Waandishi wa habari Tanzania hamjitambui

Waandishi wa habari Tanzania hamjitambui

Waandishi wa habari wapo kumi tu Tanzania ,Namba moja ni Jenearali Ulimwengu wengine in wasaka tonge
 
Waandike Habari za Simba na yanga, Diamond. Habari za uchunguzi bado ufinyu wa Mawazo na uthubutu ni tarizo. Wanatanguliza siasa sana. Tatizo taaluma hii inahitaji personal values
 
Hawa ni kama waalimu; miaka nenda rudi unadai stahiki zako hata dalili ya kupewa huzioni..

Natamani sana kufahamu mwenzetu upo kwenye kundi gani kwenye jamii yetu (mfanyakazi, mkulima, mfanyabiashara, mwekezaji, nk) ambalo kimsingi umeweza kudai stahiki zako chini ya utawala huu wa awamu ya tano, na mara moja ukapatiwa kwa wakati!

Tuanzie hapa kwanza kabla ya kuyalaumu hayo makundi mengine yakiwemo ya hao walimu, waandishi wa habari, nk.
 
Hata nyie mnaotokwa povu hapa jf ni makanjanja tu.Hata nyie mnaweza kuandika tu hizo habari mnazozitaka kupitia magazeti iwe makala au maoni.Tatizo kila mmoja ni bingwa wa kutokwa povu akiwa nyuma ya keyboard tena akiandika kupitia jf, mnataka nani asacrifice maisha yake na ya familia yake? Kiherehere kibaya!!
 
Mkuu hapo Paskali Mayalla naye yuko kwenye hiyo list? Ngoja aje atuaambie wao waandishi wa habari ni kweli ngawajitambui? Maana huwa namuona anasema wapinzani hawajui wanataka nini, ngoja aje atuambie waandishi wa habari wao wanataka nini.
 
Pascal Mayalla
Wewe ni mwandishi tunayekutambua zaidi humu!
Njoo ujibu hizi tuhumu za kutokujitambua, maana kwa mfano hilo la Gwanda, sijui kama kuna sehemu ulishawahi kulipigia kelele mwana...


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Mbona pesa alizokuwa analipwa na hao mabwana zake alikula yeye na Kabwe tu!!
Kila mtu abebe mzigo wake.
Ukweli tasinia ya habari ni vichwa maji mwenzenu kabendera mpk leo mnajua kbs nn kilichopelekea yeye akawa ndani mpk sasa

Hamjatoa ushirikiano wowote usaliti wenu hautawapeleka popote mtatafunwa mmoja mmoja mpk mtaisha

Na wengine mnashangilia kwa yaliyomkuta mwenzenu

sent from toyota Allex

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata hao wanaotwiti twiti huko kina Zitto baada ya mama kuomba msaada na kusema Erick ndiye aliyekuwa akimtegemea kwenye matibabu yake wangekuja na hata harambee kumchangia kupitia hukohuko twita kwa kuweka namba angepata hela ya matibabu......nimeona namba ya rambirambi tu.

Kuna watu wanatumia matatizo ya kabendera kama faida kisiasa.......ili waonekane.....kwa umaarufu wao isingeshindikana kumpatia hela ya matibabu.Ila unafiki ni mwingi sana.
 
Back
Top Bottom