia hii ya divide and rule wanafanya yafuatayo kulingana na ukubwa wa maslahi wanayoyakusudia kuyapata kwenye bara au nchi husika.

1. nchi inayokubali inapewa misaada ya kifedha na mikopo na nchi inayokataa inanyimwa
2. Jirani yako anaekubali anapewa silaha kubwa na mafunzo ya kijeshi na wewe unaekataa hupewi silaha hizo, hivyo uko hatarini kupigwa na jirani yako.
3. nchi inayokubali inatembelewa na viongozi wakuu na watalii kutoka magharibi wakati nchi inayokataa haitembelewi na watalii hawaendi. Kama vile mtoto mtundu anavyonyimwa kupewa pipi.
4. Nchi inayokubali viongozi wake wanaruhusiwa kukwea pipa na kutembelea nchi za magharibu, wakati iliyokataa viongozi wake wanapigwa marufuku. hapa wanajua kuwa waafrika wanapenda sana kwenda nchi hizo kuficha hela, kufanya manunuzi au kufanya matanuzi.
5. nchi inayokubali inasamehewa madeni yake wakati ile inayokataa deni linabaki palepale na kutakiwa ilipe haraka vinginevyo......
6. Inayokataa inawekewa vikwazo vya kiuchumi wakati inayokubali hilo jambo inapewa fursa mbalimbali za kiuchumi, kisiasa na kielimu.
7. na mwisho kiongozi anayekataa wanaweza kumpindua, kushindwa kwenye uchaguzi na hata kuuawa.

Hakuna kiongozi wa Afrika anayetaka kimojawapo kati ya hivyo hapo juu kimtokee yeye, na kama yuko basi ni mmoja au ameshapinduliwa, shindwa uchaguzi au kufa tayari.
 
Gadafi,Magufuri,Mugabe, Nyerere, Mandela, Samora, Iddi Amin,Haile Selasia walichukukiwa na wazungu kwa kutetea uafrika wao. Wengi waliitwa madikteta
 

Word
 
KUNA NJIA MBILI ZA KUPAMBANA NA TATIZO, MOJA KUPAMBANA NALO KIMYA KIMYA NA KULIMALIZA KIMYA KIMYA, PILI, NJIA YA KUPIGA KELELE KUSHINDANA NA TATIZO, TANZANIA IMEAMUA KUSHINDANA NA SHETANI KIMYA KIMYA, HATUTUMII NJIA ZA WENGINE KUPIGA MAKELELE
 
Kama tunashindwa kujitoshereza kwa chakula na rasilimali zote muhimu tunazo,tutaweza kweli kupambana na wazungu kuhusu ushoga,wakati tunahitaji dollar zao?
Nigeria ina mafuta,lakini wananchi wake wanapanga foleni kununua Tena kwa bei juu.
Congo Kuna msdini,lakini kampuni zote zinazochimba,zinatoka ulaya,
Bongo Kuna ardhi na maji kibao,lakini tunasubili msaada wa ngano kutoka Ukraine,nchi iliyopo vitani!hatuna pesa ya kuwekeza kwenye kilimo,lakini tuna bilioni 500+kila mwaka kununua ndinga mpya za watumishi serikali kuu,
Kipindi Cha Kikwete na Lowasa,Kanda ya ziwa kulikuwa na shida ya huduma ya maji,na ziwa Victoria lipo!yakafanyika maamuzi magumu,miundombinu ikawekwa Ili maji yatumike,kagera,mwanza,na sasa hv inabidi yafike singida mpaka Dodoma,
Tunahitaji maamuzi ya kuthubutu kama haya,bila hivyo vijana waachwe wabomolewe tu
 
hii vita inataka umakini mkubwa sana na siyo hiyo papara ya kutoa matamko hovyo hovyo mradi tu uonekane tunapinga ushoga
 
TANZANIA IMEAMUA KUSHINDANA NA SHETANI KIMYA KIMYA, HATUTUMII NJIA ZA WENGINE KUPIGA MAKELELE[/B]

Kushindana na shetani kwa kuwauwa binadamu wenzenu kisa tu wanapigwa pumbu??

[emoji12][emoji12][emoji12][emoji12][emoji12] The irony is too much pilipili [emoji1787]

Hakuna hiyo kitu. We sema tu mashoga wamewapiga bao, hamna kitu mtawafanya.

Kuna maeneo kila siku nawaona wamejiachia wanasasambua makalio na hamna venye mnafanya lolote.
 
Tunapaswa tuonyeshe kweli hatuutaki ushoga kwa vitendo hebu angalia swala mikopo ya vyuo vikuu hadisasa wapo wanafunzi baadhi hawahapewa pesa za kujikimu nikuzungushwa tu mfano NIT unataka watoto wafanyaje wanaishije wapeni pesazao wajikimu tuepushe majanga kama hayo
 
Nimekuelewa mleta mada, namna yetu ya ku- deal na hilo jambo la ushoga ni kweli imekaa kiupole upole, ukiachia mbali taarifa iliyotolewa na serikali kuhusu hilo jambo, bado sijaona viongozi wakuu wa nchi wakikemea hilo jambo hadharani, kwa kurudia ili kila mmoja huko nje aujue msimamo wetu.
 
Taja eneo husika tukawashughulikie
 
Toa taarifa mara uwaonapo tukawashughulikie shughuli pevu
 
*Tulipanda Usiku, tunavuna Mchana.*ila MATUNDA HAYAFANANI na MBEGU ZETU tulizootesha USIKU.
Ushoga, ulawiti, usagaji

Tulipoamua sote kuwa wafanyakazi, wajasiriamali na watumishi (wanaume kwa wanawake) hatukutafakari vyema.

Tulipoamua kuingia mtaani na kujipotosha juu ya haki sawa bila kujua undani halisi wa haki, fursa na wajibu hatukutafakari ya kesho.


Tulipoamua kufanya hayo yote, hatukuwaza vyema juu ya familia. Hatukuwaza juu ya misingi na malezi ya watoto wetu. Hatukuwaza nani atabaki nyumbani kusimamia jukumu kuu la nyumbani.

Tukaanza kuwakebehi akina mama wa nyumbani na kuwaita majina mabaya. Tukawaita magolikipa, chuma ulete, wajaza vyoo, mizigo, punching bags na kila jina tuliloona linatosha kuwafanya wachukie kusimamia jukumu lao kuu ambalo wengi wetu mama zetu walilifanya ndiyo maana leo tupo imara na tunawaona kama walikuwa wanawake wa chuma.

Wanawake nao walipoona imezidi, na kwamba akiwa dokta, mwanasheria, mfanyabiashara n.k ndo anaonekana bora na wa kisasa, nao wakaingia mzigoni.

Walipoelezwa kuwa maisha ni kusaidiana, bila kujua kuwa mama kusimamia jukumu la mji wake ndiyo msaada mkubwa kwa mumewe kuliko misaada yote, nao wakaingia kingi. Baba anaondoka na mama anaondoka. Mji unabaki na mtu ambaye huitwa housegirl au houseboy au ndugu wa mume au mke ambao nao wana ndoto zao, tabia zao, changamoto na mahitaji yao ambayo sasa yakawa ndiyo msingi wa malezi ya watoto wa baba na mama watafutaji.

Haijazidi miaka 30 toka huu mchakato usambazwe zaidi kupitia mifumo yetu ya kielimu, kisiasa na kijamii, Sasa tumeanza kuvuna matunda ya haki sawa, matunda ya kusaidiana, matunda ya mwanamke anaweza, matunda ya mkutano wa Beijing, na matunda ya kila aina ya utumbo tulioutafuna bila kuuosha. Sasa bakteria wa utumbo huo wameanza kutuozesha.

Mwelekeo huu wa matendo na matukio ya ushoga waweza kuwa mwanzo wa magumu mengi ambayo tutapitia kama jamii na taifa.

Wazungu na mashirika yao yaliyojificha kupitia taasisi za misaada chini ya dini, afya, siasa, elimu na sanaa wanajua ni kizazi gani kiliandaliwa ili kuja kuzalisha watoto ambao watapokea elements za LGBT (rejeeni haya mambo ya haki sawa yalianza kusambazwa zaidi lini nchini).

Sasa wanachofanya ni kuanza kuvuna matunda ya watoto wengi ambao hawakuelewa vyema na wazazi wao. Watoto waliokabidhiwa kwa walezi tofauti na wazazi wao kama vile wasaidizi wa kazi, walimu na wakufunzi wa dini.

Wengine ni watoto walioanza kutazama vipindi vya TV vyenye maudhui yanayoonesha ushoga wakiwa wadogo kuanzia miaka ya 90 mwishoni na 2000 mwanzoni kuelekea 2010 na hata sasa kila tamthilia ya nje inayooneshwa nchini ina viashiria vya ushoga. Bado hatujashtuka.

Wazungu na washirika wao wanajua kizazi walichokiandika nao watazalisha kizazi dhaifu zaidi yao. Na ndiyo mchezo wenyewe unapoanzia.

Juzi Waziri wa Afya Dada Umy Mwalimu alisema na kuwakumbusha akina mama juu ya majukumu yao ya msingi ya kulea familia zao kuliko kujitokeza mitaani kama watafutaji na wafanyabishara zaidi. Akasema kuwa wasishindane na wanaume.

Kama Waziri ameona changamoto, tuna kila sababu ya kuona hili tatizo na kulichukulia kuwa tatizo la kitaifa.

Tulidanganywa tukadanyika. Leo tuna watoto ambao hata mzazi akiteseka, akiugua au hata akifa hawana uchungu maana wamelelewa zaidi na watu baki kuliko wazazi wao. Tuna watoto ambao wanathamini zaidi watu wa nje na marafiki kuliko walio wazaa. Na hawana mahusiano chanya na familia.

Ikumbukwe ukifanikiwa kuvunja bond ya familia, umeangamiza taifa zima.

Tumetikisa na tunaendelea kuvunja taasisi ya familia kwa kugeuza msingi wa majukumu kiasi kwamba kuna nyumba huwez kujua baba ni nani na mama ni nani. Utafutaji umekuwa ndo tatizo ambalo leo hii linavunja ndoa na kupelekea mauaji kitu ambacho hakikuwepo enzi za wazazi wetu wa chuma.

Na zaidi tuna familia nyingi za mzazi mmoja (single parent) ambazo zaidi kabisa ni za wanawake na watoto wao.

Hii ni kwasababu mwanamke wa kisasa mwenye kaelimu ka darasani hususani waliofika hadi vyuoni, wengi wao huona wanaweza hata wakiwa pekee yao. Mwisho ni mwendelezo wa uzinzi na mabadiliko ya ma-anko kila cku.

Matokeo yake mtoto anajifunza tabia hizo na kukosa misimamo ya kimaisha. Akifikisha umri wa balehe tu mama anabak analia na hana uwezo wa kukabiliana na mabadiliko ya mtoto wake. Na wakati huo huenda mtoto alishaambiwa baba yako alikufa au alikukataa.

Kuna mwanamama mmoja mmiliki wa taasisi moja inajihusisha na sanaa, sitaitaja jina. Naye ni single mother. Wakati mmoja alisikia wimbo uliokuwa na maadhi ya kuwatia moyo single mothers...wimbo ule ulimtia simanzi na hata akatoa machozi. Yeye ni single mother aliyefanikiwa, na alisema amefanikiwa akiwa single mother. Je kufanikiwa ndiko kulikomtoa machozi baada ya kusikiliza wimbo ule? Kwanini atoe machozi? Kwanini asifurahie tu ila hadi chozi linamtoka? Kuna mahusiano gani kati ya mafanikio na machozi? Nadhani kuna mihangaiko mingi na misukosuko na mateso mengi amepitia hadi kufanikiwa kama single mother ndiko wimbo ule ulimkumbusha hadi akatoa Machozi yake.

Hakuna mtu mwenye akili timamu anayetamani kuishi pekee yake hadi uzee wake. Watoto huja kama baraka na matunda ya familia, ila wakati wao ukifika nao huondoka na kwenda kuanzisha familia zao. Wenza hubakia wawili wakiendelea kuliwazana na kushea hisia zao hadi mwisho wao.

Hakuna anayetamani kuishi peke yake na ikiwa yupo ni wachache sana na hawakuanzisha familia.

Mfano huo utufundishe kuwa tunahitaji familia ibaki kujengwa na baba na mama na siyo vinginevyo. Huu ni msingi na ni kanuni za kimaumbile. Labda changamoto nyingine zisizoepukika ziingilie kati. Napo bado mfiwa anayo haki ya kupata mwenza mwingine ikiwa bado anahitaji.

Kama taifa tujifunze kitu na tuanze kujirekebisha kabla hatujafikia wakati ambapo kabla ya kijana wa kiume na wa kike kuoana, watalazimika kupelekwa kupimwa kama ni mwanaume kweli au kama ni mwanamke kweli.

Wakati bado hatuna sheria ya moja kwa moja juu ya ushoga, kila mtu ashike na kutunza vyema alicho nacho.

Wanawake wafanyakazi na watafutaji tengeni muda kwaajili ya watoto na waume wenu. Jueni jukumu lenu kuu na la msingi ni usimamizi wa nyumba zenu na malezi ya watoto na waume zenu. Mengine hufuata baada ya hilo. Kubwa zaidi kumbukeni kuwa na utiifu na adabu kwa waume wenu bila kujali uwezo wenu kiuchumi.

Msisahau kuwa mwanamke mtumishi ni daraja la 3 katika ubora wa mke. Hivyo pamoja na hilo jitahidini sana kuweka uzito kwenye familia zenu maana utumishi una mwisho, ila familia ni mwendelezo wa maisha na vizazi vyenu.

Nanyi wanaume jitahidini kuwapenda, kuwafundisha, kuwahurumia na kuwahakikishia usalama wake na watoto wenu. Msiwachokoze ili wasiwe na uchungu nanyi. Mtakosa baraka. Mkumbuke kutoa sadaka kwa watoto wenu ili milango yenu ifunguliwe.

Pia tambueni kuwa jukumu la kwanza kuhakikisha usalama na ustawi wa familia ni lenu bila kujali mke ana kipato au hana kipato. Na ikiwa wake wenu wanawasaidia iwe ni katika utafutaji ambao mnaufahamu na kuusimamia. Na kama ni watumishi, watieni moyo na kusimamia vipato vyao visitawanyike na mwisho wakatawanya na familia zao kwa kiburi.

Na zaidi muwe na muda wa kukaa na familia ili kujua wapi kuna tatizo na kurekebisha mapema.
Kumbukeni kuwa mwanaume mtumishi naye pia ni daraja la tatu la ubora wa mume. Hivyo ule udhaifu utaokuwa unajitokeza kwenye familia ni lazima kutafuta namna ya kuupunguza ili watoto wenu waje kuwa imara zaidi yenu.

Pia wanafamilia tianeni moyo katika changamoto zenu kwa kuvumiliana na kuhurumiana.

Tanbihi...

Uimara wako ni matokeo ya yule mama ambaye sasa ni mzee. Ikiwa alikuwa mtumishi, ubora wako unauona, ikiwa alikuwa mfanyabiashara pia vilevile na ikiwa alikuwa golikipa bado ubora wako ni matokeo ya muda na jitihada zake.

Amua aina ya familia yako kulingana na malezi bora uliyopewa na siyo unayoona kwenye TV na kuambiwa na wengine.

Tunavuna matunda ya tulichopanda usiku na sasa tunashangaa kuona matunda hayana mbegu kama zile tulizopanda usiku.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…