MO TOWN nmekupata bt kwenye busines yeyote unaingia ukiwa umeshafanya intensive research na umecalculate rsk and benefit bt busines envronmental znatokea dat why tunasema ni kutake rsk eg; compitatiors wanaweza kuongezeka, etc dat y lazma ujtoe mhanga na kutumia soko kwa wakat mwafaka...
Hii Mada ya leo ni ya Kweli kabisa wala sibishi hata chembe, ninasema hivi nikiwa mmoja katika wazika hela mbali na Jiji, japo naamini Kinondoni was Once Porini, hata aliyewekeza Pale Mlimani city palikuwa ni pori pia japokuwa alikuwa na pesa Mingi, Namaliza kwa kushukuru kwa ushauri Mzuri sana, Bila kusahau naomba kujuzwa Kodi ya chumba kimoja ni sh ngapi pale kinondoni, Kijitonyama au sinza, Na Je wale wajasiriamali wadogo wasio na Nyumba wanaishi kwa Kupanga Nyumba Za kijitonyama, Kinondoni, Kariakoo, Posta, Mbagala au Mbezi, Tegeta kuliko na Mapori yasiyolipa? By the way jitahidini kuwekeza katika ardhi pia fanya bidii katika kazi zako uwe mjasiriamali mzuri na mwenye maendeleo Ahsanteni wana jamvi
Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
That was my word.
Mwili wote ukiwa jicho, sikio litakuwa wapi?
Hapo hujaongeza wizi unaofanywa na waajiriwa wengi kwa waajiri wao.
Na hii tabia ya kila mtu kuanzisha grocery stoo, bar au salon inakera sana!
nimetaka kuilike hii post lakini sikioni kidude cha like...in short mtazamo wako ni mzuri lakini hicho unachosema ni kingeni kwa watanzania...chamsingi watu tunatakiwa tuwe na assets sio tunanunua liability halafu tunadhani kwamba ni asset..kujenga nyumba then kuhamia humo na kukaa ni liability coz kuna maintenance costs etc vitu kibao..KWA ushauri wangu someni kitabu hichi kitawasaidia tu nyie wenye fikra mgando..za kupenda kujenga nyumba na kuhamia pembezoni mwa miji..search google.com/richdadpoordad pdf ukisoma wiki moja tu huwezi kufkiria kama mnavyowaza sasa hivi over..!!! Via Lazima ninunue Land Rover LR3..4.0...!!!IGWEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEE!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Watanzania wengi haswaaa vijana wa sasa na vijana wa zamani wengi watakufa maskini ama kuzeeka maskini kwa kuendekeza Ucommunist na sera za kizamani za utajiri ni kumiliki nyumba na gari.
Sikatai nyumba ni a very valuable asset, na ina appreciate in value with time lakini this is not necessarily the case always. Appreciation na returns za hio nyumba zinaweza zisiwe reasonable enough kujustfy wewe kufkia 40Mills au 30Mills leo hii. Hio initial investment inaweza kuchukua hata 20yrs kujirudisha tu bila kujilipa. Imagine hio 40Mills ungewekeza kwenye opportunity zingine zenye large returns, na kuhakikisha unachukua calculated risk in 20yrs si unweza kujikuta una 400Mills na mijumba ya kumwaga!
Sio kwamba wa tz wengi hatushiki mbesa, no! tunashika sanaaa sema priority ndo zinatuangusha haswaa waajiriwa wa white collar jobs. Ile breakthrough ya msomi kutoka maisha ya kawaida na kuwa mwekezaji anae ajiri watu asilimia kubwa hawaifikiii. Mtu akishika tupesa tudogo anakimbilia kutuzika mashambani huko!
Vijana wenzangu unashika tu 10mills unawahi kutuzika Mbagara kiburugwa sijui huko au Mbezi maramba mangapi sijui. Unaongezea kuzika mamilioni hadi yafike hata 50 in 4 yrs hadi umalize jumba hilo. Kisha kodi unapoke 100,000/= in 10 to 20 years haiendi mbali na hapo. Watu waliojenga Tabata in 1990's nyumba mpaka leo Tbt ni 200,000 kwa mwezi?????
Tubadilike tuwe capitalistic. Ukishika 10m ujipange izungushe ushike 50m. It all about opportunity and risk taking this is the only key kuwa billionea. Ruge keshasema fursa ziko nyingi mnoooo! Tabia ya kuzika tuiache. Nyumba ziko kibao Sinza, Masaki, Obay, Knyma kwanini uende porini? Hio 10Mills izungushe hadi ifike 300Mills ununue nyumba ya uhakika Kinondoni. This is the bigger picture!
Thanks you all!
Juzi hapa April last year, cousin wangu kauza nyumba ghorofa ya dingi yake Arusha mjini kati kati 800m, alafu kaishia zake china. Baba yake pressure ikawa inapanda na kushuka daily! Almanusura stroke.
Kijana mwenyewe usije kuzani labda teja au mvuta bangi, nooo alikuwa ndo karudi na Masters yake toka Korea. Kila mtu alisikitika! Yaani ilisikitisha ukoo mzima. Kaiba hati (Wazazi hati mchane magodoro na kuziweka! Mambo ya kijana wangu msomi nanuonesha mali utasaga meno.)
Huku na huku agust nikasikia yuko Kkoo kadosha mzigo wa maa wa Tiles, Misumari na majuisi jujuisi kitumbini. Sikuamini ikabidi nimzukie angalau nikamuombe hio chenchi amrudishie dingi yake afu atafutiwe kazi Bank atulizane na 600 kwa mwezi.
Koz mwenywe mwana wa kko sikuchelewa kumpata. Ebaneeeeeeeeeee! Nikakuta mvua ya pesa inamnyeshea. Wakongo, Wazambia wanagombeaje mzigo. Aliwakata bei hadi wachina. Mzigo unagombewa kama njugu mawe. Jusi akazifoulisha kitumbini kwa kina kemcho bahi. Nikasalimia tu na kusepa.
Alikuwa na mkno wa business,akageuka tena, juzi april karudi kwao kamrudishia dingi yake 800m cash na wmenunua plot town pale wanashusha ghorofa la ngazi 20. Magari wanayoendesha usiseme. Baba mtu kasahau yote.
Isingekuwa kujasiria mali wangebakia na kigorofa mshe.nzi mpaka leo na cousin angekua bado ana apply kazi. Chezeya maisha nyie.
Hahahaaaaaaaa! Dingi wangu akaniambia basi na wewe uza hili banda hapa kinondoni, uzame china unileteee cash yang na kuangusha kitu hata knyama tu. wala sitokulaani. Mambo gani unakaa kungoja hela ya mboga utazeeka bila kumake things happen kama mimi dingi yako. Mchezo wa sasa sio kuajiriwa.
ONYO KILA MTU NA BAHATI YAKE!!!!!!!!!!!!!
una maana wakati huo hao waliospend (let say) 40m by then kujenga nyumba Tabata wakiamua kuziuza hizo nyumba leo zitakuwa bei gani?
Na unavyoongelea ktengeneza pesa then upate 200m uje kununua nyumba Kinondoni hizo unazonunua hazina watu bali wana kaa panya? Na kama wanakaa watu ina maana watahamia wapi kama sio Tabata, Tegeta, Mbezi Maramba mangapi nk ili wakupishe wewe?
Unaonekana kuwa akili yako umeinarrow na kufikiria maeneo machache tena ya Dar es Salaam ambayo ndiyo yamepimwa na kwa kiasi fulani huduma za jamii zinapatikana lakini ukasahau kuwa Tanzania ni kubwa. Na unacho focus ni kuwa pesa zinapatikana Dar es Salaam tu ambapo wengi wenye mawazo hayo ni ya kifisadi zaidi maana dsm ni ujanja mwingi badala ya kazi. Ni kwa nini usiseme kuwa upate 200m ukaanzishe kilimo cha maharage kasulu ambayo sasa kilo moja inafikia 1800/-?
Any kind of entrepreneurship depends much on the culture of that involving area. Sasa maisha ya Dar es Salaam au hata Tanzania nyumba ni kitu ambacho ni very significant tofauti na Ulaya au US ambapo mtu anaweza kupata kazi mji mwingine akauza nyumba ya mji anaoishi na akaenda kununua nyingine huko anakoenda. Tanzania ukishauza kama nyumba ndio imetoka tena na mara nyingi huwezi kuinunua tena. Ndio maana nikamsikia yule kijana diamond akisema "hakuna baba mwenye gari bali kuna baba mwenye nyumba"!
Conclusion ya haya yote ni kuwa wataalamu wanasema Tanzania ni vigumu sana kufanya biashara ya aina yoyote kwa sababu ya rushwa na uchumi uliojaa rushwa it is not easy to predict what tomorrow will bring basing on a fact that many business here do not have perfect information kwa hiyo ni kutegeshea tu. Unachosema ni sawa na kuangalia mbele tena sana lakini bila kujua kuwa inabidi uwe na sehemu uliyosimama ili uweze kuona huko mbele.
Je baba wa huyo kijana asingepata akili ya kujenga nyumba iliyotumiwa na huyo kijana kupata mtaji unaonaje hali ya kibiashara kwa huyo kijana ingekuwaje
Acha kudanganya watu,sio kila mtu afanye biashara bwana,biashara ya kuinvest kwenye majumba,viwanja(real estate) inalipa kinoma,sio kila mtu akipata hyo mil 10 aanze kuwa mchuuzi,maana bishara unazozungumzia wewe ni za kwenye kununua malonyalonya thailand au china na kuja kuyauza!!! Anachotaka lara 1 ni kwamba anawazubaisha watu hapa ili mtu akipata tu emu kumi avizungushe kwenye biashara hili amchune lakini mtu akinvest kwenye ujenzi hawezi chunika kirahisi..So watu wangu wa nguvu jengeni bwana msimsikilize huyo,mfano mie nilinunua kiwanja kwa 3m mwaka 2013 leo kinafikia thamani ya 20m ndani ya miaka mi3,ebu niambie bishara gani ambayo inauweza wa kukuingizia faida apprx 6m kwa mwaka? 17,000/= kwa siku? Biashara gani hyo? sitoingiza hela yangu kwenye vibiashra vya uchuuzi hata siku moja nawekeza kwenye tangible things,kuna watu walifanya kama unavyowachuza leo hii wanaemea pua moja hela ya mkopo yote ilikata wakaishia kuwa na mideni tu bank pamoja na mtaani