Vodacom: Mamilioni wameacha kutumia M-Mpesa hasa vijijini, ni hatari kwa biashara yetu

Vodacom: Mamilioni wameacha kutumia M-Mpesa hasa vijijini, ni hatari kwa biashara yetu

Siyo kweli hata mimi ni wakala tunalipwa 75%
Makampuni haya yanaangalia sana maslahi yao tu kuliko jamii,mawakala wao hulipwa kamisheni ndogo sana ukilinganisha na makato wanayokuwa wamemkata mteja. Mfano ktk makato ya sh 1450 unakuta wakala analipwa si zaidi ya sh 200...
 
Ila hii tozo inaweza lipia mishahara ya waajiriwa wapya kabisa, serikali ingetangaza ajira zakutosha mama angekuwa kaupiga mwingi sana

Sent from my TECNO KITOCHI using JamiiForums mobile app
 
ukipiga hesabu ya haraka haraka endapo mtu anakudai elfu 50, na unataka umtumie apate elfu 50 kama ilivyo, inatakiwa uwe na ziada ya 8100, kiwango ambocho ni kikubwa sana, yani gharama ya kutuma, gharama ya kutolea na kodi ya uzalendo iliyopendekezwa na ndugu zungu.
 
Hawa wanatutoa kwenye lengo la katiba mpya

My take Tozo zirudi za zamani na katiba tuendelee kudai.
Screenshot_20210719-180409.jpg
 
Four days after the Electronic and Postal Communication Act (CAP 306) came into effect, the Tanzania Mobile Network Operators Association (Tamnoa) has said the business has dropped drastically, therefore asking government to amend the new charges
Walio pendekeza na kutunga hiyo sheria niwabunge wa ccm hawa jamaa bado wana chembe chembe za jiwe.mim nishauli kama siyo dhalula Kali hususani mgonjwa usitume pesa kivyovyote watakoma tuu
 
Tatizo linatokana na wabunge wanaodhani wanaweza kuwaamulia wananchi kila jambo bila kuwashirikisha na kupokea mawazo yao kabla ya kufanya majumuisho bungeni.

Hii tozo waliyoweka ilikuwa ni wazo na mbunge mmoja ambaye alisuggest kiujumla. Wazo hilo lingeweza kuwa na manufaa kama wangeshirikisha wananchi, wafanyabiashara na wadau wa uchumi especially micro economy.

Sikutarajia kuona Mwigulu kama PhD holder wa mambo ya uchumi analichukua wazo la mbunge na kuweka tozo kwa haraka bila kuangalia tozo iwe wapi, kwa Kiwango gani na viwango viwekwe kwa kuangalia Hali halisi ya uchumi na mzunguko wa pesa kiujumla.

Pia nilitarajia Mwigulu angetoa maelezo ya sababu zilizowafanya kuweka viwango vya tozo na kwa nini mtumaji na mpokeaji wakatwe ingali hii ni levy tu hapo kodi imekatwa pia tena kwa wote.

Haiingii akilini mtu anayetoa 5000 akatwe pesa yote hiyo, wamekokotoa vipi kufikia hicho Kiwango? Wamemshirikisha nani? Laiti wangeangalia record ya viwango vya miamala wangetambua kwamba watu wengi wanatumia na kutoa pesa chini ya 50,000. Hii ukimkata hayo makato plus Kodi anabaki na na pesa ndogo sana ambayo unakuwa umemuonea sana.

Mie naona Mwigulu ameshindwa kusimamia na kumshauri Rais kwenye masuala ya uchumi, ni wakati sahihi aenguliwe kwenye hiyo nafasi amefamya mengi ya hovyo kwa muda mfupi sana.

Mwigulu akiachwa hapo atakuwa kama Kabudi alivyokuwa anamuingiza chaka Magufuli. Huyu sio wa kumchekea.
 
Na bado tutaendelea kutokuitumia hii huduma mpaka wakatane wao kwenye mishahara yao
Nalog off
 
Back
Top Bottom