Wabongo mkija majuu au ughaibuni acheni unafiki, majungu na ukora mnaliabisha Taifa lenu

Wabongo mkija majuu au ughaibuni acheni unafiki, majungu na ukora mnaliabisha Taifa lenu

Mkuu Qualification siyo ishu,kuna watu wanaingiza mpunga mrefu na hawana hizo qualification unazotaka wewe.

Fursa zipo kibao,wewe unachotakakiwa ni kuzimwaga humu hapa na namna ya kuzifikia.Tunafahamu kufika huko ndiko tatizo,wewe inapaswa utusaidie namna ya kufika huko kwakuwa unauzoefu hata kama ni kwa pesa tutalipa.
Umeshindwa kujibu swali Dogo tu, sasa hata ukipewa fursa una uwezo wa kumuelewesha consular ni kwa nini akupe viza?
 
Umeshindwa kujibu swali Dogo tu, sasa hata ukipewa fursa una uwezo wa kumuelewesha consular ni kwa nini akupe viza?
Hiyo visa unaweza kunyimwa vilevile hata kama ukimuelewesha consular,jambo la msingi ni kuwsshirikisha watanzania namna gani ya kupata visa kwa urahisi na siyo blah blah.

Huu ujuaji ndiyo jamaa anaouzungumzia hapo,mkikaa huko nje huwa mnaonaga watanzania wenzenu ni wajinga na hawana akili.

Kwa kifupi watanzania muishio nje mna roho mbaya sana
 
Siyo vizuri kuwa kisiwa. Ni vizuri kushosolaiz na kujichanganya kigumu hivyo hivyo.

Kuna nature kama kifo na kuuguwa. Japo mibongo mingi ni mitambo ya umbea hivyo hivyo tu itasaidia.

Lakini tabia zetu mtoni ni mbofumbofu na kukera.
Nasemaje hapa duniani ukitaka kuwa na amani kuwa mwenyewe mwenyewe tu, shirikiana na watu penye ulazima tu, watu wanakera mno...
 
Mkuu wewe unafahamu mambo kibao tu ambayo unapaswa kuwasaidia wabongo wafike huko na kufanikiwa hata kama si mimi,wasaidieni watanzania na muache roho mbaya
Nimekuuliza, wewe ushajiridhisha hizo fursa sijawahi kuziweka hapa?

Hujajibu.

Yani unataka mtu akusaidie, lakini unaanza kwa kumu antagonize kwanza.

Kijumlajumla, bila ushahidi.

Huyo mtu atakusaidiaje?
 
Hiyo visa unaweza kunyimwa vilevile hata kama ukimuelewesha consular,jambo la msingi ni kuwsshirikisha watanzania namna gani ya kupata visa kwa urahisi na siyo blah blah.

Huu ujuaji ndiyo jamaa anaouzungumzia hapo,mkikaa huko nje huwa mnaonaga watanzania wenzenu ni wajinga na hawana akili.

Kwa kifupi watanzania muishio nje mna roho mbaya sana
Mbona EBM anawapa free consultation gharama bundle lako tu?

Au mpaka mpigwe agency fee ndio roho zenu ziwe kwetu kwamba sasa umepewa mchongo?

Halafu Mimi nipo Bongo ujuwe nikitaka viza ya Marekani ni SAA mbili asubuhi tu.

Nina vigezo vyote wanavyotaka Wamarekani na kikubwa ni family ties na intention to leave US after short stay.
 
Wewe hubebeki, halafu unapenda kulaumu watu wengine kwa matatizo yako mwenyewe.
Mkuu habebeki kivipi?
Mambo mengine madogomadogo ni ya kueleweshana tu, kuna watu wana ndoto za kwenda nje lakini wanakosa abc's za namna ya kufanya ili waje huko. So ni jambo la kujitoa hasa nje ya hapo unaweza kuwaona watu hawako serious.

Mfano kuna mtu ana ndoto ya kwenda kufanya kazi nje lakini hajui huko wanahitaji watu wa fani gani, skilled au unskilled n.k. Wengine hawajui hata kutofautisha passport na visa, wengine hata uhamiaji hawajawahi kusogea. Kwa hiyo nyie mliopo nje endeleeni kuwapa madini vijana wanaotaka kutoka nje kusaka fursa nzuri zaidi
 
Acha uongo
Sasa unauliza swali halafu hutaki jibu.

Wewe ushajiwekea negative thinking kwa hiyo husaidiki.

Badala ya kutaka kujua hao wawili ilikuwaje, nimewezaje kuwasaidia, unaniita muongo.

Hata kama nilikuwa na nia ya kukusaidia, unaondoa nia hiyo.

Wewe mwenyewe una negative mentality, ndiyo maana nikasema hubebeki.

Yani wewe mwenyewe huna mentality ya kuweza, hivyo ni vigumu mtu mwingine kukusaidia.
 
Back
Top Bottom