Wabongo kwa kujiita C.E.O mitandaoni utafikiri hata wanajua maana na kirefu cha herufi hizi. Sio mbaya kujiinua ila huu ni ulimbukeni.

Haahhahah c.e.o anapitisha kapu achangiwe wakacheze ndondo mbagala
 
Uko sahihi huwa nikimkuta mtu anabiashara yake mahali kubwa au ndogo kimoyo moyo nasema Mungu bariki maana si mchezo aisee kuendesha biashara hasa tz
Sawa ila sio CEO, HUYO NI MMILIKI WA DUKA LAKE.
 
Mkuu,

Inaonekana kama wanakuumiza sana wakipost hivyo eeh?

Watu wamenyimwa u CEO wa kweli, wewe unawanyima mpaka u CEO wa kujifurahisha wenyewe?

Mbona unakuwa mnoko hivyo?
 
Mkuu,

Inaonekana kama wanakuumiza sana wakipost hivyp eeh?

Watu wamenyimwa u CEO wa kweli, wewe unawanyima mpaka u CEO wa kujifurahisha wenyewe?

Mbona unakuwa mnoko hivyo?
Haha mimi ni mnoko ila sio mnonko zaidi ya C.E.O feki.

Unajiita ceo wakati una jiko unajipikia dukani kwa kuogopa gharama za mama ntilie haha
 
Chief Executive Officer ndie yeye na akiwa hayupo biashara itafungwa huenda ana ndoto kubwa ila kaanza kidogo
Sasa hapo unaleta maana yako pekee na una i-force iwe utakavyo. Goodluck.

YOU ARE A SHOP OWNER NOT A C.E.O

ACHENI MAZINGAOMBWE.
 
Wanajitabiria.
 
Kabisa mkuu, udeal na TRA, Halmashauri na matawi yake, na ulipie fremu bado na wewe ubakiwe na ya kula halafu usiwe CEO?
Na u deal na wakopaji na wateja wanaosusa mara bidhaa kuadimika sokoni mara kupanda bei mara friji haligandishi mara umeme haupo siku nzima
Yani sio tu CEO ni Champion kabisa๐Ÿ™Œ๐Ÿ™Œ๐Ÿ™Œ
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ