Vivutio vya utalii Tanzania na faida za utalii wa ndani

Vivutio vya utalii Tanzania na faida za utalii wa ndani

Yani mbongo anamchulia mchina POA kuwa ni low class tourist? Wonders shall never end gadambln [emoji23][emoji23]
Mkuu Mchina hajawahi kua high quality tourist wenyewe ni industrious sio kwenye utalii.....hawezi kutoa msada wa bure au kutumia hela kwanjiri ya kuendeleza nchi ya mgine.....mtalii wa kichina hawezi kununua Malaya na kumhonga $20,000 au kumjengea hawala nyumba wanatakaga ngono za bwerere tena of low quality
 
kwahilo tutajishusha class, na Tznia itakua destination of low class tourist.....ndomaana boda boda haruhusiwi kubabe watalii kutoka airport yetu...biashara inahitaji "quality and class" ni neno pana katika biashara ya utalii bro.
tunachotaka ni wananchi wengi wa Tanzania wanufaike kutokana na utalii pia mapato yaongezeke serikalini, sioni faida ya kusifiwa kuwa Tanzania kuna hotel kubwa za kitalii au Tanzania ni destination ya high class tourist wakati wanufaika wakubwa ni watu wachache tena yawezekana sio watanzania.
Tunataka faida kubwa sifa baadae.
 
tunachotaka ni wananchi wengi wa Tanzania wanufaike kutokana na utalii pia mapato yaongezeke serikalini, sioni faida ya kusifiwa kuwa Tanzania kuna hotel kubwa za kitalii au Tanzania ni destination ya high class tourist wakati wanufaika wakubwa ni watu wachache tena yawezekana sio watanzania.
Tunataka faida kubwa sifa baadae.
Mkuu the formular is:
Low quality service=Low profits=Low government revenues= poor services

High quality service=high profits=more government revenues=economic development
 
Mkuu the formular is:
Low quality service=Low profits=Low government revenues= poor services

High quality service=high profits=more government revenues=economic development
haya wachina wasije sasa.
 
Watali wa ki china ni masikini faida yao ndogo sana hawana lexurious spending habits....wanalala hosteli kwa vikundi, cheap airline tena ya kwao vyakula vyao wanakuja navyo, bora tungekomaa na wa utalii wa ndani, nawa japani, Europe, na Africa kuna strong middle class....kuliko hao watafuta masoko kwa bidha zao duni sio watali
Hakuna ubaguzi kwenye biashara, Mwenye hela ndogo atanunua kidogo tulichonacho, mwenye nyingi tutampa zaidi.
 
Sawa ila shida nimoja tu, we shall compromise our quality.....badala ya kua na hotel tutakua na lodge badala kua na first class restaurant tutakua na mama ntilie....kwasababu ya uwezo wa wateja wetu of low class.
Chamsingi walipie na kisha waingie Ngorongoro na Serengeti. Tukifanikiwa kukusanya watalii wengi mengine yatafuata
 
Watali wa ki china ni masikini faida yao ndogo sana hawana lexurious spending habits....wanalala hosteli kwa vikundi, cheap airline tena ya kwao vyakula vyao wanakuja navyo, bora tungekomaa na wa utalii wa ndani, nawa japani, Europe, na Africa kuna strong middle class....kuliko hao watafuta masoko kwa bidha zao duni sio watali
sawa ni ww
 
Sekta ya utalii ni sekta nyeti sana nchini ambapo inaiingizia nchi pesa nyingi za kigeni.Lakini pamoja na hayo nchi yetu kwa asilimia kubwa inategemea watalii kutoka nje ndo waje kuona wanyama wetu na vivutio vingne.

Hivyo basi mimi nitoe ushauri wangu kwa wizara hiyo kuangalia namna gani ya kuboresha vivutio vingne kwa niaba ya watanzania tofauti na kutegemea hifadhi za wanyama tu ukizingatia watanzania ni wavivu,hawapendi na sio wepesi kutumia hela zao kwenda kuangalia wanyama.

Kwa kufanya ivo serikali inaweza ikakusanya pesa nyingi kwa mwaka kulinganisha na sasa japokua sina data kamili ya idadi ya watanzania wanaotembelea hifadhi zetu kwa mwaka.

Hivyo basi serikali ichukue jukumu la kutenga na kuboresha maeneo ya kustarehe mf;-nyerere square(dodoma) na maeneo mengine kama hayo nchini na sehemu izo zizungushiwe wigo ambapo tutakua yunaingia kwa viingilio maalumu tofauti na sasa mtu anaenda kupiga picha,anachafua mazingira bule n.k

Pia serikali iandae maeneo ya watoto kwenda kucheza na kubembea kama ilivo uraya hiyo nayo iwe kwa kiingilio maalumu nayo pia inaweza kuongeza makusanyo kwa mwaka.


Mods naombeni mnisaidie kupangilia mawazo lengo na kufikisha ujumbe kwa serikali ili kujenga uchumi wa kati.
 
Kama huu mkoa wa Dar... Open space zote ziliachwa kwa madhumuni hayo, ya kuweka garden za kupumzikia, bembea za watoto na pia kufanyia shughuli zingine za kawaida kila mtaa...

Tatizo zimevamiwa zote na hakuna anayejali kwa sasa...

Awamu hii at least nyumba nyingi zilizojengewa kwenye maeneo ya wazi zimeshabomolewa, bado kuendelezwa...



Cc: mahondaw
 
Wadau wa Jukwaa heshima kwenu.

Kwa niaba ya Shirika linalojihusisha na Utalii Tanzania -TANAPA pamoja na Bodi ya Utalii-Tanzania. Kuwaletea hii platform hapa Jamiiforums itakayohusiana na mambo ya utalii, ili kuhamasisha zaidi utalii wa ndani.

Karibu pia Utushirikishe sehemu ambayo uliwahi kutembelea ndani ya nchi yetu na ikavutia sana. Au kama ulikutana na changamoto yoyote iseme. Nakaribisha pia Maoni, Mapendekezo na ushauri kuhusiana na mambo ya utalii. Nawakaribisha sana, kama utakuwa na swali lolote! Litapatiwa ufumbuzi.

Karibuni Wote.

Tanzania ni nzuri yenye vivutio vya kila aina.

IMG_20191123_205204.jpeg
FB_IMG_1574531317983.jpeg
FB_IMG_1574531261344.jpeg


Baadhi ya vivutio ambavyo vinasimamiwa kikamilifu na Shirika la Hifadhi za Taifa la Tanzania (TANAPA) ni pamoja na hifadhi ya Taifa ya Arusha, Gombe, Katavi, Mlima Kilimanjaro, Mahale, Mikumi, Manyara, Ruaha, Rubondo, Serengeti, Saadan, Tarangire, Udzungwa, Kitulo, Mkomazi na Saanane.
Na Kuna hifadhi nyingine mpya Tatu ambazo ni Hifadhi ya Nyerere (Selous), Hifadhi ya Kigosi na Hifadhi ya Mto Uggala.

Hapa chini nitakuletea sifa za Hifadhi moja hadi nyingine.

1.Hifadhi ya Taifa ya Arusha(Arusha National Park)
Hifadhi ya Taifa ya Arusha kuwa ina ukubwa wa kilomita za mraba 328.4, iko umbali wa kilomita 62 (kiasi cha mwendo wa saa moja kwa gari) kutoka mji wa kitalii wa Arusha.

‘’Hifadhi hii ina maeneo matatu muhimu ambayo ni bonde la Ngurdoto (Ngurdoto Crater), maziwa ya Momella ambayo kila moja hutoa mandhari tofauti pamoja na Mlima Meru wenye urefu wa mita 4566 (futi 14990), hali ambayo inaifanya hifadhi kuwa na mazingira ya baridi’’ anasema Mbugi.

Ikumbukwe kuwa hifadhi hii ni maarufu kwa wanyama jamii ya tumbili wajulikanao kama Mbega weusi na weupe. Wanyama wengine wanaopatikana katika hifadhi hii ni pamoja na Twiga,pundamilia, Nyati na digidigi.

Unaweza kuwaona Chui wakibarizi katika vivuli vya matawi ya miti inayokingwa na maaguko ya maji huku makundi kadhaa ya batamaji yakitafuta wadudu katika maziwa ya Momella.

Zaidi ya aina 400 za ndege wamethibitika kupatikana ndani ya hifadhi hii. Safari za miguu na kupanda milima Meru ni moja ya burudani muhimu katika hifadhi ambapo mpandaji anahitaji kati ya siku 3-4 za kupanda mlima.

Wakati mzuri wa kutembelea hifadhi hii ni kati ya mwezi Juni na Februari ingawa mvua inaweza kunyesha mwezi Novemba. Kuna maeneo ya malazi ndani ya hifadhi yenye hadhi tofauti tofauti kama hoteli, nyumba za wageni na makambi ya kupuga mahema ingawa wageni pia wanawezakupata malazi eneo nje ya hifadhi katika mji wa Usa River na Arusha mjini.

2. Hifadhi ya Mahale

Hifadhi hi inaundwa inaundwa na vilima vilivyojipanga na kufunikwa na misitu minene ikiwa na jumla ya kilomita za Mraba 1613. Kama ilivyo hifadhi ya jirani ya kaskazini ya Gombe, hifadhi ya milima ya Mahale ni makazi ya jamii adimu zilizobakia za sokwe barani Afrika.

Mabaki ya matunda yaliyoliwa na kinyesi kibichi ni miongoni mwa alama zitakazokuongoza mgeni hadi kuwafikia viumbe hawa katika misitu iliyopo katika mlima huo na hifadhi hii ipo Maharibi mwa Tanzania ikiwa inapakana na Ziwa Tanganyika.

Ukifika hapo utaona na sehemu ya asili ya watu wa kabila la Watongwe walipokuwa wakiaabudia mizimu yao milimani, kisha kurudi ziwani na kujitumbukiza kwenye maji baridi na maangavu.

Wakati mzuri wa kutembelea hifadhi hii ni kipindi cha kiangazi, kati ya mwezi Mei na Octoba.

4.Gombe

Hifadhi ya Taifa ya Gombe ni ndogo kuliko zote nchini ikiwa na jumla ya kilomota za mraba 52 lakini ina umaarufu mkubwa unaotokana na kuwa na wanyama aina ya Sokwe.

Gombe ni moja ya makzi ya machache yaliyosalia ya Sokwe duniani. Ipo kilomita 16 kaskazini mwa mji wa Kigoma, hifadhi hii ni ukanda mwembamba wa msitu wa mlima unaokatizwa na miteremko mikali inayoingia katika mwambao mwa Ziwa Tanganyika.

Wanyama wengine wanaopatikana katika hifadhi hii ni pamoja na Kima wenye mikia myekundu na kima wa rangi ya bluu na wale wanyama jamii ya Paka hawapo katika hifadhi hii kama vile Simba na Chui hivyo kuifanya kuwa salama kwa safari za miguu.

Unaweza kwenda kutembelea hifadhi hii kwa ndege za abiria au za kukodi kutoka Dar es Salaam hadi Kigoma mjini na baadaye kwa boti mpaka makao makuu ya hifadhi, kadhalika kuna huduma za treni kutoka Mwanza na Dar es Salaam pamoja na barabara itokayo Mwanza, Mbeya na Dar es Salaam.

Wakati mzuri wa kutembelea hifadhi hii ni wakati wa kiangazi, Julai mpaka Octoba kwani Sokwe hawapendi kutembea nyakati za mvua.
 
Umeweka Makala fupi sana mkuu, ulitakiwa utambulishe vivutio vyote tulivyonavyo na mahali vilipo ili kuwavutia wasomaji kabla hujakaribisha maswali.
Kuna watanzania wengi hawajui idadi ya mbuga na vivutio vingine.
Kwakuwa umekuja hapa kwa niaba ya TANAPA, nadhani uzi huu unaweza kuwa suluhisho kama mtakuwa wabunifu
 
Umeweka Makala fupi sana mkuu, ulitakiwa utambulishe vivutio vyote tulivyonavyo na mahali vilipo ili kuwavutia wasomaji kabla hujakaribisha maswali.
Kuna watanzania wengi hawajui idadi ya mbuga na vivutio vingine.
Kwakuwa umekuja hapa kwa niaba ya TANAPA, nadhani uzi huu unaweza kuwa suluhisho kama mtakuwa wabunifu
Navileta mkuu wangu.
 
Northen zone nimebakisha Mkomazi National park tu, na kilimanjaro National Park ndio eneo nililojikita zaidi
 
4.Gombe

Hifadhi ya Taifa ya Gombe ni ndogo kuliko zote nchini ikiwa na jumla ya kilomota za mraba 52 lakini ina umaarufu mkubwa unaotokana na kuwa na wanyama aina ya Sokwe.


Gombe ni moja ya makzi ya machache yaliyosalia ya Sokwe duniani. Ipo kilomita 16 kaskazini mwa mji wa Kigoma, hifadhi hii ni ukanda mwembamba wa msitu wa mlima unaokatizwa na miteremko mikali inayoingia katika mwambao mwa Ziwa Tanganyika.


Wanyama wengine wanaopatikana katika hifadhi hii ni pamoja na Kima wenye mikia myekundu na kima wa rangi ya bluu na wale wanyama jamii ya Paka hawapo katika hifadhi hii kama vile Simba na Chui hivyo kuifanya kuwa salama kwa safari za miguu.


Unaweza kwenda kutembelea hifadhi hii kwa ndege za abiria au za kukodi kutoka Dar es Salaam hadi Kigoma mjini na baadaye kwa boti mpaka makao makuu ya hifadhi, kadhalika kuna huduma za treni kutoka Mwanza na Dar es Salaam pamoja na barabara itokayo Mwanza, Mbeya na Dar es Salaam.


Wakati mzuri wa kutembelea hifadhi hii ni wakati wa kiangazi, Julai mpaka Octoba kwani Sokwe hawapendi kutembea nyakati za mvua.


IMG_20191123_220316.jpeg
IMG_20191123_220340.jpeg
IMG_20191123_220452.jpeg
 
5. Katavi

Hifadhi ya Taifa ya Katavi, ina ukubwa wa eneo la kilomita za mraba 4471, iko juu ya uwanda mpana wa mafuriko kusini magharibi mwa Tanzania katika mkoa wa Katavi zamani Rukwa. Mandhari kuu katika hifadhi hii ni maeneo yenye maji maji yene majani, mimea mithili ya mitende pamoja na mto Katuma.


Katavi inasifika kwa kuwa na idadi kubwa ya Mambo na voboko na ni kawaida kuyaona makundi makubwa ya Tembo ya kila majani katika mabwawa huku miili yao ikiwa imefunikwa na maji na magugu.


Hifadhi hii inafikiwa kwa ndege za kukodi kutoka Dar es Salaam na Arusha na kwa Gari kutoka Mbeya na pia kwa kupitia mkoani Kigoma wakati wa kiangazi Mei-Octoba na kuanzia katikati ya Desemba hadi Februari. Inafikika pia kwa reli kutoka Dar es Salaam kupitia Tabora hadi mpanda na kwa gari kutoka Mpanda.

IMG_20191123_220801.jpeg
IMG_20191123_220825.jpeg
download%20(1).jpeg
 
Back
Top Bottom