Vyuo vya private na migpa mikubwa kwa nini?

Vyuo vya private na migpa mikubwa kwa nini?

Kama kungekuwa na mtihani wa mwisho wa necta kama diploma ya ualimu, naamini vyuo vikuu vya private visingekuwa na wahitimu wenye GPA kubwa namna hiyo. Wanatumia advantage ya closed system kumwaga GPA kama njugu kwa wateja wao. Serikali iliangalie hili kwa jicho la mamba.

Mkuu umenena
 
Mtoa uzi huu hana ufahamu wa kutosha kuhusu elimu ya Tz. Kwa taarifa yako watu wenye division III waliotoka shule za kata wana akili nyingi mno kuliko wale waliopata division I kutoka shule za academics na 'International'. Kumbuka waliopata division III toka shule za kata ni wale waliosoma wenyewe bila walimu, maabara, dawati, vitabu, umeme, usafiri, bweni, chakula, n.k. hivyo waliweza kutumia akili na vipaji vyao wao wenyewe hadi wakapata hiyo division III. sasa wanapofika Chuo Kikuu kwenye mazingira bora ya kusoma na kujifunzia yenye walimu, maabara, vitabu, umeme, bumu la bodi ya mikopo, n.k huwa wanakuwa bora sana kuliko wale kuku wa kizungu waliotoka shule za International (spoon fed students) ambao wengi wao huchaguliwa vyuo vya government visivyokuwa na walimu wenye morali, vitendea-kazi na udahili wa wanafunzi wengi wasiolingana na vitendea kazi vilivyoko (walimu, maabara, mabweni, nk.). Asilimia 80 ya wakufunzi wa vyuo vya umma wanaacha kufundisha vyuo vyao na kwenda kufundisha vyuo vya private kupata chochote kitu mifukoni. Hivyo wale wanafuzi waliotoka shule za kilalahoi huwa wanakutana na walimu na mazingira bora vyuo vya private na wale waliotoka shule za vigogo wanakwenda kukutana na shule za government zisizokuwa na walimu na mazingira duni ya kusoma na kujifunza inakuwa sasa ngoma draw nkondo igwa. Utashangaa wanafunzi waliojiunga chuoni na dision III za shule za kata unasoma bila kupata supplementary kuliko wale waliojiunga na division I ya kupewa kule international secondary school ingawa wanajua Kiingereza kizuri kuliko wale wa Kata.
REPLY TO KAVULATA
MBONA WENGI TU WAMETOKA SHULE ZA PRIVATE WAPO VYUO VYA PRIVATE.WENGI WALIOTOKA SHULE ZA GVT WAPO VYUO VYA GVT BWANA MBONA,MFANO KUACHUO FULANI CHA GVT WAMEJAA WATU KUTOKA GOVERMENT.NA PIA WATU WENGI KUTOKA SHULE ZA GOVT ADVANCE NDIO WANAFANYA VIZURI FORM SIX ,PIA WENGI HAWAA UWEZO WA KUJILIPIA PRIVATE,WENGI VYUO VYA PRIVATE WANAJILIPIA ADA BILA KUTEGEMEA BOOM,MFAO MTU ANALIPA ADA YA SEMISTER MILIONI NDUGU,JE MTOTO WA MKULIMA ANAWEZA KWENDA HUKO?WENGI NI WASHUA WAPO VYUO VYA PRIVATE.HALAFU VYUO VINGI VYA PRIVATE HATA LECTURE ZAKE LAINI ZA KUBEMBELEZA NDUGU WE PELELEZA NDUGU UONE MIMI SHAHIDI MKUU.MIMI SISEMI KWA MAJUNGU HUO NDIO UKWELI.
 
Wengi wa graduates kutoka Private universities hawana lolote. GPA ya 4.6 ya LLB hata kiingereza ni taabu. Kwenye Law school ndiyo utakuta wengi wana referral kibao.
 
WE JAMAA BOYA KWELI, TUMAINI MAKUKIRA NANI KAKWAMBIA KUNA MWANACHUO ANAPATA GPA 4.7 LLB? KUPATA 3.5 NI SHIDAA, FANYA UTAFITI KAKA USIKuRUPUKE

Hahahah mitihani yenu ninayo ni rahisi kupita maelezo
 
Wengi wa graduates kutoka Private universities hawana lolote. GPA ya 4.6 ya LLB hata kiingereza ni taabu. Kwenye Law school ndiyo utakuta wengi wana referral kibao.

Umema mkuu
 
acha majungu we kiumbe mbona elimu yako haikusaidii....! Kama machaguo yangu nimechagua 2 private utasema nimepata division three mbaya kwa kuwa nipo private! Think b4 u done that's why unapata GPA ndogo unakurupuka mpigamsul!
 
Ngoja nikuambie kitu, Private Universities hata waalimu wao hawana vigezo vya kufundisha University! Nimemaliza chuo cha serikali, kuna jamaa zangu wa3 wote wana GPA za 3.1. mmoja anafundisha SAUT, mwingine MWENGE, mwingine RUCO.. unategemea nini kuajiri wasiojua...Obvious hata mwanafunzi akiandika pumba atampatia marks tu.

Naomba management za vyuo private waangalie kuanzia kwenye kuajiri, wazingatie 3.5 and above!

Pameanza kuwepo utamaduni wa vijana wa kileo kusema vitu kwa seeping statements na generalizations bila utafiti. Yaani mtu anakurupuka na ki-assumption chake na kuhitimisha ndio ukweli.

Vyuo vyote vinadhibitiwa na Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania. Na moja wapo ya conditions muhimu kwa kila chuo ni kuhakikisha members of faculty wanakuwa na sifa zinazotakiwa. Moja ya sifa hizo ni GPA isiyopungua 3.5 kwa Wakufunzi wanafunzi (TA)wenye Shahada ya kwanza na 4 kwa Wahadhiri Wasaidizi/Shahada za Uzamili. Haitokaa itokee mtu mwenye GPA chini ya 3.5 Undergraduate afanye kazi katika taasisi za elimu ya juu, iwe za umma au binafsi.

Najua kuna cases chache zilikuwepo wakati vyuo hivi vinaanza hasa hasa miaka ya 2000, lakini si kwa hivi sasa. Na kama wapo vihiyo ni wa kujificha sana. Ukiripoti TCU wanawajibishwa mara moja.

Tuache kueneza propaganda zisizo na mashiko wala ushahidi.
 
1.mfumo wa elimu ya tanzania kuanzia form one mpaka form six unazipendelea shule za serikali kwa kuzipa nafasi ya kuchagua wanafunzi waliofaulu tu na makapi wanaachiwa ndugu zangu wa private.


MAELEZO HAYA YANATOA FUNDISHO KUWA ELIMU YA SERIKALI SI BORA KULIKO YA PRIVATE NA SERIKALI KAZI YAO NI KUHARIBU FUTURE ZA WATOTO ALAFU WANAWAACHA ILI TENA WAOKOLEWE NA PRIVATE SCHOOLS KIDATO CHA TANO NA SITA BAADA YA KUACHWA.


KIFUPI NI KWAMBA PRIVATE SECTORS WAMEONYESHA UWEZO MZURI WA KUWAFUNDISHA WATOTO NA KUFAULU NA HAPA HAKUNA ANAEBISHA KWA SABABU WANAFUNZI WOTE WANASOMA KWA SYLLABUS MOJA NA MITIHANI NI ILE ILE ILA TATIZO LINAKUJA VYUONI AMBAPO WATU HAWANA SAME SYLLABUS NA MITIHANI YAO NI TOFAUTI NA NDIPO UNAANZA KUSIKIA MAJINA YA AJABU AJABU KWA HIVI VYUO KISA WANAFUNZI WAKE WANA GPA KUBWA.



2.udahili wa vyuoni na hoja za wanaosema vyuo vya watu binafisi havina ubora.

-kwanza vyuo hivi vinadahili wanafunzi wenye marks za chini sana mpaka hata three za 17 lakini mwisho wanapata GPA kubwa za 4 na kuendelea(si maneno yangu bali ni hoja ya watu hao)

MAJIBU KWA HOJA HII.

kabla hujafikiri chochote kuhusu majibu kwa hili unapaswa kujua pia kwa nini shule za private zinachukua wanafunzi hata waliofeli la saba lakini wanaibuka na one?



MAPUNGUFU KATIKA HOJA YA MATOKEO KAMA KIPIMO CHA UBORA WA MWANAFUNZI.
-kwanza matokeo yanayotazamwa na wengi ni ya form six pekee,hawajui kuna wanafunzi wana one na two za form six na wapo udsm ama udom ama mzumbe ama sua ila form four walikuwa na four ama three za kuchechemea na waliokolewa na private, ama hawajui kuna wanafunzi wana three za 17 form six ila wana wana one za single digit O level ila kisa wapo vyu vya kitongoji ni tatizo.


NADHANI PIA MMEJIFUNZA KITU HAPA JUU YA UBORA WA MWANAFUNZI KUWA UNATEGEMEA MAMBO MENGI SANA NA HATA UFAULU WA MWANAFUNZI UNATEGEMEA MAMBO MENGI SANA IKIWEMO YEYE MWENYEWE NA MAZINGIRA YA SHULE AMA CHUO

MWISHO NINGESHAURI WATU MJIPAMBANUE KWA MAFANIKIO YENU BAADA YA KUMALIZA VYUO KAMA UBORA WA ELUMU YENU NA SI KULAZIMISHA KUPATA SIFA KISA UMESOMA CHUO FULANI AMA KUMUBEZA MWINGINE KISA KASOMA CHUO FULANI.


1. Naungana nawe kushangaa tabia ya ajabu ya watu wanaojiita wamesoma kujisifia vyuo walivyosoma badala ya uwezo binafsi. Mwisho wa siku (generally speaking) hutaheshimika kwa jina la chuo chako isipokuwa quality ya unachokifanya/sema. Vinginevyo, labda utembee na label itakayokutambulisha ulikotoka (which is nonesense).

2. Je, ni kweli mfumo wa elimu unapendelea shule za serikali? Swali hili lina pande nyingi za shilingi. Hivi tunaposema serikali inapendelea shule zake tunaaminisha nini? Selection? Au mazingira ya ufundishaji na hamasa ya walimu kufanya kazi?
Kuhusu selection, mambo yamebadilika siku hizi. Zamani, ukienda shule za binafsi ilionekana huna uwezo kwa sababu mazingira ya shule za umma yalikuwa bora na hivyo watu walikimbilia mazingira bora. Siku hizi, kwa sababu ya ubovu wa shule za umma (sijui kama ndio kupendelewa?) mambo yamebadilika. Wazazi wengi wenye uwezo wa fedha wanawapeleka watoto wao shule binafsi. Ushahidi wa hili ni kwamba shule nyingi nzuri za binafsi hufanya selection kabla ya shule za serikali. The best brains (wengi) wenye uwezo kifedha wanaenda shule za binafsi, waliobaki (wasio na uwezo au kwa sababu za kiuchumi) wanaenda shule zetu za kata kusubiri kufeli.
Hivyo utaona kuwa upendeleo unaosemekana kufanywa na serikali kwa shule zake kwa maana ya selection ni nadharia tu. Wengi "wanaopendelewa" kwenda kwenye shule za umma, na wenywe nafasi kiuchumi, hawaendi labda wakipangwa shule zenye nafuu kama zile za serikali (za zamani) kwa imani kwamba kule kuna walimu na wnaafundisha.

3. Kwa nini shule za binafsi zinafanya vizuri?
Well, sababu ni nyingi. Moja, nyingi (hasa zile zenye majina) zinawalipa walimu wake vizuri na zina mifumo inayowabana wafundishe kwa ufanisi. Kwa mfano wakati mwalimu mpya mwenye Shahada anaweza kulipwa 400K serikalini, mwenzake anaweza kulipwa mpaka 1,500K kwenye shule binafsi. Wakati mwalimu wa serikalini hana morali ya kufundisha na hajawekewa mfumo wa kumdhibiti kufundisha, mwenzake wa shule binafsi ana morali na anadhibitiwa afundishe.

4. Hali ikoje vyuo vikuu (private v/s public)?.

Ili tuone kama yanayoendelea sekondari ndiyo yanayoendelea Vyuo Vikuu, ni vyema kujiuliza ubora wa elimu unategemea nini? Ubora wa elimu ya juu unategemea mambo mengi. Lakini kwa uchache kuna mambo manne makubwa.

Moja, ni mitaala/curriculum bora inayotafsiriwa kwa ufanisi kazini. Mtaala bora ni ule unaomnoa mwanafunzi wa elimu ya juu kumwelezesha kuboresha maisha ya jamii katika eneo alilosomea kwa ufanisi.

Pili, ubora wa members of the Faculty/wanataaluma waliobobea kwenye maeneo yao. Kuanzia ngazi ya chini kabisa ya TA mpaka juu, ni lazima Chuo Kikuu kihakikishe kina watu wenye uwezo kitaaluma kwa maana ya ufundishaji makini na kufanya tafiti zenye kuchangia katika body of knowledge kwa maeneo yao. Ndio maana kigezo cha kupanda madaraja kwa Walimu/Academicians wa vyuo vikuu si muda kazini bali idadi na kiwango cha tafiti walizofanya.

Tatu, ubora wa mazingira ya kufundishia na kujifunzia. Hapa tuna maana ya vifaa, vitabu, machapisho, maabara zenye viwango, mfumo mzuri wa kuwezesha wanafunzi kujenga tabia ya kutafiti na kadhalika.

Nne, ni ubora wa wanafunzi wanaochaguliwa. Hatuzungumzii matokeo/grades (ambazo nyingi zinaleta maswali mengi kuliko majibu) bali uwezo halisi wa wanafunzi (thinking, reasoning, originality, imagination, talents na kadhalika). Mtu anaweza kuwa na Division III kwenye mazingira mabovu lakini kichwa kimetulia kuliko mwenzake mwenye Division I ya kukaririshwa na mwalimu.

Baada ya kuangalia vigezo hivyo, sasa tuvigeukie vyuo vyetu kwa swali la jumla: Je, vinakidhi vigezo vya kutoa elimu bora? Je, vina teaching staff wenye sifa? Je, vina mitaala bora? Je, vina mazingira bora ya ufundishaji na kujifunzia? Je, ni kweli kuwa Vyuo vya Umma ni bora kuliko vile vya Binafsi?

Huenda tukatofautiana mitizamo (na mara nyingi watu hutetea vyuo walivyosoma/biases). Lakini kwa mtazamo wangu, huwezi kuchora mstari ulio wazi(clear) wa ubora kati ya vyuo vya serikali na vile vya umma. Nitajieleza.

Nchi hii kwa sasa ina vyuo vikuu ishirini na sita (26) ukiacha vile vishiriki. Katika hivyo 26, ni tisa (9) tu ndivyo vilivyo vya serikali na vilivyobaki vyote ni vya binafsi kwa maana ya kumilikiwa na mashirika ya kidini, wafanyabiashara binafsi.

Pamoja na ukweli wa mambo kuwa ni vyuo vichache sana vya umma vyenye advantage ya umri/ukongwe (Mlimani, Muhimbili SUA etc) vilivyoanza siku nyingi, vyuo vyetu vingi vya binafsi vinakabiliwa na changamoto ya uchanga kwani vingi vilianza miaka ya 2005 na vichache vikianza miaka ya 1997/8.

Kwa hiyo ni kweli kuwa Mlimani wana advantage kubwa. Kwa mujibu wa Mkandala (VC), chuo hicho kina zaidi ya Walimu/Faculty Members 600 wenye PhD (waliobaki ni au wanasoma au wanatarajia kusoma), na wanafanya sana tafiti zinazopatikana mtandaoni. Kwa upande wa ufundishaji, kwa kweli waliosoma pale mtakubaliana nami kuwa inategemea na Shule/College/Faculty. Lakini kimsingi ufundishaji sio kivile ingawa kina advantage ya resource nyingi za kumwezesha mwanafunzi kuelimika. Nenda East Africana pale Library unakutana na kila takataka inayoitwa desa kuanzia thesis za tangu miaka na miaka, vitabu, machapisho na kadhalika. Hali hii haipo kwenye vyuo vingi vigeni. Na advantage nyingine ni aina ya wanafunzi wanaochaguliwa, wengi wao wana uwezo wa kujisimamia na kusoma. The same to Muhimbili/SUA.

Lakini vyuo vingine vilivyobaki, hali ni tofauti kidogo. Kwa upande wa faculty members (moja wapo ya kigezo cha ubora) unaweza kukuta kuna chuo kina hadi watu watano wenye PhD (na wote ni maadministrators mfano SMMUCo, MUM, TEKU nk) na waliobaki ni ndugu zangu wenye shahada za mtaji. Tena unaweza kushangaa hata mwenye Bachelor ndio Dean wa Faculty (nenda TEKU, SMMUCo, UoA, MUCCOBs etc). Kwa upande wa mazingira ya kufundishia unaweza kukuta Chuo kina kajengo kamoja (UoA) na mambo yanaenda.

Kwa hiyo tukizungumzia ubora, tutakuwa tunakurupuka kudai kuwa vyuo hivi vinatoa elimu inayotegemewa. Ingawa naelewa vyuo hivi vingi vinatumia wahadhiri wa vyuo vikongwe kufundisha wanafunzi wao, lakini bado kuna walakini wa ufanisi. Mfano wanafunzi wa Masters Makumira wanafundishwa kozi nyingi na wahadhiri wa Mlimani (ambao huenda pale kwa muda mfupi) na wanafundisha kwa bidii kuliko wanavyofundisha kwenye ajira zao (lakini muda wa wiki mbili kufundisha kozi ya ya units 4-6 ni sawa?).

Hata hivyo huwezi kusema ni vyuo vya serikali peke yake. Constituent colleges za Mlimani na SUA nk zilizofumuka miaka ya majuzi nazo zinakabiliwa na hali hiyo hiyo. Nenda MUCE, MUCCOBS utakutana na yale yale unayokutana nayo TEKU, MWUCE, Mount Meru na kadhalika. Kwamba vigezo halisi vya kutoa elimu shindanishi havipo (havina wahadhiri wa kudumu wenye sifa, vinafundisha kwa mtindo wa zima moto, vina shida za utawala/ukabila/udini na matatizo mengine).

Hitimisho langu ni kwamba, huwezi kuja na sweeping statement ya "vyuo binafsi ni hovyo" kwa kuzingatia ushahidi nilioutoa hapo juu. Hata hivyo changamoto hizi tunazoziona katika vyuo vyetu vichanga (vya umma na binafsi) zinaweza kukabiliwa kadri muda unavyokwenda. Kama ushahidi wa manufaa ya umri, leo ukienda SAUT (kilichoanza mwaka 2003) utashangaa kinavyojitahidi kwenye ubora na kamwe huwezi kukibeza (na hadhi yake ni kubwa kuliko Mzumbe). Kina wahadhiri wengi seniours na waliobaki wanasoma, na kinajitahidi kwa resources. Nenda Kariuki (private) utaona kinavyojitahidi. Lakini kwa upande wa pili, vyuo vyote vichanga (UDOM, SJUT pamoja na colleges kama Ushirika nk) utakuta yale yale iwe ni public au private.

REFERENCES (Kwa wasio na allege ya kusoma):

Makulilo, V. B. (2012). The proliferation of private universities in Tanzania: Quality compromised?: University of Bayreuth, Germany: Wudpecker Journal of Educational Research Vol. 1(4), pp. 51 - 66, October 2012

Sifuna, D. N. & Sawamura, N. (2010). Challenges of Quality Education in Sub-Saharan African Countries: New York, Nova Science Publishers, Inc.,


Mosha, H. J. (2000). Conceptualizing Quality of Education. In Galabawa, J.C.J, et al. The Quality of Education in Tanzania: Issues and Experiences: Institute of Kiswahili Research, University of Dar es Salaam.
 

1. Naungana nawe kushangaa tabia ya ajabu ya watu wanaojiita wamesoma kujisifia vyuo walivyosoma badala ya uwezo binafsi. Mwisho wa siku (generally speaking) hutaheshimika kwa jina la chuo chako isipokuwa quality ya unachokifanya/sema. Vinginevyo, labda utembee na label itakayokutambulisha ulikotoka (which is nonesense).

2. Je, ni kweli mfumo wa elimu unapendelea shule za serikali? Swali hili lina pande nyingi za shilingi. Hivi tunaposema serikali inapendelea shule zake tunaaminisha nini? Selection? Au mazingira ya ufundishaji na hamasa ya walimu kufanya kazi?
Kuhusu selection, mambo yamebadilika siku hizi. Zamani, ukienda shule za binafsi ilionekana huna uwezo kwa sababu mazingira ya shule za umma yalikuwa bora na hivyo watu walikimbilia mazingira bora. Siku hizi, kwa sababu ya ubovu wa shule za umma (sijui kama ndio kupendelewa?) mambo yamebadilika. Wazazi wengi wenye uwezo wa fedha wanawapeleka watoto wao shule binafsi. Ushahidi wa hili ni kwamba shule nyingi nzuri za binafsi hufanya selection kabla ya shule za serikali. The best brains (wengi) wenye uwezo kifedha wanaenda shule za binafsi, waliobaki (wasio na uwezo au kwa sababu za kiuchumi) wanaenda shule zetu za kata kusubiri kufeli.
Hivyo utaona kuwa upendeleo unaosemekana kufanywa na serikali kwa shule zake kwa maana ya selection ni nadharia tu. Wengi "wanaopendelewa" kwenda kwenye shule za umma, na wenywe nafasi kiuchumi, hawaendi labda wakipangwa shule zenye nafuu kama zile za serikali (za zamani) kwa imani kwamba kule kuna walimu na wnaafundisha.

3. Kwa nini shule za binafsi zinafanya vizuri?
Well, sababu ni nyingi. Moja, nyingi (hasa zile zenye majina) zinawalipa walimu wake vizuri na zina mifumo inayowabana wafundishe kwa ufanisi. Kwa mfano wakati mwalimu mpya mwenye Shahada anaweza kulipwa 400K serikalini, mwenzake anaweza kulipwa mpaka 1,500K kwenye shule binafsi. Wakati mwalimu wa serikalini hana morali ya kufundisha na hajawekewa mfumo wa kumdhibiti kufundisha, mwenzake wa shule binafsi ana morali na anadhibitiwa afundishe.

4. Hali ikoje vyuo vikuu (private v/s public).

Ili tuone kama yanayoendelea sekondari ndiyo yanayoendelea Vyuo Vikuu, ni vyema kujiuliza ubora wa elimu unategemea nini? Ubora wa elimu ya juu unategemea mambo mengi. Lakini kwa uchache kuna mambo matatu manne makubwa.

Moja, ni mitaala/curriculum bora inayotafsiriwa kwa ufanisi kazini. Mtaala bora ni ule unaomnoa mwanafunzi wa elimu ya juu kumwelezesha kuboresha maisha ya jamii katika eneo alilosomea kwa ufanisi.

Pili, ubora wa members of the Faculty/wanataaluma waliobobea kwenye maeneo yao. Kuanzia ngazi ya chini kabisa ya TA mpaka juu, ni lazima Chuo Kikuu kihakikishe kuwa kina watu wenye uwezo kitaaluma kwa maana ya ufundishaji makini na kufanya tafiti zenye kuchangia katika body of knowledge kwa maeneo yao. Ndio maana kigezo cha kupanda madaraja kwa Walimu/Academicians wa vyuo vikuu si muda kazini bali idadi na kiwango cha tafiti walizofanya.

Tatu, ubora wa mazingira ya kufundishia na kujifunzia. Hapa tuna maana ya vifaa, vitabu, maabara zenye viwango, mfumo mzuri wa kuwezesha wanafunzi kujenga tabia ya kutafiti na kadhalika.

Nne, ni ubora wa wanafunzi wanaochaguliwa. Hatuzungumzii matokeo/grades (ambazo nyingi zina maswali mengi kuliko majibu) bali uwezo halisi wa wanafunzi (thinking, reasoning, originality, imagination, talents na kadhalika).

Baada ya kuangalia vigezo hivyo, sasa tuvigeukie vyuo vyetu kwa swali la jumla: Je, vinakidhi vigezo vya kutoa elimu bora? Je, vina teaching staff wenye sifa? Je, vina mitaala bora? Je, vina mazingira bora ya ufundishaji na kujifunzia?

Huenda tukatofautiana. Lakini kwa mtazamo wangu, huwezi kuchora mstari ulio wazi/clear wa ubora kati ya vyuo vya serikali na vile vya umma.

Nchi hii kwa sasa ina vyuo vikuu ishirini na sita (26) ukiacha vile vishiriki. Katika hivyo 26, ni tisa (9) tu ndivyo vilivyo vya serikali. Vilivyobaki vyote ni vya umma.

Pamoja na ukweli wa mambo kuwa ni vyuo vichache sana vya umma vyenye advantage ya umri/ukongwe (Mlimani, Muhimbili SUA etc) vilivyoanza tangu uhuru, vyuo vyetu vingi vya binafsi vinakabiliwa na changamoto ya uchanga kwani vingi vilianza miaka ya 2005 na vichache vikianza miaka ya 1997/8.

Kwa hiyo ni kweli kuwa Mlimani wana advantage kubwa. Kwa mujibu wa Mkandala (VC, chuo kina zaidi ya Walimu/Faculty Members 600 wenye PhD (waliobaki ni au wanasoma au wanatarajia kusoma), na wanafanya sana tafiti zinazopatikana mtandaoni. Kwa upande wa ufundishaji, kwa kweli waliosoma pale mtakubaliana nami kuwa inategemea na Shule/College/Faculty. Lakini kimsingi ufundishaji sio kivile ingawa kina advantage ya resource nyingi za kumwezesha mwanafunzi kuelimika. Nenda East Africana pale Library unakutana na kila takataka inayoitwa desa kuanzia thesis za tangu miaka na miaka, vitabu, machapisho na kadhalika. Hali hii haipo kwenye vyuo vingi vigeni. Na advantage nyingine ni aina ya wanafunzi wanaochaguliwa, wengi wao wana uwezo wa kujisimamia na kusoma. The same to Muhimbili/SUA.

Lakini vyuo vingine vilivyobaki, hali ni tofauti kidogo. Kwa upande wa faculty members (moja wapo ya kigezo) unaweza kukuta kuna chuo kina hadi watu watano wenye PhD (na ni maadministrators mfano SMMUCo, MUM, TEKU nk) na waliobaki ni ndugu zangu. Tena unaweza kushangaa hata mwenye Bachelor ndio Dean wa Faculty. Kwa upande wa mazingira ya kufundishia unaweza kukuta Chuo kina kajengo kamoja (UoA) na mambo yanaenda.

Kwa hiyo tukizungumzia ubora, tutasema uongo kuwa vyuo hivi vinatoa elimu inayotegemewa. Ingawa naelewa vyuo hivi vingi vinatumia wahadhiri wa vyuo vikongwe kufundisha wanafunzi wao. Mfano wanafunzi wa Masters Makumira wanafundishwa kozi nyingi na wahadhiri wa Mlimani (ambao huenda pale kwa muda mfupi) na wanafundisha kwa bidii kuliko wanavyofundisha kwenye ajira zao.

Hata hivyo huwezi kusema ni vyuo vya serikali peke yake. Constituent colleges za Mlimani na SUA nk nazo zinakabiliwa na hali hiyo hiyo. Nenda MUCE, MUCCOBS utakutana na yale yale unayokutana nayo TEKU, MWUCE, Mount Meru na kadhalika. Kwamba vigezo halisi vya kutoa elimu shindanishi havipo.

Hitimisho langu ni kwamba, huwezi kuja na sweeping statement ya "vyuo binafsi ni hovyo" kwa ushahidi nilioutoa hapo juu. Hata hivyo changamoto hizi tunazoziona katika vyuo vyetu vichanga (vya umma na binafsi) zinaweza kukabiliwa kadri muda unavyokwenda. Kama ushahidi wa manufaa ya umri, leo ukienda SAUT (kilichoanza mwaka 2003) utashangaa kinavyojitahidi kwenye ubora na kamwe huwezi kukibeza (na hadhi yake ni kubwa kuliko Mzumbe). Kina wahadhiri wengi seniours na waliobaki wanasoma, na kinajitahidi kwa resources. Nenda Kariuki (private) utaona kinavyojitahidi. Lakini kwa upande wa pili, vyuo vyote vichanga (UDOM, SJUT pamoja na colleges kama Ushirika nk) utakuta yale yale iwe ni public au private.

REFERENCES (Kwa wasio na allege ya kusoma):

Makulilo, V. B. (2012). The proliferation of private universities in Tanzania: Quality compromised?: University of Bayreuth, Germany: Wudpecker Journal of Educational Research Vol. 1(4), pp. 51 - 66, October 2012

Sifuna, D. N. & Sawamura, N. (2010). Challenges of Quality Education in Sub-Saharan African Countries: New York, Nova Science Publishers, Inc.,


Mosha, H. J. (2000). Conceptualizing Quality of Education. In Galabawa, J.C.J, et al. The Quality of Education in Tanzania: Issues and Experiences: Institute of Kiswahili Research, University of Dar es Salaam.
sawa tumekupata mkuu lakii kwenye education ya juu bado private uiversities hazijawa na uwezo mkubwa wa kiushindani na publick universities ndio maana wanaweka vigezo nafuu.kama wanauwezo kiushindani basi wakeke vigezo kama vya vyuo vya public universities/vivyo kwa upande wa sekondary private schools zimesha jijengea advantage but kuanzia advance kwenda juu not yet
 
kumekuwepo na wimbi kubwa la watu na hata mada zikibeza na kutilia shaka uwezo na ubora wa vyuo vya binafisi kiasi cha wengine kuviita majina ya ajabu ajabu.

kwa mkutadha huo nimeona bora niwaeleweshe wote wanaojigamba kwa majina ya vyuo vyao na si ubora wao kuwa elimu waliyoipata bado haijawasaidia na hawajakombolewa na kuwajengewa uwezo wa kufikiria,kung'amua na kutambua ukweli halisi ulivyo na nitawashauri warudi darasani wakasome upya ili wapate uwezo wa kuona mambo kwa usahihi wake.

BACK TO TOPIC.
napenda kuweka wazi ukweli huu na watu waniambie kama ni sahihi kwa wanavyofikiria.

1.mfumo wa elimu ya tanzania kuanzia form one mpaka form six unazipendelea shule za serikali kwa kuzipa nafasi ya kuchagua wanafunzi waliofaulu tu na makapi wanaachiwa ndugu zangu wa private.


-shule za serikali form one zinachukua wanafunzi walio na ufaulu wa juu na kwa kiasi kikubwa wanafunzi wanaokosa kuchaguliwa kwa sababu ya marks zao kuwa za chini wanaenda kujaribu bahati yao private.

-matokeo ya form two necta yakitoka shule za private pamoja na kwamba ziliachiwa wanafunzi wengi wenye marks za kawaida zinaibuka kidedea dhidi ya shule za serikali ambazo zilichagua wanafunzi wazuri tu

-matokeo ya kidato cha nne yakitoka shule za private zinafanya vizuri tena kuliko za serikali pamoja na kwamba shule za serikali zilichagua wanafunzi wazuri tu.


MAELEZO HAYA YANATOA FUNDISHO KUWA ELIMU YA SERIKALI SI BORA KULIKO YA PRIVATE NA SERIKALI KAZI YAO NI KUHARIBU FUTURE ZA WATOTO ALAFU WANAWAACHA ILI TENA WAOKOLEWE NA PRIVATE SCHOOLS KIDATO CHA TANO NA SITA BAADA YA KUACHWA.

mimi mwenyewe ni mwathirika maana darasa zima tulikula za uso kwenda form one hakuna hata mmoja aliyepenya,ndipo wanafunzi watano tukaokolewa na private ya huko home na kati ya hao ni mmoja tu ndio alishia form four ila wengine walichanja mbuga mpaka vyuoni.


SABABU ZA UBOVU WA ELIMU SERIKALINI ZINAJULIKANA NA SITAZITAJA ILA ITOSHE TU KUSEMA KUWA SABABU NYINGI ZINAZOATHIRI ELIMU SEKONANDARI HATA KWENYE VYUO VIKUU VYA SERIKALI SABABU HIZO ZIPO NA ZINAFANYA KAZI YA KUPUNGUZA UFAULU WA WANAFUNZI HUKO ALAFU WENYE KUKOSA MAARIFA YA KUFIKIRI WANASEMA WAKIPATA GPA NDOGO NDO ELIMU ILIKUWA NZURI KUMBE WAMEATHIRIKA NA MAZINGIRA MABOVU ZIKIWEMO TARATIBU.

-wanafunzi wanaofeli form four kwa kupata angalau three ya mwisho na four za mwanzo serikali inawaacha ambao wengi wao ni wa shule za serikali na ndio hao serikali ilituambia ndio waliostahili kusoma ilipowachagua form one,hawa wanafunzi inabidi waende private kutafuta bahati yao huko, wengi wao kati ya hawa huwa wanafaulu tena na kuthibitisha kumbe wanaweza kufaulu ila walifeli kulingana na kusoma serikalini na si ajabu tena hawa serikali ikawataka.


KIFUPI NI KWAMBA PRIVATE SECTORS WAMEONYESHA UWEZO MZURI WA KUWAFUNDISHA WATOTO NA KUFAULU NA HAPA HAKUNA ANAEBISHA KWA SABABU WANAFUNZI WOTE WANASOMA KWA SYLLABUS MOJA NA MITIHANI NI ILE ILE ILA TATIZO LINAKUJA VYUONI AMBAPO WATU HAWANA SAME SYLLABUS NA MITIHANI YAO NI TOFAUTI NA NDIPO UNAANZA KUSIKIA MAJINA YA AJABU AJABU KWA HIVI VYUO KISA WANAFUNZI WAKE WANA GPA KUBWA.

mfano wanafunzi wanalundikwa lecture hall ukute wapo 400,humo wapo hawasikii kabisa najua maana wanafunzi wengi wanakimbilia mbele ili angalau wasikie na wakichelewa wanakaa nyuma na kusikia ndo inakuwa utata,wengine hawaelewi lakini hawawezi kusema hawaelewi na inabidi wakaushe tu nk nk alafu wakipata GPA ndogo wanalalamika wanapoona wale wa vyuo vya vitongoji wamepata GPA kubwa wakati wenzao walifundishwa darasani wanafunzi 40 tu,wasipoelewa wanauliza na wote wanasikia,lecturer akizingua ama haeleweki analipotiwa na kubadilishwa ama kutimulimuliwa.


mbona hamsemi mashule ya private yanavyofanya vizuri kwenye mitihani ya kitaifa ambapo kuna mtihani mmoja?


ama huko hamuoni kama wanapata one na two wengi na hata one kali kali kiasi hata cha tanzania one wengi kutokea huko?

nini tofauti ya mifumo ya shule za private na vyuo vya private katika ufanisi?nini tofauti ya shule za serikali na vyuo vya serikali katika ufanisi?

mbona pia hamuulizi kwa nini shule za serikali pamoja na kujichagulia wanafunzi wazuri lakini bado zinafelisha badala ya kufaulisha?

ingekuwaje kama siku moja shule za private zichague wanafunzi waliofaulu alafu makapi yaende serikalini?watu wangetoka kweli?haki ya nani itakuwa kiama,naamini hata division four zinaweza kukosa kabisa kwenye necta na wanafunzi wote kubaki na zero.


ingekuwaje kama mfumo wa elimu ungetaka kuwa wanafunzi wa shule za binafisi waendelee kuwa wa binafisi mpaka vyuoni?kwa kuwa wanafunzi wa shule za serikali ndio wanaongoza kufeli je mpaka kufikia form six kuingia chuoni serikali ingebaki na asilimia ngapi ya wanafunzi ilioanza nao na je ingeonekanaje kama ubora ungeangaliwa kwa ufaulu tu kama wanavyofanya watu wetu wenye uwezo mdogo wa kufikiri?hizo one nyingi leo sizingekuwa private universities?



2.udahili wa vyuoni na hoja za wanaosema vyuo vya watu binafisi havina ubora.

-kwanza vyuo hivi vinadahili wanafunzi wenye marks za chini sana mpaka hata three za 17 lakini mwisho wanapata GPA kubwa za 4 na kuendelea(si maneno yangu bali ni hoja ya watu hao)

MAJIBU KWA HOJA HII.

kabla hujafikiri chochote kuhusu majibu kwa hili unapaswa kujua pia kwa nini shule za private zinachukua wanafunzi hata waliofeli la saba lakini wanaibuka na one?

unapaswa pia kujua kwa nini shule za private zinachukua wanafunzi wenye three za mwisho na div four kusoma advance alafu wanaibuka na division one na two na hata three kwa combination zote hata za sayansi?


HAPA SITAKI KUPIGIA DEBE SHULE NINAYOIJUA ILA NAJUA KAMA WATU NI WAJASIRI WATAKUJA HAPA KUTOA USHAHIDI KUWA WAO WALIPATA FOUR O LEVEL SHULE ZA SERIKALI ILA WAKAENDA PRIVATE NA KUIBUKA NA ONE AMA TWO YA FORM SIX NECTA NA WALIENDA UDSM AMA UDOM AMA MZUMBE AMA SUA.

UKISHAPATA MAJIBU HAYO NI VYEMA UKAJARIBU KUYAUNGANISHA TENA KWA MATOKEO YA GPA KUBWA ZA VYUO VYA BINAFISI.

JE UMEWAHI KUJIULIZA INGEKUWAJE KAMA VYUONI KUNGEKUWA NA PAPER MOJA KWA VYUO VYOTE?JE PRIVATE WANGEONEKANA MABOYA AMA WANAWEZA?hayo majibu kila mtu anayo yake.

-UBORA WA WANAFUNZI WA CHUONI UNAPATIKANA KWA VIGEZO VIPI HASA?

nimefatilia kwa kiasi kikubwa kwa wenye hoja hizi nikabaini wanaangalia matokeo ya wanafunzi ya kidato cha sita tu huku mengine wakiyaacha kabisa kuyaangalia.

NASEMA KUNA MAKOSA MAKUBWA SANA HAPA NA WATU HAWATAACHA KULALAMIKIA VYUO VYA BINAFISI KWA SABABU YA UFINYU WAO WA KUFIKIRI NA NDIO MAANA NIMESHAURI HAWA WARUDISHWE TENA SHULE UPYA WAKAJENGEWE UWEZO WA KUFIKIRIA.

MAPUNGUFU KATIKA HOJA YA MATOKEO KAMA KIPIMO CHA UBORA WA MWANAFUNZI.
-kwanza matokeo yanayotazamwa na wengi ni ya form six pekee,hawajui kuna wanafunzi wana one na two za form six na wapo udsm ama udom ama mzumbe ama sua ila form four walikuwa na four ama three za kuchechemea na waliokolewa na private, ama hawajui kuna wanafunzi wana three za 17 form six ila wana wana one za single digit O level ila kisa wapo vyu vya kitongoji ni tatizo.

SASA JE TUTUMIE MATOKEO YAPI KUSEMA HUYU MWANAFUNZI NI BORA?TUKITUMIA YA SIX NI MWAKE ATAONEKANA ALIFAULU VIZURI LAKINI TUKITUMIA YA O LEVEL NANI ATASEMA HUYU NI MWANAFUNZI BORA?
swali kwa nini mnatumia hasa matokeo ya kidato cha sita tu na mnasahau kuchukua historia ya matokeo yote mpaka ya form four?

mbona udsm ina watu walikuwa na four O Level ama nacho ni chuo cha kitongoji? NAJUA WATU WATASHANGAA HAPA LAKINI NDIO UKWELI WENYEWE.

KIDOGO NINGEPENDA KUELEZA KWA NINI UDSM INACHUKUA WANAFUNZI WENGI WENYE MATOKEO MAZURI YA FORM SIX.

kwanza udsm ni chaguo na ndoto za wanafunzi wengi kusoma hapo(ila haikuwa mimi) na sababu ni za kihistoria,mpaka leo ndicho chuo kinachojulikana na wengi hasa watu wa zamani ambao ni wazazi wetu kwa hiyo wengi tumejengwa tokea mwanzo kuwa hicho ndio chuo kikuu,ukisema kwingine wazee wanakushangaa sawa na watakavyomshangaa mtu atakaekuja hapa aseme yeye ni engineer wa kemikali mana wao wanajua injia ni yule wa civili engineering tu.

kwa hiyo udsm inapata request nyingi sana na wote tunajua utaratibu wa kuchagua ni kuanza na aliye bora zaidi kushuka chini,japo nao udsm wanaangalia sana matokeo ya six na ndio mana hawajali sana kama o level uligonga four ama three ya mwisho.

na sababu nyingine ni kwamba udsm ina uwezo mdogo wa kuchukua wanafunzi wanaostahili kusoma degree,na ninawahakikishia kuwa hata wanafunzi wenye div three za 17 wapo eligible kusoma udsm kama tu wana C tatu O level na principle mbili Advance ila kutokana na uwezo mdogo wa udsm ku accomodate wanafunzi ndio inawaacha.



-sababu zilizopelekea hawa wanafunzi waliofeli kufeli hazizingatiwi katika kuangalia ubora wa wanafunzi,mtu katoka shule ya serikali haina hata walimu amekomaa mwenyewe akapata three yake ya 17 alafu unasema hana uwezo wa kupata GPA ya 4.5 kumbe anao uwezo kama akifundishwa na kupewa kila kinachostahili. na wanapofika vyuo vya private elimu inaonekana kumbe ni nyepesi maana wanafundishwa vizuri,sasa kwa ni nini wasifaulu na kupata GPA ya 4?

ngoja nitoe mfano mmoja,kuna shule moja kali ya private arusha nilimtembelea rafiki yangu ambaye ni sister(katoliki) na yeye ndo alikuwa mkuu wa shule ile,ilikuwa kipindi cha kuchagua wanafunzi wa kuingia kidato cha kwanza.
kwa kuwa ananiamini sana akaniambia nisahishe mitihani ya kiingereza nikakataa,baadae akaniambia nisahishe ya hesabu nikakataa ila akanilazimisha,ikabidi nikubali,nikasahisha na marks za wanafunzi wote zikawa tayari.

sasa vigezo vya shule ile kuchagua wanafunzi ndio vilinishangaza ila nikajifunza kitu baada ya kuelekezwa.

-kwanza wanaangalia mwanafunzi katoka wapi?na shule ipi?na kukoje huko?hapa wanaweza kumchukua mwanafunzi hata mwenye marks ndogo kabisa ila ameonyesha uwezo fulani baada ya kuangalia alikotoka na kubaini kuwa huyu katoka eneo ambalo elimu iko chini sana na hivyo atakuwa mzuri ila mazingira ndio yanamfanya asijue. ama wanaweza kumuacha mwanafunzi mwenye ufaulu wa wastani aliyetoka shule bora kabisa japo amefikisha marks kwa kuangalia kuwa amepata marks za kawaida sana pamoja na kuwa katika mazingira bora zaidi na shule bora zaidi.

sister akanipa mfano wa mwanafunzi aliyekuwa form three wakati ule 2012 ambaye ndio alikuwa akiongoza darasani,akaniambia yule mwanafunzi alipata marks ndogo sana ila walilazimika kumchukua kwa kuwa waliona katokea ndani kabisa maporini huko arusha kwa wamasai ambako elimu ni kitendawili na walihisi atakuwa mzuri sema tu huko elimu ni mbovu kupindukia,alipoanza form one wakadili nae kumfundisha english kwa ukaribu zaidi na baada ya mwezi wa sita tu akaanza kuongoza mitihani ya shuleni licha ya mwanzo kuanza na namba za mwishomwisho,aliongoza necta ya form two na hata form three bado alikuwa moto.


NADHANI PIA MMEJIFUNZA KITU HAPA JUU YA UBORA WA MWANAFUNZI KUWA UNATEGEMEA MAMBO MENGI SANA NA HATA UFAULU WA MWANAFUNZI UNATEGEMEA MAMBO MENGI SANA IKIWEMO YEYE MWENYEWE NA MAZINGIRA YA SHULE AMA CHUO

MWISHO NINGESHAURI WATU MJIPAMBANUE KWA MAFANIKIO YENU BAADA YA KUMALIZA VYUO KAMA UBORA WA ELUMU YENU NA SI KULAZIMISHA KUPATA SIFA KISA UMESOMA CHUO FULANI AMA KUMUBEZA MWINGINE KISA KASOMA CHUO FULANI.

tunataka akina Stive Jobs hapa,tunataka kina Newton hapa,tunataka kina Eisten hapa,tunataka kina GALILEO GALILEI hapa na wengine wengi,hatutaki majina ya vyuo ama shule. show your quality of education to innovations and is when we shall appriate your quality.



Na dhani amepata somo hyo. Atuachie vyuo vyetu vya private
 
sawa tumekupata mkuu lakii kwenye education ya juu bado private uiversities hazijawa na uwezo mkubwa wa kiushindani na publick universities ndio maana wanaweka vigezo nafuu.kama wanauwezo kiushindani basi wakeke vigezo kama vya vyuo vya public universities/vivyo kwa upande wa sekondary private schools zimesha jijengea advantage but kuanzia advance kwenda juu not yet

Inawezekana ni kwa sababu ya muda mfupi tangu vianzishwe kama nilivyoeleza, hali ambayo ni hiyo hiyo kwa vyuo vya umma vilivyoanzishwa miaka ya 2000.
Mfano huwezi kulinganisha mfumo wa utoaji wa elimu SAUT (Private) na UDOM (Public). Difference ni muda [Reference ukitaka utapata]. Na huwezi kutofautisha yanayoendelea MUCCOBS (Public) na Mwenge (Private). Vyote hivyo vinashirikiana matatizo yanayotokana na uchanga wake na vyote viko Moshi [reference ni uchunguzi wangu uliodumu kwa miezi miwili mwaka 2011].

Hoja inayojengwa hapa ni kwamba matatizo ya vyuo vyetu hayako categorized kwa misingi ya umiliki. Ingawa naelewa pia kuwa vyuo vya private vimekuwa vikisukumwa na motive ya kuifanya elimu kuwa biashara zaidi kuliko huduma. Ndio maana vingi haviwalipi vizuri watumishi wao, hali inayofanya wafanye kazi huku wakitafuta pa kwenda.
 
Wewe halafu MANAGEMENT nyingi za vyuo vya private wanawakomand WAHADHIRI wawape G.P.A kubwa


Kuna Lecturer wa Mathematics (Foundation analysis) anaitwa Sembuche alikamata nusu ya darasa Tumaini University ya Iringa, Management ikamfukuza, SUA walimchukua na wakampa mkataba mpaka amestafu na kushika ni kama kawaida.
 
Pameanza kuwepo utamaduni wa vijana wa kileo kusema vitu kwa seeping statements na generalizations bila utafiti. Yaani mtu anakurupuka na ki-assumption chake na kuhitimisha ndio ukweli.

Vyuo vyote vinadhibitiwa na Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania. Na moja wapo ya conditions muhimu kwa kila chuo ni kuhakikisha members of faculty wanakuwa na sifa zinazotakiwa. Moja ya sifa hizo ni GPA isiyopungua 3.5 kwa Wakufunzi wanafunzi (TA)wenye Shahada ya kwanza na 4 kwa Wahadhiri Wasaidizi/Shahada za Uzamili. Haitokaa itokee mtu mwenye GPA chini ya 3.5 Undergraduate afanye kazi katika taasisi za elimu ya juu, iwe za umma au binafsi.

Najua kuna cases chache zilikuwepo wakati vyuo hivi vinaanza hasa hasa miaka ya 2000, lakini si kwa hivi sasa. Na kama wapo vihiyo ni wa kujificha sana. Ukiripoti TCU wanawajibishwa mara moja.

Tuache kueneza propaganda zisizo na mashiko wala ushahidi.

Hizo sio propaganda, ndio ukweli uliopo! Hakuna haja ya kutajana majina, ila vyuo vingi private havina wakufunzi wenye sifa! Ishu ya TCU ipo lakini reality ni tofauti! Wanajua wenyewe wanachofanya
 
Kuna Lecturer wa Mathematics (Foundation analysis) anaitwa Sembuche alikamata nusu ya darasa Tumaini University ya Iringa, Management ikamfukuza, SUA walimchukua na wakampa mkataba mpaka amestafu na kushika ni kama kawaida.
kama ni kweli basi walijua ataharibu soko maana inawezekana ni kanuni ya kubembeleza wateja."sababu ukiwapa masup mengi wateja wanaweza shift udom.so udom imefanya kuwe na competition kubwa ,vyuo vya private vingi vinakubwa na hili janga.
 
kama ni kweli basi walijua ataharibu soko maana inawezekana ni kanuni ya kubembeleza wateja."sababu ukiwapa masup mengi wateja wanaweza shift udom.so udom imefanya kuwe na competition kubwa ,vyuo vya private vingi vinakubwa na hili janga.

hata udom hawawezi kuwachukua hao kwa sababu niliangalia cut off point za udom kwa upande wa masomo ya biashara unatakiwa upate kuanzia cut off ya point 5 na kuendelea it means uwe na div 2 au div 1 ya form 6.
 
hata udom hawawezi kuwachukua hao kwa sababu niliangalia cut off point za udom kwa upande wa masomo ya biashara unatakiwa upate kuanzia cut off ya point 5 na kuendelea it means uwe na div 2 au div 1 ya form 6.
mara ya mwisho udom zilishushwa point mpaka 2.5 ndugu .walishindwa kupata watu wakashusha,so wakapata watu wengi bila hivyo walikuwa wanakosa watu,na watu wengi nawajua wameenda kusoma pale na 2.5 cut off point kwa course za busness
 
Nenda zako huko unatetea kufeli kwako form6 ! kiukweli haingii akilini unakuta miG.P.A mikubwa wakati wanafunzi wanaochukuliwa kwenye hivi vyuo wanaufaulu hafifu na mbaya kama sio mchafu! ingekuwa vyuo hivi vya PRIVATE vinachukua CREAM kama zilivyo SPECIAL SCHOOLS mimi nisingeongea kitu !!

MIMI SIJAWAHI KUFELI,ila sikuchaguliwa kujiunga form one shule za serikali lakini si kwa sababu nilifeli bali uchache wa shule wakati ule,pamoja na hayo hapa nchini kuna shule kama nne hizo special school na moja ilikuwepo kwenye kanda yangu ambayo ni tabora boys,

lakini niliweza kuwaburuta kibao hao unaowaita special students waliotokea tabora boys nilipotinga top ten kikanda kati ya mikoa mitatu wakati ule necta form two,na huko ndo kufeli kwangu,form four nako nilizidi wanafunzi wengi tu ambao unawaita ni special waliokuwa hapo tabora boys,na hata form six sikufeli na chuo nilichokuwa napenda nisome kilikuwa UDOM pamoja na upya wake wakati ule ila niliamua kubadili chuo baada ya kupata ushauri,na hata hiyo form six nimezidi mamia ya wanafunzi kimatokeo waliowahi kusoma hizo special school,sasa ucream unaouzungumzia ni upi?ama unafikiri nilikuwa nafanya NECTA ya kwangu peke yangu?

naona umeshindwa kujibu hoja na unataka kuhamisha mjadala uwe wa kunijadili mimi na si kuijadili topiki uliyoianzisha mwenyewe, huo ni uwezo mdogo tu unakusumbua.

nakushauri ufungue topiki ya kunijadili mimi kama umeshindwa kujadili na kutetea hoja zako,ili huko ndiko unijadili kwa wigo mpana lakini hapa naona tayari umeelemewa mpaka unataka kuikimbia mada na umekuwa mtoa mitusi kama kawaida ya watu wasio na uwezo wa kujadili kwa hoja.
 
,Mshinga mimi nimesomea TABORA SPECIAL SCHOOL(TABORABOYS)! ngoja nikuulize swali umesomea shule gani O-LEVEL,A-LEVEL ,Umesoma chuo gani na mwaka gani? nikukamate vizuri uabike humu jamvini!
 
Back
Top Bottom