Waandishi Wa Habari Mmetia Aibu Kwenye Press Baada Ya Mchezo Wa Young Africans Na Mamelod Sundowns

Elimu ndio shida tutalaumiana sana ila kuwa na elimu duni Kuna waumiza sana watanzania Nina uhakika hata wewe kazi Yako japo sijui lakini unaifanya kwa kiwango Cha chini sana shida ni elimu na mazingira ya kazi
Watu wameshupaa kupata A tu ili wapate vyeti, tuition zinafundisha kufaulu mtihani tu,wahitimu wengi siku hizi ni mabogus
 
Tanzania ina watu wenye sifa za kuitwa waandishi wa habari wachache sana. Hawa wengine wote ni ''wajanja'' waliotumia ujinga wa wabongo kujiita waandishi kwa sababu wanajua kuzungumza kama cherehani. Hivi Maulid Kitenge yule unaweza kumwita ni mwandishi? Kwa kifupi siyo waandishi tu ila kila sehemu na fani ina vilaza wengi.
 
Uelewa wa mambo ndiyo shida. Kwa mfano wewe kwa uelewa wako unahisi kila mtu humu jukwaani aliifuatilia hiyo press baada ya mechi?

Hebu weka hoja yako kwamba wameuliza maswali gani ambayo yamewadharirisha!
 
Waandishi wa kibongo washazoea taarifa za umbea umbea tu...huwa najiuliza sijui hawaangalii pre na post matches conference za UEFA na EPL?

Pia naishauri TFF waweke utaratibu katika hizi mechi za kimataifa wawachague baadhi ya waandishi wa habari (wanaojua kingereza) wawe wanawahoji makocha na wachezaji kabla na baada ya mechi...wengine watege tu microphones zao tu kupata contents.
 
Wewe unaweza au ushamba tu
 
Kocha wa Jwaneng walipofungwa goli 6, mwandishi anauliza how do you feel today after the game?mwandishi alikemewa kama mbwa na wengine waliofuata wakanywea kuuliza! Hawa waandishi wa bongo ukikaa vibaya kama ni kocha wanaweza kukuuliza hata kwanini leo hujafuatana na mkeo kwenye hii game.
 
Sio waandishi wa habari tu sector zote... Mbona madaktari wanapasua wagonjwa vichwa baada ya miguu🙄🙄. Afu kiingereza sio lugha mama yetu. Hatuitaki asee.
 
Mechi ya leo ilikua na maswali mengi sana ya kuuliza hasa mbinu za mchezo. Kuna mahali tunakwama, angalia hata mechi zetu hizi za ligi kuu huwa hawaulizi maswali mazuri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…