Vodacom: Mamilioni wameacha kutumia M-Mpesa hasa vijijini, ni hatari kwa biashara yetu

Eti nimemsikia Mwigulu akibwabwaja kuwa walipunguza kodi kwenye betting ili kuwashawishi watanzania kutokutumia betting companies za nje
 
Kuna rafiki yangu alitaka nimkopeshe hela ndogo. Nimegoma kumtumia mpaka alipokuja kuitwaa kwa mkono wala hakuwa mbali. Kuna hela naidai naenda keshokutwa kuifuata, ni mgomo nimeweka siwezi tuma au kupokea hela within 10km, si ni bora hiyo 2000 nimlipe bodaboda nimuongezee mzunguko kwa wajasiriamali kuliko niwape CCM na mademu zao
 
Mwigulu Bado anandoto za urais so anajaribu kumharibia mama bila kujua anajiharibia pia
 
Zungu alishauri vyema sana, kukatwa sh 50 tu.
Hata wangeongeza sh 200 kwa muamala mbona wangepata pesa kibao tu
 
Good, CCM ni shetani
 
CCM tunaupiga mwingi. Bunge limepitisha sheria kisha Mama akasaini. Wananchi wamegomea sasa inabidi bunge liitwe kwa dharura lifute hiyo sheria.
Mwigulu na Majaliwa wakifuta hiyo sheria bila kuitisha bunge tutajua hatuna bunge bali kikao cha wa.huni!
 
Maisha yanakuwa magumu kila kukicha..roho za kwanini za Wabunge ndizo zimetufikisha hapa.Kazi yao ni ndioo
 
Makampuni haya yanaangalia sana maslahi yao tu kuliko jamii,mawakala wao hulipwa kamisheni ndogo sana ukilinganisha na makato wanayokuwa wamemkata mteja. Mfano ktk makato ya sh 1450 unakuta wakala analipwa si zaidi ya sh 200, kiasi kinachobi wanajua wao, wanailaumu Serikali ila wao ndo wanaona wanahaki yakuwapunja mawakala na selikali yaina haki yakupata gawio... Kama wanauchungu 1-wapunguze makato wao kwanza ili kuwavutia wateja,2-waongeze kamisheni ziwe kama zamani.Hapo ndo watakuwa nahaki yakulalamikia biashara kuwa mbaya. Bora niichangie serikaliyangu kuliko kumnufaisha mwenyekampuni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…