Vivutio vya utalii Tanzania na faida za utalii wa ndani

Vivutio vya utalii Tanzania na faida za utalii wa ndani

6.Ziwa manyara.

Hifadhi hii ya Taifa ya Ziwa Manyara ni maarufu kwa Simba wanaopanda miti na lipo ndani ya hifadhi ambayo ina ndege wengi zaidi ya aina 400 wanaovutia wakiwemo ndege aina ya Korongo ambao huonekana kama pazia kubwa jeupe.


Idadi kubwa ya wanafunzi hapa nchi wanatembelea hifadhi hii na kujionea maajabu yaliyopo ambapo ni pamoja na kujionea wanyama kama Simba, Nyati, Tembo, Nyani, Chui, Pundamilia, na wanyama wengine wanaokula majani na wanaona chemichemi za maji moto yanayobubujika kutoka ardhini bila kukauka kwa mamilioni ya miaka.


Hifadhi hii ipo umbali wa kilomita 126 kutoka Arusha mjini, na wakati mzuri wa kutembelea hifadhi hii ni kuanzia mwezi June hadi Desemba.

IMG_20191123_221232.jpeg
IMG_20191123_221305.jpeg
 
7. Ruaha.
Hifadhi ya Ruaha ndiyo hifadhi kubwa kuliko zote Tanzania ambapo ina ukubwa wa kilomita za mraba 20,226 na ni ya pili kwa ukubwa katika Bara la Afrika baada ya hifadhi ya Kafue iliyopo nchini Zambia.


Ni maarufu kwa kuwa na wanyama aina ya Kudu wakubwa na wadogo ambao hupatikana kwa wingi ambapo hustawi wa hifadhi hii unategemea mto ruaha ambao aina mbalimbali za Samaki, Mamba na viboko hupatikana katika mto huu.


Wanyama kama Pofu na swala hunywa maji katika mto huo wa Ruaha ambao ni mawindo makubwa ya wanyama wakali wakiwemo Simba, Chui, Mbweha, Fisi na Mbwa mwitu. Pia eneo hili Tembo hukusanyika kwa wingi kuliko eneo lolote la hifadhi zilizopo katika nchi za Afrika Mashariki.


Katika hifadhi hii utajionea Magofu yanayosadikiwa kuwa yalikuwa makazi ya watu wa kale katika Kijiji cha Isimila kiasi cha Kilomita 120 kutoka Iringa. Magofu haya ni miongoni mwa historia ya kale barani Afrika.


Wakati mzuri wa kutembelea hifadhi hii ili kuangaliwa wanyama wakubwa ni wakati wa kiangazi kuanzia Mei hadi Desemba, lakini kuangalia ndege na maua wakati wa masika ni Januari –April .


IMG_20191123_222256.jpeg
IMG_20191123_222323.jpeg
 
8. Rubondo.


Hifadhi hii ya Taifa ni kisiwa ambacho kipo pembezoni mwa Ziwa Victoria, ziwa ambalo ni la pili kwa ukubwa duniani likiwa linazungukwa na nchi Tatu, Tanzania, Uganda na Kenya.


Kisiwa hiki kinaundwa na visiwa tisa vidogo vidogo ambapo kisiwa hiki cha Rubondo ni makazi na mazingira muafaka ya kuzaliana Samaki wakiwemo Sato na Sangara wenye ukubwa wa uzito wa kilo hadi 100.


Wanyama wanaopatikana katika hifadhi hiyo ni pamoja na Viboko,Pongo, Nzohe, Fisi maji, Mamba na Pimbi, wanabadilishana makazi na wanyama wengine waliohamishiwa katika hifadhi hii kama Sokwe, Tembo, Mbega weusi na weupe na Twiga.


Wakati mzuri wa kutembelea ni wa Kiangazi June-Agosti aidha wakati wa masika Novemba-Machi kwa ajili ya kuona maua na vipepeo na vile vile Desemba-Februari kwa kuwaona ndege wahamiaji.

Rubondo inajulikana pia kama JURASSIC ISLAND...
IMG_20191123_222922.jpeg
IMG_20191123_222947.jpeg
 
9.Saadani.

Hifadhi hii ipo ufukweni mwa bahari ya Hindi na ni hifadhi pekee Afrika Mashariki inayoungana na Bahari na ipo umbali wa Kilomita 100 kaskazini Magharibi mwa Dar es Salaam na umbali kama huo kusini Magharibi mwa bandari ya Tanga.


Ilianzishwa kama pori la akiba mwaka 1960 na ilitangazwa rasmi kuwa hifadhi ya Taifa mwaka 2005 na ukifika hapo unaweza kuona wanyama kama Simba, Chui, Fisi, Tumbili, swala na ngedere na mtalii mbali ya kuona wanyama pia unapata nafasi ya kuogelea na wakati wa kutembelea ni wakati wowote kwa mwaka ingawa wakati wa masika barabara zinaweza kutopitika kirahisi.


IMG_20191123_223313.jpeg
IMG_20191123_223421.jpeg
IMG_20191123_223450.jpeg
 
10. Udzungwa.

Hifadhi hii ya Milima ya Udzungwa ina hazina nyingi za mimea, ndege na wanyama ambao hazipatikani sehemu nyingine duniani.


Kati ya aina sita za jamii ya nyani wanapatikana katika hifadhi hii, mbili hupatikana katika hifadhi hii pekee; Mbega mwekundu wa Iringa (Iringa red colobus Monkey) na Sanje Crested mangabey’’ ambaye alikuwa hajulikani hadi mwaka 1979 na ndege mbalimbali.


Kivutio kikubwa zaidi ni Mto Sanje ambao unatoa maporomoko ya maji yenye urefu wa mita zipatazo 170 yakianguka kupitia msituni na kutua mithili ya mianzo ya ukungu bondeni.


IMG_20191123_223839.jpeg
IMG_20191123_223901.jpeg
IMG_20191123_223920.jpeg
 
11. Kitulo.

Awali hifadhi hii ilijulikana kwa jina la Elton Plateau baada ya Mvumbuzi Fredrick Elton kupia eneo hili mnamo mwaka 1870, mwaka 1960 Shirika la Chakula na Kilimo (FAO)ilichukua eneo hili kwa ajili ya ukulima wa ngano na ufugaji wa Kondoo.


Baadaye likageuzwa kuwa shamba la Ng’ombe ambalo lipo hadi leo. Mwaka 2005 Kitulo likatangazwa kuwa hifadhi ya Taifa na ni hifadhi ambayo ina maua aina mbalimbali na zaidi ya aina 30 hupatikana Kitulo pekee.


Pia ndiyo eneo pekee Tanzania ambapo ndege aina ya Tandawala machaka (Denhams Bustard) wana makazi na ndani ya hifadhi hii kuna miti aina ya Cidar yenye urefu wa zaidi ya mita 50 na inakadiliwa kuwa mirefu kuliko yote duniani.


Kitulo inafikiwa kwa gari kutoka Chimala kilomita 78 Mashariki mwa mji wa Mbeya. Reli ya TAZARA hupita karibu na hifadhi hii.


IMG_20191123_224418.jpeg
IMG_20191123_224444.jpeg
IMG_20191123_224506.jpeg
IMG_20191123_224533.jpeg
 
Naomba kuona ramani Nyerere national park
Wadau wa Jukwaa heshima kwenu.
Kwaniaba ya Shirika linalojihusisha na Utalii TANZANIA-TANAPA!!
pamoja na Bodi ya Utalii-Tanzania.

Kuwaletea hii platform hapa Jamiiforums itakayohusiana na mambo ya utalii, ili kuhamasisha zaidi utalii wa ndani.

Karibu pia Utushirikishe sehemu ambayo uliwahi kutembelea ndani ya nchi yetu na ikavutia sana. Au kama ulikutana na changamoto yoyote iseme.
Nakaribisha pia Maoni, Mapendekezo na ushauri kuhusiana na mambo ya utalii.

Nawakaribisha sana, kama utakuwa na swali lolote! Litapatiwa ufumbuzi.
Karibuni Wote.

Tanzania ni nzuri yenye vivutio vya kila aina.

View attachment 1270533View attachment 1270534View attachment 1270535

Baadhi ya vivutio ambavyo vinasimamiwa kikamilifu na Shirika la Hifadhi za Taifa la Tanzania (TANAPA) ni pamoja na hifadhi ya Taifa ya Arusha, Gombe, Katavi, Mlima Kilimanjaro, Mahale, Mikumi, Manyara, Ruaha, Rubondo, Serengeti, Saadan, Tarangire, Udzungwa, Kitulo, Mkomazi na Saanane.
Na Kuna hifadhi nyingine mpya Tatu ambazo ni Hifadhi ya Nyerere (Selous), Hifadhi ya Kigosi na Hifadhi ya Mto Uggala.

Hapa chini nitakuletea sifa za Hifadhi moja hadi nyingine.

1.Hifadhi ya Taifa ya Arusha(Arusha National Park)
Hifadhi ya Taifa ya Arusha kuwa ina ukubwa wa kilomita za mraba 328.4, iko umbali wa kilomita 62 (kiasi cha mwendo wa saa moja kwa gari) kutoka mji wa kitalii wa Arusha.


‘’Hifadhi hii ina maeneo matatu muhimu ambayo ni bonde la Ngurdoto (Ngurdoto Crater), maziwa ya Momella ambayo kila moja hutoa mandhari tofauti pamoja na Mlima Meru wenye urefu wa mita 4566 (futi 14990), hali ambayo inaifanya hifadhi kuwa na mazingira ya baridi’’ anasema Mbugi.


Ikumbukwe kuwa hifadhi hii ni maarufu kwa wanyama jamii ya tumbili wajulikanao kama Mbega weusi na weupe. Wanyama wengine wanaopatikana katika hifadhi hii ni pamoja na Twiga,pundamilia, Nyati na digidigi.


Unaweza kuwaona Chui wakibarizi katika vivuli vya matawi ya miti inayokingwa na maaguko ya maji huku makundi kadhaa ya batamaji yakitafuta wadudu katika maziwa ya Momella.

Zaidi ya aina 400 za ndege wamethibitika kupatikana ndani ya hifadhi hii. Safari za miguu na kupanda milima Meru ni moja ya burudani muhimu katika hifadhi ambapo mpandaji anahitaji kati ya siku 3-4 za kupanda mlima.


Wakati mzuri wa kutembelea hifadhi hii ni kati ya mwezi Juni na Februari ingawa mvua inaweza kunyesha mwezi Novemba. Kuna maeneo ya malazi ndani ya hifadhi yenye hadhi tofauti tofauti kama hoteli, nyumba za wageni na makambi ya kupuga mahema ingawa wageni pia wanawezakupata malazi eneo nje ya hifadhi katika mji wa Usa River na Arusha mjini.

2. Hifadhi ya Mahale

Hifadhi hi inaundwa inaundwa na vilima vilivyojipanga na kufunikwa na misitu minene ikiwa na jumla ya kilomita za Mraba 1613. Kama ilivyo hifadhi ya jirani ya kaskazini ya Gombe, hifadhi ya milima ya Mahale ni makazi ya jamii adimu zilizobakia za sokwe barani Afrika.


Mabaki ya matunda yaliyoliwa na kinyesi kibichi ni miongoni mwa alama zitakazokuongoza mgeni hadi kuwafikia viumbe hawa katika misitu iliyopo katika mlima huo na hifadhi hii ipo Maharibi mwa Tanzania ikiwa inapakana na Ziwa Tanganyika.


Ukifika hapo utaona na sehemu ya asili ya watu wa kabila la Watongwe walipokuwa wakiaabudia mizimu yao milimani, kisha kurudi ziwani na kujitumbukiza kwenye maji baridi na maangavu.


Wakati mzuri wa kutembelea hifadhi hii ni kipindi cha kiangazi, kati ya mwezi Mei na Octoba.

4.Gombe

Hifadhi ya Taifa ya Gombe ni ndogo kuliko zote nchini ikiwa na jumla ya kilomota za mraba 52 lakini ina umaarufu mkubwa unaotokana na kuwa na wanyama aina ya Sokwe.


Gombe ni moja ya makzi ya machache yaliyosalia ya Sokwe duniani. Ipo kilomita 16 kaskazini mwa mji wa Kigoma, hifadhi hii ni ukanda mwembamba wa msitu wa mlima unaokatizwa na miteremko mikali inayoingia katika mwambao mwa Ziwa Tanganyika.


Wanyama wengine wanaopatikana katika hifadhi hii ni pamoja na Kima wenye mikia myekundu na kima wa rangi ya bluu na wale wanyama jamii ya Paka hawapo katika hifadhi hii kama vile Simba na Chui hivyo kuifanya kuwa salama kwa safari za miguu.


Unaweza kwenda kutembelea hifadhi hii kwa ndege za abiria au za kukodi kutoka Dar es Salaam hadi Kigoma mjini na baadaye kwa boti mpaka makao makuu ya hifadhi, kadhalika kuna huduma za treni kutoka Mwanza na Dar es Salaam pamoja na barabara itokayo Mwanza, Mbeya na Dar es Salaam.


Wakati mzuri wa kutembelea hifadhi hii ni wakati wa kiangazi, Julai mpaka Octoba kwani Sokwe hawapendi kutembea nyakati za mvua.


View attachment 1270564View attachment 1270565View attachment 1270566
 
Hee!kumbe huu ni ubunifu😅
Aiseeh! jamaa kaja na wazo zuri sana. 😎 juzi hapa nilikuwa nafanya utalii wa ndani na mimi hususani katika wilaya ya RUNGWE, kiukweli hii wilaya imebarikiwa sana na yenyewe kwa vitu vingi. Changamoto nipale sisi wenyewe tumeshindwa kuvitangaza vivutio vyetu.

Ya laiti huu uzi nao siku zausoni ukawa na mwenendo mzuri kama wa walevi na wanywa pombe, tutaweza kufahamu vitu vingi sana.

Labda kwa uchache tu Rungwe Kuna ziwa Ngosi, kijungu, daraja la Mungu, water falls za aina tofauti tofauti, Msitu wa asili, mazao ya kilimo ya kila aina.
Rungwe pia ndio wilaya pekee ambayo msimu wa Parachichi duniani, upo katika kipindi ambacho hakuna nchi yeyote Duniani inayozalisha kwa wakati huo kuanzia mwezi 11 - 3.
 
Aiseeh! jamaa kaja na wazo zuri sana. 😎 juzi hapa nilikuwa nafanya utalii wa ndani na mimi hususani katika wilaya ya RUNGWE, kiukweli hii wilaya imebarikiwa sana na yenyewe kwa vitu vingi. Changamoto nipale sisi wenyewe tumeshindwa kuvitangaza vivutio vyetu.

Ya laiti huu uzi nao siku zausoni ukawa na mwenendo mzuri kama wa walevi na wanywa pombe, tutaweza kufahamu vitu vingi sana.

Labda kwa uchache tu Rungwe Kuna ziwa Ngosi, kijungu, daraja la Mungu, water falls za aina tofauti tofauti, Msitu wa asili, mazao ya kilimo ya kila aina.
Rungwe pia ndio wilaya pekee ambayo msimu wa Parachichi duniani, upo katika kipindi ambacho hakuna nchi yeyote Duniani inayozalisha kwa wakati huo kuanzia mwezi 11 - 3.


Hivi ndo lile ziwa wanalosema watu huruhusiwi kuoga...!
 
Back
Top Bottom