Vivutio vya utalii Tanzania na faida za utalii wa ndani

Vivutio vya utalii Tanzania na faida za utalii wa ndani

Habari mkuu!!!!
Hongera kwa kuanzisha uzi mzuri sana unao tukumbusha kutembelea vivutio vyetu
NIngependa tu kuongezea tu yakua kwa sasa Tanzania Bara ina jumla ya hifadhi 22 ambazo zipo chini ya mamlaka ya usimamizi wa hifadhi Tanzania yaani TANAPA na hii ni kutokana na ongezeko la hifadhi sita (6) mpya ambazo zilikua mapori ya akiba na sasa zimekua hifadhi za taifa.

Hifadhi zilizoongezeka ni
1. Burigi chato National park
2. Nyerere National park
3. Ibanda-kyerwa National park
4.Rumanyika-Karagwe National park
5. Kigosi National park
6. Ugalla river National park.

Pia Tanzaia tumebarikiwa kuwa na bonde la Ngorongoro ambalo lenywe linasimamiwa na (NCAA) yaani Ngorongoro Conservation Area Authority lilianzishwa mwaka 1959 ikiwa lengo lake kubwa ni kulinda lasilimali za wanyamapori pamoja na kuulinda utamaduni wa kimaasai. Hii ni sehemu pekee kwa Afrika ambayo wanyama pamoja na binadamu jamii ya kimaasai huishi kwa pamoja.

Pia Taznzania tumebahatika kuwa na maeneo yanayojulikana kama Game Reserve.
Haya ni maeneo yaliyo anzishwa kwa lengo kubwa la kuhifadhi na kulinda Wanyamapori na mazingira.
Katika maeneo haya ndo sehemu ambapo uwindaji wa wanyamapori hufanyika lakini ni kwa kibali maalumu.
mfano wa sehemu hizo ni Moyowosi game reserve, Usangu game reserve nk.

Pia tuna sehemu za kuvutia zijulikanazo kama Marine park and reserve.
Haya ni maeneo yyalianzishwa kwa sharia ya Marine park and reserve act no.29 of 1994 ikiwa na lengo la kulinda maeneo haya hasa kwakua ni maeneo muhimu kwa uzalianaji wa samaki, kulinda matumbawe, kulinda mikoko, kulinda mazalia ya ndege na viumbe vidogo vidogo vya majini.
Maeneo haya ni
1.Bongoyo island marine reserve
2.Mbudya island marine reserve
3.Pangavini island marine reserve
4.Funguyasini island marine reserve
Hivo vyote vinapatikana dar es saalam

Pia vipo
1. Mafia island marine park-Mafia pwani
2.Mnazi bay Ruvuma estuary marine park-Mtwara


Nikipata mda ntaeelezea kuhusu Wildlife management areas,Game controlled areas,Forest reserve na Historical sites.
 
Naaam! Vizuri sana, hivi karibuni natia nanga na kutumia mfumo wa "Kata Funua, 323 by 8" katika kuelezea na kuonyesha masuala mbalimbali ya kitalii na historia tanabiha.
 
Habari mkuu!!!!
Hongera kwa kuanzisha uzi mzuri sana unao tukumbusha kutembelea vivutio vyetu
NIngependa tu kuongezea tu yakua kwa sasa Tanzania Bara ina jumla ya hifadhi 22 ambazo zipo chini ya mamlaka ya usimamizi wa hifadhi Tanzania yaani TANAPA na hii ni kutokana na ongezeko la hifadhi sita (6) mpya ambazo zilikua mapori ya akiba na sasa zimekua hifadhi za taifa.

Hifadhi zilizoongezeka ni
1. Burigi chato National park
2. Nyerere National park
3. Ibanda-kyerwa National park
4.Rumanyika-Karagwe National park
5. Kigosi National park
6. Ugalla river National park.

Pia Tanzaia tumebarikiwa kuwa na bonde la Ngorongoro ambalo lenywe linasimamiwa na (NCAA) yaani Ngorongoro Conservation Area Authority lilianzishwa mwaka 1959 ikiwa lengo lake kubwa ni kulinda lasilimali za wanyamapori pamoja na kuulinda utamaduni wa kimaasai. Hii ni sehemu pekee kwa Afrika ambayo wanyama pamoja na binadamu jamii ya kimaasai huishi kwa pamoja.

Pia Taznzania tumebahatika kuwa na maeneo yanayojulikana kama Game Reserve.
Haya ni maeneo yaliyo anzishwa kwa lengo kubwa la kuhifadhi na kulinda Wanyamapori na mazingira.
Katika maeneo haya ndo sehemu ambapo uwindaji wa wanyamapori hufanyika lakini ni kwa kibali maalumu.
mfano wa sehemu hizo ni Moyowosi game reserve, Usangu game reserve nk.

Pia tuna sehemu za kuvutia zijulikanazo kama Marine park and reserve.
Haya ni maeneo yyalianzishwa kwa sharia ya Marine park and reserve act no.29 of 1994 ikiwa na lengo la kulinda maeneo haya hasa kwakua ni maeneo muhimu kwa uzalianaji wa samaki, kulinda matumbawe, kulinda mikoko, kulinda mazalia ya ndege na viumbe vidogo vidogo vya majini.
Maeneo haya ni
1.Bongoyo island marine reserve
2.Mbudya island marine reserve
3.Pangavini island marine reserve
4.Funguyasini island marine reserve
Hivo vyote vinapatikana dar es saalam

Pia vipo
1. Mafia island marine park-Mafia pwani
2.Mnazi bay Ruvuma estuary marine park-Mtwara


Nikipata mda ntaeelezea kuhusu Wildlife management areas,Game controlled areas,Forest reserve na Historical sites.
Asante Sana Kiongozi.
 
Y
Hivi ndo lile ziwa wanalosema watu huruhusiwi kuoga...!
Haswaa japo niimani zauongo tu watu wanadai wengi wanaenda kuogelea japo sio sehemu zote maana ni ziwa lililotokana na mlipuko wa volcano (historical theories).

Ukija kwa wasafwa ambao ni wenyeji wanakwambia, lilimeza mtu likakimbia na kwenda kujifisha pale juu ya mlima.
 
Wadau wa Jukwaa heshima kwenu.

Kwa niaba ya Shirika linalojihusisha na Utalii Tanzania -TANAPA pamoja na Bodi ya Utalii-Tanzania. Kuwaletea hii platform hapa Jamiiforums itakayohusiana na mambo ya utalii, ili kuhamasisha zaidi utalii wa ndani.

Karibu pia Utushirikishe sehemu ambayo uliwahi kutembelea ndani ya nchi yetu na ikavutia sana. Au kama ulikutana na changamoto yoyote iseme. Nakaribisha pia Maoni, Mapendekezo na ushauri kuhusiana na mambo ya utalii. Nawakaribisha sana, kama utakuwa na swali lolote! Litapatiwa ufumbuzi.

Karibuni Wote.

Tanzania ni nzuri yenye vivutio vya kila aina.

View attachment 1270533View attachment 1270534View attachment 1270535

Baadhi ya vivutio ambavyo vinasimamiwa kikamilifu na Shirika la Hifadhi za Taifa la Tanzania (TANAPA) ni pamoja na hifadhi ya Taifa ya Arusha, Gombe, Katavi, Mlima Kilimanjaro, Mahale, Mikumi, Manyara, Ruaha, Rubondo, Serengeti, Saadan, Tarangire, Udzungwa, Kitulo, Mkomazi na Saanane.
Na Kuna hifadhi nyingine mpya Tatu ambazo ni Hifadhi ya Nyerere (Selous), Hifadhi ya Kigosi na Hifadhi ya Mto Uggala.

Hapa chini nitakuletea sifa za Hifadhi moja hadi nyingine.

1.Hifadhi ya Taifa ya Arusha(Arusha National Park)
Hifadhi ya Taifa ya Arusha kuwa ina ukubwa wa kilomita za mraba 328.4, iko umbali wa kilomita 62 (kiasi cha mwendo wa saa moja kwa gari) kutoka mji wa kitalii wa Arusha.

‘’Hifadhi hii ina maeneo matatu muhimu ambayo ni bonde la Ngurdoto (Ngurdoto Crater), maziwa ya Momella ambayo kila moja hutoa mandhari tofauti pamoja na Mlima Meru wenye urefu wa mita 4566 (futi 14990), hali ambayo inaifanya hifadhi kuwa na mazingira ya baridi’’ anasema Mbugi.

Ikumbukwe kuwa hifadhi hii ni maarufu kwa wanyama jamii ya tumbili wajulikanao kama Mbega weusi na weupe. Wanyama wengine wanaopatikana katika hifadhi hii ni pamoja na Twiga,pundamilia, Nyati na digidigi.

Unaweza kuwaona Chui wakibarizi katika vivuli vya matawi ya miti inayokingwa na maaguko ya maji huku makundi kadhaa ya batamaji yakitafuta wadudu katika maziwa ya Momella.

Zaidi ya aina 400 za ndege wamethibitika kupatikana ndani ya hifadhi hii. Safari za miguu na kupanda milima Meru ni moja ya burudani muhimu katika hifadhi ambapo mpandaji anahitaji kati ya siku 3-4 za kupanda mlima.

Wakati mzuri wa kutembelea hifadhi hii ni kati ya mwezi Juni na Februari ingawa mvua inaweza kunyesha mwezi Novemba. Kuna maeneo ya malazi ndani ya hifadhi yenye hadhi tofauti tofauti kama hoteli, nyumba za wageni na makambi ya kupuga mahema ingawa wageni pia wanawezakupata malazi eneo nje ya hifadhi katika mji wa Usa River na Arusha mjini.

2. Hifadhi ya Mahale

Hifadhi hi inaundwa inaundwa na vilima vilivyojipanga na kufunikwa na misitu minene ikiwa na jumla ya kilomita za Mraba 1613. Kama ilivyo hifadhi ya jirani ya kaskazini ya Gombe, hifadhi ya milima ya Mahale ni makazi ya jamii adimu zilizobakia za sokwe barani Afrika.

Mabaki ya matunda yaliyoliwa na kinyesi kibichi ni miongoni mwa alama zitakazokuongoza mgeni hadi kuwafikia viumbe hawa katika misitu iliyopo katika mlima huo na hifadhi hii ipo Maharibi mwa Tanzania ikiwa inapakana na Ziwa Tanganyika.

Ukifika hapo utaona na sehemu ya asili ya watu wa kabila la Watongwe walipokuwa wakiaabudia mizimu yao milimani, kisha kurudi ziwani na kujitumbukiza kwenye maji baridi na maangavu.

Wakati mzuri wa kutembelea hifadhi hii ni kipindi cha kiangazi, kati ya mwezi Mei na Octoba.

4.Gombe

Hifadhi ya Taifa ya Gombe ni ndogo kuliko zote nchini ikiwa na jumla ya kilomota za mraba 52 lakini ina umaarufu mkubwa unaotokana na kuwa na wanyama aina ya Sokwe.

Gombe ni moja ya makzi ya machache yaliyosalia ya Sokwe duniani. Ipo kilomita 16 kaskazini mwa mji wa Kigoma, hifadhi hii ni ukanda mwembamba wa msitu wa mlima unaokatizwa na miteremko mikali inayoingia katika mwambao mwa Ziwa Tanganyika.

Wanyama wengine wanaopatikana katika hifadhi hii ni pamoja na Kima wenye mikia myekundu na kima wa rangi ya bluu na wale wanyama jamii ya Paka hawapo katika hifadhi hii kama vile Simba na Chui hivyo kuifanya kuwa salama kwa safari za miguu.

Unaweza kwenda kutembelea hifadhi hii kwa ndege za abiria au za kukodi kutoka Dar es Salaam hadi Kigoma mjini na baadaye kwa boti mpaka makao makuu ya hifadhi, kadhalika kuna huduma za treni kutoka Mwanza na Dar es Salaam pamoja na barabara itokayo Mwanza, Mbeya na Dar es Salaam.

Wakati mzuri wa kutembelea hifadhi hii ni wakati wa kiangazi, Julai mpaka Octoba kwani Sokwe hawapendi kutembea nyakati za mvua.

Gharama ni kubwa sana kufanya utalii kwa mtu wa kawaida
 
Woyooooo
FB_IMG_1575629253822.jpeg
 
Uzi unaleta burudani umeshusha madini ya uhakika.nimejifunza kitu,baadhi ya nyuzi Kama hizi wengine ndo zilitushawishi kujiunga JF.mambo ni fire [emoji91][emoji91][emoji91].Mungu ibariki Tanzania,Mungu ibariki Afrika[emoji1241]

Sent from my itel A32F using JamiiForums mobile app
 
Follow me on Twitter for tourism and wildlife fact in Tanzania
Karibuni wadau hapa utapata taarifa zote za Utalii nchini Tanzania
Capture%2B_2019-12-06-09-28-32.jpeg
Capture%2B_2019-12-06-09-29-35.jpeg
Capture%2B_2019-12-06-09-29-48.jpeg
Capture%2B_2019-12-06-09-29-59.jpeg
 
>>Hili ni tangazo la biashara. Naamini limelipiwa inavyostahili.

>>TANAPA na mamlaka zingine za utalii punguzeni viingilio kuvuta wazawa zaidi kutembelea vivutio hivi. Mkumbuke kutalii sio sehemu ya utamaduni wetu.
 
Baada ya kchombo kikubwa cha habari duniani CNN kulitaja eneo la ngorongoro kuwa eneo namba moja ambalo kila mtalii duniani angetamani kuliona afrika kampuni ya fasaribookings.com ineitaja nchi yetu ya Tanzania kuwa ndio nchi yenye vivutio vingi duniani .

Tunaipongeza serkali ya awamu ya tano kwa kuzidi kupiga hatua katika kujitangaza kuvutia watalii


USSR
Screenshot_20191230-230414.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
We jamaa unamapenzi ya dhati kwili na hii awamu ya 5,? au kunamgao unapata maana kila baada ya nusu saa lazma uanzishe uzi hum jukwaani

Ni hayo tu:
 
Tanzania hua inaongoza kila kitu, mara uchumi, mara umasikini, utasikia Magufuli anaongoza. Hata sijui nini hatuongozi.
 
Back
Top Bottom