Waafrika tulipotoshwa kuhusu Chifu Mangungo wa Msovero sio mjinga, Watanzania tuiombe familia yake msamaha na tumuenzi kama shujaa wa uwekezaji

Waafrika tulipotoshwa kuhusu Chifu Mangungo wa Msovero sio mjinga, Watanzania tuiombe familia yake msamaha na tumuenzi kama shujaa wa uwekezaji

Mkuu acha kuhalalosha ujinga uliofanywa na huyo chief kwa kutumia kigezo cha uwekezaji katika karne hii.Maana hata kinachofanyika Sasa hivi bado ni ujinga kama alioufanya huyo chief,hamna Taifa lolote la watu wanajielewa akupe ardhi yake eti wewe uwekeze-ni ujinga wa kiwango cha PHD kwa nini wasiwekeze watu wako??
Kwa nini hao wawekezeaji wasiwekeze katika Nchi zao waje kuwekeza kwako,kwanza wanaua ubunifu wa watu wako na unaimarisha chumi za Mataifa yao kuliko lako-sasa hizo ni akili au matope?
Chifu mimi nimetumia Thesis yangu kuonesha Mangungo sio mjinga alichokifana kugawa ardhi kwa wawekezaji ndio kinafanywa saiv na viongozi wa Afrika. Nikiamini uwekezaji sio ujinga. Sa unanifokea wakati katika hiyo mikata sijaweka dole gumba mimi.
 
Hata ukisoma historia Mjerumani alidhamiria kuifanya tanganyika ifanane na ujerumani. Check mfano ramani ya mji wa tanga imekopiwa toka moja ya mji wa ujerumani, ni kichaa tu cha Hittler ndicho kilichoiponza ujerumani.
 
Maisha ya mwafrika yalikuwa bora Sana enzi ya ukoloni kuliko baada ya UHURU, kwa maana wakulima awakuwaza kuhusu soko wao jukumu lao lilikuwa ni kulima tu ishi ya soko sio wao, wafanyabiashara wa kiafrica walifanya biashara pasipo bughudha, ajira zilikuwa tele viwandani na mashambani, elimu na afya ilikuwa bora.
Ni tamaa tu ya wapigania UHURU ndio imeleta shida zote hizi, wao walipigania maslai yao binafsi kwa kuwahadaa waafrika wawape sapoti lakini lengo lilikuwa wao ndio walambe asali.
 
Hata ukisoma historia Mjerumani alidhamiria kuifanya tanganyika ifanane na ujerumani. Check mfano ramani ya mji wa tanga imekopiwa toka moja ya mji wa ujerumani, ni kichaa tu cha Hittler ndicho kilichoiponza ujerumani.
Sure kabisa.
 
Maisha ya mwafrika yalikuwa bora Sana enzi ya ukoloni kuliko baada ya UHURU, kwa maana wakulima awakuwaza kuhusu soko wao jukumu lao lilikuwa ni kulima tu ishi ya soko sio wao, wafanyabiashara wa kiafrica walifanya biashara pasipo bughudha, ajira zilikuwa tele viwandani na mashambani, elimu na afya ilikuwa bora.
Ni tamaa tu ya wapigania UHURU ndio imeleta shida zote hizi, wao walipigania maslai yao binafsi kwa kuwahadaa waafrika wawape sapoti lakini lengo lilikuwa wao ndio walambe asali.
Watakupinga ingaw ndio ukweli.

Hata kuwarudisha kwao hatukua sahihi. Mana kama sasa bado tunaangaika kuwasha waje kututembelea kwa kigezo cha utalii
Kuna watu watasema ugaguzi ungekuwa mwingi . Binafsi naona hata sasa tunabaguana wenyewe kwa wenyewe
 
Nachopendea ungwini unaweza kuufirimba upendavyo kujenga hoja; hauna kanuni za kueleweka. Kesho wewe mwenyewe au mwingine anaweza akajenga hoja on the same character kuonesha jinsi alivyokuwa mpumbavu na hoja zikakubalika vile vile!

By the way huwa najiuliza how comes mkataba kati ya Chief wa kaeneo kadogo kama Msowero uliepelekea territory kubwa kama Tanganyika iliyokuwa na thousands of chiefdoms kutwaliwa yote na Germans?

Je, wote wiliingia mkenge kama Mangungo? Au mkataba wa Mangungo ulitumiwa na Germans kuonesha machifu wengine "you see, others have surrendered their chiefdoms; you don't have other options but to abide"?

In short, sijawahi kuelewa mkataba wa Mangungo "kuuza" Tanganyika yote.
 
Watakupinga ingaw ndio ukweli.

Hata kuwarudisha kwao hatukua sahihi. Mana kama sasa bado tunaangaika kuwasha waje kututembelea kwa kigezo cha utalii
Kuna watu watasema ugaguzi ungekuwa mwingi . Binafsi naona hata sasa tunabaguana wenyewe kwa wenyewe
Mwafrika zamani alichukuliwa utumwani tena kwa msaada wa mwafrika mwenzake kwa nguvu kwenda utumwani leo hata kesho maelf ya vijana wa kiafrica wakishinda kwenye ofisi mbalimbali za ubalozi wakililia viza huku maelfu kwa maelfu wakihatarisha maisha yao baharini wakililia kwenda utumwani kwa hiari. SAsa UHURU una maana gani kama vijana wa kiafrica wanazikimbia nchi zao zenye fursa ya raslimali tele na kwenda kuwa ma cheap labour utumwani. Zamani waliitwa watumwa siku hizi jina limeadvance wanaitwa diasporas.
 
Kosa kubwa Sana la Mwalimu Nyerere ni kuacha mazuri ya mkoloni yaani alimchukia mkoloni na mazuri yake yote. Kwa hali ya SAsa Ili kumaliza tatizo la ajira nchini mfumo wa elimu wa mkoloni ndio jawabu, na sio mfumo huu wa elimu siasa. Mwalimu alikosea Sana kuingiza siasa kwenye mfumo wa elimu matokeo ni kuzalisha Jamii ya blah blah angalau Wakenya wao mfumo wao wa elimu ni ule tangu mkoloni kwa kufanyia maboresho tu.
 
Chifu mangungo hakuwa mjinga, watanzania tulipotoshwa, tunapaswa kuiomba familia yake msamaha

Kwa miaka mingi sana chifu mangungo ameendelea kuonekana kama mfano wa kiongozi mjinga hasa pale linapotokea swala la mikataba. Lakini je Mangungo alikuwa mjinga kweli?

Chifu mangungo ni nani?

Naomba ninukuu kidogo kipande cha historia fupi kuhusu chifu Mangungo kutoka katika uzi wa ndugu humu Jf KILABA

"Mangungo simultaneously for all his people and Dr. Peters for alt his present and future associates hereby concluded a treaty of Eternal Friendship.

Mangungo offers all his territory with all its civil appurtenances to Dr. Karl Peters, as the representative of the Society for German Colonization, for the exclusive and universal utilization for German colonization.

Dr. Karl Peters, in the name of the Society for German Colonization declares his willingness to take over the territory of the Sultan Mangungo with all rights for German Colonization subject to any existing suzerainty of Mwenyi Sagara.

In pursuance thereof, Sultan Mangungo hereby cedes all the territory of Msovero, belonging to him by inheritance or otherwise for all time, to Dr. Karl Peters, making over to him at the same time all his rights.

Dr. Karl Peters in the name of the Society for German Colonization undertakes to give special...attention to Msovero when colonizing Usagara.

This treaty has been communicated to the Sultan Mangungo by the interpreter Ramzan in a clear manner and has been signed by both sides, with the observation of the formalities valid in Usagara the Sultan on direct enquiry having declared that he was not in anyway dependent upon the Sultan of Zanzibar, and that he did not even know the existence of the latter.

Sgd. Dr. KARL PETERS
Sgd. MANGUNGO

This contract has been executed legally and made valid for all time before a great number of witnesses, we testify herewith:
Kwagakinga (mark);
Sultan Mangungo’s son of Golola (mark);
Sultan Mangungo’s second son of Draman (mark);
Graf Pfeil August Otto;
Mark of the intepreter Ramazan etc.
Dr. Karl Juhlke.
Msovero Usagara November 29, 1884.

Kwa tafsiri isiyo rasmi, kwa Kiswahili unasomeka hivi:
Mangungo, Sultan wa Msovero katika Mwenyisagara, na Dk. Karl Peters. Mangungo sambamba na watu wake wote na Dk. Peters kwa niaba yake na washirika wake wengine wajao kwa pamoja wanaweka mkataba wa Urafiki wa Kudumu.

Mangungo amekubali kutoa himaya yake yote pamoja na watu wake na hadhi yake kwa Dk. Karl Peters, kama mwakilishi wa Umoja wa Ukoloni wa Kijerumani (Society for German Colonization), kwa ajili ya matumizi ya moja kwa moja ya koloni la Kijerumani.

Dk. Karl Peters, kwa niaba ya jina la Umoja wa Ukoloni wa Ujermani anatangaza dhamira yake ya kuitwaa himaya yote ya Sultan Mangungo na haki zote kwa ajili ya Koloni la Ujerumani inayohusisha kila kona na amali za Mwenyi Sagara.

Katika kutekeleza hilo, Sultan Mangungo anakabidhi himaya yote ya Msovero, inayomilikiwa na yeye mwenyewe kwa urithi au kwa namna yoyote ile kwa nyakati zote, kwa Dk. Karl Peters, na wakati huo huo kumkabidhi haki zake zote.

Dk. Karl Peters kwa niaba ya Umoja wa Ukoloni wa Kijerumani anakusudia kuweka mkazo maalum kwa eneo la Msovero wakati wa kuitawala Usagara.

Mkataba huu umewasilishwa kwa Sultan Mangungo na mkalimani Ramzan katika dhana ya wazi kabisa na umesainiwa na pande zote, kwa kuzingatia taratibu zilizopo katika Usagara, Sultan baada ya kuhojiwa moja kwa moja alikiri kwamba hakuwa na ushirika ama kutegemea kwa namna yoyote Sultan wa Zanzibar, na kwamba hakuwa hata akimfahamu.

Imesainiwa. Dk. KARL PETERS
Imesainiwa. MANGUNGO

Mkataba huu umefanyika kihalali kabisa na umehuishwa kwa nyakati zote mbele za mashahidi wengi, ambao tunakiri hapa:
Kwagakinga (dole gumba);
Golola mtoto wa Sultan Mangungo (dole gumba);
Draman mtoto wa pili wa Sultan Mangungo (dole gumba);
Graf Pfeil August Otto.
Dole gumba la mkalimani Ramazan etc.
Dk. Karl Juhlke.
Msovero Usagara Novemba 29, 1884.



KWANINI MANGUNGO ALIONEKANA MJINGA?

Historia ilipoandikwa baada ya kupata uhuru , iliwahesabu watu wote waliopambana na wazungu kama mashujaa mfano Mkwawa. Bila kujali utawala wa hao machifu kama ulikuwa wa haki au laa. Historia haikutazama watawala hawa machifu kama watu walio pambania madaraka yao bali inawahesabu kama mashujaa kwa kuwa ilipambana tu mzungu.

Baada ya uhuru watu walisoma hadithi kama "KIBANGA AMPIGA MKOLONI". waliosoma kwa kipindi hicho walimuona Kibanga kama shujaa kwa kumpiga mzungu ( mkoloni). Lakini je Kibanga wa mwaka 1960 bado ni shujaa leo hii au ataonekana anafukuza "WAWEKEZAJI" ?

Kwahiyo kama KIBANGA alionekana shujaa kwa kumpinga mkoloni kipindi cha kutaka kujitawala ni wazi historia yoyote iliyoandikwa kwa kipindi hiko ingemtazama mtu yeyote yule aliyeshirikiana na wakoloni kipindi wanaingia Afrika kama mtu mjinga na msaliti kwa jamii yake.


KWANINI NASEMA MANGUNGO SIO MJINGA?


Kilichotokea kati ya Mangungo na machifu wengine waliopigana na wazungu ni uelewa tu. Mangungo aliona mbali ambapo wengine hawakuona kwa kipindi kile. MANGUNGO aliwaona wazungu kama wawekezaji mapema sana kuliko machifu wenzake. Kile alichokifanya Mangungo kuwaona wazungu kama wawekezaji ndio hiki tunakiona leo na sisi kuwa wazungu wanauwezo wa kuwekeza katika nchi zetu za kiafrika na uchumi ukakua.

JE MANGUNGO ALIAHIDIWA NINI KWA WAZUNGU?

Binafsi naamini tofauti na mkataba wa kuichukua ardhi na kiutawala tunaoambiwa kuwa ndio huo MANGUNGO alisaini lakini inaonesha wazi kwamba Mangungo alielezwa kuwa kama wazungu watalichukua eneo basi watakuja na mamba yafuatayo ;

mashine ( matreka) za kilimo kama treka nk

Ujenzi wa hospital za kisasa kwa (kipindi hicho)

Ujenzi wa shule

Ujenzi wa maghala ya kuhifadhia chakula

Ujenzi wa barabara

Ujenzi wa mabwawa ya kuzalisha umeme

Ujenzi wa reli ya kisasa kwa wakati huo

Ujenzi wa madaraja katika maeneo yasiyopitika kipindi cha masika

Upatikanaji wa huduma za maji safi .

Je upi unaweza kuwa uthibitisho wa hizo ahadi hadi kupelekea MANGUNGO kukubali?

Ukilitazama vizuri hilo eneo la Msovero ambalo ndio inaelezwa kuchukua eneo kubwa la KILOSA ya leo utagundua yafuatayo.

Maeneo mengi ya wilaya hiyo yana mashamba makubwa ya mkonge yaliyolimwa na mwekezaji wa Mangungo. Kuanzia Msowero ya leo , Gairo, Kimamba, Ludewa, Kilosa mjini ya leo, Chanzuru, Kivungu, Zombo , Mikumi, Kilangali , Malangali ,Ngaite, Melela Mvomero inayopakana na kilosa , ILONGA had maeneo ya dumila nk

Hayo ni maeneo machache sana yanayoonesha mwekezaji alitekeleza kweli ahadi yake ya kuinua kilimo.

Maeneo ya Kilosa mengi yalijegwa hospital. Mfano hospital ya Kilosa , Kimamba , vituo vya afya kama maeneo ya Ludewa , Mkata , na vingine ambavyo vilijegwa na wajerumani . Hivyo vitu havikuwepo kabla ya mkataba wa MANGUNGO.

Uwepo wa barabara kama ya kutoka Kilosa hadi Mikumi kupitia Zombo, barabara ya kutoka Kilosa hadi Morogoro mjini kupitia Mkata na ile kupitia Ludewa ni ushahidi tosha kuwa mwekezaji alifanya yale aliyoahidi mbele ya chifu Mangungo.

Uwepo wa njia ya reli inayopita tokea Morogoro mjini pale kichangani na kupita maeneo kama Mkata, Kimamba, Kilosa mjini ya sasa, Mkadage huko hadi Pwaga na kuingia Mpwapwa hii inaonedha jinsi gani mkataba wa chifu Mangungo na machifu wa kiluguru na wa kizingua ulizaa matunda kwa maeneo yao kiuwekezaji.

Uwepo wa shule ya KIZUNGUZI (kizu boys)

Ajira kwa vijana Uwepo wa huduma za malazi kwa wafanyakazi. Ajira ilipatikana kwa manamba japo mshahara haukuwa mkubwa lakini ukibadili thamani ya mshahara wa kipindi hicho unafanana na baadhi ya mishahara ya baadhi ya watu wanaolipwa hivi leo. Si kwamba hata hivi leo watu hawalalamiki udogo wa mishahara.

Nyumba za watumishi zilijegwa kila kwenye stesheni , kwenye kila kituo chao cha kukusanyia mikonge mfano Kimamba, ludewa , Chanzuru Msiwero , Kivungu nk. Hapa inaonesha ni jinsi gani mkataba aliosaini abwana mangungo haukuwa mbaya kama tunavyoaminishana leo hii.


Bado kama hayo hayatoshi ukipita maeneo ya Ilonga utaona jinsi wajerumani walivyopaendeleza katika kilimo na vituo vya utafiti wa kilimo walijenga ( hapa mtanikosoa kama walijenga wajerumani au waingereza).


Kwa wale watu walio bahatika kuishi Sagara ya zamani au Kilosa ya leo wanaweza kuwa mashahidi . Mji wa kilosa wa leo unaoneka ni mji uliokuwa wa kifahari enzi ya wawekezaji wa Mangungo ( ambao waliitwa wakoloni hapo awali) kabla ya kubadilishwa jina tena na kuitwa wawekezaji kama alivyowaita Mangungo na kizazi cha sasa . Kilosa ulikuwa mji kimbilio la wageni toka mikoa mbali mbali Tanzania. Usifikiri katika "engo" ya manamba kupata mchanganyiko wa kabila katika eneo la kilosa bali hata huduma ziliwavuta vijana wa zamani kwenda kuishi Kilosa.

Je kunyonywa kiuchumi ndio kunatufanya tumuone Mangungo alikuwa mjinga?


Binafsi namuona Bwana Mangungo kama kiongozi aliyeuona uwekezaji tangu mapema. Kwani kama kuhusu kunyonywa bado hadi leo kama taifa bado tuna mikataba mingi ya kinyonyaji isiyoacha alama kwa taifa kuliko ile ya msovero iliyoacha hata reli ,magofu ya nyumba na hospital.
Wapo watakaosema ujinga wa Mangungo ni kuiachia ardhi kwa wazungu kulima pamba na mikonge huku wenyeji kuishi kwa njaa. Binafsi naamini kwa nyakati hizo kulikuwa na watu wachache sana wenye uwezo wa kulima mamia ya ekari kama wawekezaji. Wengi walilima kujikimu kwani ni miaka zaidi ya 70s sasa tangu Mzungu atuachie ardhi yetu lakini kuna maeneo tangu kuumbwa kwa dunia hayajawahi kulimwa na wazawa. Vijana wanashinda kwenye vituo vya kubeti huku redio zikihamasisha nguvu ya buku katika kushinda kamali. Kwa mawazo kama hayo hatuoni kama bwana Mangungo aluoba mbali kuingia mikataba na wawekezaji?

Wapo watakaosema ujinga ni kuwa alisaini bila kuelewa chochote . Binafsi naona si kweli, kwani kama ni kweli Mangungo alisaini kitu asichoelewa historia ingeonesha kutokea mgogoro baina ya mwekezaji na Mangungo. Katika hali ya kawaida mtu akwambie muingie makubaliano ya kulichukua eneo lako lote la ardi na kiutawala na ukakubali bila kumuuliza shughuri atakazofanyia eneo lako. Pili, mkata ulisainiwa kisha Karl na wenzake wakaondoka kurudi Ujerumani . Kama wangekuwa ni walaghai basi pale waliporudi kutekeleza uwekezaji wao lazima pangetokea ugomvi na kutoelewana. Maana katika hali ya kawaida ukimpa mtu eneo alime au akae alafu ghafla unamwona anakuja na fundi wake wanajenga nyumba , hospitali, reli bila kwenda kuwahoji.

MANGUNGO ALIKUWA KIONGOZI MWANADIPLOMASIA

Kwajinsi sasa jamii ya Kiafrika inavyomsifu kiongozi mwenye mahusiano mazuri na wazungu kama kiongozi bora na mwanadiplomasia basi ni wazi Mangungo alikuwa nguli zaidi kama mwanadiplomasia wa mwanzoni kabisa.

NINI WITO WANGU KWA JAMII

Niwakati sasa wa jamii yetu kubadili mtazamo juu ya chifu Mangungo kwa kumchukulia kama kiongozi mjinga na kumwona kama kiongozi wa mwanzoni kuhamasisha uwekezaji nchini. Kumwona Mangungo kama kiongozi mjinga kumeifanya hata familia yake isijulikane leo hii ksma zinavyojulikana familia za ma chifu wengine. Kwakuwa sasa viongozi wetu wamerudi kule kule kuwapokea wazungu na kufanya nao shughuri za maendeleo kama ujenzi wa miundombinu ya maji , barabara, reli, hospitali, na shule jambo ambalo hata Mangungo ndilo alilifanya kwa ustadi basi hatuna budi kumuenzi Mangungo kama mwasisi wa uwekezaji nchini.
Natamani sasa hata familia yake iliyobaki tuiombe msamaha kama taifa kwakuwa tulilewa mvinyo wa uhuru kiasi ya kuwaona waliopinga kushirikiana na wazungu kuwa ndio MASHUJAA.

Nawasaliim
KATIBA ya eneo alilokuwa anatawala Mangungo ilikuwa inasemaje juu ya umiliki wa ardhi?, Kama hakukuwepo katiba utambanaje mwekezaji akikiuka masharti?,
KIFUPI: Mangungo aliingia chaka, ingawa hasitahili kulaumiwa sana, Kwasababu hakuwa na uelewa juu ya hilo jambo ( mkataba). Ila inasikitisha Sana siku hizi watu wamepata elimu na wanaingia mikataba ya ajabu.
 
Mangungo alikuwa genius kama hawa mageneus wetu wanaotuletea wawekezaji na maelfu ya watalii, Chief Mangungo kumbe aliliona hili kitambo na kumleta Mzungu mwekezaji, bila shaka Mangungo naye alitengeneza filamu ya Royal tours zama hizo wakaja akian Karl Peters na Bwana Ramzani dalali.
 
Akili ya Bwana Ramzani haina tofauti na akili ya Mhindi aliyepo Tanzania na sisi kumuona mzawa, Bwana Ramzani zama zile alikuwa Dalali hawa ndugu zake kwa sasa ni madali wa resources zetu na wengine wameenda mbali nao kuwa slave master in foreigner land and disgusing as natives.
 
Hapa naona kuna afrocentric historians na Eurocentric historians mchuano ni mkali. Nani yupo sahihi na Nani hayupo sahihi ni kama Imani za dini, kila mtu abakie na kile anaamini
Wewe kama umesoma hiyo mitazamo yote miwili ilitakiwa uwe na point ya kufanya decision ya usahihi na ukosefu. Huwezi kusema kila mtu abaki na mtazamo wake. Hii siyo dini, hata dini inakosolewa.
Chief alizingua. Ethiopia walipigana kuanzia 1800 mpka 1930s. Yeye alishindwa nini mpka akubali kutoa ardhi na miliki ya watu wake?

Na kama Mangungo alikuwa sahihi maana yake harakati za Uhuru hazikuwa sahihi?
 
Mkuu acha kuhalalosha ujinga uliofanywa na huyo chief kwa kutumia kigezo cha uwekezaji katika karne hii.Maana hata kinachofanyika Sasa hivi bado ni ujinga kama alioufanya huyo chief,hamna Taifa lolote la watu wanajielewa akupe ardhi yake eti wewe uwekeze-ni ujinga wa kiwango cha PHD kwa nini wasiwekeze watu wako??
Kwa nini hao wawekezeaji wasiwekeze katika Nchi zao waje kuwekeza kwako,kwanza wanaua ubunifu wa watu wako na unaimarisha chumi za Mataifa yao kuliko lako-sasa hizo ni akili au matope?
Shida watu hawaelewi kitu kimoja. Concept nzima ya kuwekeza ni ubepari. Ubepari haujawai kuwa mfumo sahihi kwa maendeleo ya waafrika duniani.
 
Hata ukisoma historia Mjerumani alidhamiria kuifanya tanganyika ifanane na ujerumani. Check mfano ramani ya mji wa tanga imekopiwa toka moja ya mji wa ujerumani, ni kichaa tu cha Hittler ndicho kilichoiponza ujerumani.
Mkuu ulishawaisikia mjerumani anamponda Hittler popote pale?
Bila Hittler Ujerumani ingekuwa shithole kabisaaa
 
Watakupinga ingaw ndio ukweli.

Hata kuwarudisha kwao hatukua sahihi. Mana kama sasa bado tunaangaika kuwasha waje kututembelea kwa kigezo cha utalii
Kuna watu watasema ugaguzi ungekuwa mwingi . Binafsi naona hata sasa tunabaguana wenyewe kwa wenyewe
Hivi umesema hii mada ni thesis yako?
Yaani unafanya research ya historia. Kwamba wewe ni historian, mwafrika, kutoka Tanganyika na haya ndiyo mawazo yako? Au unasapoti ili mada yako ipate wachangiaji?

Excuse my language. No offense intended.
 
IMG_4935.jpg
 
Hivi umesema hii mada ni thesis yako?
Yaani unafanya research ya historia. Kwamba wewe ni historian, mwafrika, kutoka Tanganyika na haya ndiyo mawazo yako? Au unasapoti ili mada yako ipate wachangiaji?

Excuse my language. No offense intended.
Mkuu nisamehe kwa kutumia lugha vibaya
Thesis niliyoisemea hapo sijamanisha research proposal au desertion inayowasilishwa na mwanafunz atakae master au PhD.

Nilimanisha ile maana hii

Thesis

a statement or theory that is put forward as a premise to be maintained or proved.
"his central thesis is that psychological life is not part of the material world"
Synonyme: theory, contention, argument, line of argument, proposal, proposition, premise, assumption, presumption, hypothesis, postulation, surmise, supposition, belief, idea, notion, opinion, view, theme, subject, topic, text, matter, theorem
 
Back
Top Bottom