Vyombo vya Habari vya Kimataifa vinapata faida gani kuzusha uongo kuihusu Tanzania na Rais Magufuli ?!. Angalia uongo/uzushi wa The Guardian la UK!

Kwa mwandishi mkubwa kama wanavyokuita, hukustahili kuandika na kukosoa ukweli.

Ivi wewe mayalla, kwanini usipite njia ya mkato kwa kwenda moja kwa moja kwa Rais nakuomba nafasi unayoipigania kuipata serikalini?

Hawa mnaowaita mabeberu kwanini waichukie tanzania tu, mnanini cha kuzidi nchi zingine duniani?
Maendeleo yapo tanzania tu?

Acha ulimbukeni mdogo wangu, hizi imani ni za kitoto za kuamini baba yako ana nguvu za kuweza kupiga kila mwanaume.
 
Huyu jamaa tufike mahali tususue post zake tusiwe tunachangia Kwa sababu anasumbuliwa na vitu viwili
1.uccm(tabia za kishetani)
2.ukabila(ubinafsi Wa kujiona mjuaji)

Swelana.
Vp safari hii atamuangushia tena Erick Kabendera?? Maana naona kama kuna kahoja anataka kukijenga kama kawaida yake.
 
Kwani wanataka taarifa zetu za nini si wafatilie maisha yao sisi nchi huru waache upuuzi wao kenge hao wanaua watu weusi huko kwao af wanataka kutuingilia hadi huku kwetu
 
Swali kwanini waiseme vibaya Tz na why iwe wakati wa utawala huu? ukiona hivyo ujue kuna jambo halipo sawa jambo tunajificha kwenye kivuli cha uzalendo.
 
Very soon mayalla anaingia kwenye ignore list yangu, kashakuwa mp.uu.zi siku hizi. Kweli huwezi kuongea huku unakula na kama ukiongea basi lazima utasifia chakula unachokula.
 
Ukishakula nyama ya mtu huwezi kuacha.

Pole sana Kabendera huko uliko
 
Hawa ni watu waongo sana eti wanazungumzia mpaka ule utani wa Rc Makonda kuhusu kula bata wao wanasema Rais ndo aliagiza

Mie nadhan ni wakati muafaka kwa Taifa kuwa kitu kimoja kwenye Agenda za Kitaifa kupinga haya mapotoshi
 
mkuu, ukweli ni upi? huo ukweli umetangazwa na nani?

Kenya iliyopima wananchi wake kwa maelfu na yenye population ndogo kuliko sisi ina maambukizi zaidi ya 1,000 na vifo karibia 50.... huku Tanzania, hakuna taarifa zozote rasmi kwa hiyo tafsiri yake ni kwamba imeruhusu watu waendelee ku speculate.

na tunaojua kidogo hesabu za kujumlisha na kutoa tuta speculate kama ifuatavyo:

tutalinganisha na Z'bar yenye population ya watu 1.5M huku taarifa rasmi zinaonyesha kuwa kuna vifo 16. so, hatutakuwa tumefanya makosa kimahesabu tukisema Tanganyika yenye population around 55M vifo ni zaidi ya 500!

for lack of transparency kwa upande wetu, tumeruhusu hata wasio Watanzania nao wa speculate kivyao (TZ US Embassy, WHO, CNN, BBC, DW, VoA, Aljazeera, nk).

tusimlaumu mtu. hili tumelikoroga wenyewe, tulinywe!

na tumeshuhudia siku za karibuni watu wakizikwa kila mahali chini ya usimamizi wa magari yenye namba za usajiri zinazoanzia SM.

mkuu, tumekwenda shule japo si kubwa sana ujue!
 
Mzee wangu Mayalla umenichekesha sana hapa

27. and won his nickname ‘The Bulldozer’ as a minister, as a populist who likes to fly in the face of convention. Sentence hii hata mimi imenipiga change, hizi lugha za wenzetu, aliyeelewa hapo, msaada afadhali!.
 
Hao wanaosema serikali inaficha data za Corona virus. Si wangelitoa zao za ukweli? Alafu usimpangie mtoa mada cha kuandika hii ni haki yake kwa mujibu wa katiba ya JMT ibara ya 18.
 
Ni haki yake ya kikatiba.
 
Lawama zote kwa Mkapa mwaka 1995
 
Paschal hebu tumegee mrejesho wa kikao cha Wizara ya Mambo ya nje na Balozi wa Marekani.

Kama Tanzania angejua mwanamke nisingefikiria hata kumchiti, jinsi ninavyo mthamini na kumpenda kwamwingine singeenda...
 
Mkuu kwa msisitizo wa takwimu nawe ni mwanahabari mbobezi, hebu tupe takwimu zako binafsi tukuamini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…