Vyakula vipi umekula pindi umepigika vilivyo?

Vyakula vipi umekula pindi umepigika vilivyo?

1. Mkate na maji. Hapo ni kipindi nikiwa Chuoni. Wenzangu walikuwa wakinipitia room kwangu tukale mghahawani, nilikuwa nikiwaambia nipo "busy". Wakishaondoka tu, nafunga mlango, nachukua mkate wangu "kabatini" na kikombe cha maji na kuanza kuubugia kwa haraka nisije nikakutwa. Kwanza, mkate wenyewe nilikuwa naula kwa bajeti ili usiishe kabla ya muda nilioupangia.

2. Katika harakati za utafutaji nikiwa mikoani, kuna kipindi mambo ya kifedha yaliniendea kombo. Kuna wakati nilikuwa nikinywa kikombe cha uji wa sh 300/= (wa kununua kwa mama lishe) mara moja kwa siku, saa moja Jioni hadi kesho yake tena saa moja Jioni ndiyo nije kuunywa mwingine, na kuna wakati nilishinda njaa na kulala njaa bila kula chochote, na kuna wakati nilijipikia uji mkavu - haukuwa na sukari wala limao, ni maji na unga tu, na mambo yakasonga mbele.

Hayo ni kwa uchache tu, lakini matukio ni mengi. Ndiyo maana wakasema"ukiliona dume la nyani limenenepa ujue limekwepa mishale mingi"
 
Nilishawahi kula ugali na tomato ila ilikuwa ni kwasababu nilichelewa kutafuta chakula na nilikuwa mkoani( mbeya). Lile baridi lilijua kunifunza adabu ule usiku.

Maana sehemu nilipokuwa kutoka hadi kwenda town kulipochangamka ilikuwa mtihani na Mbeya unajua balaa lake usiku baridi kali la mwezi wa sita.

Hotpot ilikuwa na ugali wa mchana, aiseee niliruka nao na tomato ile njaa ilikuwa inauma hadi kwenye mifupa.
 
Bado sijawahi kula vya ajabu ata niwe katika hali gani...
Mana mi kila mtu ni ndugu.

Na huwa mkweli kabisa sina haja ya kujibana nafika kwa mtu namwambia ukweli bana eeeh mi sijala nina njaa..
😂😂😂😂😂😂😂
 
KATIKA MIDA HILE YA KUTAFUTA , INAFIKIA HATUA UNAKULA ILI UISHI YAANI UNAKULA CHOCHOTE ,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,, MIMI NSHAKULA UGALI NA CHUMVI................MIXER MAJI YA KUNYWA................................








































WEWE JE ?
Hatari na nusu. Unga ulikosa hata wa uji. Unaenda kwa jirani unasubiri hadiwapike ule. Jirani mkuda anasubiri uondokendipoale
 
Back
Top Bottom